Ballali aitikisa serikali

Mtanzania

JF-Expert Member
May 4, 2006
4,816
678
Ballali aitikisa serikali
(Tanzania Daima)
na Charles Mullinda na Kulwa Karedia

KUNA kila dalili kwamba, mwenendo wa mambo serikalini si mzuri baada ya aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dk. Daudi Ballali, kueleza nia yake ya kutaka kurejea nyumbani kukabiliana na tuhuma zinazomkabili na kuwaweka bayana wahusika wakuu wa sakata hilo.

Nia hiyo ya Dk. Ballali ya kutaka kuwaanika wahusika wakuu wa uchotaji fedha katika akaunti ya ulipaji madeni ya nje (EPA), ndiyo inayowaumiza vichwa viongozi wa juu serikali na waliokuwa madarakani wakati wa utawala wa awamu ya tatu.

Habari za hivi karibuni zilizolifikia Tanzania Daima Jumapili, zinaeleza kuwa, wafanyabiashara, baadhi ya viongozi wa juu serikalini na wale waliostaafu, kwa siku kadhaa sasa wamekuwa wakihaha kuhakikisha kuwa Dk. Ballali harejei nchini.

Kwamba, mikakati ya viongozi hao ni pamoja na kuhakikisha kuwa hata kama Dk. Ballali akirejea, hafanikiwi kivifikia vyombo vya habari au vile vya sheria kwa sababu, hatua hiyo inaweza kuibua kashfa kubwa kwa serikali.

Habari hizo zinaeleza kuwa, Dk. Ballali ambaye siku chache zilizopita alikuwa akijiandaa kurejea nyumbani, alipanga mara tu baada ya kuwasili, angekutana na waandishi wa habari kuwaeleza kile anachokijua kuhusu kashfa ya uchotaji fedha za EPA kwa kuonyesha ushahidi wa vielelezo.

Habari hizo zilieleza zaidi kwamba, Dk. Ballali ambaye kwa siku kadhaa tangu uteuzi wa wadhifa wake wa ugavana ulipotenguliwa akihusishwa na kashfa hiyo, alianza kuwasiliana na wanasheria maarufu nchini ili kupata msaada wa kisheria wa kupambana na tuhuma zinazomkabili.

Alipanga kwenda mahakamani akiwa na vielelezo hivyo vya maandishi, vinavyoonyesha jinsi waliokuwa wakubwa wake kikazi walivyokuwa wakimuagiza kulipa mabilioni ya fedha kwa kampuni zilizotajwa kuhusika na ufisadi wa BoT.

Inaelezwa kuwa, mikakati hiyo ya Dk. Ballali iliwashtua wakubwa ambao walianza kupanga ajenda za kuhahakisha kuwa harejei nchini.

Hilo linathibitishwa na taarifa zilizolifikia gazeti hili mwanzoni mwa wiki hii, zilizodai kuwa uraia wa Dk. Ballali una utata, hivyo anaweza asirejee nchini kwa sababu si raia wa Tanzania.

Taarifa hizo zilidai zaidi kwamba, Dk. Ballali aliukana uraia wa Tanzania na kuchukua uraia wa Marekani wakati akifanya kazi katika moja ya mashirika makubwa ya kimataifa nchini humo.

Kwamba, hata hatua ya Marekani kutengua visa yake, haimfanyi Dk. Ballali kuwa na ulazima wa kurejea nchini kwa sababu ana uraia wa nchi nyingine.

Gazeti hili liliwasiliana na Waziri wa Fedha kupitia simu yake ya kiganjani Jumatano wiki hii kuomba miadi ya kukutana naye kwa ajili ya kupata ufafanuzi wa madai hayo.

Waziri Meghji alieleza kuwa muda wake kwa siku zilizobakia kabla ya kwenda bungeni anautumia kwa ajili ya vikao, lakini aliahidi kuwasiliana na gazeti hili siku iliyoafuata (Alhamis), ili kutoa ufafanuzi wa madai haya kutokana na unyeti wake.

Katika hali ya kushangaza, Waziri Meghji hakutekeleza ahadi yake siku hiyo na alipotafutwa siku hiyo jioni, alitoa ahadi nyingine ya kutafuta muda wa kuzungumza na gazeti hili siku ya Ijumaa, jambo ambalo hakulitekeleza pia.

Tanzania Daima liliendelea kumtafuta Waziri Meghji Ijumaa jioni, lakini simu yake ya kiganjani ilikuwa ikiita bila majibu kama ilivyokuwa Jumamosi kwa simu yake kuita bila kupokelewa pia.

Hata hivyo, Alhamisi wiki hii, gazeti hili lilimkariri Waziri Meghji alipokuwa akizungumza na baadhi ya waandishi wa habari katika viwanja vya Ofisi Ndogo ya Bunge, Dar es Salaam kuwa hatazungumza tena kuhusu sakata hilo la ufisadi kwa sababu sasa limefika katika ngazi nyingine.

Baadhi ya wadadisi waliokuwa eneo hilo walieleza kuwa, Waziri Meghji amelazimishwa kukaa kimya ili kuondoa mkanganyiko wa kauli kutoka kwa viongozi wakuu serikali.

Mmoja wa watumishi wa taasisi ya fedha aliyekuwa eneo hilo alisema, sababu nyingine inayomfunga mdomo Meghji, ni kuibuka kwa tetesi kuwa makandarasi wadogo waliopewa tenda ya kujenga minara miwili ya BoT, hawakuwa na sifa stahiki.

“Mambo yameingiliana, mama (Meghji) lazima akatae kuzungumza, huku kuna ufisadi huku kunaibuka ubora na uimara wa jengo, kuna makarandasi wadogo hapa ambao walipewa tenda kinyemela, hawakuwa na sifa za kujenga, hawa wakifuatiliwa, yanaweza kuibuka mapya,” alisema mtumishi huyo ambaye jina lake tunalo.

Gazeti hili pia lilijaribu kumtafuta Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe kupitia simu yake ya kiganjani ili kuzungumzia uraia wa Dk. Ballali na mahali alipo sasa baada ya visa yake kutenguliwa nchini Marekani bila mafanikio, simu yake ilikuwa haipatikani.

Wakati hali ikiwa hivyo serikali, kwa upande wa wanasiasa kadhaa walioongea na gazeti hili walieleza kushangazwa kwao na ukimya wa serikali kuhusu Rais wa Awamu ya Nne, Benjamin Mkapa ambaye kambi ya upinzani imekuwa ikimtuhumu siku nyingi kuwa alikiuka miiko ya uongozi kwa kufanya biashara Ikulu.

Kiongozi mmoja wa kambi hiyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alisema kuwa Rais Kikwete asifikiri vita ya ufisadi iliyoanzishwa na kambi ya upinzani imekwisha baada ya kumuondoa Dk. Ballali katika wadhifa wa ugavana.

Alisema, kambi ya upinzani inafahamu kuwa Dk. Ballali ametolewa kafara ili kunusuru viongozi wa juu waliopo katika safu ya ungozi wa sasa serikali na wale walio nje waliohusika katika kashfa ya uchotaji wa fedha hizo.

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibroad Slaa ambaye alizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, alisisitiza kuwa Rais Mkapa anapaswa kukamatwa na kufunguliwa mashitaka kwa kosa la kutumia rasilimali za nchi vibaya.

“Mimi niko wazi katika hili, Mkapa si kwamba ajitokeze, bali anapaswa kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa kosa hilo. Ni jambo lisilovumiliwa, kuona kiongozi wa nchi anachukua asilimia 85 ya rasilimali za taifa na kulibakizia taifa asilimia 15.

“Nasisitiza, Mkapa si wa kuombwa ajitokeza kusema chochote, anapaswa kukamatwa, Rais Kikwete amkamate Mkapa… ni mhalifu, alikiuka maadili ya uongozi akiwa Ikulu, ni kama Chiluba tu.

“Rais Kikwete anapaswa atuambie kama Mkapa alivunja sheria au hakuvunja sheria kwa kufanya biashara akiwa Ikulu, tena si Mkapa tu, bali yeye na waziri wake, walijichukulia mradi mkubwa tu wa serikali bila ya kufuata taratibu au kushinda tenda yoyote, nasisitiza jamani huu ni uhalifu,” alisema Dk. Slaa kwa kusisitiza.

Mkapa amekuwa akituhumiwa kwa muda mrefu kuwa alitumia vibaya madaraka yake katika kipindi cha miaka kumi alichokaa madarakani.

Viongozi kadhaa wa upinzani wamekuwa wakidai kuwa akiwa madarakani, aliitumia kofia ya urais kujitajirisha yeye binafsi, familia na marafiki zake.

Kwa uchache, mali zinazodaiwa kuwa alichuma akiwa Ikulu ni pamoja na kuanzisha kampuni yake ya biashara, ANBEM, ambayo mkewe ni mshirika wake kibiashara.

Pia, anadaiwa kusajili kampuni binafsi, yeye na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona, iitwayo Tanpower Resources Company, ambayo aliisimamia kununua asilimia 85 ya uliokuwa mradi wa makaa ya mawe wa Kiwira, mkoani Mbeya.

Kwamba, aliutumia wadhifa wake wa urais kuhakikisha kampuni yake hiyo inaingia mkataba wa kuizuia Tanesco megawati 200 za umeme katika gridi ya taifa, kampuni ambayo mkewe na mtoto wake ni wakurugenzi.

Mbali na wapinzani, Mkapa pia aliwahi kutuhumiwa na mmoja wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) anayeheshimika hapa nchini, Joseph Butiku kuwa alipageuza Ikulu kuwa mahali pa kufanyia biashara.

Katika hatua nyingie, Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, amesema sheria ya vyama vya siasa iliyopo sasa, ina upungufu mkubwa unaomnyima nguvu za kisheria za kubana matumizi ya fedha zenye shaka za vyama vya siasa.

Tendwa aliyasema hayo juzi, ofisini kwake alipozungumza na gazeti hili kuhusu matumizi makubwa ya fedha ya vyama vya siasa wakati wa kampeni za uchanguzi na madai ya baadhi ya vyama kumegewa fedha zilizochotwa EPA na kuzitumia katika kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.

Alisema, vyama vyote vilivyoshiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, vimekwishawasilisha ripoti zake za fedha, lakini hana mamlaka ya kisheria ya kuhoji ripoti hizo, isipokuwa kuzipokea na kuzitunza ofisini kwake.

“Vyama vyote vilivyoshiriki uchaguzi mkuu mwaka 2005 vimeshawasilisha ripoti zao za fedha, ripoti hizo ninazo, lakini sheria inasema chama kinaweza kupata fedha toka kwa wafadhili wa ndani au nje na ni lazima vitoe taarifa ya fedha kwa msajili wa vyama vya siasa.

“Lakini mpaka sasa sina taarifa hizo, kama walipata fedha za misaada kutoka kwa wafadhili toka chama chochote, sheria nayo iko kimya haisemi mimi kama msajili iwapo nawajibika kufanya uchunguzi wa mapato yoyote ya chama ambayo si ruzuku ya serikali.

“Ndio maana nimekwishapeleka mapendekezo serikalini ili sheria hizi zifanyiwe marekebisho, kwa kweli zina kasoro, na marekebisho haya ya sheria niliyopeleka, ndio yamepitishwa katika nchi za Zambia na Msumbuji, wanalichukua toka hapa kwangu, wamerekebisha kidogo tu, mimi nimepeleka tangu mwaka 1995, lakini hayajapitishwa,” alisema Tendwa.

Hata hivyo alisema, kama kuna mtu ana ushahidi wa tetesi zilizopo sasa kuhusu baadhi ya vyama kupatiwa fedha zilizoibwa kutoka EPA, ampelekee na yeye atawaita wahusika na kuwaomba taarifa zao za fedha, lakini alirejea kauli kwamba akishapatiwa taarifa hizo, hana uwezo wa kuchukua hatua yoyote wala kuchunguza.

Alisema, shaka waliyonayo wananchi wengi inatokana na utata wa maelezo yanayotolewa na viongozi wa serikali kuwa fedha zilizochotwa kutoka EPA na kupewa Kampuni ya Kagoda Agriculture zilikuwa maalumu kwa kazi za usalama wa taifa.

“…Kagoda Agriculture Company na masuala nyeti ya usalama wa taifa wapi na wapi? Agriculture na ulinzi na usalama vina uhusiano gani? Inatia shaka kwa kweli, jina la kampuni na sababu zilizotolewa haviendani kabisa,” alisema Tendwa kwa mshangao mkubwa.

Tangu Rais Kikwete atengue uteuzi wa Dk. Ballali kama Gavana wa BoT kwa tuhuma za kuhusika na upotevu wa sh bilioni 133 za EPA, kumekuwa kukitolewa kauli za kumtaka achukue hatua zaidi dhidi ya walioshirikiana na Dk. Ballali katika ubadhirifu huo.

Kauli nyingi zinazotolewa sasa zimekuwa zikiwalenga baadhi ya viongozi wakuu waliokuwa madarakani wakati wa upotevu wa fedha hizo, akiwemo Rais mstaafu Mkapa ambaye kwa mara kadhaa ameshutumiwa na watu mbalimbali wakiwemo wana CCM kuwa, alitumia vibaya madaraka ya urais, hivyo kumtaka Rais Kikwete kuchukua hatua zaidi.
 
Mkapa si kwamba ajitokeze, bali anapaswa kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa kosa hilo. Ni jambo lisilovumiliwa, kuona kiongozi wa nchi anachukua asilimia 85 ya rasilimali za taifa na kulibakizia taifa asilimia 15. Mkapa si wa kuombwa ajitokeza kusema chochote, anapaswa kukamatwa, Rais Kikwete amkamate Mkapa… ni mhalifu, alikiuka maadili ya uongozi akiwa Ikulu, ni kama Chiluba tu.

“Rais Kikwete anapaswa atuambie kama Mkapa alivunja sheria au hakuvunja sheria kwa kufanya biashara akiwa Ikulu, tena si Mkapa tu, bali yeye na waziri wake, walijichukulia mradi mkubwa tu wa serikali bila ya kufuata taratibu au kushinda tenda yoyote, nasisitiza jamani huu ni uhalifuMkapa amekuwa akituhumiwa kwa muda mrefu kuwa alitumia vibaya madaraka yake katika kipindi cha miaka kumi alichokaa madarakani.

akiwa madarakani, aliitumia kofia ya urais kujitajirisha yeye binafsi, familia na marafiki zake. mali zinazodaiwa kuwa alichuma akiwa Ikulu ni pamoja na kuanzisha kampuni yake ya biashara, ANBEM, ambayo mkewe ni mshirika wake kibiashara. yeye na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona, iitwayo Tanpower Resources Company, ambayo aliisimamia kununua asilimia 85 ya uliokuwa mradi wa makaa ya mawe wa Kiwira, mkoani Mbeya.

Kwamba, aliutumia wadhifa wake wa urais kuhakikisha kampuni yake hiyo inaingia mkataba wa kuizuia Tanesco megawati 200 za umeme katika gridi ya taifa, kampuni ambayo mkewe na mtoto wake ni wakurugenzi. Mbali na wapinzani, Mkapa pia aliwahi kutuhumiwa na mmoja wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) anayeheshimika hapa nchini, Joseph Butiku kuwa alipageuza Ikulu kuwa mahali pa kufanyia biashara.
 
1. Gazeti hili liliwasiliana na Waziri wa Fedha kupitia simu yake ya kiganjani Jumatano wiki hii kuomba miadi ya kukutana naye kwa ajili ya kupata ufafanuzi wa madai hayo.

2. Waziri Meghji alieleza kuwa muda wake kwa siku zilizobakia kabla ya kwenda bungeni anautumia kwa ajili ya vikao, lakini aliahidi kuwasiliana na gazeti hili siku iliyoafuata (Alhamis), ili kutoa ufafanuzi wa madai haya kutokana na unyeti wake.

3. Katika hali ya kushangaza, Waziri Meghji hakutekeleza ahadi yake siku hiyo na alipotafutwa siku hiyo jioni, alitoa ahadi nyingine ya kutafuta muda wa kuzungumza na gazeti hili siku ya Ijumaa, jambo ambalo hakulitekeleza pia.

4. Tanzania Daima liliendelea kumtafuta Waziri Meghji Ijumaa jioni, lakini simu yake ya kiganjani ilikuwa ikiita bila majibu kama ilivyokuwa Jumamosi kwa simu yake kuita bila kupokelewa pia.

5. Hata hivyo, Alhamisi wiki hii, gazeti hili lilimkariri Waziri Meghji kuwa hatazungumza tena kuhusu sakata hilo la ufisadi kwa sababu sasa limefika katika ngazi nyingine. Waziri Meghji amelazimishwa kukaa kimya ili kuondoa mkanganyiko wa kauli kutoka kwa viongozi wakuu serikali.

6. Mmoja wa watumishi wa taasisi ya fedha aliyekuwa eneo hilo alisema, sababu nyingine inayomfunga mdomo Meghji, ni kuibuka kwa tetesi kuwa makandarasi wadogo waliopewa tenda ya kujenga minara miwili ya BoT, hawakuwa na sifa stahiki.

7. “Mambo yameingiliana, mama (Meghji) lazima akatae kuzungumza, huku kuna ufisadi huku kunaibuka ubora na uimara wa jengo, kuna makarandasi wadogo hapa ambao walipewa tenda kinyemela, hawakuwa na sifa za kujenga, hawa wakifuatiliwa, yanaweza kuibuka mapya,”
 
JK hawezi kutoa hiyo amri kwa sababu anafahamu fika tukifika hapo hata yeye hayuko salama kwani madhambi yake yanajulikana na uncle Ben.
 
Na huyu Mkapa anayo hoteli nchini Afrika ya kusini,na siku ya ufunguzi alimwalika Nelson Mandela lakini Mandela kwa kuwa ni mtu wa walala hoi alisusa na hakuhudhuria kabisa akijua fika kuwa fedha iliyotumika ilikuwa ya wavuja jasho ,wanaoibiwa fedha yao mchana kweupe..
 
..we wasted a lot of time kumlaumu Sumaye kwa shamba la eka 7 pale kibaigwa.

..wakati wote huo mafisadi walikuwa wanachota mabilioni BOT.

..WATANZANIA TUMELAANIWA?
 
..we wasted a lot of time kumlaumu Sumaye kwa shamba la eka 7 pale kibaigwa.

..wakati wote huo mafisadi walikuwa wanachota mabilioni BOT.

..WATANZANIA TUMELAANIWA?

Muungwana alikuwa kinara wa Kashfa ya Kibaigwa thru Waandishi wa Habari ili walalahoi wasione upande wa pili wa shilingi uliowaruhusu "KUIBA BoT" huku wakiacha watoto wengi wanakufa kwa magonjwa yanayotibika na wajawazito wengi wakifa kwa kukosa huduma bora.
Hivi ni Lazima Ballali arejee ndiyo tupate ushahidi? Kama anaamini aliamriwa kusaini kwanini asianike makabrasha hayo kwenye vyombo vya habari na hasa kupitia jamboforums, manake sanner zipo, email zipo sasa afanye kazi ya kuwaumbua Vigogo ili asife peke yake.
 
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibroad Slaa ambaye alizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, alisisitiza kuwa Rais Mkapa anapaswa kukamatwa na kufunguliwa mashitaka kwa kosa la kutumia rasilimali za nchi vibaya.“Mimi niko wazi katika hili, Mkapa si kwamba ajitokeze, bali anapaswa kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa kosa hilo. Ni jambo lisilovumiliwa, kuona kiongozi wa nchi anachukua asilimia 85 ya rasilimali za taifa na kulibakizia taifa asilimia 15.

Narudia kusema tena. Kuna mkutano wa mafisadi walikaa pale zanzibar wakajiaminisha na wakaondioa MIIKO YA UONGOZI bila update na Kujiridhisha kuwa viogozi Wa TZ sasa wanaweza kufanya upuuzi wowote wakiwa madarakani. I tell you!! RUKSA ILE ITAWAUMBUA MPAKA KABURINI...Kuanzia pale Hata katibu kati wacha mbunge alijua sasa kuwa UONGOZI NI "DILI"..UONGOZI NI MRADI!!!! Walitokwa na aibu mpaka wakafanya mbinu rushwa kuitwa TAKRIMA ili kuifikia "dili" What a shame!!! Kati ya watu ambao walitumia dili hiyo "vizuri" na kujiridhisha kuwa yuko salama salamini Ni BW MKAPA! Kupitia njia ya kujilegenezea maadili ya uongozi na kuikubalisha kuwa hilo ni muafaka, viongozi wengi wakafuata hoja hiyo kichwa kichwa... NOW THEY HAVE TO PAY THE PRICE!!!!

Lakini, Bado muda wa kujisahihisha upo. Kama kuna kiongozi yeyote anaptia hizi post abadilike maramoja. kinachompata mtu kama Mkapa Hakipendezi. Nafikiri funzo liko wazi kwa wale ambao wanapania uongozi sikuzijazo.UONGOZI SIO JAMBO LA MCHEZO MCHEZO. KUWANYONYA WALE UNAOWAONGOZA NI KINYUME NA HAKI NA USAWA WA KIUTU!

Waongoze unaowaongoza "Wajitegemee kiuchumi"..WOTE..na wewe unaye Waongoza "usiwategemee" wale unao waongoza..UJITEGEMEE BILA KUPITIA JASHO LAO!! Mkapa didnt do that..ametutumia!!! So sorry!![/COLOR]
 
Huyo Balali..Anachelewa nini?...Si atafute Camera tu ajirekodi, atutumie Majina !!awataje!!..ajitaje!!..Vyovyote vile...
Hili ni JIZI...Ni Kuulize swali..Hivi wewe Unae isoma Hii post Yangu Huja wahi kui ibia selikali?....
Asilaumiwe mtu!!!
Kwanza Tujue hizo hela ziko wapi?..ni wakina nani alafu ziludishwe..basi..!!
Ajabu yetu ni kwamba Mwizi alie iba suluali ya mtumba ya thamani ya shilingi 5000 ana chomwa moto hadi kufa..na wananchi wenye asira kali...Lakini Balali anasubiliwa awataje wenzake...
anaweza akawa Muongo ...aka wapakazia wenzake...
Hata kama ni kweli..Yeye ndie Mwizi kama wezi wengine...
 
..we wasted a lot of time kumlaumu Sumaye kwa shamba la eka 7 pale kibaigwa.

..wakati wote huo mafisadi walikuwa wanachota mabilioni BOT.

..WATANZANIA TUMELAANIWA?

hivi kweli huyu jamaa na kashfa zake ziliwezaje kusikika kuliko, za hawa mafisadi wengine?
 
hivi kweli huyu jamaa na kashfa zake ziliwezaje kusikika kuliko, za hawa mafisadi wengine?

Kwasababu alikuwa anataka kuwa rais, mtandao wakammaliza kwa data za ukweli na uwongo.

Huenda hata yeye ana madudu yake mengine, maana siamini kwamba ni Mkapa tu alikuwa anafanya deals Ikulu, kwa vyovyote hata huyo ana deals zake. Ila Sumaye sio fisadi mkubwa kama Mkapa.
 
Ila Sumaye sio fisadi mkubwa kama Mkapa.

wote kundi moja mkuu, ndio maana zero hakuamini Mkapa, alipomutpa kwenye urais maana alijua kuwa kwa kuzingatia "urafiki" wao, atampitisha yeye kwanza kuwa rais, nakumbuka deal ya NMB ambayo mkuu alishashika mgawo toka kwa wa-South kuibinafsisha, wabunge wakaja juu ikapona na yeye akaomba kujiuzulu Mkapa akakataa, hawa wote ni wamoja tu, Mkapa alikuwa siku zote in private akilalamika kuwa hana PM, lakini hakumtoa hata siku moja WHY?

Mtandao wanajua uchafu wote wa Mkapa, wala sio siri ila the question ni kama wao ni wasafi maana itaishia kuwa aibu, cha muhimu hapa ni Balali kuzungumza, popote alipo maana akirudi bongo hawezi sema kitu!
 
MTZ mtu alietangaza kuwa mfanyabiashara yoyote atakaesaidia upinzani atakuwa matatani asiwe fisadi? HUYU anaweza akawa NO.1 kwani alichofanya hata watu wenye mitaji midogo waliogopa kusupport upinzani...So far nae alishirikiana na Matajiri haohao...Hukuona Chimwaga mambo yalivyokuwa? matajiri gani walikuwa upande wake?..CCM as Whole Mafisadi...wanachofanya sasa ni kulindana...
 
Hivi JK asipomrudisha Ballali nini kitatokea? Naona sasa anapima upepo
tu kujua kama asuke au anyoe.

Siamini kabisa JK anataka kumshughulikia Ballali maana inaelekea uchafu wa BOT umeishia mlangoni kwake.

Hivi Watanzania pamoja na kujua kote tunaibiwa, tumeendelea kukaa kimya na mwaka 2010 tutamchagua JK na mawaziri wake kwa kishindo?

Tukiruhusu wakaguzi wapitie kila wizara kwenye awamu ya Mkapa, naona tutagundua hatuhitaji misaada wala kukopa. Tunaweza kutandaza reli ya kisasa nchi nzima.
 
JK hawezi kutoa hiyo amri kwa sababu anafahamu fika tukifika hapo hata yeye hayuko salama kwani madhambi yake yanajulikana na uncle Ben.

Hapo ndipo ninaposhindwa kuwaelewa watu wanaompigia kelele Kikwete achukue hatua. Atachukua hatua gani kama na yeye ni mhusika mkuu?
 
Ukweli ni kwamba serikali haimtaki Balali arudi. Siku za karibuni mama yake na kaka zake wamekuwa wakiandamwa na UWT pale Bongo wakitaka wampelekee ujumbe akae kimya. Wanasema kama atazungumza basi si serikali tu ya sasa itakayoyumbishwa, lakini wote Mkapa na Mwinyi watakuwa hatiani. Nasikia Mwungana ameshapanga plan B.
 
Hii scandal itaishia tu hivi hivi watu walishakula pesa ndo imetoka!

Kwani waliokula Goldenberg na Angloleasing Kenya leo si wapo na wanapeta? Na hizi ni pesa nyinyi zaidi BoT!

Sasa unadhani waliokula BoT watafanyiwa kitu?

Thubutu!
 
Hii scandal itaishia tu hivi hivi watu walishakula pesa ndo imetoka!

Kwani waliokula Goldenberg na Angloleasing Kenya leo si wapo na wanapeta? Na hizi ni pesa nyinyi zaidi BoT!

Sasa unadhani waliokula BoT watafanyiwa kitu?

Thubutu!


And that is the sad story of our land. We as a people are totally resigned to the fact that there is nothing we can do.

Afadhali ya hao akina Goldenberg na AngloLeasing, angalau wanao akina John Githongo wanaopigia kelele nje, lakini wanajulikana wapo. Kwani Ballali anazuiwa na nani kutueleza tu yote yaliyotokea na sisi tutachambua?
 
Ukweli ni kwamba serikali haimtaki Balali arudi. Siku za karibuni mama yake na kaka zake wamekuwa wakiandamwa na UWT pale Bongo wakitaka wampelekee ujumbe akae kimya. Wanasema kama atazungumza basi si serikali tu ya sasa itakayoyumbishwa, lakini wote Mkapa na Mwinyi watakuwa hatiani. Nasikia Mwungana ameshapanga plan B.
Ndio wale wanaBeijing?
 
Hizi speculations za kwamba Balali a.k.a Dalali anakuja nchini zinatoka wapi? Watu wanaandika habari ili wauze gazeti nasi twazikomalia! Kwa utajiri aliyo nao Balali anaweza ishi popote hata US wakimletea noma. Guys, Balali alikuwa ni mmoja tu wa mfumo wa mafisadi hapa nchini, hata hiyo fukuzwa yake ni danganya toto. hakuna kitakacho endelea zaidi ya hapo, hii serikali ni ya kisanii ndugu zangu. Kama tunauchungu tuingie barabarani kushinikiza Balali arudi..inaweza saidia..japo mabomu ya machozi wengi mnayaogopa saaaana. System nzima ya CCM inahusika na scandal hii...mmh na JK ndo mwenyekiti wake....ati ajitie kitanzi?
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom