Budget kubwa lakini hakuna maji hicho ni kitu gani? Zero minusIfikapo mwaka 2030 Shida ya maji safi na salama Tanzania huenda ikasalia kuwa historia | Bajeti mpya ya maji ya Rais Samia ni karibu mara tatu zaidi ya ile ya FY2020|21.
Rais Samia Suluhu Hassan kwenye bajeti yake ya maji ya kwanza ametenga jumla ya Tshs 589.4BL kwaajili ya Uchimbaji na Usambazaji wa maji safi na salama mjini na vijijini nchi nzima, bajeti hii ni sawa na ongezeko la 284% kutoka Tshs 207.5BL zilizotolewa kwaajili ya Uchimbaji na Usambazaji huo wa maji safi na salama FY2020|21,Bajeti hii ya Rais Samia ni karibu maratatu zaidi ya ile ya mtangulizi wake,
Kwakuwa Rais Samia Suluhu Hassan ni mwanamke na kwakuwa zaidi 80% ya wanaopata adha ya maji mjini na vijijini ni wanawake hatimaye rais huyu mnyenyekevu ameamua kwa vitendo " Kuwatua Ndoo Vichwani " wanawake wenzake kwa kutenga kiasi hiki kikubwa cha fedha kwaajili ya Uchimbaji na Usambazaji wa maji mjini na vijiji,kiasi hiki cha fedha ya maendeleo hakijawahi kutengwa na serikali yeyote tangu uhuru,Heko Rais Samia.
Wastani wa upatikanaji wa maji safi na salama mjini na vijini ni 79.15% huku mjini ikiwa ni 86% na vijijini ni 72.3% huku lengo la Serikali lilikuwa ni kufikia 85% mwaka 2025 na 90% ifikapo mwaka 2035 but kwa kasi hii ya Rais Samia ambapo thamani ya bajeti ya maji ya mwaka mmoja ya Rais Samia ni sawa na thamani ya miaka mitatu ya bajeti ya maji ya Serikali iliyofanya makisio hayo,kwa lugha rahisi kabisa " Mwaka mmoja wa maji wa Rais Samia ni sawa na miaka mitatu ya maji ya mtangulize wake " au 1:3 yaani malengo ya maji ya Miaka 10 kwenye Serikali iliyopita yatatekelezwa kwa miaka 3.3 tu na Rais Samia, Kama kuna mtu wa kuombewa zaidi kwa sasa Tanzania basi ni Rais Samia.
#Nchi yenu iko katika Uelekeo Sahihi zaidi pengine tangu kuasisiwa kwake,
VIVA SAMIA VIVA ||VIVA TANZANIA VIVA