nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
• Barabara, reli, umeme, madini, kuikomboa nchi
na Asha Bani
KAMBI ya Upinzani Bungeni imetoa vipaumbele sita vya mchanganuo wa bajeti mbadala watakayoiwasilisha katika Bunge la Bajeti litakaloanza Juni 7, mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za Bunge, Naibu Katibu Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Christina Lissu Mughwai, alisema kipaumbele cha kwanza katika bajeti hiyo kitaelekezwa kwenye miundombinu.
Alisema kipengele cha pili katika hotuba ya bajeti hiyo itakayotolewa na Waziri Kivuli wa Fedha, Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu Kiongozi wa kambi hiyo ni umeme.
Alisema katika miundombinu wataweka msisitizo kwenye barabara zote muhimu ambazo hazijaanza ili zinze kuanzia mwaka huu wa fedha pamoja na upanuzi wa Bandari ya Mtwara.
Alisema wataboresha Reli ya Kati ili iweze kufanya kazi ya kusafirisha mizigo na abiria kwa kiwango cha kuridhisha mpaka hapo fedha za kujenga reli mpya itakapopatika pamoja na Shirika la Ndege la Taifa liweze kuongezewa mtaji wa kulifufua hatimaye lijiendeshe kibiashara na kwa ufanisi zaidi.
Kuhusu kipaumbele cha umeme alisema wataangalia umeme wa makaa ya mawe 1500MW (Souther power complex) migodi ya Mchuchuma, Ngaka na Kiwira, umeme wa gesi (Mtwara gas pipeline) 300 MW kutoka Mtwara, Dar es Salaam hadi Mwanza kwa kutumia PPP kati ya wawekezaji binafsi na NSFF.
"Pia kutakuwa na mradi kabambe wa kusafirisha na kusambaza umeme mijini na vijijini chini ya TANESCO na REA (Rural Energy Agency)," alisema Christina.
Alisema kipaumbele cha tatu ni kuwezesha ukuaji wa sekta za uzalishaji na hasa ukuaji wa uchumi wa vijijini kwa kuboresha miundombinu, upatikanaji wa maji safi na salama sambamba na kuongeza ubora wa bidhaa za kilimo na kupeleka umeme vijijini.
Kipaumbele cha nne ni kusimamia maendeleo ya rasilimali watu, kuwekeza kwenye ubora wa elimu, huku akieleza watahakikisha watoto wanaomaliza kidato cha nne wanapata mafunzo ya ufundi ili waweze kujiajiri wanaporudi vijijini.
Alieleza bodi ya mikopo ya elimu ya juu inapata fedha za kutosha kutoka kodi ya uendelezaji ujuzi na kwamba 2/3 ya kodi hiyo ambayo inakwenda Hazina ibaki kwenye bodi ili kukidhi mahitaji ya mikopo.
"Kimsingi lengo la bajeti yetu katika elimu ni kupata elimu bora na si wingi wa majengo ya shule ama wanafunzi wanaomaliza shule na kuanzisha pensheni kwa wazee wote wenye umri zaidi ya miaka 60," alisema Christina.
Alisema wataanzisha pia bima ya afya kwa wananchi wote itakayokuwa ya lazima kwa watu wote, wafanyakazi na wasio wafanyakazi na ichangiwe na wananchi wenyewe pamoja na serikali. Alisema kipaumbele cha tano ni kuimarisha utawala bora na katika hilo wanapendekeza kuwepo na fedha za kuwezesha mchakato wa kuandika katiba mpya ili Watanzania wote waweze kushiriki mchakato wa katiba mpya.
Wataimarisha pia TAKUKURU kwa kuanzisha kitengo maalumu kwa ufisadi mkubwa sambamba na mfumo mpya wa kudhibiti mgongano wa maslahi, wafanyabiashara wanaruhusiwa kisheria kuwa wanasiasa ili mradi kusiwe na mgongano wa kimasilahi, kuwe na uwazi wa kutangaza mali za kiongozi.
Pia kuanzisha ofisi ya bajeti ya Bunge ili kuweka uwazi zaidi kwenye bajeti ya serikali ambapo kwa sasa wabunge hawahusishwi katika kupanga bajeti ya serikali, tunapendekeza itungwe sheria ya bajeti itakayowezesha kuanzishwa kwa ofisi ya bajeti, ikiwa ni pamoja na kuweka mazingira mazuri ya watu kufanya biashara na kupunguza urasimu katika ngazi mbalimbali," alisema Christina.
Katika kipaumbele cha sita ni kuimarisha usimamizi wa mashirika ya umma kwa kuanzisha Office of Public Enterprises, CHC kusimamia hisa za mashirika yote ya umma yaliyobinafsishwa kama kampuni mama.
Katika kuzingatia hilo kambi hiyo pia itaanzisha ‘National Investiment Fund' kwa ajili ya kutoa mitaji kwa mashirika ya umma na mapato yake kutokana na asilimia ya faida za mashirika inayokwenda kwenye bajeti.
Pia kusimamia matumizi ya fedha za royalty (mrabaha) kutoka kwenye madini na mafuta na kuanzisha mamlaka ya mafuta na kuibadili TPDC kuwa shirika la kibiashara na mafuta (Petrotan) na Shirika la Gesi (TanGas).
Katika hotuba yake Zitto ataainisha vyanzo vipya vya mapato na kuboresha vilivyopo katika mchanganuo wa kupunguza bei ya mafuta kwa asilimia 40.
Alisema vyanzo vingine vya mapato vitakuwa katika kusimamia kupanua wigo wa kodi kwa kuweka lengo la kukusanya mapato ya ndani sawa na 20% ya pato la taifa na kuongeza wigo wa walipa kodi.
Katika vyanzo hivyo vya mapato pia vitaangalia mfumo mpya wa utawala wa kodi, mfano makampuni yanayofanya kazi hapa nchini lakini yamesajiliwa nje na hivyo wanalipa kodi huko walikosajiliwa.
Kufuta kodi ya presumptive ambayo inasababisha makampuni madogo (SME) yasijisajili kwani hiyo inasababisha ukwepaji kodi katika sekta isiyo rasmi.
Atapunguza pia exemptions (misamaha ya kodi) mpaka asilimia 1% ya pato la taifa kutoka 4.5 ya sasa, sambamba na kufuta sitting allowance na kupunguza matumizi yasiyo na maana kwenye maofisi. Alieleza kuwa kodi ya mapato kwa makampuni yote yatakayojisajili katika soko la mitaji kuwa ni 20% na 25% ya PAYE zibaki kwenye halmashauri husika badala ya kupeleka zote TRA. Mashirika ambayo serikali ina hisa yajisajili katika Soko la Mitaji (DSE) ili hisa za serikali ziweze kuuzwa na kuweka sheria kali za kuzuia ukwepaji kodi kwa mashirika makubwa ya nje na hasa kampuni za madini na mafuta.
na Asha Bani
KAMBI ya Upinzani Bungeni imetoa vipaumbele sita vya mchanganuo wa bajeti mbadala watakayoiwasilisha katika Bunge la Bajeti litakaloanza Juni 7, mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za Bunge, Naibu Katibu Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Christina Lissu Mughwai, alisema kipaumbele cha kwanza katika bajeti hiyo kitaelekezwa kwenye miundombinu.
Alisema kipengele cha pili katika hotuba ya bajeti hiyo itakayotolewa na Waziri Kivuli wa Fedha, Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu Kiongozi wa kambi hiyo ni umeme.
Alisema katika miundombinu wataweka msisitizo kwenye barabara zote muhimu ambazo hazijaanza ili zinze kuanzia mwaka huu wa fedha pamoja na upanuzi wa Bandari ya Mtwara.
Alisema wataboresha Reli ya Kati ili iweze kufanya kazi ya kusafirisha mizigo na abiria kwa kiwango cha kuridhisha mpaka hapo fedha za kujenga reli mpya itakapopatika pamoja na Shirika la Ndege la Taifa liweze kuongezewa mtaji wa kulifufua hatimaye lijiendeshe kibiashara na kwa ufanisi zaidi.
Kuhusu kipaumbele cha umeme alisema wataangalia umeme wa makaa ya mawe 1500MW (Souther power complex) migodi ya Mchuchuma, Ngaka na Kiwira, umeme wa gesi (Mtwara gas pipeline) 300 MW kutoka Mtwara, Dar es Salaam hadi Mwanza kwa kutumia PPP kati ya wawekezaji binafsi na NSFF.
"Pia kutakuwa na mradi kabambe wa kusafirisha na kusambaza umeme mijini na vijijini chini ya TANESCO na REA (Rural Energy Agency)," alisema Christina.
Alisema kipaumbele cha tatu ni kuwezesha ukuaji wa sekta za uzalishaji na hasa ukuaji wa uchumi wa vijijini kwa kuboresha miundombinu, upatikanaji wa maji safi na salama sambamba na kuongeza ubora wa bidhaa za kilimo na kupeleka umeme vijijini.
Kipaumbele cha nne ni kusimamia maendeleo ya rasilimali watu, kuwekeza kwenye ubora wa elimu, huku akieleza watahakikisha watoto wanaomaliza kidato cha nne wanapata mafunzo ya ufundi ili waweze kujiajiri wanaporudi vijijini.
Alieleza bodi ya mikopo ya elimu ya juu inapata fedha za kutosha kutoka kodi ya uendelezaji ujuzi na kwamba 2/3 ya kodi hiyo ambayo inakwenda Hazina ibaki kwenye bodi ili kukidhi mahitaji ya mikopo.
"Kimsingi lengo la bajeti yetu katika elimu ni kupata elimu bora na si wingi wa majengo ya shule ama wanafunzi wanaomaliza shule na kuanzisha pensheni kwa wazee wote wenye umri zaidi ya miaka 60," alisema Christina.
Alisema wataanzisha pia bima ya afya kwa wananchi wote itakayokuwa ya lazima kwa watu wote, wafanyakazi na wasio wafanyakazi na ichangiwe na wananchi wenyewe pamoja na serikali. Alisema kipaumbele cha tano ni kuimarisha utawala bora na katika hilo wanapendekeza kuwepo na fedha za kuwezesha mchakato wa kuandika katiba mpya ili Watanzania wote waweze kushiriki mchakato wa katiba mpya.
Wataimarisha pia TAKUKURU kwa kuanzisha kitengo maalumu kwa ufisadi mkubwa sambamba na mfumo mpya wa kudhibiti mgongano wa maslahi, wafanyabiashara wanaruhusiwa kisheria kuwa wanasiasa ili mradi kusiwe na mgongano wa kimasilahi, kuwe na uwazi wa kutangaza mali za kiongozi.
Pia kuanzisha ofisi ya bajeti ya Bunge ili kuweka uwazi zaidi kwenye bajeti ya serikali ambapo kwa sasa wabunge hawahusishwi katika kupanga bajeti ya serikali, tunapendekeza itungwe sheria ya bajeti itakayowezesha kuanzishwa kwa ofisi ya bajeti, ikiwa ni pamoja na kuweka mazingira mazuri ya watu kufanya biashara na kupunguza urasimu katika ngazi mbalimbali," alisema Christina.
Katika kipaumbele cha sita ni kuimarisha usimamizi wa mashirika ya umma kwa kuanzisha Office of Public Enterprises, CHC kusimamia hisa za mashirika yote ya umma yaliyobinafsishwa kama kampuni mama.
Katika kuzingatia hilo kambi hiyo pia itaanzisha ‘National Investiment Fund' kwa ajili ya kutoa mitaji kwa mashirika ya umma na mapato yake kutokana na asilimia ya faida za mashirika inayokwenda kwenye bajeti.
Pia kusimamia matumizi ya fedha za royalty (mrabaha) kutoka kwenye madini na mafuta na kuanzisha mamlaka ya mafuta na kuibadili TPDC kuwa shirika la kibiashara na mafuta (Petrotan) na Shirika la Gesi (TanGas).
Katika hotuba yake Zitto ataainisha vyanzo vipya vya mapato na kuboresha vilivyopo katika mchanganuo wa kupunguza bei ya mafuta kwa asilimia 40.
Alisema vyanzo vingine vya mapato vitakuwa katika kusimamia kupanua wigo wa kodi kwa kuweka lengo la kukusanya mapato ya ndani sawa na 20% ya pato la taifa na kuongeza wigo wa walipa kodi.
Katika vyanzo hivyo vya mapato pia vitaangalia mfumo mpya wa utawala wa kodi, mfano makampuni yanayofanya kazi hapa nchini lakini yamesajiliwa nje na hivyo wanalipa kodi huko walikosajiliwa.
Kufuta kodi ya presumptive ambayo inasababisha makampuni madogo (SME) yasijisajili kwani hiyo inasababisha ukwepaji kodi katika sekta isiyo rasmi.
Atapunguza pia exemptions (misamaha ya kodi) mpaka asilimia 1% ya pato la taifa kutoka 4.5 ya sasa, sambamba na kufuta sitting allowance na kupunguza matumizi yasiyo na maana kwenye maofisi. Alieleza kuwa kodi ya mapato kwa makampuni yote yatakayojisajili katika soko la mitaji kuwa ni 20% na 25% ya PAYE zibaki kwenye halmashauri husika badala ya kupeleka zote TRA. Mashirika ambayo serikali ina hisa yajisajili katika Soko la Mitaji (DSE) ili hisa za serikali ziweze kuuzwa na kuweka sheria kali za kuzuia ukwepaji kodi kwa mashirika makubwa ya nje na hasa kampuni za madini na mafuta.