TRACE
Senior Member
- Jul 4, 2008
- 120
- 46
Wandugu,kila mara utakuta watu wakilalamika kuwa HALMASHAURI,MJI,MANISPAA AU JIJI yao hayana maendeleo wakati raslimali wanazo.Naomba niwaulize swali la msingi wao pamoja na wewe unayesoma hapa kuwa waweza kujua mipango ya HALMASHAURI,MJI,MANISPAA AU JIJI juu ya bajeti itakayotumika mwaka wa fedha 2010/11 na kama mambo yakiwa siyo yale waliyoyapanga uweze kuwa na uwezo wa kufuatilia na kuhoji ?
Kama jibu utaniambia kuwa ni kazi ya Diwani au Mbunge wako kujua hilo je,ulipomchagua uliangalia/utaangalia uwezo wake wa kufuatilia ili aweze kukuelemisha na kukufungua macho wewe uweze kujua ?
Na Je,kama yote kwako hujawahi kuyawaza unafikiri lini ni muda muafaka kwako kujua jinsi matayarisho ya bajeti yanaanza na jinsi yanavyoathiri maendeleo ya HALMASHAURI,MJI,MANISPAA AU JIJI yetu na kisha lawama tunawatupia wengine badala ya kujilaumu wenyewe?
Itakuwa vizuri tukilijadili hili hapa kwa kina kwani hapa kuna watu wa kila aina na uwezo tofauti
Nawakilisha
Kama jibu utaniambia kuwa ni kazi ya Diwani au Mbunge wako kujua hilo je,ulipomchagua uliangalia/utaangalia uwezo wake wa kufuatilia ili aweze kukuelemisha na kukufungua macho wewe uweze kujua ?
Na Je,kama yote kwako hujawahi kuyawaza unafikiri lini ni muda muafaka kwako kujua jinsi matayarisho ya bajeti yanaanza na jinsi yanavyoathiri maendeleo ya HALMASHAURI,MJI,MANISPAA AU JIJI yetu na kisha lawama tunawatupia wengine badala ya kujilaumu wenyewe?
Itakuwa vizuri tukilijadili hili hapa kwa kina kwani hapa kuna watu wa kila aina na uwezo tofauti
Nawakilisha