Bakhresa kwa Makonda, Mwakyembe na Tido, na Nilichojifunza Binafsi

pinno

JF-Expert Member
Jan 17, 2013
1,213
1,228
Kuna video nimeiona, nashindwa tu kuiweka hapa,

ila watanisaidia wenye nayo, maana ipo sana tu mtandaoni,

inamuonesha Mzee SSB, akiingia msibani, kwenye msiba wa wafanyakazi watano wa Azam Media, kuelekea kiti kwake, anampita Katibu wa CCM ndugu Polepole, anampita Rc wa Dar es salaam, almaarufu kama mungu wa Dar, DAB, Makonda, anampita waziri mwenye dhaman na michezo habari na burudani, Mhe Mwakyembe, anasogea kwenye kiti chake anakaa, anampa mkono mzee wa pembeni yake ambaye, sura sio ngeni ila sijamtambua vizuri.

Na anaendelea na taratibu nyingine, wakati huo huo, jicho la kamera, linamtazama Mhe Mwakyembe, na Makonda, ni kama vile wanataka kutoa mkono wa pole kwa mzee, wasalimiane nae, ila wanaona tena kama itifaki itakuwa haijakaa sawa, basi wanabaki wasijue la kufanya, na yeye ni kama vile hana taimu nao, au ukute hata hajawajua. (Inawezekana kabisa akawa hawajui)

Mara anakuja Tiddo, ambaye ni mwajiriwa wake, kama Mkurugenzi wa Azam media ,mzee anasimama anamsalimia Tiddo kwa adabu na heshima.

My take :

1. Mzee anathamini Wafanyakazi wake, na kuwashobokea hao, zaidi ya viongozi wa kisiasa, ambao kwa kawaida mabosi wengi mtaani wangefanya kinyume na hapo,

2. Mzaa yupo busy na mambo yake, na hivi Magu anabadilisha badilisha mawazir na wakuu wa mikoa, ukute jamaa hata hajui in person wazir wa michezo ni nani, watu wake wanajua, kampuni zake zinajua, ila yeye in person hana muda wa kufuatilia hayo na hayana umuhimu kwake.

3. Anapenda kuishi kawaida sana
 
IMG-20190712-WA0016.jpg

😂😂
 
Hahahaa! ukiwa tajiri,lolote utakalofanya utasifiwa tu,ingekua masikini ndio kafanya hivyo,angetupiwa kila aina ya matusi,angeonekana ana dharau pia,mfanyabiashara kama Bakhresa ni lazima awe anawajua hao viongozi,wafanya biashara hufuatilia kwa ukaribu sana mambo ya siasa na uongozi kwani yana impact kubwa sana kwenye biashara zao.
 
Fact
Hahahaa! ukiwa tajiri,lolote utakalofanya utasifiwa tu,ingekua masikini ndio kafanya hivyo,angetupiwa kila aina ya matusi,angeonekana ana dharau pia,mfanyabiashara kama Bakhresa ni lazima awe anawajua hao viongozi,wafanya biashara hufuatilia kwa ukaribu sana mambo ya siasa na uongozi kwani yana impact kubwa sana kwenye biashara zao.
 
Bashite hapo yupo like what...huyu mzee ananipita bila kunipa mkono hanijui mi nani?

Mzee nimependa maisha yake,pia naona ana busara mno maana hata wanae licha ya kusoma vyuo vya ughaibuni.maisha mazuri.investment za kila aina.Nyumba za kifahari na kupangilia migari ya kila aina hawana kelele kabisa.yani mtoto wa bakhresa umkite anapigana na kulumbana na mtu halafu anauliza "unanijua mi nani*?
 
Hahahaa! ukiwa tajiri,lolote utakalofanya utasifiwa tu,ingekua masikini ndio kafanya hivyo,angetupiwa kila aina ya matusi,angeonekana ana dharau pia,mfanyabiashara kama Bakhresa ni lazima awe anawajua hao viongozi,wafanya biashara hufuatilia kwa ukaribu sana mambo ya siasa na uongozi kwani yana impact kubwa sana kwenye biashara zao.

Yeye binafsi hafuatilii, ila amemuajiri Tiddo ili afuatilie, hapo vipi?
 
Kuna video nimeiona, nashindwa tu kuiweka hapa,

ila watanisaidia wenye nayo, maana ipo sana tu mtandaoni,

inamuonesha Mzee SSB, akiingia msibani, kwenye msiba wa wafanyakazi watano wa Azam Media, kuelekea kiti kwake, anampita Katibu wa CCM ndugu Polepole, anampita Rc wa Dar es salaam, almaarufu kama mungu wa Dar, DAB, Makonda, anampita waziri mwenye dhaman na michezo habari na burudani, Mhe Mwakyembe, anasogea kwenye kiti chake anakaa, anampa mkono mzee wa pembeni yake ambaye, sura sio ngeni ila sijamtambua vizuri.

Na anaendelea na taratibu nyingine, wakati huo huo, jicho la kamera, linamtazama Mhe Mwakyembe, na Makonda, ni kama vile wanataka kutoa mkono wa pole kwa mzee, wasalimiane nae, ila wanaona tena kama itifaki itakuwa haijakaa sawa, basi wanabaki wasijue la kufanya, na yeye ni kama vile hana taimu nao, au ukute hata hajawajua. (Inawezekana kabisa akawa hawajui)

Mara anakuja Tiddo, ambaye ni mwajiriwa wake, kama Mkurugenzi wa Azam media ,mzee anasimama anamsalimia Tiddo kwa adabu na heshima.

My take :

1. Mzee anathamini Wafanyakazi wake, na kuwashobokea hao, zaidi ya viongozi wa kisiasa, ambao kwa kawaida mabosi wengi mtaani wangefanya kinyume na hapo,

2. Mzaa yupo busy na mambo yake, na hivi Magu anabadilisha badilisha mawazir na wakuu wa mikoa, ukute jamaa hata hajui in person wazir wa michezo ni nani, watu wake wanajua, kampuni zake zinajua, ila yeye in person hana muda wa kufuatilia hayo na hayana umuhimu kwake.

3. Anapenda kuishi kawaida sana
Komredi Polepole alitimba msibani na jezi ya Lumumba FC?!

Nauliza tu!
 
Huyu mzee ni kama kastaafu shughuli zake.miradi yote kawaachia wanae kwa sasa.
Mi nahisi hivo
Hahahaa! ukiwa tajiri,lolote utakalofanya utasifiwa tu,ingekua masikini ndio kafanya hivyo,angetupiwa kila aina ya matusi,angeonekana ana dharau pia,mfanyabiashara kama Bakhresa ni lazima awe anawajua hao viongozi,wafanya biashara hufuatilia kwa ukaribu sana mambo ya siasa na uongozi kwani yana impact kubwa sana kwenye biashara zao.
 
Huyu mzee ni mtu aliyeanza ALIF kwa kijiti. Alikuwa na kaduka kaa kuuza viatu, akaanzisha machine ndogo za kawaida za ice cream za kons. Miaka ya early 80s Kaka yangu alikuwa anafanya kazi Abu Dhabi, alishakutana naye kwenye ndege ya Air Tz, akiwa amebeba maboxi ya cons za ice cream.

Pesa zake kazitengeneza kwa jitihada nyingi na subira, kwa hivyo hawezi kuwa na woga wa wanasiasa, na katika globalization ya leo, kesha jijenga vizuri sana, hatishiki.

Pia ni mtu muungwana sana, hapendi majivuno,anasaidia masikini na wanyonge, mpenda haki
 
Back
Top Bottom