BAKWATA wasema sikukuu ya Idd itaswaliwa kitaifa Moshi, mgeni rasmi waziri mkuu Majaliwa

real G

JF-Expert Member
Feb 7, 2013
5,227
5,287
BARAZA Kuu la Waislamu wa Tanzania (Bakwata), limesema Sikukuu ya Idd el-Fitr kitaifa itaswaliwa Moshi mkoani Kilimanjaro, Juni 25 au 26 kutegemea na mwandamo wa mwezi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu wa Bakwata, Salim Abeid, swala ya Idd el-Fitr itaswaliwa kwenye Uwanja wa Chui mbele ya Shule ya Msingi Mwenge kuanzia saa 1.30 asubuhi.

Katibu Mkuu wa Bakwata alisema swala hiyo itafuatiwa na Baraza la Idd litakalofanyika kwenye Ukumbi wa Chuo cha Polisi (CCP) Moshi baada ya swala ya Adhuhuri.

Alisema mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, na pia watakuwepo viongozi mbalimbali. Waislamu nchini kila mwaka hujumuika na wenzao duniani kusherehekea sikukuu hiyo baada ya kumaliza mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani

Chanzo: Habarileo
 
INSHAALAH!!!
TUNAWATAKIA SIKU KUU NJEMA,,,NDUGU ZETU WAISLAAM,, MSHEHREHEKEE KWA AMANI.

TUKO PAMAJA SANA!!!!
 
Bakwata wako kama branch ya CCM ndio maana mdau kasema hivyo hapo juu.

Nakupa mfano, Eid hii mwezi umeshaandama jana jioni (24/06/2017) ina maana Eid mosi ni leo ila Bakwata hawataki kutangaza kwa kua katika sherehe hii kuna viongozi wa kisiasa wameshaarikwa na wameambiwa eid ni jumatatu sasa wanaona wakisema ni leo itakuaje kwa bwana mkubwa wao aliyealikwa jumatatu? Ina maana Bakwata imeacha kufanya kazi ya Mungu sasa inafanya kazi kuifurahisha serikali.
Tulia kwa umakini angalia utendaji wa Bakwata utaelewa nasema nini, hili la eid nimekupa kama dondoo tu.

Eid al-Fitr: Saudi Arabia declares Sunday first day
Screenshot_2017-06-25-08-06-29.png
Screenshot_2017-06-25-08-06-43.png
Screenshot_2017-06-25-08-06-02.png

Unayo wewe !?
 
Karne ya 22 ni kesho tu, nyie bado mpo karne ya 4! , mnapanga kwa kuangalia mwezi!! Loh, Gari hili la vilaza silipandi.
 
Bakwata wako kama branch ya CCM ndio maana mdau kasema hivyo hapo juu.

Nakupa mfano, Eid hii mwezi umeshaandama jana jioni (24/06/2017) ina maana Eid mosi ni leo ila Bakwata hawataki kutangaza kwa kua katika sherehe hii kuna viongozi wa kisiasa wameshaarikwa na wameambiwa eid ni jumatatu sasa wanaona wakisema ni leo itakuaje kwa bwana mkubwa wao aliyealikwa jumatatu? Ina maana Bakwata imeacha kufanya kazi ya Mungu sasa inafanya kazi kuifurahisha serikali.
Tulia kwa umakini angalia utendaji wa Bakwata utaelewa nasema nini, hili la eid nimekupa kama dondoo tu.

Eid al-Fitr: Saudi Arabia declares Sunday first day
View attachment 530246View attachment 530247View attachment 530248
Post yako inaonyesha kuna nchi ambazo hazikuona mwezi na zimetangaza jmtatu kuwa ni siku kuu ! Kuna tofauti gani na Bakwata ? ....swali la nyongeza, tukiona mwezi sisi East Africa, Saudi wanaweza kutufuata ? Kama jibu ni hapana, kwanini sisi tuwajibika kuwafuata hali ya kuwa mwezi jaukuonekana ?

Sent from my Infinix HOT 4 using JamiiForums mobile app
 
Karne ya 22 ni kesho tu, nyie bado mpo karne ya 4! , mnapanga kwa kuangalia mwezi!! Loh, Gari hili la vilaza silipandi.
Nyie mna akili sana ndo maana mnasheherekea Birthday ya Yesu mwezi na siku asokuwa amezaliwa ! Yaani ya uzushi. Hivi kuna akili gani kununua sanamu la Yesu dukani ?....mpo karne gani watu msiojua tofauti ya Mungu na sanamu ?!

Sent from my Infinix HOT 4 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom