Sitachoka
JF-Expert Member
- Nov 17, 2011
- 3,027
- 1,299
Sijapendezwa hata Kidogo kwa Kagasheki Kujiuzulu, Makosa ni kweli yalifanyika kwenye Oparation hii lakini amini nakwambia waliofanya makosa ni kina Emanuel Nchimbi,pamoja na Vuai Nahodha.
Kwanini natafakari kwa huyu mzee Kagasheki,kwanza amejitahidi kupambana na Majangili kwa nguvu zote mpaka kufikia kuomba msaada kwa Rais amsaidie,maana majangili wana mtandao mpana.
Najaribu kufikiria kwamba majangili inasemekana ni makada kutoka chama chake (Ccm) Je, kwa njia hizo uoni kwamba Kagasheki ameingizwa tu kwenye hatia apate kibano atolewe?
Majangili yalikuwa yamebanwa kiasi fulani,Kagasheki alijitahidi mno kupambana na Majangili,hivyo majangili yalikuwa yanatumia mpaka Wabunge wampinge Kagasheki,Jamani mtandao wa Ujangili una mikono mipana sana na mirefu.
Je kuondoka kwa Kagasheki mustakabali wa pembe za ndovu itakuaje?
Msimamo wangu Kagasheki amepatwa na bahati mbaya ya kisiasa,lakini waliotakiwa waondoke ni kina Mzengo Pinda,Nchimbi, Vuai, Chikawe, Mkuchika, ambao Wizara zao ndiyo zenye kuhusika na matukio makubwa sana ambao wananyooshewa kidole na Wananchi,' kama kung'olewa macho Kibanda,Kuuwawa Mwangosi,Kung'olewa kucha Ulimboka,na mateso ya kila aina ya raia,pamoja na mabomu kupigwa wana Chadema kwenye mikutano yao,na waziri akiendelea kufyatua tumbo tu kama wanaokufa ni Dagaa.
Huyu Nchimbi alishapoteza uhalali wa kuwa waziri, Sasa kama Oparation ya maliasili,hawa wanajeshi waliingiaje kutoa vichapo?
Nakubali kabisa kuliandaliwa mazingira ya Kuhujumu zoezi Jema la kupambana na Majangili na kuishia kupambana na Wafugaji.Mungu ttusaidie kwa hili, Hongera Kagasheki,nitaendelea kukupa heshima yangu kwako,wewe ni Shujaa.
Kwanini natafakari kwa huyu mzee Kagasheki,kwanza amejitahidi kupambana na Majangili kwa nguvu zote mpaka kufikia kuomba msaada kwa Rais amsaidie,maana majangili wana mtandao mpana.
Najaribu kufikiria kwamba majangili inasemekana ni makada kutoka chama chake (Ccm) Je, kwa njia hizo uoni kwamba Kagasheki ameingizwa tu kwenye hatia apate kibano atolewe?
Majangili yalikuwa yamebanwa kiasi fulani,Kagasheki alijitahidi mno kupambana na Majangili,hivyo majangili yalikuwa yanatumia mpaka Wabunge wampinge Kagasheki,Jamani mtandao wa Ujangili una mikono mipana sana na mirefu.
Je kuondoka kwa Kagasheki mustakabali wa pembe za ndovu itakuaje?
Msimamo wangu Kagasheki amepatwa na bahati mbaya ya kisiasa,lakini waliotakiwa waondoke ni kina Mzengo Pinda,Nchimbi, Vuai, Chikawe, Mkuchika, ambao Wizara zao ndiyo zenye kuhusika na matukio makubwa sana ambao wananyooshewa kidole na Wananchi,' kama kung'olewa macho Kibanda,Kuuwawa Mwangosi,Kung'olewa kucha Ulimboka,na mateso ya kila aina ya raia,pamoja na mabomu kupigwa wana Chadema kwenye mikutano yao,na waziri akiendelea kufyatua tumbo tu kama wanaokufa ni Dagaa.
Huyu Nchimbi alishapoteza uhalali wa kuwa waziri, Sasa kama Oparation ya maliasili,hawa wanajeshi waliingiaje kutoa vichapo?
Nakubali kabisa kuliandaliwa mazingira ya Kuhujumu zoezi Jema la kupambana na Majangili na kuishia kupambana na Wafugaji.Mungu ttusaidie kwa hili, Hongera Kagasheki,nitaendelea kukupa heshima yangu kwako,wewe ni Shujaa.