JAYJAY
JF-Expert Member
- Oct 31, 2008
- 7,291
- 7,235
leo asubuhi mida ya saa 12 na nusu nimekuta zogo kubwa kweli kuhusiana na mchango wa kununua umeme kwenye nyumba moja, si unajua nyumba zenye wapangaji wengi. jamaa walikuwa wanakoromeana ile mbaya, kisa ni kuwa jamaa mmoja kakataa kuchangia na kusababisha nyumba nzima kulala bila umeme. naomba kuuliza hivi hakuna namna ya kupima kila mtu anatumia umeme kiasi gani, au hakuna kifaa ambacho kinaweza kufungwa na kila mpangaji akafahamu matumizi yake na hivyo kupunguza malalamiko na magomvi. maana hili ni tatizo kubwa kweli kweli kwenye nyumba zenye wapangaji wengi na mimi mwenyewe limewahi kunikuta hili!