mayenga
JF-Expert Member
- Sep 6, 2009
- 4,118
- 1,966
Ni takribani wiki mbili sasa mchakato WA kumpata mgombea ndani ya Chama tawala umemalizika.Katika michakato yote ambayo chama hiki imefanya,Ni wazi kuwa mchakato huu ulikuwa na changamoto kubwa kuliko yote.
Wanachama wakongwe na wenye heshima zao kabla hata mchakato kuisha,walijitokeza na kuonesha kwa jinsi ambavyo hawakuridhika na mwenendo WA mambo.Sophia Simba,Nchimbi,Kimbisa na wengineo,SI watu WA kubeza ndani ya chama,Ni watu ambao wana mchango uliotukuka ndani ya chama.
Hisia zao,ziliungwa mkono na wajumbe wa mkutano Mkuu ambao waliimba bila kujali kuwa mbele Yao Yuko Mwenyekiti na wazee wakongwe chamani.Kitendo,cha kumtaka mgombea ambaye hakuwa kwenye majina yale matano,ilikuwa Ni changamoto ya aina yake,kwa maneno yake mwenyewe Rais anakiri kuwa hakuwa kushuhudia.
Katika viunga vya mji wa Dodoma,hali haikuwa shwari.Makundi ya kila aina yalionesha hisia za wazi.Kila mmoja kwa nafasi yake alieleza kutoridhika na mchakato kwa namna tofauti.
Mzee mkongwe na mwanachama WA siku nyingi mwenye kadi namba 8na mwasisi WA chama,Mzee Kingunge,hakutaka kuvumilia.Aliwaita waandishi nyumbani kwake na bila kupepesa aliongea maneno mazito.Itakuwa Ni ukosefu wa fadhila kama anaweza kumbeza Mzee yule.Mzee huyu kama amesikilizwa vema,anachosema Ni procedural irregularities zilizojitikeza na wala hazungumzii kufaa na kutofaa kwa mgombea aliyepatikana.
Mzee huyu anasema kanuni ambazo ndo msingi wa mchakato zimevunjwa.Mpaka sasa hakuna majibu ya kuridhisha,badala yake Msekwa na Nape,wamekuwa na majibu mepesi mno.
Ni wazi kuwa kila aliyekuwa mgombea anafahamu kanuni,na bahati nzuri nyinyi wagombea waliokatwa mmekuwa wasimamizi WA kanuni hizo.Jaji Ramadhani umekuwa msimamizi WA haki,na sasa umeijongea altare ya bwana,Ni wazi kuwa ukiongea lipi lilitokea,ukweli utakuweka huru.
Wassira,wewe ndo umeandaa ilani ya chama,chama umekitetea kwa Kila hali katika dhoruba na machafuko yaliyo kikumba,jitokeze PIA utuambie Ni kipi kilikupata mpaka ukakatwa na kushindwa kukurupuka.
Bilal na Pinda nyie Ni watu muhimu katika taifa itakuwa Ni aibu kuzidi kuwawajibisha watendaji ndani ya serikali,kama mlishindwa kusimamia kanuni ambazo ziliwaengua na hata msijulikane kama mliingia kumi bora,ishirini bora au thelathini bora.
Mzee wangu Kitine wewe Ni mkurugezi WA usalama mstaafu,Balozi Maiga uadilifu Wako hautiliwi shaka.Sasa Ni kipi kiliwapata.
Jitokezeni mtuambie.
Wanachama wakongwe na wenye heshima zao kabla hata mchakato kuisha,walijitokeza na kuonesha kwa jinsi ambavyo hawakuridhika na mwenendo WA mambo.Sophia Simba,Nchimbi,Kimbisa na wengineo,SI watu WA kubeza ndani ya chama,Ni watu ambao wana mchango uliotukuka ndani ya chama.
Hisia zao,ziliungwa mkono na wajumbe wa mkutano Mkuu ambao waliimba bila kujali kuwa mbele Yao Yuko Mwenyekiti na wazee wakongwe chamani.Kitendo,cha kumtaka mgombea ambaye hakuwa kwenye majina yale matano,ilikuwa Ni changamoto ya aina yake,kwa maneno yake mwenyewe Rais anakiri kuwa hakuwa kushuhudia.
Katika viunga vya mji wa Dodoma,hali haikuwa shwari.Makundi ya kila aina yalionesha hisia za wazi.Kila mmoja kwa nafasi yake alieleza kutoridhika na mchakato kwa namna tofauti.
Mzee mkongwe na mwanachama WA siku nyingi mwenye kadi namba 8na mwasisi WA chama,Mzee Kingunge,hakutaka kuvumilia.Aliwaita waandishi nyumbani kwake na bila kupepesa aliongea maneno mazito.Itakuwa Ni ukosefu wa fadhila kama anaweza kumbeza Mzee yule.Mzee huyu kama amesikilizwa vema,anachosema Ni procedural irregularities zilizojitikeza na wala hazungumzii kufaa na kutofaa kwa mgombea aliyepatikana.
Mzee huyu anasema kanuni ambazo ndo msingi wa mchakato zimevunjwa.Mpaka sasa hakuna majibu ya kuridhisha,badala yake Msekwa na Nape,wamekuwa na majibu mepesi mno.
Ni wazi kuwa kila aliyekuwa mgombea anafahamu kanuni,na bahati nzuri nyinyi wagombea waliokatwa mmekuwa wasimamizi WA kanuni hizo.Jaji Ramadhani umekuwa msimamizi WA haki,na sasa umeijongea altare ya bwana,Ni wazi kuwa ukiongea lipi lilitokea,ukweli utakuweka huru.
Wassira,wewe ndo umeandaa ilani ya chama,chama umekitetea kwa Kila hali katika dhoruba na machafuko yaliyo kikumba,jitokeze PIA utuambie Ni kipi kilikupata mpaka ukakatwa na kushindwa kukurupuka.
Bilal na Pinda nyie Ni watu muhimu katika taifa itakuwa Ni aibu kuzidi kuwawajibisha watendaji ndani ya serikali,kama mlishindwa kusimamia kanuni ambazo ziliwaengua na hata msijulikane kama mliingia kumi bora,ishirini bora au thelathini bora.
Mzee wangu Kitine wewe Ni mkurugezi WA usalama mstaafu,Balozi Maiga uadilifu Wako hautiliwi shaka.Sasa Ni kipi kiliwapata.
Jitokezeni mtuambie.