Bajeti hii inamsulubu mwananchi wa kawaida

Kiukweli serikali imechemka kutusomea bajeti kwa mbwembwe lakini cha ajabu bado inaendelea kubaki usingizini kwa kuondoa kodi kwenye sekta za kuingiza kodi kubwa na kutegemea ulevi kuongeza makusanyo. Hapa serikali imekosa mshauri haina wachumi, bora tuombe uzima 2015 ifike kwanza wawe super sub. Mungu awe nasi sote wadau
 
kodi za kwenye simu binafsi nazikubali kwani hazina direct impact na maisha ya kawaida ya mtanzania. Isitoshe matumizi holela ya simu na sms yamezidi mno, pengine hii italeta nidhamu kidogo.

kasheshe ni kwa ndg zangu mawakala wa m-pesa, tigopesa n.k, ilivyo tu walikuwa wanalalamika commission ndogo, sasa tena kodi, nahisi hali itakuwa tete zaidi

Mkuu naona unakwenda mbele halafu unarudi nyuma.Uliposema uwepo wa kodi katika simu hautaleta madhara ya moja kwa moja nilitarajia ungekuja na hoja ya kitafiti kutetea hoja yako,Umeniacha hoi pale ulipodai kodi hizi zitaongeza nidhamu kwasababu matumizi holela ya simu.Kwahiyo ndiyo sababu ya kuweka hiyo kodi yaani uwaadhibu watu kwaajili ya matumizi holela ya simu?Zaidi ya yote pia unakiri kile kitakacho tokea ktk huduma M-pesa,Tigo-pesa,nk,Wateja wa hizi huduma watapungua,Vijana wengi waliojiajiri kuendesha hizi huduma huko mitaani watafunga biashara zao.Hapa hamumkomoi mtumiaji wa simu ila mtaathiri biashara za vijana wengi mitaani.
 
Uwe mzalendo pia! mafuta ya magari juu, road licence juu, simu ukimtumia mwanafunzi laki mbili lazima serikali ichukue Tzs.20,000/=!!!!!, kumbuka usafiri umepanda mwezi uliopita!!, Insurance companies nazo zimeongeza kodi zao!!.

Hiyo tshs.mbili unayosema sio kidogo na hivyo gharama za mazao na bidhaa nyingine juu!! uwe unatafakari kwanza sio kwa kuwa una laptop mbele yako tu unaweza kuleta viroja!!!!

Kwa gharama hizo za mafuta umeme lazima utakuwa juu na hivyo gharama za uzalishaji viwandani juu!!

Binafsi nahisi unafuu ni mdogo mno kwani ukigusa mafuta hata kwa kiwango kidogo namna gani repercussion yake itagusa sehemu nyingi.
Pia nimesikitika kuhusu kodi ya magari kupangwa bila kujali matumizi.Mwenye pickup ya cc1800 analipa kodi sawa na aliye na gari ndogo ya kutembelea,nahisi hii si sahihi.
 
Kwa wenye corolla kuna la Tsh50000 na wale wenye magar yenye engine zaid ya cc1500 nao Tsh 50000 imeongezeka. Swali hapo je fire nao watapandisha?
 
Mkuu naona unakwenda mbele halafu unarudi nyuma.Uliposema uwepo wa kodi katika simu hautaleta madhara ya moja kwa moja nilitarajia ungekuja na hoja ya kitafiti kutetea hoja yako,Umeniacha hoi pale ulipodai kodi hizi zitaongeza nidhamu kwasababu matumizi holela ya simu.Kwahiyo ndiyo sababu ya kuweka hiyo kodi yaani uwaadhibu watu kwaajili ya matumizi holela ya simu?Zaidi ya yote pia unakiri kile kitakacho tokea ktk huduma M-pesa,Tigo-pesa,nk,Wateja wa hizi huduma watapungua,Vijana wengi waliojiajiri kuendesha hizi huduma huko mitaani watafunga biashara zao.Hapa hamumkomoi mtumiaji wa simu ila mtaathiri biashara za vijana wengi mitaani.

Ila ujue serikali ye yote inajiendesha kutokana na kodi, kwahiyo ukitaka kila mmoja asifeel impact maana yake usikusanye kodi kabisaa, na hapo sijui hiyo serikali utaiendeshaje!

Ila yale yanayogusa maisha ya mwananchi wa kawaida (mfano mafuta) ondoa au usipandishe kodi
 
Back
Top Bottom