Balozi wa REDDS 2008 arejesha Taji na Zawadi

Keil

JF-Expert Member
Jul 2, 2007
2,214
803
BALOZI wa REDDS 2008 Angela Luballa ametamka rasmi leo kwamba ameamua kurudisha Taji hilo la Balozi wa kinywaji cha Redds wa Mwaka 2008 ambalo ni wiki moja tangu avalishwe kwenye mashindano ya kumtafuta Miss Vodacom Tanzania 2008.

Luballa ambaye pia alishika nafasi ya tatu katika shindano la kumsaka Miss Tanzania, amesema kuwa imani yake haimruhusu kuwa Balozi wa REDDS.“Imani yangu kwa Yesu ni kubwa mno na hainiruhusu mimi kuwakilisha REDDS, hivyo nimeamua kurejesha taji na zawadi za fedha nilizopewa,”alisema Luballa. “Nimerudisha taji hili si kwa shinikizo la mtu yeyote bali ni imani yangu, siwezi kuwa balozi wa REDDS.

''Luballa ambaye inaaminika ni mtoto wa mchungaji ana imani ya kanisa lao ambalo haliruhusu kujihusisha na kitu chochote kinachohusu pombe. Luballa anasali katika Kanisa la World Alive International Outreach lililopo Sinza. Mrembo huyo alisema kuwa tayari ameshaiarifu Kamati ya Miss Tanzania na kurudisha taji na fedha Sh milioni 2.5 alizopewa kwa kutwaa taji hilo.

Source: Haki-Ngowi
 
....duuh, shs million 2.5 kazidindishia?! .....ama kweli huyo kaingiwa na 'pepo watakatifu' !!!!!! :D
 
duh kaali kweli wa kupepewa huyu naona ni mapepe!
hajatulia haaaataa kidoogo!
yaani hiii imani kipindi chooote cha kutembea na b..hakuwa nayo ?
 
Hongera mtoto wa mchungaji. Mi nadhani ni vyema binti mdogo kama huyu akaonyesha principal. Nadhani ilibidi ashauriane na familia yake na amefanya vyema kukataa kuhusika na kitu ambacho imani yake haiendani nayo. Hata kama binafsi mi naona si sahihi lakini nam-admire kwa kuonyesha principal. Sasa hii ni kasheshe kwa Miss Tanzania na Redds...
 
Mambo matata na utatanishi mkubwa... Sikujua kama kuna makanisa yanakubaliana na mchakato mzima wa mashindano ya Ulimbwende lakini yanagomea suala zima la kuhusiana na Pombe...

Kweli kuna utata katika dini zetu.!
 
BALOZI wa REDDS 2008 Angela Luballa ametamka rasmi leo kwamba ameamua kurudisha Taji hilo la Balozi wa kinywaji cha Redds wa Mwaka 2008 ambalo ni wiki moja tangu avalishwe kwenye mashindano ya kumtafuta Miss Vodacom Tanzania 2008.


Wakati anapokea hiyo zawadi imani yake ilikuwa wapi? Kwanini amesubiri wiki nzima kufikia uamuzi wake huo kama hakushinikizwa?
 
Wakati anapokea hiyo zawadi imani yake ilikuwa wapi? Kwanini amesubiri wiki nzima kufikia uamuzi wake huo kama hakushinikizwa?

Na siku anapokea zawadi na wazazi walikuwepo kumsapoti kwenye party aliyoandaliwa, au imani hiyo ameanza baada ya wiki moja toka apokee zawadi?, na hiyo ni imani gani inayoruhusu mchakato mzima wa kutafuta miss, na kukataza redds? au pombe kwa maana nyingine! Lol, sijawahi ona hii.....
 
huyu mrembo hakutendea watanzania HAKI...nadhani hakutakiwa in first place hata kushiriki..kwa vile kwa kushiriki haya mashindano ni wazi lazima utwae moja ya zawadi au upewe cheti cha ushiriki...na mashindano yenyewe kwa wenye imani kali ni dhambi.....

..nadhani wenye kosa wengine ni kina lundenga kwani hupenda kuokota warembo pasipo kuwashirikisha wazaazi wao...utakuta huyu mrembo alishiriki pasipo wazaazi kujua ..na hata angeshinda lazima wangemshinikiza arudishe zawadi...

si mara ya kwanza ...kuna wakati baba wa mrembo mmoja ....nadhani NARGIS MOHAMED or something like that ..aligombana na hii kamati kwa kitendo cha kumrubini...mtoto wao kushiriki na kama sikosei alirudisha zawadi pia..

wadhamini sasa wakati umefika kuwataka waandaaji wawaapishe washiriki wote mwakani kuwa .....wanaapa kuelewa mantiki nzima ya mashindano...na kwamba wanajua kwamba mashindano hayaingiliani na imani yao ya dini au vinginevyo na kwamba pamoja na kuwa wana zaidi ya miaka kumi na nane ..wameshauriana na watu wao wa karibu ie...wazazi,mchumba[wachumba],walimu[ie kuna vyuo vinapingana na imani.....na lazima fomu isainiwe na mrembo na kushuhudiwa na watu wawili wa karibu waliotajwa......
..ikifanyika hivi haitawezekana mrembo kujitoa au vyovyote..its LIKE a SECURITY DECPARATION....au sio ...wanasheria mnasemaje ..nadhani mtaiweka hiii sawa...mimi sio lerned fellow...
 
Mie nahisi karudisha wa sababu zingine,

ila kama ni hiyo inaweza kuwa sawa,mara nygi hawa watu wa Miss Tanzania wamekuwa wakiwatumia hao mamiss kwa huduma zao binafsi kama Viburudisho,

Mie nina Mtoto wa daada yangu alishawahi kushiriki Umiss na madhara yake mpaka leo Binti ashikiki kwa wazee na vijana wa umri wangu ili khali mpwa wangu ni mdogo sana..

Mie siwezi kumruhusu mtoto wangu kushiriki Urembo.wewe ulishawahi kuona zaidi ya silimia 10 ya mamiss wanaolewa,wanamegwa na wazee wa umri wa baba zao.

Mzee kashtuka ....
 
Kwa tabia za wasichana wetu wa siku hizi kurubuniwa na vilaki huyu kurudisha 2.5m na kusamehe 3m ya mshahara wa mwaka tumsifu tena sana.Mimi wiki hiyo 1 nachukulia ni muda aliokua anatafakari afanyeje.Mi nimeshaoa lakini huyu ni binti wa kumuongeza kwenye ukoo wowote,hongera angeja na kama umejua kwakua mameneja wa Tbl wanalalamikiwa sana kwa kuwarubuni warembo
 
Heri nusu shari kuliko shari kamili,mpaka hapo umejitahidi dada wa watu.
 
Mie nahisi karudisha wa sababu zingine,

ila kama ni hiyo inaweza kuwa sawa,mara nygi hawa watu wa Miss Tanzania wamekuwa wakiwatumia hao mamiss kwa huduma zao binafsi kama Viburudisho,

....
Kweli atakuwa na sababu nyingine ya kurudisha zaidi ya imani yake ya dini na pombe. But imani yake ya kidini inatosha!
 
naheshimu uamuzi wake lakiini, wakati anakwenda kugombea hakujua kwamba redds ni pombe na sio juice? Mwanza si alikwenda? au redds alifikiri ni kinywaji cha coca cola? kasoma wapi eti huyu dada, lafudhi yake imeniacha njia panda, kama hataki nataka kusema vile? all the best sis, next time fikiria kwanza umezibia wenzako sasa , wale happy go lucky
 
Dini ni bangi.....ndio.....

huyu mdada waakati akijiunga na mashindano ya kupita akiwa nusu uchi huku mapedejee wakimumchungulia toka chini hakujua kuwa imani yake hamruhusu?.....kutembea nusu uchi kunapelekea matamanio yanayoleta dhambi ya uzinifu......REDDS pombe sawa na kutembea nusu uchi je?......wewe mtoto hueleweki
 
Dini ni bangi.....ndio.....

huyu mdada waakati akijiunga na mashindano ya kupita akiwa nusu uchi huku mapedejee wakimumchungulia toka chini hakujua kuwa imani yake hamruhusu?.....kutembea nusu uchi kunapelekea matamanio yanayoleta dhambi ya uzinifu......REDDS pombe sawa na kutembea nusu uchi je?......wewe mtoto hueleweki

KUNA MCHUNGAJI MMOJA YUPO ITIGI- (UPM) huita WOKOVU NUSU GLASS AU "WOKOVU POA", "HALF-DOSE SALVATION", MAKANISA POA,....!
POMBE KIDOGO, DISKO KIDOGO, VIMINI KWA CHATI, GIRL FRIEND WA STORY ETC....!
MAFUNDISHO HAYA DHAIFU YA "MUNGU HAANGALII MAVAZI BALI MOYO WA MTU" NDO YANAYO LETA YOTE HAYA.!
NI SAWA NA MWIMBAJI MMOJA WA "ETI INJILI" ALISHIRIKI NA KUPOKEA TUZO YA "KILI MUSIC AWARD"
KUEPUKA MAMBO KAMA HAYA NDO MAANA NAWAFAGILIA WATUMISHI WASIOKARIBISHA UPUUZI KANISANI KAMA VILE KAKOBE, KIMARO (mwanza-mirongo) CHARLES MPANDE , WILLIAM YINDI
NA WENGINE WASIOKUBALI MICHANGANYO.
NA NIPO KINYUME NAO "WATUMISHI POA"
( WAPO WENGI ILI KUJAZA WATU..!
 
mi nafikiri hakuna wa kualaumiwa
maana mama na baba walkuwa kwenye shuguri,,na hao wachungaji wakati
ananyakua taji kabla ya hili walijua atalaumiwa nani jamani????????????

RED'S nanyie angalien vizuri uko kwenu labda kuna mtu ana gundu au kuna viongzi wenu wachafu wanawachafua watoto wa watu ndio maana wanakimbia!!1just for info nasikia kuna kijana anaitwa GEORGE KAVISHE
ANAUMWA HUUU UGONJWA WETU NA AMEKUWA AKITEMBEA NA WAREMBO TOFAUTI SANA ILA NINACHOSEMA UKIMWI HAUTAISHA KWA ATYLE HII
ONA

KILA MISS

LUNDEGA YULEYULE

KAVISHE NAEEEEEEEEEE YUPO

PREDESHE 3456 NAE YUPO

JACK PEMBA YUPO ULIZENI BAGAMOYO WALIVYOFANYIWA FUJO YA PESA HAO!!!!


WITO UKIONA NDUGU YAKO ANAINGIA HUKO MKANE KABISA NA UKOOwwW
 
Huyu binti hapa alikuwa anaongea bila wasi wasi wowote kuhusu kuwa muwakilishi wa REDDS. Inaelekea kapata shinikizo kutoka kwa wazazi wake, vinginevyo yeye inaelekea alikuwa hana matatizo yoyote ya kuwa muwakilishi wa REDDS. Click hiyo link hapo chini ili umsikie.

http://dailynews.habarileo.co.tz/st...ador2008AngelaLubalaTalksOnHerTitle.flv&id=46

Hapa binti wa Luballa anaimba I am your angel ulioimbwa na R. Kelly na Celine Dion
http://dailynews.habarileo.co.tz/streaming/?vid=ReddsAmbassador2008AngelaLubalaisAdivatoo.flv&id=43

[media]http://www.youtube.com/watch?v=hnjbJygpC0o[/media]
 
amakweli ya leo kali,,,hilo kanisa linakataza kuwakilisha Bia (Redds) bali linamkubalia kushiliki udhalilishwaji wa Lundega??????!!!!!!!!!! Najua hapa kijiweni (JF) kuna wachambuzi wazuri na nina waamini sana,,nasubiri pia kusikia mengi toka kwao maana hapa haiwezekani imani imruhusu kuvaa nguo ambazo ni sawa na kuwa mtupu mbele ya watu,,halafu imani hiyohiyo imkataze kuwa mwakilishi wa Redds ambayo ingemuwezesha kushiriki kazi nyingi za jamii na hivyo kulitangaza neno la mungu vyema....hapa tunahitaji jibu toka kwa muhuni lundega
 
huyu Binti Hapa Alikuwa Anaongea Bila Wasi Wasi Wowote Kuhusu Kuwa Muwakilishi Wa Redds. Inaelekea Kapata Shinikizo Kutoka Kwa Wazazi Wake, Vinginevyo Yeye Inaelekea alikuwa Hana Matatizo Yoyote Ya Kuwa Muwakilishi Wa Redds. Click Hiyo Link Hapo Chini Ili Umsikie.

http://dailynews.habarileo.co.tz/st...ador2008angelalubalatalksonhertitle.flv&id=46

Hapa Binti Wa Luballa Anaimba I Am Your Angel Ulioimbwa Na R. Kelly Na Celine Dion
http://dailynews.habarileo.co.tz/streaming/?vid=reddsambassador2008angelalubalaisadivatoo.flv&id=43

http://www.youtube.com/watch?v=hnjbjygpc0o

nimemsikia Mwenyewe Hapa......!
"anasema Yupo Proud Kuwa Miss Reds....!

Enyi Watumishi Nusu Glass...... Mnatupa Kazi Kumtetea Yesu Huku Mitaani......! Japo Nyie Mna Ma-taito Makubwa 'reverend, Aposto, Bishop, Mpakwa Mafuta , N.k.'
mnakuwaje Upande Wa Mungu Huku Mnampa Sapoti Adui.....?
tena Wazazi Ambao Ni Mchungaji Alikuwepo ....!
shame Upon Fake Gospels....!
 
Hii Inanikumbusha Miaka Ya Nyuma Pia Alitokea Mmoja Pale Assemblies Of God - Tabata (tag)
Jamani Mnavyomchafua Yesu Kwa Kuipenda Dunia Mnatutia Mashaka.....!
NDO MAANA WENGINE NAO WANAKUMBATIA MASHOGA...!
YAANI KANISANI KUWE NA "ANTI MUDDY, ANTI MABELLA, ANT MISH, ANT HASSAN ANTI ETC?"
MIMI NASEMA MTAWAPATA HAO HAO WANAOPENDA KUCHANGANYA CHANGAYA NA MTAWAPOTEZA WENGI....! LAKINI SASA NI MDA WA KUCHANGAMKA NA KUMTAZAMA YESU KWANI INJILI POTOFU ZINADHIHIRIKA WAZI...!
 
Back
Top Bottom