Abby Newton
JF-Expert Member
- Nov 12, 2017
- 1,227
- 2,197
Nimepigiwa simu na mpwa wangu ambaye ni miongoni mwa abiria walionusurikana, kuwa treni iliyokuwa ikitoka Dar - Kigoma imepata ajali kilometa chache kutoka stesheni ya Dodoma.
Inasemekana watu kadhaa wamejeruhiwa na inadaiwa watu 3 wamepoteza maisha.
Naomba wahusika wafuatilie.
======
UPDATES:
10:05pm
Ajali ya treni iliyokuwa inatokea Dar kwenda Bara imetokea muda wa saa moja kasoro, Maeneo ya Zuzu Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Kati na Itiga. Taarifa za awali ni kwamba watu 25 wamejeruhiwa. Vifo hadi sasa ni Vitatu ambavyo ni Mfanyakazi mmoja wa treni na abiria wawili.
Shirika la reli limepeleka Mabasi kubeba abiria na Majeruhi na Wanapelekwa Dodoma kupata huduma ya kwanza hospitali ya General.
Abiria wote wanapelekwa Manyoni sababu kuna Treni ya abiria saa sita inatokea bara. Kwasababu haiwezi kupita sehemu ya ajali, abiria watapanda hiyo Treni iliyokuwa ikitoka bara kwenda Dar. Itageuzia manyoni na abiria Waliokuwa wanaenda Dar watapanda mabasi ambayo yamekwisha andaliwa.
Mvua imenyesha sana, kuna uwezekano kuna makalavati yamekatika.
Ajali ilipotokea ni Km 40 kutoka Dodoma.
Taarifa zaidi zinafuata.
Zaidi, soma:
PICHA:
Inasemekana watu kadhaa wamejeruhiwa na inadaiwa watu 3 wamepoteza maisha.
Naomba wahusika wafuatilie.
======
UPDATES:
10:05pm
Ajali ya treni iliyokuwa inatokea Dar kwenda Bara imetokea muda wa saa moja kasoro, Maeneo ya Zuzu Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Kati na Itiga. Taarifa za awali ni kwamba watu 25 wamejeruhiwa. Vifo hadi sasa ni Vitatu ambavyo ni Mfanyakazi mmoja wa treni na abiria wawili.
Shirika la reli limepeleka Mabasi kubeba abiria na Majeruhi na Wanapelekwa Dodoma kupata huduma ya kwanza hospitali ya General.
Abiria wote wanapelekwa Manyoni sababu kuna Treni ya abiria saa sita inatokea bara. Kwasababu haiwezi kupita sehemu ya ajali, abiria watapanda hiyo Treni iliyokuwa ikitoka bara kwenda Dar. Itageuzia manyoni na abiria Waliokuwa wanaenda Dar watapanda mabasi ambayo yamekwisha andaliwa.
Mvua imenyesha sana, kuna uwezekano kuna makalavati yamekatika.
Ajali ilipotokea ni Km 40 kutoka Dodoma.
Taarifa zaidi zinafuata.
Zaidi, soma:
Taarifa ya ajali ya Treni katika eneo la Bahi jijini Dodoma
YAH: TAARIFA YA AJALI YA TRENI B17 NA KICHWA CHA TRENI CHENYE NAMBA 9004 Dar Es Salaam Tarehe 3 Januari 2021 Uongozi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Unasikitika Kutangaza tukio la Ajali lilitokea Maeneo ya Kigwe-Bahi umbali wa Kilomita 508 Kutokea Dar Es Alaam na Kilomita 58 Kutokea Dodoma...
www.jamiiforums.com
PICHA: