Bahati inapogeuka umbo la mitihani

Himidini

JF-Expert Member
May 8, 2013
5,534
4,185
^^
Classmate wangu huyu tulipotezana nilipohama shule nikiwa kidato cha pili.Tangu wakati huo sikupata mawasiliano yake ikizingatiwa kuwa wakati ule hata hizo simu hatukujua kama zipo.Lakini milima haikutani binadamu hukutana.
Tumekutana nae na isingekuwa yeye kunitambua bila shaka kwa kona nyingi na mahangaiko ya hapa na pale mjini basi pengine ingenichukua miaka mingine kuonana au tusionane tena maishani.
....
Aliniita katikati ya umati wa watu.Nilipogeuka kutazama sikumtambua.Alikuwa ni dada ambaye tayari mabadiliko mengi ya mwili.Alionekana mwenye afya njema sana.Aliponitajia jina lake,,mambo mengi yalipita akilini mwangu.Nilimkumbuka katika mengi.Tuliahidi kukutana tuongee vizuri na kwa kirefu
....
Siku ilipofika alikuja ninapotafutia riziki yangu ya kila siku.Hapo ndipo nilipojifunza kuna watu wanapitia mambo mazito katika ndoa zao! Ana tatizo katika ndoa yake,tatizo kubwa ni KUKOSA MTOTO. Alikuwa akitiririka machozi.
....
Lakini kama kuna mtu anaemfahamu vizuri historia ya dada huyu,mmojawapo ni mimi,,tumesoma nae tumekimbia nae mchakamchaka! Jambo moja ambalo sitalisahau kwa dada huyu ni ule usiku wa saa 5 alipogonga mlango (shule ilikuwa ya kutwa) kuomba msaada wangu nimpeleke hospitali. Niliwaamsha rafiki zangu tusaidiane kumbeba.Alikuwa akivuja damu nyingi sana. Hospitali ilikuwa mwendo wa kilometa 6.5 hivii hivyo tulipeana zamu kumbeba. Tukiwa karibu na kufika,nguvu zilimuishia kabisa akaniita na kuniambia 'kama ntakufa waambie nyumbani ni kwa sababu nimetoa mimba,ni mimba ya sita kutoa' nilishituka mpaka nywele zilisisimka. Hata hivyo Mungu ni Mwema,alipata matibabu na akapona
....
Siri hiyo niliishi nayo huku picha za vipande vya nyama nyama vilivyokuwa vikitolewa kwa mkasi wa Mganga wakati nachungulia dirishani usiku ule,zikiumiza hisia zangu.
....
Sasa juma lililopita,dada ananisimulia alipata mume mwenye sifa zote za ndoto ya mwanamke kumpata.Mwenye nyumba,kazi nzuri na pesa ya kutosha. Lakini nyumba haina mtoto,sauti nzuri ya mtoto hakuna,utamu wa neno baba au mama hakuna! Yeye anasema kuolewa ilikuwa bahati!
....
Mimi nae sina adabu! Nikamuuliza kuhusu mimba alizotoa! Akasema mumewe hajui hilo. Akasema amemruhusu mumewe aoe mke mwingine,, Lakini mumewe anasema yeye ni mshika dini hivyo mtoto watapata tu,asihofu na avumilie.Nikamshauri ajifanye wanaenda hospitali kupima uzazi ili iwe njia ya kumjulisha mumewe kuwa hana uzao,,akasema atajaribu japo hataki kuipoteza bahati ya mume,kwani ameteseka kukaa benchi kwa miaka mitano bila kuolewa! Anasema akiacha bahati hii atasumbuka.
....
Ilinisikitisha Ikaniachia Maswali bila majibu,,
Mapito ya maisha yana mengi.
^^
 
Sihukumu, nisije nikahukumiwa kwa kipimo kile kile. Ila mabinti wajifunze kutokana na hili.

^^
Yaani kila nikimfikiria najawa huruma sana,, Naam alikuwa anajiachia sana kwa sababu mazingira ya wakati ule alikuwa mzuri sana.. Ikiwa malipo ya matendo yetu tunayapata hapa hapa duniani,basi tunahitaji mioyo ya chuma! Let me stop here! It pains me
^^
 
Bado hii hadithi yako haijaelezea kwa nini hajapata mtoto!
Nijuavyo mimi kutoa mimba hakusababishi kukosa mtoto! Labda kutolewa kizazi. Hebu [MENTION]Dr.mo[MENTION] unisaidie labda.
 
Bado hii hadithi yako haijaelezea kwa nini hajapata mtoto!
Nijuavyo mimi kutoa mimba hakusababishi kukosa mtoto! Labda kutolewa kizazi. Hebu [MENTION]Dr.mo[MENTION] unisaidie labda.

^^
Si hadithi unavyodhani,, ila huyu dada alinidokeza kuwa hana kizazi na kwa hali aliyokuwa nayo ya machozi ilikuwa ngumu kwangu kumhoji kwa undani. Si vizuri mtu anapotaka umsikilize hapo hapo ugeuke hakimu wa kumhoji maswali ya kukuza hatia (guilty)
^^
 
Pole yake,ila cha kukumbuka hapa ni kwamba matendo yetu ya leo ndo yanatafsiri maisha ya kesho,ni makosa alifanya miaka mingi iliyopita,inapasa asahau na amshukuru mungu kwa yote hapo kesho yake itakuwa na afya
 
Bado hii hadithi yako haijaelezea kwa nini hajapata mtoto!
Nijuavyo mimi kutoa mimba hakusababishi kukosa mtoto! Labda kutolewa kizazi. Hebu [MENTION]Dr.mo[MENTION] unisaidie labda.

Hii inawezekana mana malipo ya matendo yako ni hapahapa duniani...la msingi tuache kutoa mimba...na tuache ngono zembe...
 
Dah ni funzo kwa mabinti...kutoa mimba siyo suluhu...ni heri ukazaa tu...

^^
Mi nadhani hata wanaume wawe resposible kwa maana moja ya watu waliokuwa na mahusiano na dada huyu ni Mtendaji wa Kata,,japo alikuwa na uwezo ila alikataa kumuoa dada huyu na akamtishia kumfanyia kitu kibaya. Hivyo akalazimika kutoa mimba hiyo.
^^
 
Dah aiseeh! Namsikitikia kwakweli. Kuna binti pia amemalza juz tu form four tayari ameshatolewa kizazi kwa sababu hiyo ,najaribu kutafakari nini hatma yake baadaye katka ndoa yake nabaki kumhurumia kwakweli!! So sad!
 
^^
Mi nadhani hata wanaume wawe resposible kwa maana moja ya watu waliokuwa na mahusiano na dada huyu ni Mtendaji wa Kata,,japo alikuwa na uwezo ila alikataa kumuoa dada huyu na akamtishia kumfanyia kitu kibaya. Hivyo akalazimika kutoa mimba hiyo.
^^

Ni kweli lakini pia wew kama binti inabidi ufikilie kwa upande wako hasa negative effects za kutoa mimba...

Binafsi sioni mwanaume kukataa mimba au kukataa kukuoa ndiyo sababu ya wewe kutoa mimba...ona sasa leo una kila kitu ila umekosa mtoto na kukosa uko umesababisha wewe mwenyewe..

Tunapokataliwa tusikimbilie kumkuhumu mtoto kwa kumtoa....wewe kama binti chukua jukumu la kuwa mzazi..hakika Mungu hatakuacha katika malezi ya huyo mtoto mana ameiona nafsi yako ya kukubali kila aina ya matusi kutoka katika jamii inayotuzunguka mana kuzalia nyumbani inahitaji moyo...lakini Hili pia tulichukulie kama changamoto tusitoe mimba..
 
Tunafumbwa macho na starehe za mda mfupi na kusahau maisha ya mbele ambayo ni marefu na yanahitaji tumaini la jana. Kamkosea sana Mungu watoto 6? Akatubu halafu amlilie sana Mungu!
 
Ni kweli lakini pia wew kama binti inabidi ufikilie kwa upande wako hasa negative effects za kutoa mimba...

Binafsi sioni mwanaume kukataa mimba au kukataa kukuoa ndiyo sababu ya wewe kutoa mimba...ona sasa leo una kila kitu ila umekosa mtoto na kukosa uko umesababisha wewe mwenyewe..

Tunapokataliwa tusikimbilie kumkuhumu mtoto kwa kumtoa....wewe kama binti chukua jukumu la kuwa mzazi..hakika Mungu hatakuacha katika malezi ya huyo mtoto mana ameiona nafsi yako ya kukubali kila aina ya matusi kutoka katika jamii inayotuzunguka mana kuzalia nyumbani inahitaji moyo...lakini Hili pia tulichukulie kama changamoto tusitoe mimba..

^^
Asante sister nadhani kila msichana angejua uzito wa busara ulizosema hapa hususani adolescents bila shaka abortion ingefutika ktk kamusi ya dunia.
^^
 
Last edited by a moderator:
Dah aiseeh! Namsikitikia kwakweli. Kuna binti pia amemalza juz tu form four tayari ameshatolewa kizazi kwa sababu hiyo ,najaribu kutafakari nini hatma yake baadaye katka ndoa yake nabaki kumhurumia kwakweli!! So sad!

^^
Kumbe haya mambo yanaanza kuwa utamaduni,,hali kadhalika kuna mdada mmoja japo hakusoma amefanyiwa operesheni mwaka jana akaondolewa kizazi,
Tatizo ni nini? Uhuru wa mabinti umevuka mipaka? Au mimba kabla ya ndoa si hofu tena? Je vijana wamegeuka Devil's workshop kwa kukosa kazi za kufanya? Hata sielewi niwaze nini kilicho sahihi
^^
 
Ndio faida ya kuchoropoa hiyo! akubali matokeo tu..na bora mume wake ajue ili angalau atafute plan B.
 
^^
Asante sister nadhani kila msichana angejua uzito wa busara ulizosema hapa hususani adolescents bila shaka abortion ingefutika ktk kamusi ya dunia.
^^

Nashukuru....mana haya mambo bwana binti siku zote ndo anakuwa mwathirika kwa asilimia kubwa....mwanaume yeye ataoa mwingine na atazaa mwingine...wewe binti unakosa mtoto wa kuja kukutunza uzeeni unabaki kusema ningejua...na vilio juu...
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom