CM 1774858
JF-Expert Member
- May 29, 2021
- 4,984
- 4,083
Bajeti moja ya barabara,madaraja na viwanja vya ndege ya Rais Samia FY2021|22 inaweza kujenga mara mbili ya barabara zote za lami zilizojengwa kwa miaka mitano iliyopita,
"Hakuna kama Samia "
Kasi ya Rais Samia Suluhu Hassan katika kuwaletea maendeleo endelevu Watanzania hawa masikini inatetemesha,
Rais huyu katika kutambua ili nchi yeyote ile hapa duniani iendelee kwa kasi lazima iwe na miundombinu ya barabara iliyo rafiki na madhubuti,
Rais Samia Suluhu Hassan tayari kwenye bajeti yake ya kwanza yaani FY2021|22 ametoa TZS 2trilioni,
Fedha hii ni kwa ajili ya ujenzi wa barabara na madaraja,
Kwa msiofahamu,bajaeti hii ni sawa na ongezeko la 100% la Bajeti ya serikali iliyopita ambayo ilitenga Tshs 1trilioni FY2020|21
Sikia hii, Kama gharama ya kujenga kilometa moja ya" lami" kwa kiwango cha kimataifa ni TZS 1BL/Km,
Bajeti hii ya Rais Samia inaweza kujenga jumla ya kilometa mpya 2,000 za lami kwa mwaka huu mmoja wa fedha wa 2021|22,
Kilometa hizi za lami ni sawa na 18.3% ya barabara zote km 10,941 zilizowahi kujengwa tangu tupate Uhuru,
Nakama mwendo ni huu mpaka kufikia FY2030|31 basi barabara zote km 33,649 nchi nzima huenda zitakuwa zimejengwa kwa kiwango cha lami,
Katika historia ya nchi hii kama kuna mtu anatakiwa kuombewa kwa nguvu zote basi ni huyu Mama,
Kwamsiofahamu,Hayati Rais Magufuli kwa miaka yake mitano alifanikiwa kujenga Jumla ya km 1,004,
Taarifa hii ni kwamujibu wa National Bureau of Statistics (NBS),
Kwa lugha rahisi Bajeti moja ya barabaraba ya Rais Samia inaweza kujenga marambili (X2) ya barabara zote zilizojengwa kwa miaka mitano mfululizo ya Serikali ya awamu ya tano ( A comparative analysis|advantage )
Raha Sana kuwa na Rais mwenye speed kama Mama Samia Suluhu
VIVA SAMIA VIVA || VIVA MPANGO VIVA