mwanamichakato
JF-Expert Member
- Mar 20, 2015
- 887
- 705
Mabadiriko chanya katika taifa lolote lile uambatana na maumivu..Wana wa Israel walipotoka Misri kwenda nchi ya ahadi {yenye asali na maziwa} hawakutembea kwenye tambalale..Walivuka milima na mabonde,walivuka bahari na kupigana vita hata mwisho wa safari yao.
Taifa letu ni tajiri sana..Limejaa kila aina ya utajiri,Tumepofushwa sana na wageni waliokuja na kupata fulsa ya kututawala..Tukatuvisha ufahamu hasi juu ya utajiri wetu wa fikra na maliasiri.Uchumi wetu hauwezi kuwa imara ikiwa tutawategemea watu toka nje wauendeshe,wautawale,wausimamie..Uwekezaji wa ndani unanihusisha mimi na wewe ni muhimu sana katika maendeleo endelevu ya taifa letu sasa na baadae.
Utekelezwaji wa bajeti ya Wizara ya Fedha unategemea sana mapato,Ni aibu kwetu sote kutegemea misaada.Hivyo ukusanyaji wa kodi,tozo toka vyanzo vya ndani vitapewa kipaumbele pasipo shaka.Hata hivyo ni rai ya kuwa taasisi za umma zenye athari mseto katika utekenyaji wa uchumi zishiriki kikamirifu ili kuwezesha mazingira wezeshi kwa wafanyabiashara,wawekezaji,wajasiliamali ili kufikia malengo,kiu,nia,dhamira,ndoto na maono .
Uchocheaji tanuru la uchumi wa taifa letu ufanyike kimkakati na kwa makusudi ili kukidhi haja na matakwa mtambuka leo,kesho na keshokutwa.Ukamuaji wa maziwa uendane na malisho stahiki apatayo ngombe mzazi..tusikamue hata kumfanya ndama akose maziwa ya kunyonya na kuishi.
Taifa letu ni tajiri sana..Limejaa kila aina ya utajiri,Tumepofushwa sana na wageni waliokuja na kupata fulsa ya kututawala..Tukatuvisha ufahamu hasi juu ya utajiri wetu wa fikra na maliasiri.Uchumi wetu hauwezi kuwa imara ikiwa tutawategemea watu toka nje wauendeshe,wautawale,wausimamie..Uwekezaji wa ndani unanihusisha mimi na wewe ni muhimu sana katika maendeleo endelevu ya taifa letu sasa na baadae.
Utekelezwaji wa bajeti ya Wizara ya Fedha unategemea sana mapato,Ni aibu kwetu sote kutegemea misaada.Hivyo ukusanyaji wa kodi,tozo toka vyanzo vya ndani vitapewa kipaumbele pasipo shaka.Hata hivyo ni rai ya kuwa taasisi za umma zenye athari mseto katika utekenyaji wa uchumi zishiriki kikamirifu ili kuwezesha mazingira wezeshi kwa wafanyabiashara,wawekezaji,wajasiliamali ili kufikia malengo,kiu,nia,dhamira,ndoto na maono .
Uchocheaji tanuru la uchumi wa taifa letu ufanyike kimkakati na kwa makusudi ili kukidhi haja na matakwa mtambuka leo,kesho na keshokutwa.Ukamuaji wa maziwa uendane na malisho stahiki apatayo ngombe mzazi..tusikamue hata kumfanya ndama akose maziwa ya kunyonya na kuishi.