Bajeti ya serikali sasa imenitoa tongotongo

Gibiba

Senior Member
Jun 22, 2016
114
27
Nianze kwa kuishukuru serikali ya rais Magufuli kwa kuthubutu kukabili miradi ya maendeleo kwa kutegemea vyanzo vya ndani.

Lakini zaidi niishukuru sana serikali kwa mara ya kwanza kuvunja rekodi kwa kutenga zaidi ya 40% ya bajeti hiyo kwa kuielekeza katika miradi ya maendeleo.

Hii tu ni ishara tosha kwamba ile dhana ya hapa kazi tu ni dhahiri kuwa ni elimu kwa vitendo na sii nadharia.Hapa Mh.rais "conglatulation"

Kikubwa nilichokibaini kwa watanzani ni genge kubwa la wakwepa kodi. Ikumbukwe kuwa kila kunapokucha mahitaji ya mtanzani yanaongezeka na itambulike kuwa vivyo hivyo gharama za maisha pia zitaongezeka.

Kwa watanzania wavivu na mawakala wa wakwepa kodi, hili limekuwa kinyume.

Binafsi nimeanza biashara tangu mwaka 2008 kama mjasiriamali mdogo na tangia hapo nimekuwa mlipa kodi mzuri na sikuona adha yeyote kwa maana natambua jasho langu ni sehemu muhimu katika ujenzi wa taifa. Hata hivyo viwango vya kodi vimeendelea kubadilika kila mwaka, mimi na wazalendo wengine tumeendelea kulipa kodi vizuri sambamba na hayo mabadiliko ya viwango vya kodi.

Kichekesho sasa ni kwa serikali ya hapa kazi,nimepata kugundua kuwa liko wimbi kubwa la watu hawakuwahi lipa kodi na hawako tayari kulipa kodi. Lakini kundi hili kwa tafiti tu za haraharaka ndio wa kwanza kupaza sauti kulia maisha magumu maana ni wavivu.

Kelele zimeibuka kila kona na hasa kwa wanasiasa ambao kazi yao ni kukimbizana na matukio.Hali hii pia imenifanya kugundua kumbe kundi kubwa la wenye nacho ndio walikuwa wakwepa kodi wakubwa, lakini zaidi walikuwa kwenye misamaha ya kodi isiyo na tija.

Viinua mgongo vya wanasiasa vilikuwa kwenye misamha ya kodi licha ya kwamba wao haohao ndio watunga sheria.Sasa sheria ni msumeno serikali ya hapa kazi tu imekuja na mifumo mipya ya ukusanyaji kodi.

Mawakala wa wakwepa kodi milango yao imefungwa, sasa ni kilio kila kona. mara ooo anabana demokrasia, mara ooo anaingilia mihimili mingine ya serikali na mengine makubwa kwamba yeye ni dictator uchwara.

Tungeyajua yoote haya kama sii umahiri wa Dr.Magufuli?Wako watu walikula kiulaini kwa kutegemea jasho la wenzao mf. wamiliki wa nyumba, MC na wengine. Sasa hivi wanalipa kodi licha ya kuwa wanalalamika.

Hivi ni kweli wao kutoza kodi kwa wapangaji ni halali lakini wao kutozwa na serikali sii halali?

Ndugu zangu! Ya Mungu mpeni Mungu na ya kaisari mwachieni kaisari.

Niwaombe watanzani wenzangu tujenge utamaduni wa kulipa kodi maana ni kitendo cha uzalendo na kwa kufanya hivyo utajijenga vyema kutumia cha kwako halali.

Na ukiujenga utamaduni huu, hutafikiri kuonewa na hali utaiona ya kawaida kabisa. Zaidi hapa ni kuthubutu na kumuunga mkono rais wetu katika mpango wa kulisukuma taifa kuufikia uchumi wa kati.

Sote tulipe kodi, tuache kulialia mitandaoni.
 
Kachukue buku saba
Unafanya biashara gani ww nani akujui
Udalali unaofanya ndo ulipe kodi
Jipendekeze labda utafikiriwa maana ujui unachokiongea
 
Kulipa kodi sio shida ila unalipa kodi ngapi? unapata tatu unalazimishwa kutumia nne uwiano wa maisha uko wapi?
 
Nakubaliana na dhana nzima ya ulipaji kodi lakini kodi za hovyo hovyo zinakera... unawezaje kulipishwa kodi kwa kuhifadhi fedha za mshahara bank wakati ulishakatwa PAYE... angalau ingekuwa ni bank inakatwa hiyo VAT afadhali maana wao wanaingiza through service fee... but bank hawataki kupoteza wanasukumia zigo kwa mteja pathetic
 
Umesema vyema sana, Kuna watanzania wamezaliwa mpaka wanastaafu hawajawahi kulipa kodi. Kodi ndio kipato cha serikali, na kama tunahitaji maendeleo lazima tukusanye kodi na kupambana na rushwa.
 
Kachukue buku saba
Unafanya biashara gani ww nani akujui
Udalali unaofanya ndo ulipe kodi
Jipendekeze labda utafikiriwa maana ujui unachokiongea
Kwan umejuaje kuwa sina biashara mkuu?
 
Kwan umejuaje kuwa sina biashara mkuu?
Wenye biashara wanaweza kuongea utumbo kama ww
Sikuiz kuna ongezeko la kodi linaitwa gross sales Kodi ya bishaa sio faida inakula hadi mtaji 30 percent
Kuna kitu kinaitwa rairway rav kwenye uingizaji wa magar
Kuna ongezeko la kodi asilimia 100 yani nenda TRA ulipe kodi ya mapato kwa mtaji wa milion 5 kodi milion2.5 + kwa mwaka bado frame bado wafanyakazi bado usafi ulinzi umeme maji maintanance bado marejesho bank
Ww udalali unakufaa ujui biashara
 
Wenye biashara wanaweza kuongea utumbo kama ww
Sikuiz kuna ongezeko la kodi linaitwa gross sales Kodi ya bishaa sio faida inakula hadi mtaji 30 percent
Kuna kitu kinaitwa rairway rav kwenye uingizaji wa magar
Kuna ongezeko la kodi asilimia 100 yani nenda TRA ulipe kodi ya mapato kwa mtaji wa milion 5 kodi milion2.5 + kwa mwaka bado frame bado wafanyakazi bado usafi ulinzi umeme maji maintanance bado marejesho bank
Ww udalali unakufaa ujui biashara
Kwa hiyo usipolipa kodi na hayo mengine yanakwepeka?mbona usiwatake matajiri wenye nyumba nao wasikutoze kodi ya frem?
 
Nakubaliana na dhana nzima ya ulipaji kodi lakini kodi za hovyo hovyo zinakera... unawezaje kulipishwa kodi kwa kuhifadhi fedha za mshahara bank wakati ulishakatwa PAYE... angalau ingekuwa ni bank inakatwa hiyo VAT afadhali maana wao wanaingiza through service fee... but bank hawataki kupoteza wanasukumia zigo kwa mteja pathetic

Kwani kabla ya hapo ulipokuwa unawekewa hela mshahara ulikuwa hukatwi pesa na bank. Na fikiri tatizo ni pia watanzania huwa hatupendi contracts/mkataba zetu kila mahala tunamwaga wino.

Na uhakika kabisa hujui mkataba wako na mtandao wa simu wako unalipishwa kwa staili gani na quality of services ipo je. Ila ulipoenda kununua hiyo namba yako ya simu hukuomba mkataba na wenda kabisa hujui wana ku bill vipi. Hata wakiamua kukata salio wala hujui kwa sababu hujui mkataba wako upo je.
 
Umesema vyema sana, Kuna watanzania wamezaliwa mpaka wanastaafu hawajawahi kulipa kodi. Kodi ndio kipato cha serikali, na kama tunahitaji maendeleo lazima tukusanye kodi na kupambana na rushwa.
mbona hamuelewek mnatetea nn?huyo aliestaaf mshahara wake haikua na makato ikiwemo kodi?acheni ujinga
 
Kwani kabla ya hapo ulipokuwa unawekewa hela mshahara ulikuwa hukatwi pesa na bank. Na fikiri tatizo ni pia watanzania huwa hatupendi contracts/mkataba zetu kila mahala tunamwaga wino.

Na uhakika kabisa hujui mkataba wako na mtandao wa simu wako unalipishwa kwa staili gani na quality of services ipo je. Ila ulipoenda kununua hiyo namba yako ya simu hukuomba mkataba na wenda kabisa hujui wana ku bill vipi. Hata wakiamua kukata salio wala hujui kwa sababu hujui mkataba wako upo je.


Umemuelewa lakin? Payee na mikataba vina uhusiano gani?
 
Mtoa mada umesema kweli lakini subiri matusi kutoka kwa vijana Wa mfalme Mbowe pale ufipa.


Ofisi ya chama tu imewashinda kujenga alafu wanataka kumfundisha kazi Magufuli!!!

Ama kweli Nyumbu ni Nyumbu tu ,kutoka tarangire hadi saadani.
 
Unajaribu kuwa mtabiri lakini natumia staha kwa kukwambia ni vyema ukauliza kuliko kubashiri kwanza ufahamu hakuna mkataba rasmi kati ya mtoa huduma na mtumiaji kuna kitu kinaitwa SLA nitafafanua SLA ni makubaliano ambayo huwa ni kipengele kidogo katika mkataba kinaitwa service level agreement ...hiki humpa mtoa huduma mamlaka ya bila taarifa kwa mpokea huduma Kubadili kwa tija gharama za utoaji huduma bila kuathiri sheria ya mamlaka ya simu na mawasiliano ya mwaka 2003 ingawaji sheria hiyo imeshafanyiwa marekebisho chungu nzima baada ya TCRA kuwa na mamlaka ya udhiti wa makampuni ya simu.

Turudi kwenye hoja yangu ambayo hukuijibu ya PAYE kukatwa kisha pesa hizo kabla sijazitumia nikatwe tena VAT badala ya bank kukatwa maana ndio mlaji.... kwa sasa hilo na reserve maana waziri wa fedha kupitia Mkurugenzi wa TRA wameshalitolea maelekezo kwa mabank. Bwana MkamaP pamoja na kula samaki uwezo wako wa kupambanua mambo haujakomaa!!!!
Kwani kabla ya hapo ulipokuwa unawekewa hela mshahara ulikuwa hukatwi pesa na bank. Na fikiri tatizo ni pia watanzania huwa hatupendi contracts/mkataba zetu kila mahala tunamwaga wino.

Na uhakika kabisa hujui mkataba wako na mtandao wa simu wako unalipishwa kwa staili gani na quality of services ipo je. Ila ulipoenda kununua hiyo namba yako ya simu hukuomba mkataba na wenda kabisa hujui wana ku bill vipi. Hata wakiamua kukata salio wala hujui kwa sababu hujui mkataba wako upo je.
 
Unajaribu kuwa mtabiri lakini natumia staha kwa kukwambia ni vyema ukauliza kuliko kubashiri kwanza ufahamu hakuna mkataba rasmi kati ya mtoa huduma na mtumiaji kuna kitu kinaitwa SLA nitafafanua SLA ni makubaliano ambayo huwa ni kipengele kidogo katika mkataba kinaitwa service level agreement ...hiki humpa mtoa huduma mamlaka ya bila taarifa kwa mpokea huduma Kubadili kwa tija gharama za utoaji huduma bila kuathiri sheria ya mamlaka ya simu na mawasiliano ya mwaka 2003 ingawaji sheria hiyo imeshafanyiwa marekebisho chungu nzima baada ya TCRA kuwa na mamlaka ya udhiti wa makampuni ya simu.

Turudi kwenye hoja yangu ambayo hukuijibu ya PAYE kukatwa kisha pesa hizo kabla sijazitumia nikatwe tena VAT badala ya bank kukatwa maana ndio mlaji.... kwa sasa hilo na reserve maana waziri wa fedha kupitia Mkurugenzi wa TRA wameshalitolea maelekezo kwa mabank. Bwana MkamaP pamoja na kula samaki uwezo wako wa kupambanua mambo haujakomaa!!!!

SLA -service level of agreement inaweza kuwa part ya mkataba ama isiwepo. SLA ni constraints ktk mkataba ila sio kwamba ni mkataba. SLA, kwa mfano inaweza sema kuwa Uptime iwe 99% ama 10%.
Mkataba ni makubaliano kati ya mtumiaji na mlaji. Naamini huu mkataba upo hata kama ni virtually, ama namna yoyote ile ama kwa maneno ama kwa niaba ya, huu mkataba upo.

Kwenye hoja yako ya awali ya PAYE. Nimekujibu virtually, lakini naona jibu hukuliona ngoja niliweke bayana kuwa, hata mwaka juzi kama PAYE yako ilikuwa inapitia bank ilikuwa inakatwa na BANK, kama ADD-ON services kwa bank. Yani ulipokuwa una draw PAYE yako ama kwa cashier ama kwa ATM PAYE yako ilikuwa inakatwa. Jua kwamba, iwe mwaka juzi miaka 10 iliyopita ulikuwa unakatwa, ila hii PAYE ilikuwa haikatwi tu enzi zile za dirishani.

Sasa kinachokuchanganya nafikiri ni kwanini serikali iidai bank kutoka PAYE yako ambayo imeshakatwa. Nafikiri ujaribu kuelewa demarcation. Demarcation ya PAYE yako ni peer-to-peer ndo inaishia, yani ya wewe na serikali. Lakini kwa vile bank wamefanya biashara na wewe kwa PAYE yako basi peer-to-peer ya bank na serikali ni mlinganyo tofauti. VAT sio point-to multpoint. Hapa ni kwamba, bank ina peers wawili bank-to-PAYE na bank-to-VAT ya serikali. Ama kwa namna nyingine hapa nikujaribu kusema ya kwamba kwa vile PAYE yako imeshakatwa kodi basi ukichukua hiyo pesa ukaenda kununua mihogo na viazi basi huyo mfanyabiashara hatakiwi kulipa VAT maana hiyo hela uliyolipa ilikuwa PAYE na imeshakatwa.

Jaribu kuiona service ya ATM ni product kama mihogo, na pia Bank ni muuza product mihogo ama viazi, put it in that way. Ni wazi hela PAYE yako ikiwa bank haikatwi, ila ukinunua product ya bank kama ATM kwa kuwidhdraw bank inakata pesa yako, kwa kuuzia bidhaa hiyo, na kwa vile wamekuuzia bidhaa basi bank anapaswa kupeleka 18% OUT of aliyokukata. Hili limetolowa maelezo sana na watu na viongozi wenyewe , naamini sihitaj kurudia rudia mziki ule ule.
 
Back
Top Bottom