Balozi huyu ni Mbaguzi?

Game Theory

Platinum Member
Sep 5, 2006
8,545
835
Je wana CHADEMA au CUF watakapo muita kwenye mikutano yao atakuja au?

Keshaitwa kuhudhuria mikutano ya jumuiya mbili za watanzania akajidai yuko bize lakini jumuiya ya abuu faraji anakwenda na CCM ndio zaidi


Mumewe ilibidi agombane na watu ndipo akaamua kuachia ngazi kutaka huo uenyekiti sasa jamani mambo haya yanakubalika?

Najisikia mnyonge sana nionapo mabalozi wetu wanapoingia kwenye ushabiki wa kiasiasa


Je sheria inasemaje?


sherehe za kuzaliwa ccm reading



107.jpg

Mgeni wa Heshima Balozi wa Tanzania Bi. Mwanaidi Maajar akiwa na Bw. Maajar na Katibu wa CCM Tawi la London Bi Suzan Mzee.

155.jpg

Mdau Wa TanzananiaOne Uk Ally Muhdin akiwa na Balozi Bi Maajar

150.jpg

Wadau wa Southhampton wakiwa na Mgeni wao Toka Bongo

145.jpg

Wadau wa Tanzania association kutoka kushoto Juma Pinto , Abuu Faraji na John Lusingu
 
Huyu Mama mimi namjua kama ni Chadema damu na U CCM ni baada ya kuchukua Ubalozi.Sasa mengine siyajui.
 
Mkuu Lunyungu heshima mbele!

Sasa ndugu mbona unamwaga the dataz hapa...unataka mama awe jobless ghafla kama kijana wa Ngoyai? mzee mkuu wa kaya akitonywa mama akapoteza kitumbua...utalaumiwa weye..mi simo!

Brazamen..mbona weekend bado bana.....au utaratibu umebadilika...
 
Mkuu Lunyungu heshima mbele!

Sasa ndugu mbona unamwaga the dataz hapa...unataka mama awe jobless ghafla kama kijana wa Ngoyai? mzee mkuu wa kaya akitonywa mama akapoteza kitumbua...utalaumiwa weye..mi simo!

Brazamen..mbona weekend bado bana.....au utaratibu umebadilika...


Unajua naangalia hizi picha napata wazo kwamba wengi wao hawajaja Tanzania miaka mingi sana .So hata siasa kwao si Siasa walienda kupoteza muda na kupata habari za wachache wao ambao wanakuja nyumbani kila mara .Wengi wamezamia na hawawezi tena kuja TZ maana hawana PP zao na wamejiita wakimbizi.Wengine akina Faraji na Minto wao wana mission ya kuyatafuta maisha so wanatumia kila njia kuweza kula na mafisadi kwa jina la CCM chama ambacho kina mafisadi wajuzi .

Huyu kumwaga Unga hapana .Mkuu wa Kaya anajua kwamba huyu ni Mdhamini wa Chadema lakini ngeke likamwangukia na akapewa Ubalozini Mkulu ana sababu zake .Mimi wananichekesha hawa wabongo wa UK na kimbembe cha Uccm .Ni wa kweli hawa ?
 
Wanasema "Shamba la Bwana Kheri, na Mbuzi wa Bwana Kheri!" hivyo waache wafanye watakavyo..........
 
Wanasema "Shamba la Bwana Kheri, na Mbuzi wa Bwana Kheri!" hivyo waache wafanye watakavyo..........

Huhuhuu Masatu bwana sawa mkuu .

Hivi Samvulachole ni wapi walipo kupanhusa mikono kwenye uongozi wa akina Faraji ama ujumbe wa CCM UK ? Maana hii ngoma unaijua vyema njoo ubaelezee
 
Ukarabati unahitajika sana katika Balozi za Tanzania kwani wamekuwa watu ambao Mtanzania hawezi kuwafika kiurahisi labda wasikie unawapelekea mchango ,hapo ndio utawaona wakijichekesha chekesha kuna ufisadi wa fedha za Passport hadi hii leo kuna waTanzania wanakwenda mbio hawajazipata wanapewa matarehe tu kama ya mikakati ambayo utekelezaji wake ni baada ya miaka mia ndio mradi utatimia ,wakati tuliopo sasa tunakufwa na njaa.
Utapeleka picha watakwambia sio ,nenda kapige sehemu fulani ulete na risiti kama umepiga hapo ,na baada ya hapo unaambiwa subiri utapigiwa simu basi ndio imetoka hiyo ,mpaka upande presha na kuwafuatilia ,hapo utasikia zimeshapelekwa Tanzania zikifika tu utakuwa mtu wa kwanza kupigiwa simu na ukiamua kwenda Tanzania utaipata na kurudi wakati ile uliyoomba pale ubalozini zaidi ya miezi sita haijafika ajabu wanaweza wakakupigia simu ukachukue pasi yako kwani imeshakuwa tayari na imeshafika ,utashangaa unakuwa na passport mbili !!!
 
Ukarabati unahitajika sana katika Balozi za Tanzania kwani wamekuwa watu ambao Mtanzania hawezi kuwafika kiurahisi labda wasikie unawapelekea mchango ,hapo ndio utawaona wakijichekesha chekesha kuna ufisadi wa fedha za Passport hadi hii leo kuna waTanzania wanakwenda mbio hawajazipata wanapewa matarehe tu kama ya mikakati ambayo utekelezaji wake ni baada ya miaka mia ndio mradi utatimia ,wakati tuliopo sasa tunakufwa na njaa.
Utapeleka picha watakwambia sio ,nenda kapige sehemu fulani ulete na risiti kama umepiga hapo ,na baada ya hapo unaambiwa subiri utapigiwa simu basi ndio imetoka hiyo ,mpaka upande presha na kuwafuatilia ,hapo utasikia zimeshapelekwa Tanzania zikifika tu utakuwa mtu wa kwanza kupigiwa simu na ukiamua kwenda Tanzania utaipata na kurudi wakati ile uliyoomba pale ubalozini zaidi ya miezi sita haijafika ajabu wanaweza wakakupigia simu ukachukue pasi yako kwani imeshakuwa tayari na imeshafika ,utashangaa unakuwa na passport mbili !!!


Mwiba sasa umezinduka na unaongea kama mwiba kweli .Nilijua tu kwamba JF is a free University for Free Education . Unaanza kukomaa sasa .Karibu tuendelee
 
Wadau angalieni Msije Mtisha Mama wa Watu akaogopa hata Kuhudhuria Misa za Wafu. JF si-mchezo!!

Hapana yeye aende tu ila ajue kwamba tunamjua vilivyo na anapaswa kutumia Nchi na si Chama . Kama ni Chama baso iwe vyama maana ni balozi wa Watanzania .Akichukua side we know much and better .Faraji mchaga mwenzio anampa tenda zote za Ubalozini pesa zinaliwa hapo tuna mwangalia tu .Si matisho ajue tunaweza record.
 
Sula la BALOZI MWANAIDI MAJAAR kuwa mdhamini wa CHADEMA ni kweli na halina utata na nadhani wenyewe walipomchagua walilijua hili

Tatizo ni pale anapo anza kuwa Biased katisha shughuli za watanzania

Keshaitwa kwenye shughuli mbili za jumuiya mbili zinazowawakilisha Watanzania lakini kagoma kwenda kwa kisingizio cha ubize

cha ajabu muda wa jumuiya ya Faraji anao

Muda wa kwenda kwenye shughuli za CCM anao

Je wasio CCM tutajisikiaje?

Je hii ni directive toka FOREIGN au ni presha toka kwa Mumewe?

Je kama mama Majaar ni innocent je anashindwa nini kumwambia mumewe kuwa mambo yake ya CCM yatakuwa na conflict of interest?

Mwisho zaidi ni kuwa kwa sababu mwaka huu watu wameamua kuwavalianjuga hawa watawalawetu hamuoni kama mambo kama haya ni dalili za ma balozi kama Majaar kuwa katika hatari ya kuwa wabaguzi zaidi watakapo pewa nafasi kubwa zaidi za kisiasa?
 
Sula la BALOZI MWANAIDI MAJAAR kuwa mdhamini wa CHADEMA ni kweli na halina utata na nadhani wenyewe walipomchagua walilijua hili

Tatizo ni pale anapo anza kuwa Biased katika shughuli za watanzania....Keshaitwa kwenye shughuli mbili za jumuiya mbili...

Brazameni,Nakusikia usemacho Mkuu.Lakini hizo Jumuiya, hasa hizo MBILI unazozitaja hapo juu,je Ni jumuiya Rasmi?Zimeundwa chini ya Misingi gani?(Za-kidini,Kikabila,Kijinsia,kimajimbo,Kifamiliya???).Unaweza kututajia hizo jumuiya Mkuu?(Kwa manufaa ya Wa-Tz waishiyo UK)

Kwasababu wasiwasi wangu ni kwamba kama kila mtu atataka eti Balozi ahudhuriye Vipaimara,Ndoa,Mahafali,Ujio wa Ze Comedy,basi itakuwa vigumu sana,na akitoa udhuru wa kutoweza jumuika nasi,tusimlaumu jamani,tumuelewe!!.
 
Back
Top Bottom