Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia amerudishwa nyumbani kwa tuhuma za Upotevu wa Fedha Ubalozini

Ngwanakilala

JF-Expert Member
Jun 25, 2011
774
1,456
Nimemsikia Mh Rais leo alipokua anapokea ripoti ya CAG na TAKUKURU huko chamwino Dodoma akisema amemrudisha nyumbani balozi wa Tanzania nchini Ethiopia kupisha uchunguzi wa upotevu mkubwa wa fedha

Utafiti unaonyesha balozi huyu ni mama Naimi Hamza Azizi

Na suala hili lilianza kuchunguzwa tangu mwaka jana kama inyosemeka hapa chini
1585253662726.png

Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia mikononi mwa Takukuru

Friday November 15 2019


Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa (Takukuru) nchini Tanzania imekabidhiwa jalada na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki la uchunguzi la upotevu na matumizi mabaya ya fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.
Advertisement

Dar es Salaam. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeikabidhi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) jalada la kulifanyia uchunguzi upotevu wa fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Faraji Mnyepe amekabidhi jalada hilo leo Ijumaa Novemba 15, 2019 kwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo katika ofisi ndogo za wizara jijiji Dar es Salaam.

Hatua hiyo imekuja kutokana na jitihada za Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Rais John Magufuli za kupambana na kuzuia rushwa pamoja na matumizi mabaya ya fedha za umma.

Uchunguzi huo unafanyika baada ya kubainika upotevu/matumizi mabaya ya fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.

Kuhusu kiwango cha fedha kilichopotea Katibu Mkuu, Dk Mnyepe amesema kitajulikana mara baada ya Takukuru kukamilisha uchunguzi huo wa jalada walilokabidhi.
 
... ukimsachi hukosi green card kwenye kipochi na ukiendelea kutafiti zaidi lazima ukute alianzia hukoooo UVCCM! Ndio historia za hawa watu; sio wanaume sio wanawake wote wanafanana tabia linapokuja suala la "mali za umma".
 
CHADEMA et SEREKAL ya ufisad wamesahau ufisad wa CHADEMA
Nimemsikia Mh Rais leo alipokua anapokea ripoti ya CAG na TAKUKURU huko chamwino Dodoma akisema amemrudisha nyumbani balozi wa Tanzania nchini Ethiopia kupisha uchunguzi wa upotevu mkubwa wa fedha

Utafiti unaonyesha balozi huyu ni mama Naimi Hamza Azizi

Na suala hili lilianza kuchunguzwa tangu mwaka jana kama inyosemeka hapa chini
View attachment 1400286
Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia mikononi mwa Takukuru

Friday November 15 2019


Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa (Takukuru) nchini Tanzania imekabidhiwa jalada na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki la uchunguzi la upotevu na matumizi mabaya ya fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.
Advertisement

Dar es Salaam. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeikabidhi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) jalada la kulifanyia uchunguzi upotevu wa fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Faraji Mnyepe amekabidhi jalada hilo leo Ijumaa Novemba 15, 2019 kwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo katika ofisi ndogo za wizara jijiji Dar es Salaam.

Hatua hiyo imekuja kutokana na jitihada za Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Rais John Magufuli za kupambana na kuzuia rushwa pamoja na matumizi mabaya ya fedha za umma.

Uchunguzi huo unafanyika baada ya kubainika upotevu/matumizi mabaya ya fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.

Kuhusu kiwango cha fedha kilichopotea Katibu Mkuu, Dk Mnyepe amesema kitajulikana mara baada ya Takukuru kukamilisha uchunguzi huo wa jalada walilokabidhi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu sio mjukuu wa Azizi Ally wa mtongani kwa Azizi Ally. Si wapo vizuri tangu ukoloni
Duh!.
Tukianzia kwa Aziz Ally
Kuna Dossa Aziz muasisi wa TANU alikutana na majanga.
Akaja Hamza Azizi wa polisi akakutana na majanga.
Akaja Capt. Azizi wa ATC naye yakamkuta ya kumkuta
Kuna mrembo mmoja wa familia ya Aziz naye ana yake.
Sasa Balozi Aziz!.

NB. Inawezekana ni majina tuu kufanana lakini hao Aziz wakawa ni familia tofauti na sio familia moja, lakini wakiwa ni familia moja, waandishi wa IJ inabidi wawatembelee.

Mzee wetu Maalim Mohamed Said bingwa wetu wa historia za waasisi, jee kina Aziz hao ni nasaba moja?. Tupe kisa cha Aziz Ali na Dossa Aziz watu wa kuunganisha dots tuunganishe kama yanayowatokea kina Azizi ni karma au ni ya walimwengu tuu, maana Balozi naye ni mashallah, udhaifu wa watu wetu tunaujua!, kisije kuwa ni kisa kama cha yule mama jicho gololi wa TIC au yule baby face wa SSRA.

P
 
Back
Top Bottom