Bajeti ya Tanzania ya Kambi ya Upinzani Wizara ya Fedha kwa mwaka wa fedha 2016/2017

CCM itabidi waitane Kikao cha dharura.......Ila Kabudi kashawajibu pale juu watakuwa wanajuta muda huu .......
 
Wapi wametetea kufuta posho. Tunakumbuka Lema alivyomlalua ZZK kusema haitaji posho. Unakumbuka Msigwa alisema kazi yake kule ni kuchukuwa posho.

Sasa leo ndo wameenda kutete uongo?

Pia, ahadi yao ni kuwa hawatashiuriki vikao na ni nini kimewapeleka?

Sasa Kama mpaka hapo nimekuquote na hotuba ujaelewa , nakusaidiaje?Soma hotuba kwanza Acha kutoa mapovu
 
Sio kila kitu kinakosolewa ,hii budget ya wapinzani ipo shallow

Ni kweli kabisa pale unapoamua kununua ndege kuku kwa bei ya ndege Mpya hakika wapinzani hawatufai kabisa hawa.Kama wanaweza kuligundua hili.Yaani badala ya wao kwenda kununua ndege wanaleta za kuleta oh ndege Nyumba sasa si wao wanunue mpya tu,jamani.??
 
How?Kwa facts zile unasema iko shallow?Wanakuonyesha mpaka vitabu vinavyosema?Tofauti za figure na kila kitu?Soma kwanza utachangia tu hapa tena in a competent way?Kipi kipo shallow?
Achana naye hawa ni wale watoto wa baba,hata akiambiwa baba anamaliza pesa kwa ulevi hawatakuelewa
 
Mambo ya Msingi unaleta Umbea " Mheshimiwa Spika, kabla sijatoa maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani kuhusu bajeti ya Serikali ya 2016/17, napenda kuweka rekodi sawa kuhusu upotoshaji unaofanywa na Wabunge wa CCM kwamba Bungee wa Upinzani wanaisaini mahudhurio bungeni na kuchukua posho bila kufanya kazi.

Napenda mkumbuke kwamba, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imekuwa ikisisitiza kufutwa kwa posho za vikao kwa maana ya “Sitting allowance”, lakini serikali imekuwa ikipata kigugumizi, hivyo basi Kambi Rasmi inasema kama kweli Serikali ya Rais John Pombe Magufuli inania thabiti ya kubana matumizi ya Serikali basi inoneshe uthabiti huo kwa kuifuta posho ya vikao na fedha hizo zipelekwe kwenye miradi ya maendeleo hususani kuwapatia Watanzania maji safi na salama.

Hata hivyo, tunashauri, wale wanaokaa bungeni bila kuchangia hata kwa maandishi na kuchukua posho, wafuatiliwe na wakatwe mishahara yao, kwa kuwa hawajafanya kazi na hansard itumike kuwabaini" umewasikia acha uvivu soma kwanza pu
Mambo ya Msingi unaleta Umbea " Mheshimiwa Spika, kabla sijatoa maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani kuhusu bajeti ya Serikali ya 2016/17, napenda kuweka rekodi sawa kuhusu upotoshaji unaofanywa na Wabunge wa CCM kwamba Bungee wa Upinzani wanaisaini mahudhurio bungeni na kuchukua posho bila kufanya kazi.

Napenda mkumbuke kwamba, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imekuwa ikisisitiza kufutwa kwa posho za vikao kwa maana ya “Sitting allowance”, lakini serikali imekuwa ikipata kigugumizi, hivyo basi Kambi Rasmi inasema kama kweli Serikali ya Rais John Pombe Magufuli inania thabiti ya kubana matumizi ya Serikali basi inoneshe uthabiti huo kwa kuifuta posho ya vikao na fedha hizo zipelekwe kwenye miradi ya maendeleo hususani kuwapatia Watanzania maji safi na salama.

Hata hivyo, tunashauri, wale wanaokaa bungeni bila kuchangia hata kwa maandishi na kuchukua posho, wafuatiliwe na wakatwe mishahara yao, kwa kuwa hawajafanya kazi na hansard itumike kuwabaini" umewasikia acha uvivu soma kwanza pu
Kuna watu hawasomi wanaropoka tuu, mdee ni sawa na wabunge kumi wa ccm based on mind power
 
Mkuu
Ni kweli kabisa pale unapoamua kununua ndege kuku kwa bei ya ndege Mpya hakika wapinzani hawatufai kabisa hawa.Kama wanaweza kuligundua hili.Yaani badala ya wao kwenda kununua ndege wanaleta za kuleta oh ndege Nyumba sasa si wao wanunue mpya tu,jamani.??
Mkuu sasa unataka watuletee ndege zenye mdondo, ndani ya mwaka tuu zife, hv hata wewe mkeo hakimuagizia mtoto wako gari used kwa bei ya gari mpya utanyamaza tuu na kumuacha haiagize?
 
nimesoma bajeti yote lakini sijaona kambi rasmi ya upinzani ikishauri au kutoa mawazo mbadala juu ya vyanzo vipya vya mapato,mbali na kodi ongezo kwenye vinywaji n.k
inamaana kambi rasmi ya upinzani imeridhika na vyanzo hivyo vya mapato??

sema hujasoma ujaelewa umecomment tu
 
Ni kweli kabisa pale unapoamua kununua ndege kuku kwa bei ya ndege Mpya hakika wapinzani hawatufai kabisa hawa.Kama wanaweza kuligundua hili.Yaani badala ya wao kwenda kununua ndege wanaleta za kuleta oh ndege Nyumba sasa si wao wanunue mpya tu,jamani.??
Mbona hueleweki? Yaani wapinzani waende wakanunue Ndege? Badala ya kukemea halafu ya ufisadi katika mchakato mzima wa ununuzi wa hizo Ndege ambao unaenda kufanyika, kutoka katika serikali ya hapa kazi tu inayojumulisha na ufisadi ndani yake. Naona Yale ya MV Bagamoyo yanaenda kujirudia tena.
 
Hii ndio budget mbadala?
Mbona sio walipo eleza vyanzo vipya vya mapato ambavyo tunge vitumia na kuachana na pombe na sigara?

Halafu hii hotuba wamesoma bungeni au wameitoa on line?

Kusema viinua Mgongo vya pensheni ya Wastaafu zikatwe kodi Sio mbadala, kuimarisha matangazo ya Utalii Katika baadhi ya nchi tupate watalii mil 5 Sio mbadala, pale Kurasini kuja bidhaa kutoka China Sio mbadala?Au maana ya mbadala ni nini? Yaani we jamaa nimwepesi balaaaaaa
 
Nimeangalia haraka haraka kiasi mifuko ya jamii ilichoikopesha serikali na kiasi kilicholipwa, inaelekea NSSF marejesho kutoka serikalini yalikuwa mazuri kuliko mifuko mingine japo sawa wao ndio walikopesha nyingi.
Je, inawezekana hapa pesa zililipwa kwa vile wakandarasi wa miradi walikuwa na 'mahusiano mazuri' na hazina au 10% za wadau zilikuwa nyingi!? Natafakari tu.
 
Kumbe wakina Kitillya walitakiwa kushitakiwa watu 11 lakini wamepelekwa Mahakamani watu 3, TAKUKURU mbona inafanya double standards ? Nchi haifuati utawala wa sheria ? Kunahitajika majibu ya kina.....

Kuhusu gesi kuingizia taifa shilingi Bilioni 115 katikabajeti ya mwaka huu , zile kelele kuwa uchumi wa gesi unaenda kuondoa umaskini wa mtanzania iko wapi? bora tuseme uchumi wa walevi ....lol maana wanachangia kuliko gesi na madini yote ...yaani dhahabu, Alimasi,Tanzanite,Makaa ya Mawe, Gesi, nk .......Aibu sana hii
 
Kumbe wakina Kitillya walitakiwa kushitakiwa watu 11 lakini wamepelekwa Mahakamani watu 3, TAKUKURU mbona inafanya double standards ? Nchi haifuati utawala wa sheria ? Kunahitajika majibu ya kina.....

Kuhusu gesi kuingizia taifa shilingi Bilioni 115 katikabajeti ya mwaka huu , zile kelele kuwa uchumi wa gesi unaenda kuondoa umaskini wa mtanzania iko wapi? bora tuseme uchumi wa walevi ....lol maana wanachangia kuliko gesi na madini yote ...yaani dhahabu, Alimasi,Tanzanite,Makaa ya Mawe, Gesi, nk .......Aibu sana hii

Big up bro Kwa kuisoma bajeti
 
Back
Top Bottom