Balozi dr. Deodatus Kamala: Nitagombea tena ubunge 2015

Riziki Magembe

JF-Expert Member
Apr 5, 2014
886
206
Ameyasema hayo katika kipindi cha dk 45 ITV kuwa mwaka 2015 atachukua fomu kugombea ubunge katika jimbo lake aliloangushwa mwaka 2010,atarudi tena licha kwamba wananchi walimkataa mwaka 2010 lakini sasa wanampenda maana amekua muhimu kwao.
 
...madaraka ni kama kula nyama ya binadamu,ukiionja lazima utairudia...Nafikiri tuwaachie na wengine nao watoe huduma kwa jamii,uongozi jamii ni utumishi,arudi tu Mzumbe akafundishe,tena huko chuoni ndio mchango wako utakuwa wa kitaifa zaidi
 
hivi kamala alikuwa jimbo gani?

Balozi Dr Kamala alikuwa mbunge wa Nkenge wilaya mpya ya Misenye. Mimi kama mwananchi wa mkoa wa Kagera aishie nje ya mkoa huu nasikitisha kwa wananchi wa jimbo hili kutomchagua Balozi Dr Kamala na kumchagua huyu Mhe. Asumpta. Wananchi wa jimbo la Nkenge walifanya kosa kubwa sana kumchagua huyu mama mpayukaji na mwenye siasa za kibaguzi. Binafsi tunasubiri kwa hamu mwaka 2015 Nkenge ipate mbunge mpya.
 
Balozi Dr Kamala alikuwa mbunge wa Nkenge wilaya mpya ya Misenye. Mimi kama mwananchi wa mkoa wa Kagera aishie nje ya mkoa huu nasikitisha kwa wananchi wa jimbo hili kutomchagua Balozi Dr Kamala na kumchagua huyu Mhe. Asumpta. Wananchi wa jimbo la Nkenge walifanya kosa kubwa sana kumchagua huyu mama mpayukaji na mwenye siasa za kibaguzi. Binafsi tunasubiri kwa hamu mwaka 2015 Nkenge ipate mbunge mpya.

shukrani kwa taarifa kiongozi
 
Back
Top Bottom