Balali Atazikwa Au Atachomwa?

Ipole

JF-Expert Member
Apr 15, 2008
294
10
:: Karibu [ Mgeni ]
Maskani
Tanzania
Michezo
Makala
Siasa
Uchumi
Kimataifa
Sayansi
Maisha na Jamii
Safu Maalum
Uchambuzi wa Habari
Mijadala


:: Ingia Jisajili
Baruapepe
Funguo







::Habari za Tanzania Ijumaa Mei 23, 2008

Imetolewa mara ya mwisho: 23.05.2008 0111 EAT
•
Mwili wa Balali kuchomwa moto leo

Habari Zinazoshabihiana
• Aliyesamehewa na Rais Kikwete achomwa moto 23.01.2007 [Soma]
• Ajira ya Balali serikalini utata mtupu 19.01.2008 [Soma]
• Duni Haji ampongeza JK lakini... 15.01.2008 [Soma]

*Heshima kutolewa Kanisa la Mtakatifu Stephen
*Ratiba yaonesha ndugu wa karibu tu kuhudhuria

Na Joseph Lugendo

ALIYEKUWA Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Dkt. Daudi Ballali anazikwa leo mjini Washington DC, Marekani na huenda mwili wake ukachomwa moto kwa mujibu wa taratibu za makaburi anakozikwa.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha kuaminika kutoka nchini humo, mwili wa marehemu uliohifadhiwa kwenye nyumba ya maziko ya De-Vol iliyoko mjini humo unatarajiwa kuagwa leo saa 4 asubuhi kwa saa za Marekani katika Kanisa Kuu la St.Stephen Martyr 2436 Pennsylvania Ave,NW Washington, DC 20037.

Heshima za mwisho zitatolewa kanisani hapo baada ya misa na zitahusisha ndugu jamaa na marafiki wa karibu tu na sio hadhara ya mtu yeyote anayetaka kushiriki.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Bw.Ombeni Sefue ataongoza waombolezaji kutoa heshima hizo akifuatiwa na watumishi wa Idara mbalimbali alizowahi kutumikia marehemu Ballali alipokuwa akifanyakazi kwenye Shirika la Fedha Duniani (IMF), ndugu zake waliowasili Marekani siku chache zilizopita na Watanzania wachache wanaoishi Washington DC.

Baada heshima za mwisho mwili huo utapelekwa katika makaburi ya Wakatoliki ya Get of Heaven eneo la Silver Spring, MD. Hata hivyo haijajulikana kama mwili huo utachomwa moto ama utazikwa kiafrika kwa kuteremshwa kaburini kwasababu huduma zote mbili zinakubalika katika makaburi hayo.

Ikiwa atachomwa moto, majivu yake hayataruhusiwa kugawanywa bali yatateremshwa kaburini kwa mujibu wa taratibu za kikatoliki.

Wakati huo huo chanzo chetu kingine kilichokarubu na familia hiyo hapa nchini kilidokeza kwamba mazishi hayo yamesababisha mgawanyiko na mvutano mkubwa ndani ya familia yake.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, mvutano huo sasa umeigawa familia hiyo katika makundi makuu mawili yanayopingana.

Mvutano huo umesababishwa na kutokubaliana kulikojitokeza baina ya makundi hayo ya familia juu ya mahali anapopaswa kuzikwa Dkt. Ballali.

Mtoa habari wetu alisema upande unaoongozwa na mke wa marehemu Bi Anna Muganda ulitaka Dkt. Ballali azikwe nchini Marekani alikofia wakati upande wa ndugu zake walitaka mwili wa marehemu urejeshwe nchini kwa maziko.

Akizungumza kwa simu na Majira jana jioni, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Patrick Mombo, alisema amezungumza na Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani lakini nao haukuwa na habari zozote juu ya mazishi ya Dkt. Ballali.

"Nimezungumza na Balozi, alikuwa akielekea ofisini lakini hakuwa na taarifa zozote za mazishi, sasa hivi kule ni asubuhi, nikipata taarifa yoyote nitakueleza," alisema Balozi Mombo.

Juzi Serikali katika nyakati tofauti ilitoa taarifa rasmi za kifo cha Dkt. Ballali kilichotokea Ijumaa ya wiki iliyopita Mei 16, mwaka huu.

Katika taarifa iliyotolewa na Ikulu, Rais Jakaya Kikwete alielezea masikitiko yake juu ya kifo hicho na kuelekeza kuwa taarifa zaidi juu ya mazishi yake zitatokana na uamuzi wa familia yake.

Kwa upande wa BoT, Ofisa Uhusiano Mwandamizi, Bw. Emmanueli Mwero naye alitoa taarifa ya kuthibitisha kifo hicho na kuahidi kutoa taarifa za mara kwa mara juu ya kitakachokuwa kikiendelea.

Watu mbalimbali waliotoa maoni juu ya kifo hicho, licha ya kuitaka Serikali kufanya uchunguzi ili kupata taarifa zaidi pia walipendekeza mwili wake uletwe nchini kwa ajili ya mazishi.

Hata hivyo, kinyume na mtazamo huo wa wananchi, taarifa nyingine zisizo rasmi zilidai kuwa, Dkt. Ballali, enzi za uhai wake alipendekeza kama akifa, mwili wake usiletwe nchini.

Taarifa hizo zilidai kwamba mazishi rasmi ya Dkt. Balali yanatarajiwa kufanyika leo nchini Marekani.

Wakati huo huo serikali imelaumiwa kwa kupiga chenga msiba wa gavana huyo hasa ambaye ndani ya moyo wake alikuwa na taarifa muhimu kuhusu yaliyojiri katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).

"Huyu alikuwa ni mtu muhimu hivyo serikali haikupswa kukaa kimya...kwa kweli hili limetusikitisha sana," alisema Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mbunge wa CUF, Bw. Hamad Rashid Mohamed, alipozungumza na gazeti hili.

Alisema walitegemea serikali ingetoa tamko hasa kwa kuzingatia kuwa gavana anateuliwa na Rais, hivyo hilo ni jukumu la serikali kuueleza umma kuhusu yaliyotokea badala ya kuiachia taasisi.

Bw. Rashid alisema hata kama serikali haikuona umuhimu wa kuwapatia taarifa wananchi basi ilistahili kuwaeleza jinsi ilivyosikitishwa na kifo chake hasa kwa kuzingatia kuwa kimetokea katika kipindi muhimu na uchunguzi ya 'madudu' yaliyotokea ndani ya akaunti ya EPA ukiwa unaendelea.

Alisisitiza kuwa Dkt. Ballali alikuwa na taarifa muhimu kuhusu EPA, hivyo serikali ilipaswa kutolea taarifa kifo hicho. "Watanzania walipaswa kuambiwa tangu kuugua kwake hadi kufariki," alisisitiza.

Alisema inawezekana ameacha wosia na nyaraka mbalimbali hivyo ameitaka serikali kuunda tume ya kuchunguza kifo chake. Ameshauri tume itakayoundwa itoke miongoni mwa wabunge.

Mzee Mwanakiji mtume INZI na utupe taarifa ndugu yetu huyo atachomwa moto au atazikwa tunaomba mtujulishe wana JF mlioko huko
 
Mimi nafikiri sasa jamani hii issue ya huyu Muungwana iwekwe Kapuni maana mengi yameshasemwa na kesho ndio hatma yake. Kilichobaki kumuomba Mungu Amlaze mahali pema na tujaribu kuwapa faraja ndugu wa marehemu katika suala hili zito na sio kuanza kuhoji vitu ambavyo havina msingi wowote. Mwisho namuomba Mungu ailaze roho ya Marehemu pema, Amina.
 
Muungwa husimhusishe mungu kwenye kifo cha huyu mtu mimi hapa naona tumepigwa shanga la macho.kwa upeo wangu mdogo wa akili na hata jinsi hali halisi ilivyo kuhusiana na kifo hiki mi siamini kama huyu muungwana amerestishwa in peace kama inavyosemekana na kinachonisikitisha mimi zaidi mbona hata huyu amiri mkuu ajateta kitu naombeni mnijibu kutoa wasiwasi wangu
 
Kinachonikwaza sio mavumbi yatarudije ardhini, kumbuka bin adam ni mavumbi na mavumbini atarejea. Iwe atachomwa, atazikwa...atarejea mavumbini. Kinikwazacho Askari wa Amani ni hiki:- Inakuwaje watu nyeti, tena wanaohusika au kuhusishwa na issue nyeti za nchi hii, hupoteza maisha katika wakati ambao issue hizo nyeti zimefika hatua nyeti?Mbaya zaidi, tunasahau baada ya muda mfupi.
 
Mimi nafikiri sasa jamani hii issue ya huyu Muungwana iwekwe Kapuni maana mengi yameshasemwa na kesho ndio hatma yake. Kilichobaki kumuomba Mungu Amlaze mahali pema na tujaribu kuwapa faraja ndugu wa marehemu katika suala hili zito na sio kuanza kuhoji vitu ambavyo havina msingi wowote. Mwisho namuomba Mungu ailaze roho ya Marehemu pema, Amina.

KUNTA, HESHMA MKUU,

MIMI SIKOTAYARI KUMUOMBEA HUYU FISADI ILI APATE PUMZIKO LA MILELE. HEBU FIKIRIA NI KINA MAMA WANGAPI WALIO POTEZA MAISHA KWA KUKOSA HUDUMA SAHIHI WAKATI WA KUJIFUNGUA KUTOKANA NA KUKOSA HUDUMA AU DAWA HEBU FIKIRIA NI WATU WANGAPI WANAOKUFA KWA MALARIA KWA KUKOSA HELA ZA KULIPA KUMUONA DAKTARI AU HATA KUNUNUA DAWA. YEYE NI NGAPI ALIIDHINISHA KWA MAFISADI KWA MANUFAA YAO WENYEWE!!! NATAMANI AKIFIKA AENDE MOJO KWA MOJA MOTONI ILI AWAOMBE HATA TONE LA MAJI LA KUPOOZA ULIMI. KWANI PEPO YAKE ALISHAIPATA HAPA DUNIANI. KAMA ILIVYO KUWA KWA LAZARO ALIYEKUWA ANAFUKUZWA NA TAJIRI KUOKOTA MAKOMBO YA CHAKULA KILICHO DONDOKA CHINI.
 
Big up sana ndugu yangu ulosema ni kweli kwani baada ya siku mbili tunasahau kila kitu. mimi naonelea kuundwe tume ya kuchunguza kifo cha huyu jamaa kama ilivyokushwa kuundwa tume ya kuchunguza hela ya EPA
 
:: Karibu [ Mgeni ]

"Huyu alikuwa ni mtu muhimu hivyo serikali haikupswa kukaa kimya...kwa kweli hili limetusikitisha sana," alisema Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mbunge wa CUF, Bw. Hamad Rashid Mohamed, alipozungumza na gazeti hili.

Bw. Rashid alisema hata kama serikali haikuona umuhimu wa kuwapatia taarifa wananchi basi ilistahili kuwaeleza jinsi ilivyosikitishwa na kifo chake hasa kwa kuzingatia kuwa kimetokea katika kipindi muhimu na uchunguzi ya 'madudu' yaliyotokea ndani ya akaunti ya EPA ukiwa unaendelea.

Alisisitiza kuwa Dkt. Ballali alikuwa na taarifa muhimu kuhusu EPA, hivyo serikali ilipaswa kutolea taarifa kifo hicho. "Watanzania walipaswa kuambiwa tangu kuugua kwake hadi kufariki," alisisitiza.

Alisema inawezekana ameacha wosia na nyaraka mbalimbali hivyo ameitaka serikali kuunda tume ya kuchunguza kifo chake. Ameshauri tume itakayoundwa itoke miongoni mwa wabunge.

Hii inazidi kutoa changamoto kwa sakata hili! Very very interesting! time wil come na kila kitu kitakuwa wazi hadharani.... for now lets be patients and wait!
 
Mungu ailaze roho ya Mzee Ballali mahala pema mbinguni. AMEN.

Najua siku zake za mwisho duniani hazikuwa na raha. Lazima alikuwa na mawazo mengi, alijiona kama ameonewa na kuwa scapegoat. Tuone hayo maandishi aliyoacha yatasemaje. Na ninavyosikia hao kachero waliotumwa kutoka Bongo wanaisaka hiyo karatasi.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom