:hand:Wana JF; Binafsi nimesikitishwa sana na Bajiti ya Mheshimiwa Dokta......... ambayo haikuzingatia kuwa kuna watu ambao ni walalahoi pasee! Angalia inavyotaka kodi iongezwe kwenye mawasiliano (Simu) ambayo wapika Vitumbua, Mama Ntilie, Wamachinga nk wanamiliki Simu ambazo wamenunu za Mchina ili kuwasaidia katika kufanya biashara zao. Senti wanazopata watu hawa ni "Hand to Mouth", sasa watalazimika kulipia mawasiliano kwa gharama kubwa! Wanaochota Madini kule Shinyanga, Geita, Arusha nk, Bajeti ya Mheshimiwa haiwasumbui hata kwa Senti tano! Wafanya biashara wanaopata hadi Shilingi Millioni tatu (3,000,000/=), Bajeti ya Dokta haiwasumbui, acha wapumuzike! Mfanyakazi mwenye Mshara unaofikia Millioni Mbili, PAYE anayotozwa kila mwezi ni zaidi ya Laki Sita! Jamani mimi nalazimika kukubaliana na wazo la Mstahiki Meya wa Jiji kubwa hapa Tanzania aliposema wengine labda wanafikiria kwa kutumia "Makalio"! Wana JF; tafakali, chukua hatua!