Bajeti kugusa mabenki, mabenki hayawezi kuongeza riba za mikopo kufidia kodi mpya kwenye sekta hii?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,888
143,985
Habari wadau,

Hivi kama bajeti itapitishwa huku mabenki yakikabiliwa na kodi mpya ya matumizi ya ATM kama inavyopendekezwa, mabenki haya hayawezi kuongeza riba za mikopo kufidia tozo hiyo mpya?

Nauliza swali hili kwasababu naamini benki zikiongeza riba kwenye mikopo,basi hili litakuwa pigo kubwa sana kwa wajasiliamali wengi wa nchi hii.

Kama mabenki yataanza kutafuta chanzo cha kufidia kodi hii mpya,nashauri ni bora waongeza gharama za kutumia ATM hizo au gharama ya kumiliki/kuendesha account,gharama ya kuchukua fedha ndani ya benki(kwa teller) au gharama nyinginezo kuliko kuthubutu kuongeza riba za mikopo maana mtagusa wengi na zaidi mtaongeza umasikini wa mtu mmoja mmoja.

Sitaraji kabisa uamuzi wa aina hii kwa mabenki hata hivyo lolote laweza kutokea kutegemeana na bajeti nzima ya mwaka huu.
 
Kweli kabisa....lazima waongezee upungufu uliojitokeza....hiyo pesa walikuwa wanatoza kwa matumizi Maalum,matumizi hayo bado yapo,wataangalia jinsi ya kuyafidia kwa kumtwishq mzigo mteja
 
Waongeze tu tukome.

Hii nchi bila maskini kufikia hatua ya kukamuliwa na kunyang'anywa kila kitu hakutakua na mapinduzi ya kweli ya kifikra.

Ili CCM iondoke madarakani ni lazima maskini tupitie mateso kupita kiasi ili tu'evolve na kufanya maamuzi sahihi kwa kuchagua watu sahihi.
 
Waongeze tu tukome.

Hii nchi bila maskini kufikia hatua ya kukamuliwa na kunyang'anywa kila kitu hakutakua na mapinduzi ya kweli ya kifikra.

Ili CCM iondoke madarakani ni lazima maskini tupitie mateso kupita kiasi ili tu'evolve na kufanya maamuzi sahihi kwa kuchagua watu sahihi.
Umasikini unakwamisha mambo mengi na umasikini mbaya ni wa akili
 
Waongeze tu tukome.

Hii nchi bila maskini kufikia hatua ya kukamuliwa na kunyang'anywa kila kitu hakutakua na mapinduzi ya kweli ya kifikra.

Ili CCM iondoke madarakani ni lazima maskini tupitie mateso kupita kiasi ili tu'evolve na kufanya maamuzi sahihi kwa kuchagua watu sahihi.
Hapa kuna ukweli fulani.
 
Yaani watanzania wamekaza macho kuangalia ubaoni ili wasome namba...mpaka macho yameanza kuvimba wameona mpaka namba nne tu,,sasa mpaka zifike 360 macho yatakuwa yamefyatuka Mwenye soketi zake
 
Kenya wanaotumia bank ni zaidi ya milioni 20
sisi wanaotumia bank ni milioni 3 tu
tulipaswa kuvutia zaidi watu watumie bank kwa kupunguza kodi
badala yake tumeongeza kodi
hivi hii million 3 ya watz wanaotumia bank umepata wapi? 3 out of about 59 millions people? au 3 out 33 pc of Adults? i think your misleading. yaani at average ya kila bank kuwa na wateja 52000?
 
Yaani watanzania wamekaza macho kuangalia ubaoni ili wasome namba...mpaka macho yameanza kuvimba wameona mpaka namba nne tu,,sasa mpaka zifike 360 macho yatakuwa yamefyatuka Mwenye soketi zake
Hahahaha
 
hivi hii million 3 ya watz wanaotumia bank umepata wapi? 3 out of about 59 millions people? au 3 out 33 pc of Adults? i think your misleading. yaani at average ya kila bank kuwa na wateja 52000?

Umewahi soma ripoti ya mkurabita?
hii unajua hata mkurabita ni nini?
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom