Bajeti ya Kenya ni Tsh. Trilioni 78, Tanzania ni Tsh. Trilioni 34 na Uganda Tsh. Trilioni 30

Ndugu hicho siyo kigezo cha kiuchumi kuongezeka tarakimu ni uwezo na nchi kujiendesha yenyewe kwenye bajeti yake sisi bajeti yetu ni tegemezi
Hapana budget kwanza inategemea mapato unayokusanya, huwezi ukakusanya bill800 kwa mwezi ukategemea budget ya trillion 30 kwa mwaka, hakuna mfadhili popote duniani anaweza kukupatia ongezeko la budget yako trillion 10 hayupo, ni ukweli usio pingika kuwa awamu ya Magufuli ukusanyi wa mapato uliongezeka kupita awamu zote za nyuma hivyo budget kuongezeka pamoja na kuwa utegemezi ulikuwepo.

Tuna zunguka sana , kenya kwa mwezi ina kusanya zaidi ya trillion 4 za kitanzania, maana yake uwekezaji kenya ni mkubwa kuliko tz , wingi wa viwanda, wanauza bidhaa nyingi nje ya nchi kushinda tz, mazingira mazuri ya ufanyaji biashara , serikali inakusanya Kodi ipasavyo.

Hivi kweli Tanzania ukusanyi wa Kodi trillion 1.5 kwa mwezi ni Kodi kubwa hii? Tanzania sio nchi ya kukusanya kodi kidogo kiasi hiki huku tukilalamika eti wafanya biashara wanaonewa, kama tunataka kuendelea na kushindana na mataifa mengine lazima tubadili mtazamo na fikra , bado tuna fikra na uelewa mdogo kuhusu dunia inavyokwenda.
 
Hebu tuonyeshe budget ya mwaka 2015 ilikuwa kiasi gani tujue kama tumeenda mbele au tulirudi nyuma?
Magofool alikuwa anaandaa bajeti hewa. Jiulize kwanini wizara zilikuwa zinapewa chini ya 10% ya bajeti iiyopitishwa na bunge???
Kwanini alishindwa kuajiri au kupandisha mishahara na madaraja ya watumishi???
Kwanini deni la taifa limepanda???
WATANZANIA SIO WAJINGA.
 
Hiyo bajeti wao wanachangia kiasi gani na kiasi gani ni mikopo? Alafu wao wanaweka budget mpaka za mgao wa viongozi. Ufisadi na Mikopo ya kuumiza + dead projects ni mwiba KE
 
Tusikitikw Uganda kutufatilia kwa karibu wakati n nchi Ndogo sana.
Tusipokuwa makini hata Burundi watafikia Nusu ya Budget yetu
 
Msishangilie kenya kuwa na digit kubwa, kenya wanamadeni mpk kwenye kende zao, its just a matter of time kenya kuja kuwa koloni la wachina na mabeberu wengine
 
Kwa Bajeti hizi za Africa Mashariki Kenya itazidi kupaa sana. Bajeti ya Kenya ni takriban mara mbili ya Bajeti ya Tanzania. Ukijumlisha Bajeti ya Tanzania na Uganda bado haifikii Bajeti ya Kenya...
Population ya Tanzania ni kubwa kuliko ya Kenya, Rais wao yupo serious sn tofauti na sisi
 
Magofool alikuwa anaandaa bajeti hewa. Jiulize kwanini wizara zilikuwa zinapewa chini ya 10% ya bajeti iiyopitishwa na bunge???
Kwanini alishindwa kuajiri au kupandisha mishahara na madaraja ya watumishi???
Kwanini deni la taifa limepanda???
WATANZANIA SIO WAJINGA.
Muongo, kama alikuwa na budget hewa kwanini Samia asiishushe kwa sasa kutoka trillion 36 iende trillion 20? weka data za comparison za idadi ya walio ajiliwa mwaka 2016-2021 ukilinganisha na idadi ya walio ajiliwa kuanzia mwaka 2010-2015, huwezi ukawa na mapato hafifu ukaajili watu wengi utawalipa nini? hizo ni Story za vijiweni kuwa awamu zilizo pita ajira zilikuwa nyingi , ni facts zipi zipi za uchumi, fuatilia vitu kwa kutumia vielelezo .

Deni LA Taifa kupanda ni kawaida kwa sababu kwanza uwezo wa serikali kukopa umeongezeka na awesome kulipa ni mkubwa , huwezi ulkawa na mshahara wa million 1 kwa mwezi ukakopa million 100 , lakini mbunge mwenye kipato cha million 12 kwa mwezi anauwezo wa kukopa hadi million500 maana yake anauwezo wa kulipa Deni, hivyo kwa serikali Mapato yameongezeka hivyo uwezo ni mkubwa wa kukopa kugharamia miradi ya maendeleo, SGR, stieglers gorge, ATCL, miradi ya maji, umeme, umeme.

Lakini ukopaji wetu ni mdogo ukilinganisha na nchi ya Kenya , ambapo wanakopa zaidi mara mbili yetu na kuendeleza miradi ya maendeleo haraka zaidi kwa sababu uwezo wa kulipa deni hilo ni mkubwa kulingana na uwezo wao mkubwa wa kukusanya mapato simple like that.
 
Wakenya kuwa mbele yetu isiwe sababu na wala tusiwachukie kwasababu hiyo, tujiulize shida yetu inaanzia wapi, binafsi naamini shida yetu imeanzia kwa hii kitu inaitwa CCM na vyote vilivyomo ndani yake.
Upo sahihi kutokuwa na chuki, ila haupo sahihi kwenye sababu, tofauti ipo kuanzia zama za ukoloni, Kenya iliendelezwa kielimu, kimiundombinu, kiviwanda, kilimo, na hii ilitokana na kutawaliwa na taifa moja.

Kwa upande wa Tanganyika maendeleo yalisimama baada ya mjerumani kunyang'anya koloni lake na Tanganyika ilikuwa 'undermandator' ya UN chini ya uingereza, hivyo uingereza haikuendeleza jambo lolote la elimu, afya, miundo mbinu, na kimsingi hata majengo yanayoonekana yamkoloni sehemu kubwa ni ya kijerumani licha ya uingereza kutawala zaidi ya miaka 20.

Kumbuka walituacha tukiwa hatuna wasomi, ni kujivuta hadi sasa, hivyo matatizo yetu yalianzia mbali kidogo!
 
Back
Top Bottom