Bajeti hii inatosha kuanzisha mradi wa kuku wa mayai?

Mkulima na Mfugaji

JF-Expert Member
Jul 26, 2013
1,013
1,634
Habari wakulima na wafugaji wenzangu,
Baada ya kufuga kuku wa kienyeji sasa nataka kuhamia kwenye kuku wa mayai ila nimeandaa bajeti ifuatavyo kwa ajili ya mradi huu. Nina mpango wa kuanza kufuga kuku 300.

1.Vifaranga 300 @ 2500 =750000
2.Nauli ya vifaranga =60000
3.Chakula kwa miezi 6 =1152000
4.Madawa =100000

Jumla Tsh 2062000


Makadirio ya Mapato kwa miezi 6 ya mbeleni

Kwa siku , Tray 6*6000 =36000
Kwa mwezi 36000*30 =1080000
Kwa miezi 6 1080000 *6=6480000


Mapato 6480000
Matumizi - 2062000

Jumla 4418000

Notes **** hapo sitakuwa na mfanyakazi wa kumlipa mshahahara kwani mradi uko nyumbaani hivyo familia ndio itakuwa inahusika

**** Nimeweka kuku watakaoweza kutaga ni 180 tu kwa siku ingawa idadi inaweza kuongezeka

*****Kwa upande wa chakula nitakuwa nanunua mahindi kwa wakulima kipindi cha mavuno vijijini

****, Mradi nimeuweka kwa miezi 6 kwani kipindi hiko kuku wa mayai ndio wanachanganya kutaga hivyo utakuwa unajiendesha wenyewe.

****, Banda na vifaa vya chakula na maji vyote vipo

Nahitaji ushauri, na marekebisho nilipo kosea,

Nahitaji kuanza mwezi wa kumi

Nipo Muheza Tanga
 
hapo kwenye chakula japo hujatoa mchanganuo zaidi ila inaweza kuwa bajet hafifu kidogo.
 
Mkulima na Mfugaji kwanza hongera kwa uthubutu

Pili: gharama ya umeme naona hujaiweka na kwahakika kuku wa mayai wanahitajia sana umeme kama chanzo cha joto na muangaza hasa wanapokua wadogo.

Tatu: Apo kwenye miezi 6 ya mwanzo ya kutaga naona hujaweka mchanganuo wa matumizi !
Then umesema kama mradi utajiendesha kwahiyo JUMLA YA MAPATO kwenye miezi hiyo 6 itakua siyo iyo ambayo umeiweka 4,418,000/= Lazima itapungua kutokana na matumizi ya miezi hiyo 6 yamwanzo (ushauri wangu fanya ufafanuzi wa matumizi kabisa katika iyo miezi 6 ili ujuwe NET PROFIT katika miezi hiyo, yaani usiruhusu mpaka miezi hiyo inafika ukawa bado hujui ni faida halisi gani utaingiza)

Nne: Kwenye chakula umetuorodhoshea kwamba mahindi utanunua kwa wakulima, Je umeshajua wapi utapata michanganyiko mengine wapi utapata na kwa gharama gani? Mfano Pumba nakadhalika...

Ni hayo tu kwasasa, hongera mkuu kwa uthubutu
 
Chakula nimepiga Hesabu kila mwezi nitumie gunia nne za mahindi ambayo garama zake ni 120000 kwa Huku niliko hna vitu vya kuchanganyia ni elf 20 kwa Kila gunia
hapo kwenye chakula japo hujatoa mchanganuo zaidi ila inaweza kuwa bajet hafifu kidogo.
 
Mkulima na Mfugaji kwanza hongera kwa uthubutu

Pili: gharama ya umeme naona hujaiweka na kwahakika kuku wa mayai wanahitajia sana umeme kama chanzo cha joto na muangaza hasa wanapokua wadogo.

Tatu: Apo kwenye miezi 6 ya mwanzo ya kutaga naona hujaweka mchanganuo wa matumizi !
Then umesema kama mradi utajiendesha kwahiyo JUMLA YA MAPATO kwenye miezi hiyo 6 itakua siyo iyo ambayo umeiweka 4,418,000/= Lazima itapungua kutokana na matumizi ya miezi hiyo 6 yamwanzo (ushauri wangu fanya ufafanuzi wa matumizi kabisa katika iyo miezi 6 ili ujuwe NET PROFIT katika miezi hiyo, yaani usiruhusu mpaka miezi hiyo inafika ukawa bado hujui ni faida halisi gani utaingiza)

Nne: Kwenye chakula umetuorodhoshea kwamba mahindi utanunua kwa wakulima, Je umeshajua wapi utapata michanganyiko mengine wapi utapata na kwa gharama gani? Mfano Pumba nakadhalika...

Ni hayo tu kwasasa, hongera mkuu kwa uthubutu
Gharama ya umeme ninaunganisha na ninao tumia nyumbaani na pia garama ya miezi 6 ni hiyo 2062000 baada ya hapo mradi utakuwa unajiendesha wenyewe
 
kama ni layers pure(commercial) kwenye bajet ya chakula naona ni ndogo then umedhamiria kuchanganya chakula, hawa kuku inabdi uwe na formula super au ununue cha dukani otherwise watadumaa na kuchelewa kutaga au kutotaga kwa kiwango kizuri. kiufupi usiwafanyie ubahili. ingekuwa kuroiler sawa lkn si hawa. hawataki ku beepiwa. kila la kheri mfugaji mwenzangu.
 
Asante sana je kwa uzoefu wako huwa wanakula mifuko mingapi kwa mwezi kwa kila umri?
kama ni layers pure(commercial) kwenye bajet ya chakula naona ni ndogo then umedhamiria kuchanganya chakula, hawa kuku inabdi uwe na formula super au ununue cha dukani otherwise watadumaa na kuchelewa kutaga au kutotaga kwa kiwango kizuri. kiufupi usiwafanyie ubahili. ingekuwa kuroiler sawa lkn si hawa. hawataki ku beepiwa. kila la kheri mfugaji mwenzangu.
 
Asante sana je kwa uzoefu wako huwa wanakula mifuko mingapi kwa mwezi kwa kila umri?
Mkuu najiribu ku attach chart ya Chakula hopefully itakupa mwanga. Pia waweza wasiliana nami.kwa 0752981380 whatsapp nikakuforwardia notes na Mambo ya zaida ukaongezea kwenye maktaba yako ya Ufugaji.
IMG-20190729-WA0009.jpg
 
Kwa mtu ambaye ajafuga ni hesabu nzuri kwake sana ila kwa aliyefuga changamoto na layers inataka moyo unaweza ruka kichaa kama hela ni ya mkopo kuna swala la soko kuna kipindi hiyo 6000 uuzi weka akili kichwan angalizo tafuta soko la uhakika na kuna vifo sana kwa layers nawajuza ndugu zangu mi nafuga sio rahisi hivyo kama kwenye karatasi lkn kama unaweza kupambana na changamoto na soko basi sawa ila sio kwanba kila siku ya ufugaji wako kuku 300 watataga kwa pamoja na layers wana matatizo yaweza wana pata toka kwa mama wazazi yani parent stock au kiwandani chukua kwa warranty ya mwenye vifaranga tena kama ni mara ya kwanza iwe hata doctor atoke kwake kuja kuku guides kama atakataa kaa nae mbali mana unaweza fanya kila kitu wakafika kwenye utagaji wakaanza kukata wote na madawa mengi bongo ya kuku ni fake coz ufatiliaji wa serikali ni mdg sana ila ukiweza na ukiwa na soko la uhakika mkuu nakwambia unaweza ukaacha kazi ingawa usiweke guarantee mana bana ufugaji anaweza kuja mtu akakuchallenge sokoni utajuta
 
Hapo kwenye mahesabu ya chakula weka vzur mahesabu na pia mm ni mfugaji bei ya mayai haijawai kukaa stable kila siku inabadilika hio 6000 utapata lkn kina kipindi yanafika mpaka 4500
 
kama ni layers pure(commercial) kwenye bajet ya chakula naona ni ndogo then umedhamiria kuchanganya chakula, hawa kuku inabdi uwe na formula super au ununue cha dukani otherwise watadumaa na kuchelewa kutaga au kutotaga kwa kiwango kizuri. kiufupi usiwafanyie ubahili. ingekuwa kuroiler sawa lkn si hawa. hawataki ku beepiwa. kila la kheri mfugaji mwenzangu.
Mkuu umenifurahisha sana maana mwenyew ninao, unachosema ni sahihi kabisa,wanakula kwa kwenda mbele na ni vyema zaidi ukawalisha chakula special
 
Back
Top Bottom