Bajeti Mpya: Betting ni kazi rasmi, sasa kukatwa kodi 18%

barafu

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
6,726
32,818
betting Tanzania.jpg

Hatimaye Serikali kupitia Wizara ya fedha imehalalisha mchezo wa "betting" kama kazi rasmi. Hii inatokana na Waziri wa Wizara ya Fedha kutangaza rasmi kuwa "mikeka na waanika mikeka" wanatakiwa kulipa kodi ya 18% kila mzigo.

Wale wazee wenzangu wa kuanika mikeka sasa tunaingia rasmi kama wachangiaji wa pato la Taifa kwa kuchangia kodi kila tuanikapo mikeka na kupata mzigo. Hii inatuingiza wacheza kamali kuwa "sekta rasmi" inayochangia pato la Taifa.

Kwa wanaofuatilia katika vibanda umiza na maeneo ya Uswahilini, kwa sasa vijana wengi na hata watoto wa shule wamejiingiza kwenye biashara hii kwa kasi ya ajabu sana.

Kianzio cha "kuanika mkeka" ni shilingi 500 tu, hii inafanya mpaka watoto wa shule ya Msingi kujibana na kutumia pesa zao kucheza mchezo huu.

Wakati Serikali ikiwa imefikia hatua ya kuruhusu "mchezo" huu kuwa chanzo cha pato la Taifa, ikumbuke pia kuweka taratibu za ushiriki hasa kwa watoto walio chini ya miaka 18 ambao wanaonekana kuchipukia na kushiriki kwa kasi katika mchezo huu.

Primier Betting na Meridian betting zina mawakala zaidi hata ya wale wa Mpesa na Tigopesa, wametapakaa kila kona. Wakati tunafurahia kupata "chanzo" cha Mapato ya Serikali, tukumbuke pia maadili ya Taifa, hata kabla ya Serikali kufanya huu mchezo kuwa chanzo cha mapato, vibanda umiza mtaani vilijaa pomoni, si kwamba wengi wanapenda sana kuangalia mpira, bali wengi hukaa kusubiri kama "mikeka" walioanika itaanuliwa au la!!

Kwa sasa "betting" imekuwa zaidi ya Ligi kubwa tu za Ulaya Magharibi, imesambaa mpaka kwa ligi za China, Argentina, Brazil mpaka US, Vijana, watoto na wazee sasa wanaweka mikeka mpaka kwenye mbio za farasi, mbwa na hata zile za magari ya "rangaranga"

Wazee wenzangu wa mikeka kazi imeanza, hatimaye Serikali imetutambua kama walipa kodi rasmi na wachangiaji wa pato la Taifa.

Tuhamasishane kwenye vibanda umiza ili tukajiandikishe kwenye BVR ili kuchagua viongozi bora na wazuri, kuepuka hela zetu za kodi zitokanazo na "mikeka" kuliwa na watu wachache.
 
Huku Kitaa Watu wengi Wameacha Kazi zao Kisa Betting Maana inawaingizia Pesa ya Kujikimu....HATARI Wacha walipe Kodi Bana
 
steveachi Mkuu, hio hawawezi kukubali. Serikali siku zote inataka yenyewe ndo ifaidi.
 
Last edited by a moderator:
betting compny,TBL,TCC nd zitaongeza mapato kw taifa.nakm ww ni mdau wahizo compny zote bc ww ni mzalendo wakwl
 
Mikeka unapata hela chap chap ukikimbiza mbwa unapata hela ndani ya dk 5 mpira ndani ya saa moja na nusu umeingiza hela ya mwezi ya mtumishi wa umma.
 
Aiseee
Ushauri
Usifanye betting kuwa kazi yako
Cheza kiwango unachoweza himili pale kitapo potea
Cheza kistaarabu
Usiruhusu mtoto wa miaka chini ya 18 kucheza

Hii siyo ajira rasmi maana kupoteza ni asilimia kubwa kuliko kushinda
 
Haya mabom ambayo serikali inatengeneza yakija lipuka tutatafutana...watu wanachagua kufanya kazi za kujenga nchi wanakua wajanja wajanja.. Mi kuna jamaa kama watatu nawajua wameacha kazi mafisi kwa ajili ya betting
 

Not all surprising, the majority of betting shops are in the most deprived areas. It would seem people have 'money to burn' on gambling, smoking, drinking and yet still the government need eradicating poverty or creating revenue by milking common mwananchi!!!!
 
Usitumie pesa iliyokuwa ndani ya bajet kubet utajuta , tumia pesa ya ziada kubet hutajuta... sio kielfu 10 chako cha kuacha kodi ya meza ndio ukabetie... utaanzisha ugomv na mama njerekera bure na ukose unyumba bure...
 
Serikali yetu ilishakuwa ya kufukuzia fursa zinazojitokeza, imeshindwa kubuni vyanzo vipya vya kuingiza mapato, hii imekuwa kama walivyotaka kuanza kutozesha kodi pikipiki maarufu kama bodaboda..!
 
Back
Top Bottom