real G
JF-Expert Member
- Feb 7, 2013
- 5,227
- 5,287
BARAZA Kuu la Waislamu wa Tanzania (Bakwata), limesema Sikukuu ya Idd el-Fitr kitaifa itaswaliwa Moshi mkoani Kilimanjaro, Juni 25 au 26 kutegemea na mwandamo wa mwezi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu wa Bakwata, Salim Abeid, swala ya Idd el-Fitr itaswaliwa kwenye Uwanja wa Chui mbele ya Shule ya Msingi Mwenge kuanzia saa 1.30 asubuhi.
Katibu Mkuu wa Bakwata alisema swala hiyo itafuatiwa na Baraza la Idd litakalofanyika kwenye Ukumbi wa Chuo cha Polisi (CCP) Moshi baada ya swala ya Adhuhuri.
Alisema mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, na pia watakuwepo viongozi mbalimbali. Waislamu nchini kila mwaka hujumuika na wenzao duniani kusherehekea sikukuu hiyo baada ya kumaliza mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani
Chanzo: Habarileo
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu wa Bakwata, Salim Abeid, swala ya Idd el-Fitr itaswaliwa kwenye Uwanja wa Chui mbele ya Shule ya Msingi Mwenge kuanzia saa 1.30 asubuhi.
Katibu Mkuu wa Bakwata alisema swala hiyo itafuatiwa na Baraza la Idd litakalofanyika kwenye Ukumbi wa Chuo cha Polisi (CCP) Moshi baada ya swala ya Adhuhuri.
Alisema mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, na pia watakuwepo viongozi mbalimbali. Waislamu nchini kila mwaka hujumuika na wenzao duniani kusherehekea sikukuu hiyo baada ya kumaliza mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani
Chanzo: Habarileo