Bakwata wapotoshaji:- dc kimario alivuliwa ushungi na sio hijabu

Paulo

JF-Expert Member
Jan 5, 2009
350
66
amani iwe kwenu great thinkers! Kwakweli huu upotoshaji ambao umekua ukifanywa na ccm kupitia majukwaa na vyombo vya habari na baaadae bakwata kuhusu suala na kukamatwa dc kimario inabidi tusiufumbiw macho bali tuupinge kwa nguvu zetu zote.

Kamaambavyo wengi wetu tulivyoshuhudia kweye picha jinsi dc alivyokamatwa ni kwamba kile kitambaa kidogo (ushungi) alichokua amejitanda usoni ndicho kilichomvuka na sii hijabu ambalo hutanda mwili mzima kama gauni.

Kile kitambaa kilimficha uso ili asitabulike baada ya kufanya ouvu wa kupiga kampeni za ndani hivyo ikabidi kile kitambaa kisogezwe ili uso uonekane na apigwe picha.

Hivyo ningependa kwa niaba ya wote wanaotakia mema na amani ya nchi hii kupinga upotoshaji wa dhahiri uliofanywa na baraza la maulamaa kusema eti kimario alivuliwa hijab badala ya ushungi. Wakiwa kama viongozi wa dini wafahamu kua kunena uongo ni dhambi na hata kurubuniwa na ccm ili kupenyeza uchochezi huu ni dhambi pia.

Mungu ibariki tanzania. Mungu ilinde chadema dhidi ya uongo huu unaoenezwa na taasisi ya kidini
.
 
ndugu zetu mara nyingi maamuzi yao ni jazba tu, hakuna evidence kama alivuliwa hijabu anaoekana kashika ushungi mkononi, ok la pili kama kuvuliwa hijabu ni kuivua dini je hao wanaobaka,wanalawiti na dhambi nyinginezo nao tuseme wanabaka dini au kulawiti dini tena wao kwa wao? mm nawashangaa badala ya kukaa kujadili maendeleao ya nchi,uhaba wa umeme,njaa,nk wao wanajadili chadema iombe radhi afu iweje? ndugu zetu amkeni waarabu walioleta dini wao wana mafuta sio maskini nanyi piganieni hali zenu kimaisha, mmemchagua mwenzenu kawatiia kitanzi cha umaskini kuna mlofaidika? tuangalie mustakbali wa nchi kwa sasa iman ibakie kuwa suala binafsi, yawezekana anaepiga kelele za ushungi ana dhambi kibao anayafunika kwa vile hatuoni, waza maendeleo kwa faida ya vizazi vyenu,,,,,
 
ccm imeanda mpango wote huo ili chadema wasipate kura za waislam na wanawake eti wamedhalilishwa!jana nimemsikia mbunge wa viti maalumu ccm-ms madabida analalamika kwa nini vyama vya kutetea haki za binadamu hazijalaani kitendo kile!
 
amani iwe kwenu great thinkers! Kwakweli huu upotoshaji ambao umekua ukifanywa na ccm kupitia majukwaa na vyombo vya habari na baaadae bakwata kuhusu suala na kukamatwa dc kimario inabidi tusiufumbiw macho bali tuupinge kwa nguvu zetu zote.

Kamaambavyo wengi wetu tulivyoshuhudia kweye picha jinsi dc alivyokamatwa ni kwamba kile kitambaa kidogo (ushungi) alichokua amejitanda usoni ndicho kilichomvuka na sii hijabu ambalo hutanda mwili mzima kama gauni.

Kile kitambaa kilimficha uso ili asitabulike baada ya kufanya ouvu wa kupiga kampeni za ndani hivyo ikabidi kile kitambaa kisogezwe ili uso uonekane na apigwe picha.

Hivyo ningependa kwa niaba ya wote wanaotakia mema na amani ya nchi hii kupinga upotoshaji wa dhahiri uliofanywa na baraza la maulamaa kusema eti kimario alivuliwa hijab badala ya ushungi. Wakiwa kama viongozi wa dini wafahamu kua kunena uongo ni dhambi na hata kurubuniwa na ccm ili kupenyeza uchochezi huu ni dhambi pia.

Mungu ibariki tanzania. Mungu ilinde chadema dhidi ya uongo huu unaoenezwa na taasisi ya kidini
.

Kama sikosei ni walewale waliozusha mwaka jana kuwa Kanisa Katoliki Tanzania lina jeshi linaitwa the Commission for Armed Forces na wakaiomba serikali kulitolea kauli suala hilo. Nijuavyo mimi the Commission for Armed Forces ni huduma ya kiroho (kama zilivyohuduma zingine mfano, Commission For Aids, Commission for Relief Aid, Commission for Justice and Peace etc) itolewayo kwa askari Wakatoliki wanajeshi/polisi/magereza wanaohitaji - mfano misa na ushauri mbalimbali wa mambo ya kiroho na utaratibu mwingineo wanaoukosa katika huduma za kawaida maparokiani kulingana na kazi zao. Lakini hawa jamaa hawajawahi kuthibitisha hilo jeshi liko 'based' wapi na kamanda wake ni nani au lina'recruit' akina nani na mafunzo wanapata wapi na kwa ajili gani - ya kumlinda Pengo, mapadre au nini!

Ni kweli viongozi wa dini wanapoanza kushabikia uwongo na kuhubiri uwongo basi kuna tatizo kubwa! Ni aibu kubwa!
 
Binafsi nashangaa kwani HIJAB ninayoielewa si kile kitambaa cha ushungi alichotumia huyu Dc fatma,alikuwa anaficha sura ili asitambulike na ndio maana hakuandamana na askari polisi kwa kuwa alikuwa akitimiza kazi haramu ya 'comisioner chakachua manifesto'
 
Hizi hoja za hawa ndugu zetu zimekuwa zikitolewa kwa jazba na watu wasio na mapenzi mema na mustakabali wa nchi.Ila hii sumu ya udini wanaoing'ang'ania itawatafuna sana wao wenyewe mwisho wa siku kwa kuwa upeo wa hao wanaoshabikia ni mdogo sana katika kupambanua mambo.
 
Back
Top Bottom