BAKWATA Yapinga maandamano ya Waislam tarehe 23 Dec 20011

Polen xana wakaaz wa dar es salaam kwa maafa yaliyowakuta pia kwa ndugu zetu waliopoteza maisha mwenyezi mungu aziweke roho za marehem pema peponi, mungu alitoa mungu ametwaa jina lake lihimidiwe. Wahusika wa miundo mbinu tekelezen wajib wenu wa kurekebisha miundombinu ili kunusuru maisha ya watanzania. Kwa ndugu zangu waishio mabondeni jaman hamen mabo yameharibika.
Nitakusamehe tu kwa sababu ndio post yako ya kwanza hii, lakini hapa hatuna topic ya wakazi wa Dar, na hii JF ina member dunia nzima na wanaochangia thread hii sasa hivi wapo nchi mbalimbali, kwa hiyo kama unataka kutoa pole kwa wakazi wa Dar anzisha thread yako au tafuta humu inayohusiana utaikuta.
 
Alinifurahisha sana aliposema kuwa waislam bado hawajaelewa vizuri swala la MOA na kwa msisitizo mkubwa amewaonya waislam kupinga MOA ni makosa makubwa na badala ya kuandamana juu ya hili kawashauri waislam nao kuandaa miradi yaa ya kijamii ili wawezeshwe ruzuku kama taasisi za kikristo zinavyofanya.
Ni vizuri sana kuona Sheikh anatoa maagizo ya busara wa waislam wote wa TZ na kawashauri waislam kujishuhulisha nq maendeleo na kuacha kupinga maendeleo kwenye taasisi za zinazosimamiwa na makanisa.
 
Daniel Rutoryo na Abdallah Mdangwe
SHEHE Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Alhaji Alhad Musa Salum amewataka waislamu wa mkoa huo na nchini kwa ujumla kutoshiriki maandamano yaliyoandaliwa na Umoja wa Waadhiri wa Kiislamu nchini Desemba 23, mwaka huu.

Hivi karibuni umoja huo wa wahadhiri wa Kiislamu ulitangaza kufanya maandamano hayo kupinga mambo mawili, ambayo ni makuabaliano kati ya makanisa na serikali na kuchelewa kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi.

Akizungumza na waandishi habari jana jijini Dar es Salaam, akiliwakilisha Baraza la Kuu la Waislamu (BAKWATA), Shehe Salum alisema hakubaliani na taarifa iliyotolewa na wahadhiri hao na kuwataka Waislamu wasishiriki katika maandamano hayo.

Alhaji shehe Salum alisema haamini kama maandamano yatakuwa suluhishi la upatikanaji wa haki za Waislam ikiwemo kuanzishwa Mahakama hiyo ya Kadhi.

“Sisi Baraza la Waislamu Tanzania hatuamini kama maandamano ndio suluhisho la haki za binadamu au hiyo mahakama ya Kadhi, njia hiyo ya wananchi kuandamana itaishia kupigwa mabomu tu, ”alisema Shehe Salum.
Alifafanua kwamba, sababu wanayoeleza wahadhiri hao haina mashiko kwa sababu tayari suala la uanzishwaji wa mahakma hiyo ya kadhi lipo mezani na linashughulikiwa na serikali.

“Kupinga maridhiano ya serikali na makanisa juu ya misaada wanayopewa katika huduma za jamii, hakuna mantiki yoyote la msingi ni Waislamu kujihalalishia mikataba kwa kujiwekea miundo mbinu na huduma za jamii za kutosha kielimu na kiafya ili tundelee,” alisema Shehe Salum.

Alisisitiza, “Bakwata inayo mikakati madhubuti ya kuhakikisha sheria za mahakama ya Kadhi zinaingizwa katika katiba mpya.”

Shehe huyo wa mkoa aliitaka jamii kuondoa wasiwasi kwani itajihusisha na masuala ya mirathi, ndoa, talaka na malezi ya watoto kwa Waislamu tu.Alisema serikali inapaswa kuruhusu nchi kujiunga na Jumuiya ya Kiislam DunianI (OICC) kwani jumuiya hii hutoa misaada kwa wanajamii kupitia serikalini na si kwa Waislamu pekee hii ni kwa manufaa ya watanzania wote.


Viongozi wa dini na siasa


Kuhusu viongozi wa dini, aliwataka kutojihusisha na siasa wala wanasiasa kutumia dini ili kujijengea umaarufu katika jamii kwani hiyo itapelekea kuwagawa wananchi, kutokana na imani tofauti za kidini.

Shehe Salum aliwataka wanasiasa wasijihushishe na viongozi wa dini kujinufaisha kisiasa huku pia viongozi wa dini nao wakiacha kujihusisha na masuala ya siasa ili kutopoteza imani zilizojengeka kwa wananchi

chanzo: Bakwata yapinga maandamano ya wahadhiri wa Kiislam
 
"Kupinga maridhiano ya serikali na makanisa juu ya misaada wanayopewa katika huduma za jamii, hakuna mantiki yoyote la msingi ni Waislamu kujihalalishia mikataba kwa kujiwekea miundo mbinu na huduma za jamii za kutosha kielimu na kiafya ili tundelee," alisema Shehe Salum.

Haya ndio mawazo ya mtu mwenye akili timamu. Uislamu wa namna hii utaisogeza mbele Tanzania na kupunguza ufukara unaoletwa na fikra duni za watu kama MS na Topical.
 
“Kupinga maridhiano ya serikali na makanisa juu ya misaada wanayopewa katika huduma za jamii, hakuna mantiki yoyote la msingi ni Waislamu kujihalalishia mikataba kwa kujiwekea miundo mbinu na huduma za jamii za kutosha kielimu na kiafya ili tundelee,” alisema Shehe Salum.[/URL]
Meseji sent and delivered to Malaria Sugu and Faiza Forx
 
Tanzania kuna waislam wa ukweli na waislam fake,waislam fake ndio wanaotusumbua na kurudisha nyuma maendeleo,kazi yao kubwa ni kulalama tu kila uchwao,kazi hawafanyi ila wanapenda kushinda kwenye kahawa na kucheza bao.
 
Hivi hawa wahadhiri ni watu gani?, naomba kujuzwa, niwahadhiri wa madrasa au vyuo gani?. Nikipatajibu nitarudi kujadiri.
 
Hivi hawa wahadhiri ni watu gani?, naomba kujuzwa, niwahadhiri wa madrasa au vyuo gani?. Nikipatajibu nitarudi kujadiri.
Mabingwa au Mashababi(Al-shabab)wa Mihadhara ya Kashfa za dini zingine, kama vile Khidmat Daawat'l Islamiya na wengineo!
 
Daniel Rutoryo na Abdallah Mdangwe
SHEHE Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Alhaji Alhad Musa Salum amewataka waislamu wa mkoa huo na nchini kwa ujumla kutoshiriki maandamano yaliyoandaliwa na Umoja wa Waadhiri wa Kiislamu nchini Desemba 23, mwaka huu.

Hivi karibuni umoja huo wa wahadhiri wa Kiislamu ulitangaza kufanya maandamano hayo kupinga mambo mawili, ambayo ni makuabaliano kati ya makanisa na serikali na kuchelewa kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi.

Akizungumza na waandishi habari jana jijini Dar es Salaam, akiliwakilisha Baraza la Kuu la Waislamu (BAKWATA), Shehe Salum alisema hakubaliani na taarifa iliyotolewa na wahadhiri hao na kuwataka Waislamu wasishiriki katika maandamano hayo.

Alhaji shehe Salum alisema haamini kama maandamano yatakuwa suluhishi la upatikanaji wa haki za Waislam ikiwemo kuanzishwa Mahakama hiyo ya Kadhi.

“Sisi Baraza la Waislamu Tanzania hatuamini kama maandamano ndio suluhisho la haki za binadamu au hiyo mahakama ya Kadhi, njia hiyo ya wananchi kuandamana itaishia kupigwa mabomu tu, ”alisema Shehe Salum.
Alifafanua kwamba, sababu wanayoeleza wahadhiri hao haina mashiko kwa sababu tayari suala la uanzishwaji wa mahakma hiyo ya kadhi lipo mezani na linashughulikiwa na serikali.

“Kupinga maridhiano ya serikali na makanisa juu ya misaada wanayopewa katika huduma za jamii, hakuna mantiki yoyote la msingi ni Waislamu kujihalalishia mikataba kwa kujiwekea miundo mbinu na huduma za jamii za kutosha kielimu na kiafya ili tundelee,” alisema Shehe Salum.

Alisisitiza, “Bakwata inayo mikakati madhubuti ya kuhakikisha sheria za mahakama ya Kadhi zinaingizwa katika katiba mpya.”

Shehe huyo wa mkoa aliitaka jamii kuondoa wasiwasi kwani itajihusisha na masuala ya mirathi, ndoa, talaka na malezi ya watoto kwa Waislamu tu.Alisema serikali inapaswa
kuruhusu nchi kujiunga na Jumuiya ya Kiislam DunianI (OICC) kwani jumuiya hii hutoa misaada kwa wanajamii kupitia serikalini na si kwa Waislamu pekee hii ni kwa manufaa ya watanzania wote.

Viongozi wa dini na siasa


Kuhusu viongozi wa dini, aliwataka kutojihusisha na siasa wala wanasiasa kutumia dini ili kujijengea umaarufu katika jamii kwani hiyo itapelekea kuwagawa wananchi, kutokana na imani tofauti za kidini.

Shehe Salum aliwataka wanasiasa wasijihushishe na viongozi wa dini kujinufaisha kisiasa huku pia viongozi wa dini nao wakiacha kujihusisha na masuala ya siasa ili kutopoteza imani zilizojengeka kwa wananchi

chanzo: Bakwata yapinga maandamano ya wahadhiri wa Kiislam



Hili nalo neno kutoka kwa mwenye fikra pevu kidini na kimtazamo Maralia Sugu na ndugu yako F.Fox mpo?
Ila tujadili hili ndugu,kote Bakwata wameenda sawa lakini alipofika ktk alama nyekundu mhhhhhhhhhhhh..................!!!!! Ktk katiba kadhi inatafuta nini badala ya ktk misaafu na misikiti yenu?Na hii OIC mnayong'ang'ania sababu ni misaada tu au kuna jingine?Kama ni misaada si mumkubalie Cameroon matakwa yake mpate misaada kibao. Hivi ni kweli akili zetu hazina lingine la kufikiri kujikomboa zaidi ya kutegemea misaada.Na inamaana ninyi (waislam) tu ndiyo mnaiona hiyo misaada wengine hawaioni.Ujinga huu ndiyo umetufikisha hapa tulipo mawazo na mtazamo finyu wa Viongozi wetu.
Kama kiongozi wa bakwata ana mtazamo huo na uelewa huo Je muumini wa kawaida atakuwaje?
Ila heri ya Bakwata kuliko wahadhiri wenu japo nilidhani wahadhili wangekuwa na ufahamu mpana zaidi lakini inadhihilisha kinyume chake.
 
Hivi hawa wahadhiri ni watu gani?, naomba kujuzwa, niwahadhiri wa madrasa au vyuo gani?. Nikipatajibu nitarudi kujadiri.

hapa hata mimi nilikuwa najiuliza, au ni wahadhiri wa muslim law au muslim religion as a subject/unit in the universities!!
 

"Kupinga maridhiano ya serikali na makanisa juu ya misaada wanayopewa katika huduma za jamii, hakuna mantiki yoyote la msingi ni Waislamu kujihalalishia mikataba kwa kujiwekea miundo mbinu na huduma za jamii za kutosha kielimu na kiafya ili tundelee,"
alisema Shehe Salum.

 
Mabingwa au Mashababi(Al-shabab)wa Mihadhara ya Kashfa za dini zingine, kama vile Khidmat Daawat'l Islamiya na wengineo!

are you serious mkuu! Au unatania/unakashifu tu. Kama ni kweli, watu hao wana elimu ya kiasi gani ndani ya dini husika? Ni wataalamu waliobobea au ni tia maji tia maji? Mimi nawaheshimu sana watu waliobobea katika elimu yoyote ile hata kama ni mambo ya dini isiyo yangu.
 
Hili nalo neno kutoka kwa mwenye fikra pevu kidini na kimtazamo Maralia Sugu na ndugu yako F.Fox mpo?
Ila tujadili hili ndugu,kote Bakwata wameenda sawa lakini alipofika ktk alama nyekundu mhhhhhhhhhhhh..................!!!!! Ktk katiba kadhi inatafuta nini badala ya ktk misaafu na misikiti yenu?Na hii OIC mnayong'ang'ania sababu ni misaada tu au kuna jingine?Kama ni misaada si mumkubalie Cameroon matakwa yake mpate misaada kibao. Hivi ni kweli akili zetu hazina lingine la kufikiri kujikomboa zaidi ya kutegemea misaada.Na inamaana ninyi (waislam) tu ndiyo mnaiona hiyo misaada wengine hawaioni.Ujinga huu ndiyo umetufikisha hapa tulipo mawazo na mtazamo finyu wa Viongozi wetu.
Kama kiongozi wa bakwata ana mtazamo huo na uelewa huo Je muumini wa kawaida atakuwaje?
Ila heri ya Bakwata kuliko wahadhiri wenu japo nilidhani wahadhili wangekuwa na ufahamu mpana zaidi lakini inadhihilisha kinyume chake.

Mkuu Jk alishatoa ufafanuzi kuhusu kadhi pale ktk msikiti wa Gaddafi ambapo alisema hili la kadhi linatekelezwa ila mfuko wa kuendesha mahakama hiyo utakuwa ni wa fedha za waislam na wasitegemee fedha za serikali kuendesha mahakama ya kadhi.
Sheikh Salum anavyosema swala la kadhi litaingia kwenye katiba mpya ni kweli kabisa ila ktk katiba iyo mpya swala la kadhi litaingizwa kama alivyoainisha JK kuwa, kadhi itajitegemea yenyewe kwa fedha zake na sio fedha za serikali.
 
Haya ndio mawazo ya mtu mwenye akili timamu. Uislamu wa namna hii utaisogeza mbele Tanzania na kupunguza ufukara unaoletwa na fikra duni za watu kama MS na Topical.

Sawa maalim but waje na mpango mkakati wao tuanze kupiga kazi sio kujibu tu kwamba we need to pin down contracts....wao ndo waandae na ku sign ili tuone uhai wa hayo anayoyaongea sio kutoa ngonjera tuuuuu.........tunataka vitendo sasa sio kujibizana on media. Hawa si wa kuchekea tena hawa its high time kuwapa kiti moto ili wajue we need good life hapa na akhera inshaallah.....tumekuwa wapole sana in such a way that wanasahau kama kuna watu wa kuweza ku challenge maamuzi yao

Hivi hawa bakwata mathalani baada ya haya maandamano ku fail then wao wanatoa nini tangible kuboresha hali za waumin (Haramain na muslim........... just naming few among)?? It can be more than wat we see kama tutaamua sasa kuwa na viongozi wenye upeo wa mbali na kuweza ku balance ilmu zote na sisi tuwawajibishe day n nights
 
polen xana wakaaz wa dar es salaam kwa maafa yaliyowakuta pia kwa ndugu zetu waliopoteza maisha mwenyezi mungu aziweke roho za marehem pema peponi, mungu alitoa mungu ametwaa jina lake lihimidiwe. Wahusika wa miundo mbinu tekelezen wajib wenu wa kurekebisha miundombinu ili kunusuru maisha ya watanzania. Kwa ndugu zangu waishio mabondeni jaman hamen mabo yameharibika.

kaka umetisha kwa mchano mzuri,wakati muafaka lakini sio mahali sahihi na mada sahihi,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,!
 
Back
Top Bottom