Bahati nasibu ya kuhamia Marekani-dv 2020 imeanza rasmi

Ndugu wadau,

Tuna watu wamebobea kubeza hata kwa wasiyoyajua na wengine kujipa Ujuvi huku wakiwa mbumbumbu.

Mimi ni Dalali yes,
Lakini katika hili Tutasaidiana.

Uliza chochote- na buuure,
Nitakuambia, Ila ukinihitaji ana kwa ana UTAFIDIA Muda wangu,
Lakini kiungwana na kwa Roho Safi,
-Hunilipi.

Hakuna wa kuniongopea hii kitu naijua vilivyo,
Ashindwe Mtu mwenyewe kufikia vigezo na asiwe na BAHATI.
Lakini vikiwepo hivyo na kufuata taratibu, Mchongo umenyooka.

Kwa wale wazee wa kubeza na kuropoka msivyovijua,

Wala msiache,
Endeleeni tu,
Maana Dunia inawahitaji Wajinga pia.
Wewe umeomba mara ngapi.?!
 
Hii kitu nilishacheza sana ila kupata ni ngumu labda mtoa mada atueleze vigezo vingine nje ya ile Pdf
 
Aisee mbwa kala chapati maisha magumu huu uzi ni living proof
Nime-like comment yako.
Lakini tambua,
Si kila 'like' Inamaanisha-'ku-like' Kama LIKE inavyoweza kutafsirika katika Kingereza.

Tafakari.
 
Ukishinda unapata huduma kutoka serikali ya us ama unasota mwenyewe?

Mkuu,
Swali lako umelitupa Hewani,

(Jitahidi ku-quote au ku-mention unapouliza)

Naomba nikujibu kama ifuatavyo:

Iwapo utafanikiwa kupata Visa ya aina hii,Kisheri utapata hadhi inayotambulika katika Sheria za Uhamiaji za Marekani kama 'Permanent resident'
(Mkazi wa kudumu) wa Marekani.

Mtu wa 'status' hiyo anapata KARIBIA Haki na Stahiki zote kama zile anazoweza kuzipata kutoka kwa Serikali yake Raia yeyote mwingine wa Marekani.
Lakini pia baada ya muda fulani IKIKUPENDEZA unaweza kuomba Uraia (U.S.Passport) kabisa na wanakupa bila longolongo.

Kubwa zaidi na pengine la muhimu zaidi ambalo linalofanya karibia WANADUNIA wote sasahivi wanaiendea mbio kwa kuhaha hii Bahati nasibu ni swala la kuwa hutahitajika kuomba Visa tena maishani mwako utakapohitaji kwenda aidha KUTEMBEA au KIBIASHARA Marekani.

Nani hahitaji kupanua wigo wa kufanya Biashara au hana ndoto hiyo kwa baadae?
Haya, inaweza kuwa wewe binafsi hupendi wala hutaki kusikia swala hilo vipi kuhusu familia yako?
Yaani mke na watoto wako kama unao, Je,hujafikiria kuhusu wewe kupata/kuwapa wanaokutegemea 'exposure' ?
Tambua ukipata BAHATI NASIBU hii wewe inamaanisha kuwa na wao wamepata kupitia Mgongo wako.

Uliza kingine.
 
Mkuu dalalitz ni kweli wewe uliwahi kushinda hii bahati nasibu, au tu wote tunatafuta mkuu. Samahani lakini
 
Mkuu dalalitz ni kweli wewe uliwahi kushinda hii bahati nasibu, au tu wote tunatafuta mkuu. Samahani lakini
Binafsi,
Sijawahi kupata,
Ila nimechezea watu wengi.

Wenye bahati zao wachache, wamewahi KUCHAGULIWA na mwishowe kupata kabisa VISA.

Hivyo naujua MCHAKATO huu kupitia kufanya, kuanzia mwanzo hadi mwisho.

Huku nami nikiendelea kubahatisha.
 
Naam,

Ni ile Bahatinasibu pekee na ya aina yake inayokuwezesha Mtanzania kuhamia MAREKANI,
Bila zengwe wala longolongo.

Itambulike,
Hii ni Bahati nasibu,
Inavyo vigezo na masharti maalumi a kufuata na kuzingatiwa,
Mojawapo ikiwa ni Elimu ya Juu kwa mifumo wa Elimu wa Marekani,
(Kuanzia KIDATO CHA NNE kwa TANZANIA)

Ni utaratibu wa kila mwaka kwa Nchi kadhaa teule,
TANZANIA tumo.

Ingawa zitakuwepo gharama (Ambazo hulipiwa UBALOZINI) kadiri mchakato unavyoendelea na endapo utachaguliwa,
Hatua kucheza Bahati hapa mwanzoni NI BURE.

Hata hivyo,
Unahitajika umakini kujua nini hasa kinatakiwa kujazwa ili kujiondolea uwezekano wa kuenguliwa mbeleni,
Hasa iwapo utafanya makosa wakati huu wa mwanzoni.

Narudia tena,
Utaratibu wa kuicheza ni BURE na hulazimiki kumtumia wakala kukuchezea ingawa kuepuka makosa ambayo yanaweza kukugharimu baadae ni vyema kumtumia Mtu ambae anajua na kufahamu nini kinahitajika kuanzia MWANZO,


NA HAPA NDIPO NINAPOKUJA MIMI.

Kwa gharama ndogo sana njoo tuelekezane,
Tubahatishe na tuombe Mungu huenda Bahati ikawa yako.

Nipigie:+255714591548.

La ikiwa unajiamini unaweza kufanya mwenye,
Soma maelezo kwa umakini kisha endelea,
Ila usisahau ukifanikiwa si vibaya unanikumbuka hata kwa vizawadi

https://travel.state.gov/content/da...Translations/DV-2020-Instructions-English.pdf

Nawasilisha.

Nashukuru mleta uzi, naomba unifahamishe picha wanayoitaka Kwa vigezo vyake, naweza kwenda picha studio ipi hapa mjini Dar es salaam? Maana Sitaki kufanya makosa.
 
Hii kitu nilishacheza sana ila kupata ni ngumu labda mtoa mada atueleze vigezo vingine nje ya ile Pdf
Umecheza kwamba UKACHAGULIWA Kisha ukapangiwa Usaili ndipo ukakosa (Ukanyimwa Visa)
Au hukuchaguliwa kabisa baada ya kuicheza kwa maana kuwa kukufanyi wa Usaili?
 
Umecheza kwamba UKACHAGULIWA Kisha ukapangiwa Usaili ndipo ukakosa (Ukanyimwa Visa)
Au hukuchaguliwa kabisa baada ya kuicheza kwa maana kuwa kukufanyi wa Usaili?
Mi nilishawah kucheza zaid ya mala 2 na nikawa makini kabisa kujaza ile form online na kuapload picha ambayo iko sawa na specifications walizozitoa lakini niliambulia patupu, naamini kuwa sijakosea kwasababu huo mchongo nilipewa na jamaa (Mtz)ambaye anaishi USA hivyo alinipa maelekezo yote nikayafuata....sasa sijui nilikosea nini......
 
Mi nilishawah kucheza zaid ya mala 2 na nikawa makini kabisa kujaza ile form online na kuapload picha ambayo iko sawa na specifications walizozitoa lakini niliambulia patupu, naamini kuwa sijakosea kwasababu huo mchongo nilipewa na jamaa (Mtz)ambaye anaishi USA hivyo alinipa maelekezo yote nikayafuata....sasa sijui nilikosea nini......
Ushaambiwa ni bahati nasibu sio lazima upate wewe si kuna wengine walipata ,kama huna bahati huna tu hata ucheze Mara milioni
 
Mi nilishawah kucheza zaid ya mala 2 na nikawa makini kabisa kujaza ile form online na kuapload picha ambayo iko sawa na specifications walizozitoa lakini niliambulia patupu, naamini kuwa sijakosea kwasababu huo mchongo nilipewa na jamaa (Mtz)ambaye anaishi USA hivyo alinipa maelekezo yote nikayafuata....sasa sijui nilikosea nini......
Mkuu ndio maana ikaitwa Bahati nasibu.

Kama unayo nia utaendelea kucheza.
Ukikata tamaa nayo Hewala.
Lakini, usipotoshe watu na kuwavunja moyo kwa kuwaaminisha kuwa ni ngumu kupata sema;
'INAHITAJIKA BAHATI NA KUTOKATA TAMAA'.

Lakini, kwani unakimbilia wapi ucheze mwaka huu na upate hapohapo?
Shida wengi wetu tuna Kiu ya Mafanikio ya marammoja.

Amini,-wapo waliocheza mara moja tu,
Wakachaguliwa, na mwisho kufaulu Usaili(Visa Interview) wameondoka na sasa wanamambo yao huko.

Hata hivyo nitoe ANGALIZO:
Kuchaguliwa si Tiketi ya kupata VISA,
Kwani ukichemka kufuata maelezo yao tangia awali inaweza kula kwako.
Kwahiyo kama mtu una makandokando yako hasa ya Elimu utapoteza muda kuifuatilia hii kitu, sababu jamaa wapo makini na kwao wao (Vyeti baba!)
 
Hii naijua toka nikiwa O-level na shangaz yangu ambae yupo USA ndo aliwahi kunielekeza ila niwa elimishe wengne wanaotaka kwenda USA ila kwa m binafsi wala hata sihitaji
kule inabdi uwe na pesa kama kianzio ndo maisha yako yanaweza yakaenda vzur huku ukiwa una tafta kaz maana mara ya kwanza hua n ushamba kushangaa shangaa


M nikitaka kwenda huko ntaenda ila kwa sa hv sion sababu yakwenda huko na miaka 22 sa hv nasoma pharmacy nikimalza nahtaj kua na maduka makubwa ya dawa za jumla na reja reja heka za mtaj tayar ninazo maana hela zipo na duka la jumla ya pharmacy yan kwa siku yan hapo hakuna wateja sana umeuza laki 4 hv ila siku mambo mazur milion 1-3 sa nyingine kwa siku hapo kwa mwez na bado hujagawa chet.. ili ulipwe

Chakuwa shauri jenga maisha hapa kwanza huko utaenda tu bila hata bahat na sibu weng wanaofanikiwa
maisha hua haya washinda kule m niliwah kufka maisha ya kule n akil kumkichwa na kwenda kule kwa njia ya elm nnrahs sana


Kama una kitu chakufanya jtahd ufanye ufankiwe kwanza huku ndo ujarb na kule weng niliwaona n homeless ukijtahd unapata hela ya kula na kulala sa maisha gan hayo labda kama umeyachagua

Na kama ukichaguliwa sio sababu ya wewe pupata visa na ubaloz nao una mambo yake na ukipata visa ukaenda kule unaweza ukard Tz kusalimia ila haitakiw kuzd miez mi will kwa mwaka ukizidisha tu hapo unapoteza green card yako ambayo ina kufanya uwe permanent residence na kama uki chaguliwa na ukapta interview hutakiwi kuzidisha miez 6 upo Tz una takiwa usepe la sivyo visa yako ita expire na ndo utazuiliwa we komaa na Tz wanao fankiwa huku hata kule maisha yao hua n ya raha sa we maisha huku n tabu ukienda kule una taka eesy money haya utaishia kua porn star
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom