killo
JF-Expert Member
- Jul 13, 2008
- 401
- 94
Habarini wandugu, Ndugu yangu aliibiwa bajaji yake mwanzo wa mwezi huu na nikapata taarifa kwamba Bajaji na Pikipiki zinazoibiwa huku bara huwa zinapekekwa kuuzwa Kigamboni maana kule hakuna askari polisi wengi barabarani kama ilivyo huku bara.
Kufuatia habari hizi, nikiwa naendelea na uchunguzi nikapewa habari nyingine kwamba askari polisi kupitia kitengo maalum wameendesha msako mkali hususani kwa bajaji katika eneo la Kigamboni na wamefanikiwa kukamata bajaji nyingi tu ambazo zipo kituo kikubwa cha Kigamboni.
Tulifika hapo mara moja asubuhi hii na kwakweli ziko nyingi sana japokuwa ya ndugu yangu sijaipata/Sijaikuta.
Natoa rai kwa wengine ambao wameibiwa bajaji kwamba wafike kituo kikubwa cha Kigamboni wakaangalie kama watakuta bajaji zao.
Pamoja katika ushirikiano.
Kufuatia habari hizi, nikiwa naendelea na uchunguzi nikapewa habari nyingine kwamba askari polisi kupitia kitengo maalum wameendesha msako mkali hususani kwa bajaji katika eneo la Kigamboni na wamefanikiwa kukamata bajaji nyingi tu ambazo zipo kituo kikubwa cha Kigamboni.
Tulifika hapo mara moja asubuhi hii na kwakweli ziko nyingi sana japokuwa ya ndugu yangu sijaipata/Sijaikuta.
Natoa rai kwa wengine ambao wameibiwa bajaji kwamba wafike kituo kikubwa cha Kigamboni wakaangalie kama watakuta bajaji zao.
Pamoja katika ushirikiano.