Ngwanakilala
JF-Expert Member
- Jun 25, 2011
- 774
- 1,456
Nimemsikia Mh Rais leo alipokua anapokea ripoti ya CAG na TAKUKURU huko chamwino Dodoma akisema amemrudisha nyumbani balozi wa Tanzania nchini Ethiopia kupisha uchunguzi wa upotevu mkubwa wa fedha
Utafiti unaonyesha balozi huyu ni mama Naimi Hamza Azizi
Na suala hili lilianza kuchunguzwa tangu mwaka jana kama inyosemeka hapa chini
Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia mikononi mwa Takukuru
Friday November 15 2019
Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa (Takukuru) nchini Tanzania imekabidhiwa jalada na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki la uchunguzi la upotevu na matumizi mabaya ya fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.
Advertisement
Dar es Salaam. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeikabidhi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) jalada la kulifanyia uchunguzi upotevu wa fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Faraji Mnyepe amekabidhi jalada hilo leo Ijumaa Novemba 15, 2019 kwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo katika ofisi ndogo za wizara jijiji Dar es Salaam.
Hatua hiyo imekuja kutokana na jitihada za Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Rais John Magufuli za kupambana na kuzuia rushwa pamoja na matumizi mabaya ya fedha za umma.
Uchunguzi huo unafanyika baada ya kubainika upotevu/matumizi mabaya ya fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.
Kuhusu kiwango cha fedha kilichopotea Katibu Mkuu, Dk Mnyepe amesema kitajulikana mara baada ya Takukuru kukamilisha uchunguzi huo wa jalada walilokabidhi.
Utafiti unaonyesha balozi huyu ni mama Naimi Hamza Azizi
Na suala hili lilianza kuchunguzwa tangu mwaka jana kama inyosemeka hapa chini
Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia mikononi mwa Takukuru
Friday November 15 2019
Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa (Takukuru) nchini Tanzania imekabidhiwa jalada na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki la uchunguzi la upotevu na matumizi mabaya ya fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.
Advertisement
Dar es Salaam. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeikabidhi Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) jalada la kulifanyia uchunguzi upotevu wa fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Faraji Mnyepe amekabidhi jalada hilo leo Ijumaa Novemba 15, 2019 kwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo katika ofisi ndogo za wizara jijiji Dar es Salaam.
Hatua hiyo imekuja kutokana na jitihada za Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Rais John Magufuli za kupambana na kuzuia rushwa pamoja na matumizi mabaya ya fedha za umma.
Uchunguzi huo unafanyika baada ya kubainika upotevu/matumizi mabaya ya fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.
Kuhusu kiwango cha fedha kilichopotea Katibu Mkuu, Dk Mnyepe amesema kitajulikana mara baada ya Takukuru kukamilisha uchunguzi huo wa jalada walilokabidhi.