Ifuatayo ni taarifa ya kutoka Ubalozini kwa Watanzania waishio Canada..........................................
Kwa niaba ya Mheshimiwa Balozi Peter Kallaghe, naomba kuchukua fursa
hii kuwajulisha kuwa Mheshimiwa Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje
na Ushirikiano wa Kimataifa anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi nchini
Canada kuanzia tarehe 11 Januari hadi 15 Januari, 2010.
Akiwa Ottawa Mhe. Waziri Membe atapenda kukutana na Watanzania walioko Canada. Ubalozi unafanya utaratibu wa kupata ukumbi kwa ajili ya
mkutano huo ambao utafanyika siku ya tarehe 12, Januari, 2010 jioni
saa Kumi na Mbili na Nusu hadi saa Tatu na Nusu usiku (6:30Pm-9:30Pm).
Tutawajulisha sehemu ya mkutano na anuwani ya shughuli hiyo kabla ya
mwisho wa juma hili hivyo tunaomba muweke shughuli hii katika ratiba
zenu.
Aidha, tunaomba kila atayepata ujumbe huu atusaidie kumjulisha/kuwajulisha Watanzania wenzetu ambao hatukuweza kuwatumia
barua pepe hii kutokana na kutokuwa na anuwani zao.
Kama mnavyojua shughuli ni watu na watu ndiyo sisi sote hivyo tunaomba
tujitokeze kwa wingi kuja kukutana na Mhe. Waziri Membe ambaye kama
wengi mnavyokumbuka aliishi hapa Ottawa wakati akifanya kazi kwenye
Ubalozi wetu huu.
Tunawashukuru kwa ushirikiano wenu,
Kny Balozi
Kwa niaba ya Mheshimiwa Balozi Peter Kallaghe, naomba kuchukua fursa
hii kuwajulisha kuwa Mheshimiwa Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje
na Ushirikiano wa Kimataifa anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi nchini
Canada kuanzia tarehe 11 Januari hadi 15 Januari, 2010.
Akiwa Ottawa Mhe. Waziri Membe atapenda kukutana na Watanzania walioko Canada. Ubalozi unafanya utaratibu wa kupata ukumbi kwa ajili ya
mkutano huo ambao utafanyika siku ya tarehe 12, Januari, 2010 jioni
saa Kumi na Mbili na Nusu hadi saa Tatu na Nusu usiku (6:30Pm-9:30Pm).
Tutawajulisha sehemu ya mkutano na anuwani ya shughuli hiyo kabla ya
mwisho wa juma hili hivyo tunaomba muweke shughuli hii katika ratiba
zenu.
Aidha, tunaomba kila atayepata ujumbe huu atusaidie kumjulisha/kuwajulisha Watanzania wenzetu ambao hatukuweza kuwatumia
barua pepe hii kutokana na kutokuwa na anuwani zao.
Kama mnavyojua shughuli ni watu na watu ndiyo sisi sote hivyo tunaomba
tujitokeze kwa wingi kuja kukutana na Mhe. Waziri Membe ambaye kama
wengi mnavyokumbuka aliishi hapa Ottawa wakati akifanya kazi kwenye
Ubalozi wetu huu.
Tunawashukuru kwa ushirikiano wenu,
Kny Balozi