Balali Atoweka

Mtanzania

JF-Expert Member
May 4, 2006
4,816
678
Balali atoweka

2008-05-08 10:36:59
Na Mashaka Mgeta


Gavana wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania aliyefukuzwa kazi, Dk. Daudi Balali, ametoweka nchini Marekani, na serikali haijui mahali alipo.

Jitihada za serikali, kupitia kwa Waziri wa Fedha na Mambo ya Uchumi, Bw. Mustapha Mkulo, kumsaka Bw. Balali anayehusishwa katika kashfa ya ufisadi kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika jiji la Washington nchini humo hivi karibuni, hazikufanikiwa.

``Awali tuliambiwa kwamba Balali alikuwa anatibiwa Marekani, lakini nilipokuwa huko (Marekani) hivi karibuni, nilimtafuta sana katika jiji la Washington, hakuonekana... Hatujui yupo wapi,`` alisema Bw. Mkulo, wakati akihojiwa na Nipashe jijini Dar es Salaam jana.

Hata hivyo, habari za awali zilisema kwamba Balali anatibiwa katika jiji la Boston.

Alisema timu iliyoundwa na Rais Jakaya, ikiwa inaongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. Johnson Mwanyika, inaendelea kushirikiana na vyombo vya dola, kushughulikia masuala yote yanayomhusu Gavana huyo wa zamani wa Benki Kuu.
Pia, Bw. Mkulo, alisema kwa upande mwingine, serikali imewekeza nguvu zake kuhakikisha fedha zinazodaiwa kutokana na kashfa ya EPA zinarejeshwa.

Kwa mujibu wa Bw. Mkulo, kuna mafanikio makubwa katika kuzirejesha fedha hizo, ingawa hakutaja kiasi kilichopatikana hadi kufikia jana
alipohojiwa na gazeti hili.

``Kuhusu kiasi kilichopatikana, hilo siwezi kulizungumzia lakini ninachoweza kusema ni kwamba, kuna mafanikio makubwa kuhusu kurejeshwa kwa fedha zilizofujwa kwenye EPA,``alisema.

Aidha, Bw. Mkulo, ameshindwa kuelezea athari za kiuchumi zinazotokana na baadhi ya Watanzania, kujilimbikizia mabilioni ya fedha nje ya nchi.

Alifikia hatua hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu matokeo ya ukamilishaji wa makadirio mapya ya takwimu za pato la Taifa kwa bei za mwaka 2001 kwa Tanzania Bara.

Alisema fedha zinazohifadhiwa na Watanzania nje, zinawekwa na wananchi wanaoishi ughaibuni, viongozi wa serikali na watu wengine wanaposafiri na kuamua kuwaachia ndugu zao, hususan wanaotoka huko, na wenye fedha zilizopatikana kwa njia haramu.

Hivi sasa kuna tuhuma zinazoelekezwa kwa aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Bw. Andrew Chenge, kujilimbikizia takribani Dola 1,000,000 za Marekani huko Jersey nchini Uingereza.

Ingawa Bw. Mkulo hakutaka kugusia fedha hizo, alisema kutokana na asili yake, ni vigumu kubaini kiasi cha fedha zilizohifadhiwa nje.

Hata hivyo, alisema serikali inawashawishi Watanzania wanaoishi nje, kuweka fedha zao kwenye benki za hapa nchini, ili kusaidia kuinua pato la Taifa.

Alisema uhifadhi wa fedha za wananchi wanaoishi nje ya mataifa yao, ulileta mafanikio katika nchi kama Pakistan na Philippines.

Bw. Mkulo, alitoa mfano kuwa Pakistan inapata Dola bilioni 4 za Marekani kwa mwaka, wakati Philippines ina utaratibu wa kuwatambua watu wake wanaofanya kazi nje, na kuingiza fedha zao katika akaunti zilizopo nchini humo, zinazolipwa kupitia Benki Kuu ya nchi hiyo.

Alisema kwa upande wake, Tanzania inaendeleza jitihada za kutafuta vyanzo vya fedha zilizopatikana kupitia njia zisizo halali.

``Vyombo vya dola vinashughulikia suala hilo, kwa kushirikiana na polisi wa kimataifa, Interpol,`` alisema.
 
Balali atoweka

2008-05-08 10:36:59
Na Mashaka Mgeta


Gavana wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania aliyefukuzwa kazi, Dk. Daudi Balali, ametoweka nchini Marekani, na serikali haijui mahali alipo.

Jitihada za serikali, kupitia kwa Waziri wa Fedha na Mambo ya Uchumi, Bw. Mustapha Mkulo, kumsaka Bw. Balali anayehusishwa katika kashfa ya ufisadi kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika jiji la Washington nchini humo hivi karibuni, hazikufanikiwa.

``Awali tuliambiwa kwamba Balali alikuwa anatibiwa Marekani, lakini nilipokuwa huko (Marekani) hivi karibuni, nilimtafuta sana katika jiji la Washington, hakuonekana... Hatujui yupo wapi,`` alisema Bw. Mkulo, wakati akihojiwa na Nipashe jijini Dar es Salaam jana.

Hata hivyo, habari za awali zilisema kwamba Balali anatibiwa katika jiji la Boston.

Alisema timu iliyoundwa na Rais Jakaya, ikiwa inaongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. Johnson Mwanyika, inaendelea kushirikiana na vyombo vya dola, kushughulikia masuala yote yanayomhusu Gavana huyo wa zamani wa Benki Kuu.
Pia, Bw. Mkulo, alisema kwa upande mwingine, serikali imewekeza nguvu zake kuhakikisha fedha zinazodaiwa kutokana na kashfa ya EPA zinarejeshwa.

Kwa mujibu wa Bw. Mkulo, kuna mafanikio makubwa katika kuzirejesha fedha hizo, ingawa hakutaja kiasi kilichopatikana hadi kufikia jana
alipohojiwa na gazeti hili.

``Kuhusu kiasi kilichopatikana, hilo siwezi kulizungumzia lakini ninachoweza kusema ni kwamba, kuna mafanikio makubwa kuhusu kurejeshwa kwa fedha zilizofujwa kwenye EPA,``alisema.

Aidha, Bw. Mkulo, ameshindwa kuelezea athari za kiuchumi zinazotokana na baadhi ya Watanzania, kujilimbikizia mabilioni ya fedha nje ya nchi.

Alifikia hatua hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu matokeo ya ukamilishaji wa makadirio mapya ya takwimu za pato la Taifa kwa bei za mwaka 2001 kwa Tanzania Bara.

Alisema fedha zinazohifadhiwa na Watanzania nje, zinawekwa na wananchi wanaoishi ughaibuni, viongozi wa serikali na watu wengine wanaposafiri na kuamua kuwaachia ndugu zao, hususan wanaotoka huko, na wenye fedha zilizopatikana kwa njia haramu.

Hivi sasa kuna tuhuma zinazoelekezwa kwa aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Bw. Andrew Chenge, kujilimbikizia takribani Dola 1,000,000 za Marekani huko Jersey nchini Uingereza.

Ingawa Bw. Mkulo hakutaka kugusia fedha hizo, alisema kutokana na asili yake, ni vigumu kubaini kiasi cha fedha zilizohifadhiwa nje.

Hata hivyo, alisema serikali inawashawishi Watanzania wanaoishi nje, kuweka fedha zao kwenye benki za hapa nchini, ili kusaidia kuinua pato la Taifa.

Alisema uhifadhi wa fedha za wananchi wanaoishi nje ya mataifa yao, ulileta mafanikio katika nchi kama Pakistan na Philippines.

Bw. Mkulo, alitoa mfano kuwa Pakistan inapata Dola bilioni 4 za Marekani kwa mwaka, wakati Philippines ina utaratibu wa kuwatambua watu wake wanaofanya kazi nje, na kuingiza fedha zao katika akaunti zilizopo nchini humo, zinazolipwa kupitia Benki Kuu ya nchi hiyo.

Alisema kwa upande wake, Tanzania inaendeleza jitihada za kutafuta vyanzo vya fedha zilizopatikana kupitia njia zisizo halali.

``Vyombo vya dola vinashughulikia suala hilo, kwa kushirikiana na polisi wa kimataifa, Interpol,`` alisema.

SOURCE: Nipashe
 
Mkullo aache kututia kichefuchefu kwani alikuwa anamtafuta Balali wanini? yeye si mtu sahihi wa kumtafuta Balali. Kwanza Balila alikwenda Marekani kwa kukimbia si alipelekwa na Serikali? si Kikwete na Serikali yake wametoa jibu siku nyingi kwamba hawajui anapotibiwa Balali licha ya kumlipia ghara za matibabu? Mkullo anataka nini sasa!!

Mbona Dr. Slaa aliposema Balali amekimbilia kisiwani walikataa? Mbona Balozi wa Marekani alitoa ofa ya kumrudisha balali endapo Serikali itamtaka sasa Mkullo anamtafuta Balali kimya kimya wanini? si waiombe Marekani imrudishe?
 
Wasitufanye Watanzania ni wajinga wanajua alipo hii ni kiini macho,ila waelewe Watanzania wako macho na wanajua kila wayafanyayo.
 
Hivi huyu Mkulo si ni heri angekaa kimya kuliko kuongea mambo haya ya AIBU kabisa.

Balali alipelekwa Marekani na serikali sasa iweje leo tuambiwe hajulikani, inawezekana Balali ameshakufa na maiti yake kuteketezwa na tindikali.

Jakaya siamini kama unawatumaga hawa watu wazungumze manano ya kuifedhehesha serikali yako kwa kiasi hiki, mimi siamini kama Mkulo alikuwa anatoa taarifa ya serikali ya hisia na maoni yake
 
Mkullo aache kututia kichefuchefu kwani alikuwa anamtafuta Balali wanini? yeye si mtu sahihi wa kumtafuta Balali. Kwanza Balila alikwenda Marekani kwa kukimbia si alipelekwa na Serikali? si Kikwete na Serikali yake wametoa jibu siku nyingi kwamba hawajui anapotibiwa Balali licha ya kumlipia ghara za matibabu? Mkullo anataka nini sasa!!

Mbona Dr. Slaa aliposema Balali amekimbilia kisiwani walikataa? Mbona Balozi wa Marekani alitoa ofa ya kumrudisha balali endapo Serikali itamtaka sasa Mkullo anamtafuta Balali kimya kimya wanini? si waiombe Marekani imrudishe?

Wameshatuona waTZ malimbukeni wa kutuambia kila uchafu na utumbo wanavyotaka na tunakubali hao. Yeye polisi hata amtafute? na alikuwa anaenda kumsalimia au kumsaidia kuhamishia VIJISENTI vyake Jersey island? Asituletee usanii wake wa Almeida University tena!!!

Hapa halali tena mtu ila kumkoma tu kweupeee! TUTAWAZOMEA KAMA WALIVYOKUJA KUTUFUNDISHA AEIOU YA BAJETI YA MEGHJI HADI MWISHO
 
Mkullo aache kututia kichefuchefu kwani alikuwa anamtafuta Balali wanini? yeye si mtu sahihi wa kumtafuta Balali. Kwanza Balila alikwenda Marekani kwa kukimbia si alipelekwa na Serikali? si Kikwete na Serikali yake wametoa jibu siku nyingi kwamba hawajui anapotibiwa Balali licha ya kumlipia ghara za matibabu? Mkullo anataka nini sasa!!

Mbona Dr. Slaa aliposema Balali amekimbilia kisiwani walikataa? Mbona Balozi wa Marekani alitoa ofa ya kumrudisha balali endapo Serikali itamtaka sasa Mkullo anamtafuta Balali kimya kimya wanini? si waiombe Marekani imrudishe?

Hawa jamaa wanaweza kutufanya tupate ugonjwa wa moyo shauri ya kuchukia kila saa. Hivi viongozi wetu wana kaugonjwa gani?

Siku hizi nimeacha kuchukia na badala yake nacheka tu maana ni usanii mtupu.
 
Inawezekena Balalai anaishi kwenye moja ya zile twin towers pale BOT! Just a dream...
 
Mkulo

Hii taarifa unatupa sisi, wewe kama nani kwenye kesi hii, madaraka hayo amekupa nani?

Je hujui kama kuna kamati/ tume imeundwa kwaajili hiyo?(IGP,HOSEA,MWANYIKA)

Je kwa taarifa hiyo wewe kutusomea huoni kama unatakiwa kutueleza ni kwanini hamkuitikia wito wa wamarekani walipotoa ofa ya kutukamatia balali, na nyie mlikaa kimya

Je kuja mbele yetu umetumwa na Raisi, ile kamati, au ni wewe tu umeamua kujikurupukia na kuta kutueleza unachodhani kuwa tutaamini?

``Awali tuliambiwa kwamba Balali alikuwa anatibiwa Marekani, lakini nilipokuwa huko (Marekani) hivi karibuni, nilimtafuta sana katika jiji la Washington, hakuonekana... Hatujui yupo wapi,`` alisema Bw. Mkulo, wakati akihojiwa na Nipashe jijini Dar es Salaam jana......nani alikutuma ukamtafute, na je hiyo safari ya kwenda kumtafupa pesa zilitoka fungu gani, je mkulo unaweza kunitafuta mimi hapa nilipo na ukanipata??(niko Dar)

KIKWETE STOP INSULTING US PLEASE
 
Mkullo aache kututia kichefuchefu kwani alikuwa anamtafuta Balali wanini? yeye si mtu sahihi wa kumtafuta Balali. Kwanza Balila alikwenda Marekani kwa kukimbia si alipelekwa na Serikali? si Kikwete na Serikali yake wametoa jibu siku nyingi kwamba hawajui anapotibiwa Balali licha ya kumlipia ghara za matibabu? Mkullo anataka nini sasa!!

Mbona Dr. Slaa aliposema Balali amekimbilia kisiwani walikataa? Mbona Balozi wa Marekani alitoa ofa ya kumrudisha balali endapo Serikali itamtaka sasa Mkullo anamtafuta Balali kimya kimya wanini? si waiombe Marekani imrudishe?

Kama wana nia ya kweli ya kumtafuta Ballali basi wawaambie Wamarekani tu. Watamrudisha haraka sana.
 
``Awali tuliambiwa kwamba Balali alikuwa anatibiwa Marekani, lakini nilipokuwa huko (Marekani) hivi karibuni, nilimtafuta sana katika jiji la Washington, hakuonekana... Hatujui yupo wapi,`` alisema Bw. Mkulo, wakati akihojiwa na Nipashe jijini Dar es Salaam jana.

Akutukanaye hakuchagulii tusi. Hili ni tusi kutoka serikalini kwa watanzania. Wameshatufanya majuha kupindukia.Toka lini waziri akamtafuta mtuhumiwa? Ni mara elfu serikali ikae kimya kuliko kuendeleza matusi haya.

Ila siku yao ipo......
 
Balali atoweka

2008-05-08 10:36:59
Na Mashaka Mgeta


Gavana wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania aliyefukuzwa kazi, Dk. Daudi Balali, ametoweka nchini Marekani, na serikali haijui mahali alipo.

Jitihada za serikali, kupitia kwa Waziri wa Fedha na Mambo ya Uchumi, Bw. Mustapha Mkulo, kumsaka Bw. Balali anayehusishwa katika kashfa ya ufisadi kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika jiji la Washington nchini humo hivi karibuni, hazikufanikiwa.

``Awali tuliambiwa kwamba Balali alikuwa anatibiwa Marekani, lakini nilipokuwa huko (Marekani) hivi karibuni, nilimtafuta sana katika jiji la Washington, hakuonekana... Hatujui yupo wapi,`` alisema Bw. Mkulo, wakati akihojiwa na Nipashe jijini Dar es Salaam jana.

Hata hivyo, habari za awali zilisema kwamba Balali anatibiwa katika jiji la Boston.

Alisema timu iliyoundwa na Rais Jakaya, ikiwa inaongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. Johnson Mwanyika, inaendelea kushirikiana na vyombo vya dola, kushughulikia masuala yote yanayomhusu Gavana huyo wa zamani wa Benki Kuu.
Pia, Bw. Mkulo, alisema kwa upande mwingine, serikali imewekeza nguvu zake kuhakikisha fedha zinazodaiwa kutokana na kashfa ya EPA zinarejeshwa.

Kwa mujibu wa Bw. Mkulo, kuna mafanikio makubwa katika kuzirejesha fedha hizo, ingawa hakutaja kiasi kilichopatikana hadi kufikia jana
alipohojiwa na gazeti hili.

``Kuhusu kiasi kilichopatikana, hilo siwezi kulizungumzia lakini ninachoweza kusema ni kwamba, kuna mafanikio makubwa kuhusu kurejeshwa kwa fedha zilizofujwa kwenye EPA,``alisema.

Aidha, Bw. Mkulo, ameshindwa kuelezea athari za kiuchumi zinazotokana na baadhi ya Watanzania, kujilimbikizia mabilioni ya fedha nje ya nchi.

Alifikia hatua hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu matokeo ya ukamilishaji wa makadirio mapya ya takwimu za pato la Taifa kwa bei za mwaka 2001 kwa Tanzania Bara.

Alisema fedha zinazohifadhiwa na Watanzania nje, zinawekwa na wananchi wanaoishi ughaibuni, viongozi wa serikali na watu wengine wanaposafiri na kuamua kuwaachia ndugu zao, hususan wanaotoka huko, na wenye fedha zilizopatikana kwa njia haramu.

Hivi sasa kuna tuhuma zinazoelekezwa kwa aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Bw. Andrew Chenge, kujilimbikizia takribani Dola 1,000,000 za Marekani huko Jersey nchini Uingereza.

Ingawa Bw. Mkulo hakutaka kugusia fedha hizo, alisema kutokana na asili yake, ni vigumu kubaini kiasi cha fedha zilizohifadhiwa nje.

Hata hivyo, alisema serikali inawashawishi Watanzania wanaoishi nje, kuweka fedha zao kwenye benki za hapa nchini, ili kusaidia kuinua pato la Taifa.

Alisema uhifadhi wa fedha za wananchi wanaoishi nje ya mataifa yao, ulileta mafanikio katika nchi kama Pakistan na Philippines.

Bw. Mkulo, alitoa mfano kuwa Pakistan inapata Dola bilioni 4 za Marekani kwa mwaka, wakati Philippines ina utaratibu wa kuwatambua watu wake wanaofanya kazi nje, na kuingiza fedha zao katika akaunti zilizopo nchini humo, zinazolipwa kupitia Benki Kuu ya nchi hiyo.

Alisema kwa upande wake, Tanzania inaendeleza jitihada za kutafuta vyanzo vya fedha zilizopatikana kupitia njia zisizo halali.

``Vyombo vya dola vinashughulikia suala hilo, kwa kushirikiana na polisi wa kimataifa, Interpol,`` alisema.

SOURCE: Nipashe


Mkulo ni kichaa na Mashaka Mugeta kama umevuta kiru kidogo please kaa pembeni .Yaani unavamia kuonana na mtu bila ya ahadi naye ? Mkulo alitaka nini kwa Balali ? Salaam tu ama kitu gani ? Muda wa kuwa fool umesha pita mnajimaliza wenyewe .Mashaka nadhani umekaa sana vichochoroni unachanganyikiwa .Huwezi kuvamia mtu ukasema kakimbia .Kwanza alienda kumtafutia wapi ?
 
duh!!
Huyu huyu Mkullo nimemsikia majuzi akiongelea makusanyo ya pesa za EPA ati hadi kufikia June'08 watakuwa wamekusanya 80% ya 133bn Tzs!!?Hivi JD yake inasemaje? Seems like haijui kazi yake vizuri.

Suala la Balali wala sitoshangaa wakisema hayuko Marekani cos hata aliyempeleka na kukubali kumlipia "matibabu" kwa hela ya walipa kodi wa Tanzania hajawahi kuliongelea hili suala hata siku moja! Yawezekana kabisa hivi vitu vilifanyika makusudi kabisa. No wonder Balali can be enjoying himself in Jersey Islands (home of vijisenti)!! Mukullo kama kazi yako ni kumtafuta Balali then acha uwaziri wa fedha uende ukashirikiane na Interpol/CIA/FBI etc...

Please talk about the things you know about!!
 
``Awali tuliambiwa kwamba Balali alikuwa anatibiwa Marekani, lakini nilipokuwa huko (Marekani) hivi karibuni, nilimtafuta sana katika jiji la Washington, hakuonekana... Hatujui yupo wapi,`` alisema Bw. Mkulo, wakati akihojiwa na Nipashe jijini Dar es Salaam jana.

Jamani usanii mwingine huu hata mtoto mdogo anaweza kuona. Hivi unaweza from no Where ukafika jiji la Washington ukaanza kumtafuta mtu? Huyu jamaa bado anamawazo ya kizamani hivyo. Tumesikia wangapi wamesalimishwa police dar kwa kutoka mikoani kwa lengo la kumtafuta ndugu yake dar? Fikiria mtu atoke iringa kwa lengo la kumtafuta ndugu yake dar na hapajui anapoishi atampata? Je mkulo alikuwa anasimama stesheni au sokoni amsuburi balali aje kununua samaki? Huu ubwege mwingine jamani. Je mkulo hana namba yake ya simu? Hajui alikuwa anakaa mtaa na nyumba ipi? Kwa hiyo alikuwa anaenda mtaa kwa mtaa akichungulia kuwa Balali atamuona? JK hawa mawaziri wako vipi mazee? Au uji unafata ugoko.
 
Wakuu mimi nimechungulia kidogo masuala ya sheria ya "dual natinality" kuona kama Balali lakuwa anjua alichokua akikifanza.

Mkullo hana jipya na inaonekana balali hawezi kuletwa Tanzania.

Nawaomba tufuatilie hizo sehemu nilizozikoleza na tuone kama Balali bado anaongoza kwa magoli 2-0.

Dual Nationality


"The concept of dual nationality means that a person is a citizen of two countries at the same time. Each country has its own citizenship laws based on its own policy.Persons may have dual nationality by automatic operation of different laws rather than by choice. For example, a child born in a foreign country to U.S. citizen parents may be both a U.S. citizen and a citizen of the country of birth.

A U.S. citizen may acquire foreign citizenship by marriage, or a person naturalized as a U.S. citizen may not lose the citizenship of the country of birth.U.S. law does not mention dual nationality or require a person to choose one citizenship or another. Also, a person who is automatically granted another citizenship does not risk losing U.S. citizenship. However, a person who acquires a foreign citizenship by applying for it may lose U.S. citizenship. In order to lose U.S. citizenship, the law requires that the person must apply for the foreign citizenship voluntarily, by free choice, and with the intention to give up U.S. citizenship.

Intent can be shown by the person's statements or conduct.The U.S. Government recognizes that dual nationality exists but does not encourage it as a matter of policy because of the problems it may cause. Claims of other countries on dual national U.S. citizens may conflict with U.S. law, and dual nationality may limit U.S. Government efforts to assist citizens abroad. The country where a dual national is located generally has a stronger claim to that person's allegiance.

However, dual nationals owe allegiance to both the United States and the foreign country. They are required to obey the laws of both countries. Either country has the right to enforce its laws, particularly if the person later travels there.Most U.S. citizens, including dual nationals, must use a U.S. passport to enter and leave the United States. Dual nationals may also be required by the foreign country to use its passport to enter and leave that country. Use of the foreign passport does not endanger U.S. citizenship.Most countries permit a person to renounce or otherwise lose citizenship.

Information on losing foreign citizenship can be obtained from the foreign country's embassy and consulates in the United States. Americans can renounce U.S. citizenship in the proper form at U.S. embassies and consulates abroad."

Source:Uhamiaji ya Marekani

Ninachoweza kusema ni kwamba kama kweli balali yupo marekani basi kutakuwa na kazi kwelikweli ya kumpata.
 
Lakini watz nnavyowajua hata huyu Mkulo akigombea "urahisi" kupitia Chama Cha Mabazazi atapeta tuuuuuuuu!!!!!!!!!

Ila tutakujakuchekwa sana na generation ijayo!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom