KERO Bajaji za Bunju kwenda Mapinga hakuna nauli rasmi inapelekea usumbufu kwa abiria. LATRA ingilieni kati

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Aug 29, 2022
554
1,301
Leo naleta kilio ambacho ni kero chetu wananchi tunaoishi Mapinga na maeneo yote yanayopakana na barabara ya Bagamoyo.

Kilio hiki kinahusu nauli za usafiri wa bajaji kwani madereva/wamiliki wa bajaji wamekuwa wakijipangia nauli zinazowapendeza wao kila kukicha kinyume na utaratibu.

Mwaka jana nauli zilikuwa shilingi 500, baadaye walipandisha ikawa shilingi 600, lakini mwanzoni mwa mwaka huu ilipanda zaidi ikawa shilingi 700.

Ghafla mwanzoni mwa mwezi huu, imepanda tena na sasa tunalipa shilingi 800. Yote hayo wanasingizia kupanda bei za mafuta.

Jambo hili limetushtua mno na tunaiomba Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (Latra) kuchukulia kwa uzito barua hii ili itoe taarifa rasmi ni kiasi gani cha nauli kinachopaswa kulipwa.
 
Leo naleta kilio ambacho ni kero chetu wananchi tunaoishi Mapinga na maeneo yote yanayopakana na barabara ya Bagamoyo.

Kilio hiki kinahusu nauli za usafiri wa bajaji kwani madereva/wamiliki wa bajaji wamekuwa wakijipangia nauli zinazowapendeza wao kila kukicha kinyume na utaratibu.

Mwaka jana nauli zilikuwa shilingi 500, baadaye walipandisha ikawa shilingi 600, lakini mwanzoni mwa mwaka huu ilipanda zaidi ikawa shilingi 700.

Ghafla mwanzoni mwa mwezi huu, imepanda tena na sasa tunalipa shilingi 800. Yote hayo wanasingizia kupanda bei za mafuta.

Jambo hili limetushtua mno na tunaiomba Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (Latra) kuchukulia kwa uzito barua hii ili itoe taarifa rasmi ni kiasi gani cha nauli kinachopaswa kulipwa.
Kwani latra toka lini wakapanga bei za bajaj na pikipiki..!

Kwanza sidhani kama hivyo vyombo vinachukuliwa kama vyombo vya abiria na hao latra.
 
Leo naleta kilio ambacho ni kero chetu wananchi tunaoishi Mapinga na maeneo yote yanayopakana na barabara ya Bagamoyo.

Kilio hiki kinahusu nauli za usafiri wa bajaji kwani madereva/wamiliki wa bajaji wamekuwa wakijipangia nauli zinazowapendeza wao kila kukicha kinyume na utaratibu.

Mwaka jana nauli zilikuwa shilingi 500, baadaye walipandisha ikawa shilingi 600, lakini mwanzoni mwa mwaka huu ilipanda zaidi ikawa shilingi 700.

Ghafla mwanzoni mwa mwezi huu, imepanda tena na sasa tunalipa shilingi 800. Yote hayo wanasingizia kupanda bei za mafuta.

Jambo hili limetushtua mno na tunaiomba Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (Latra) kuchukulia kwa uzito barua hii ili itoe taarifa rasmi ni kiasi gani cha nauli kinachopaswa kulipwa.
Panda ma bus halali ya bagamoyo mkuu au mikoanii.....yana Lqtra charts kabisa kwa km unazoenda
 
Back
Top Bottom