MIMI BABA YENU
JF-Expert Member
- Mar 1, 2019
- 295
- 679
Leo Februari 11, 2020 Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki amezungumza kuhusu video inayowaonesha vijana wa Kitanzania wanaosoma China wakiomba msaada wa kurejeshwa makwao.
Balozi ameeleza kuwa mpaka sasa hakuna Mtanzania hata mmoja aliyeambukizwa maradhi hayo kutokana na kufuata maelekezo wanayopata kutoka kwa mamlaka za China.
Amesema mara kwa mara huwasiliana na wanafunzi hao pamoja na serikali ya China ili kufahamu na kutatua changamoto ndogo zinazowakabili na ameishukuru serikali ya China kwa ushirikiano wanaotoa kwa vijana wa Kitanzania.
Balozi akasema dawa imegunduliwa na Idadi ya watu wanaopona imeongezeka huku Idadi ya maambukizi ikipungua kwa asilimia 50 nje ya mji wa Wuhan ambao ndio kitovu cha virusi hivyo hatari.
Balozi akasema kuwa kuishi kwa kufuata maelekezo ndilo jambo linalomfanya hata yeye kubaki hai. Amesema hawaruhusiwi hata kutoka nje na kwamba kitendo cha kukusanyika walichokifanya vijana hao ni hatari sana kwa afya zao.
Kuhusu ombi la vijana hao kurejeshwa Tanzania, Balozi Kairuki amesema hakuna usafiri wowote unaoruhusiwa kutoka ama kuingia kwenye mji wa Wuhan na kwamba Japan ilijaribu kuwaokoa vijana wake lakini kwa bahati mbaya wakaambukizwa na kuvibeba virusi hivyo mpaka nchini kwao.
Balozi akasema virusi hivyo ni hatari na kwamba serikali ya Tanzania haitafanya kitendo chochote kitakachokuja kuwadhuru Watanzania walio wengi.
Balozi huyo akasema kitendo walichokifanya vijana hao kimetokana na msongo wa mawazo unaotokana na kukaa ndani ya uzio wa makazi yao bila ruksa ya kutoka nje.
Balozi Kairuki akatoa wito kwa Watanzania kumuombea yeye na Watanzania wengine wanaoishi China ili Mwenyezi Mungu awavushe salama na kadhia hiyo. Pia amewaomba wazazi kuwapa faraja vijana wao waliopo China ili waondokane na msongo wa mawazo.
Nukta Muhimu: Tatizo lililopo China lisitumiwe kisiasa kwani serikali haiwezi kutumia nguvu kwenda kuwachukua vijana hao kwakua imejifunza kutokana na dosari zilizojitokeza wakati wa Serikali ya Japan ilipoamua kuwarudisha raia wake nchini mwao waliokuwa wanaishi China.
Sent using Jamii Forums mobile app
Balozi ameeleza kuwa mpaka sasa hakuna Mtanzania hata mmoja aliyeambukizwa maradhi hayo kutokana na kufuata maelekezo wanayopata kutoka kwa mamlaka za China.
Amesema mara kwa mara huwasiliana na wanafunzi hao pamoja na serikali ya China ili kufahamu na kutatua changamoto ndogo zinazowakabili na ameishukuru serikali ya China kwa ushirikiano wanaotoa kwa vijana wa Kitanzania.
Balozi akasema dawa imegunduliwa na Idadi ya watu wanaopona imeongezeka huku Idadi ya maambukizi ikipungua kwa asilimia 50 nje ya mji wa Wuhan ambao ndio kitovu cha virusi hivyo hatari.
Balozi akasema kuwa kuishi kwa kufuata maelekezo ndilo jambo linalomfanya hata yeye kubaki hai. Amesema hawaruhusiwi hata kutoka nje na kwamba kitendo cha kukusanyika walichokifanya vijana hao ni hatari sana kwa afya zao.
Kuhusu ombi la vijana hao kurejeshwa Tanzania, Balozi Kairuki amesema hakuna usafiri wowote unaoruhusiwa kutoka ama kuingia kwenye mji wa Wuhan na kwamba Japan ilijaribu kuwaokoa vijana wake lakini kwa bahati mbaya wakaambukizwa na kuvibeba virusi hivyo mpaka nchini kwao.
Balozi akasema virusi hivyo ni hatari na kwamba serikali ya Tanzania haitafanya kitendo chochote kitakachokuja kuwadhuru Watanzania walio wengi.
Balozi huyo akasema kitendo walichokifanya vijana hao kimetokana na msongo wa mawazo unaotokana na kukaa ndani ya uzio wa makazi yao bila ruksa ya kutoka nje.
Balozi Kairuki akatoa wito kwa Watanzania kumuombea yeye na Watanzania wengine wanaoishi China ili Mwenyezi Mungu awavushe salama na kadhia hiyo. Pia amewaomba wazazi kuwapa faraja vijana wao waliopo China ili waondokane na msongo wa mawazo.
Nukta Muhimu: Tatizo lililopo China lisitumiwe kisiasa kwani serikali haiwezi kutumia nguvu kwenda kuwachukua vijana hao kwakua imejifunza kutokana na dosari zilizojitokeza wakati wa Serikali ya Japan ilipoamua kuwarudisha raia wake nchini mwao waliokuwa wanaishi China.
Sent using Jamii Forums mobile app