Baharia; (Ujasusi, Mapenzi na Upelelezi wa kutisha)

Kudo

JF-Expert Member
Nov 2, 2017
1,809
6,081
RIWAYA; BAHARIA

NA;BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

VITABU VILIVYOPITA.
• MPANGO WA CONGO
• DAKIKA ZA MWISHO
• URITHI WA GAIDI
• OPERESHENI JICHO LA PAKA
• SAUTI YA MTUTU
• MBWA WA GETI
• KALENDA YA IBILISI

******

--Gazeti Mwananchi—

Ndege ya shirika la ndege la Tanzania imepotea dakika ishirini tangu ilipoondoka kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa JNIA. Ndege hiyo ndogo ilibeba watalaamu wa tafiti za magonjwa ya binadamu wapatao watatu. Taarifa zaidi zinasema ndege hiyo ilikuwa ikielekea jijini mwanza katika uzinduzi wa tiba ya magonjwa ya akili na ukichaa kwa binadamu na wanyama, tiba ambayo ilikuwa imegunduliwa na watalamu hao.
Hadi gazeti hili linaingia mitamboni hakuna taarifa zaidi zinazohusu ndege hiyo na wagunduzi hao wa tiba ya magonjwa ya akili...

Siku mbilli mbele..

---Gazeti la Uhuru—

Mabaki ya ndege ya ATCL yamepatikana katika pori la akiba la Inara Njombe. Taarifa zaidi zinasema hakuna mabaki ya miili ya rubani ama matabibu waliokuwamo katika ndege hiyo. Uchunguzi zaidi bado unafanyika kubaini chanzo cha ajali hiyo na utafutaji wa abiria ambao walikuwa ni matabibu bado unaendelea ili kuthibitisha ni wazima au wamepoteza maisha. Tutazidi kukupa taarifa kupitia mitandao yetu ya kijamii kuhusu kile kinachoendelea…


----1------


Miezi nane badae

Unaweza kuwa ni ushamba ndio ulikuwa unamsumbua au la basi ni vile maji hayazoeleki. Ila kwa binti huyu ilikuwa ni ushamba na uoga tu zaidi ndivyo vilivyokuwa vikimsumbua mana kila mara alikuwa anawaza ukubwa wa bahari na vipi kama chombo walichomo kikizama? Mawazo yake yalimjengea woga katika nafsi yake na kila mara alikuwa anatajiwazia namna ambavyo atakuwa anahangaika kuinusuru roho yake wakati chombo hicho alichomo kikienda mrama.
Alichukua chupa ya pombe kali na kumiminia kwenye glasi na kufakamia funda kadhaa lengo likiwa ni kuichangmsha akili yake ili iende sawa na tukio lililokuwa likiendelea mle ndani ya meli kubwa wastani ila ya kifahari sana.
Ndani ya meli ile ya kampuni ya Serengeti Marine kulikuwa kuna tukio maalumu lililokuwa linaendelea kwenye moja ya kumbi za kisasa zilizoko mle kwa matukio maalumu.

Watu wawili walikuwa wanafunga ndoa, ndoa ambayo iliandikwa karibu na kila kituo cha radio; gazeti na runinga. Ilikuwa ni ndoa ya kifahari sana kuwahi kutokea ndani ya nchi ya Tanzania.

Vigegele vilikuwa ni kama vimemzindua binti yule ambae alikuwa amekaa mwishoni kabisa mwa ukumbi ule huku akili yake ikiwa imegawanyika mara mbili, huku akiwaza maji na huku akiwaza sherehe iliokuwa inaendelea.

Aliwatizama maharusi wale ambao walikuwa wanafuraha ya ajabu nyusoni mwao.

Akatabasamu huku na yeye akiungana na wanawake wengine kupiga vigelegele.

Harusi ile ilikuwa ni ya rafiki yake kipenzi alietwa Nyamizi.

Kiukweli katika maisha yake hakuwahi kudhani kama angefikia hatua ya kupanda meli na hakuwahi lau kufikiria kuipanda hata bahati mbaya tu,ila kwa upendo aliokuwa nao kwa rafiki yake wa karibu Nyamizi ulimfanya avunje kiapo chake cha kutokuja kuutumia usafiri huo wa majini.

Nyamizi alikuwa anaolewa na mchumba wake mfanyabiashara kijana kabisa alietwa Boneka na sherehe za ndoa yao waliamua kuzifanyia ndani ya meli ya ya Mv Upendo kutoka katika kampuni za Serengeti Marine.

Angewezaje kusimamia msimamo wake wakati rafiki yake kipenzi anafurahia ndoa yake, na angeonekanaje mbele ya watu waliojua vizuri mahusiano yake na Nyamizi!

Alihudhuria harusi ile ya aina yake na kila aliengia mle ndani alikuwa ni mtu alieheshimiwa na familia za pande mbili zote yani familia ya upande wa Boneka na familia ya upande wa Nyamizi.

Vedi alikuwa amecheza muziki na kuchoka na ndipo alipoenda kupumzika kwenye viti vilivyokuwa mle ukumbini huku watu wengine wakila na kunywa kwa furaha. Maharusi walikuwa wamekaa pahali maalumu palipokuwa pameandaliwa kwa ajili yao na kila aliehitaji kuwapa chochote alifika na kupiga nao picha na kufurahi pamoja.

Vedi pamoja na watu kadhaa walikuwa wameshafanya yote na baadhi walibaki ni kula na kunywa na wengine walielekea kujipumzisha kwenye vyumba vilivyokuwa vimeandaliwa kwa ajili yao ndani ya meli ile.

Meli ile ilikuwa imetengenezwa kwa oda maalumu ili kuvutia wateja wanaopenda kujipumzisha wakati wa safari, hivyo haikuwa na shida kwa walioikodi siku hiyo kutumia vyumba hivyo kujipumzisha na wale waliohitaji kukesha waliendelea kuserebuka wakila na kunywa.

Vedi hakuwa muumini mzuri wa kukesha ama kuserebuka usiku, hivyo pombe kidogo aliokunywa alijikuta ikimchanganya na alihitaji kujipumzisha.
Alimfuata mhudumu mmoja wa meli aliekuwapo maalumu kwa ajili ya kuelekeza watu mambo kadhaa kuhusu huduma walizohitaji. Aliomba kuelekezwa sehemu ya kulala mana alichoka kwa mserebuko aliokwisha serebuka.
Mhudumu yule alimpeleka upande wa chini wa meli ambako kulikuwa kumebaki na chumba kimoja tu baada ya vingine kuwa vimeshajaa na ni kama bahati kukipata hicho alichopata.

Alipokwisha kupewa chumba, alijitupa Kwenye kitanda kidogo kilichokuwa mle ambacho kilitosha kulala mtu mmoja tu, hakuhangaika hata kuvua viatu na usingizi ukampitia.

Ilikuwa karibu saa zima tangu alale, alisikia sauti kama za mabishano kutoka ndani ya vyumba vilivyokuwa kule chini.

Hakutilia mana sana kwa sababu kulikuwa kuna hekaheka nyingi kila pande ndani ya meli ile.

Aliendelea kuuchapa usingizi huku kichwa kikimuwia uzito wa kilo kadhaa kutokana na kugida pombe.

Mzozo uliendelea na sasa waliokuwa wanazozana walikuwa karibu na chumba chake. Vedi alistuka toka usinguzini tena, ila hakusikia kilichokuwa kikiongelewa vyema kulingana na kuwa na wenge la usingizi mzito.

Mkojo!.

Mkojo haunaga adabu siku zote, alibanwa na alijisikia kujisaidia ila kwa kuwa hakuwa mzoefu katika upandaji wa meli, hakuwa amejua upande vilipo vyoo na ukichanganya woga wa kupanda meli basi hakuwa amehangaika kabisa kujua vilipo vyoo.

Akanyanyuka kufungua kile chumba na kutoka nje ambako kulikuwa kuna korido pana na ilikuwa imetenganisha vyumba kadhaa ambavyo vingi vilikuwa vimeandikwa kuonesha vinatumika na mabaharia na vingine viliandikwa kwa kiitaliano na hakuelewa vilimaanisha nini.

Alizidi kuyumba kufuata korido ile upande mwingine tofauti na ule ambao waliingilia na baharia aliempeleka kwenye vyumba vile. Aliendelea kusonga taratibu huku kila mara akiyumba na kubeua.
Korido ile ilimfikisha hadi upande ambao kulikuwa kuna ngazi zilizokuwa zikishuka chini zaidi kwenye meli ile.

Wala hakujiuliza bali alizidi kwenda huku akisoma vyumba kadhaa vilivyokuwa na maandishi.

Kwa mbali alianza kusikia migongano ya vyuma na hewa nzito upande huo alikokuwa anaelekea.

Alikuwa amefika upande wa injini ya meli ile.

Akaamua kugeuza baada ya kuhisi hali ya hewa haiwezi kuwa rafiki nae tena.

Hakupiga hata hatua tatu akaona korido nyingine akaamua kuifuata korido hiyo ambayo ilimfikisha kwenye chumba kilichokuwa wazi na makororo mengi yalioonekana kuwa ya ufundi na dumu kadhaa za mafuta.

Kibofu kilikuwa kimejaa mkojo na ni lazima akojoe la sivyo angeadhirika.
Akaona chumba kile kinamfaa kumaliza shida zake harakaharaka ili arudi kuendelea kuukata usingizi wake kwa raha zake.

Tofauti na alivyodhani kwamba chumba kile ni kidogo,chumba kile kilikuwa kina upana wa kutosha tu na baada ya kuingia alibaini kwa mbele yake kulikuwa kuna taa zinawaka.

Hakujali!

Alianza kupapatua nguo zake za ndani na kuchuchumaaa huku akiwa amejibanza nyuma ya mapipa.
Alipokamilisha hitaji lake akasimama ili atoke kwenye kile chumba, ndipo aliposikia nyayo za miguu ya mtu ikiingia kwenye chumba kile kwa mwendo wa taratibu huku akijiongelesha peke yake.

Vedi akataka kutoka ili aendelee na hamsini zake akiamini ni miongoni mwa watu tu waliokuwa kwenye sherehe ndani ya zile meli.

Ila alijikuta anasita kutoka alipokuwa na kutulia kimya kabisa.
Mtu yule alimpita taratibu na kuelekea mbele kulikokuwa kuna waka taa.

Vedi alinyanyua kichwa chake taratibu na kumtizama mtu yule ambae alikuwa amevaa kofia kubwa ya pama kichwani mwake na koti zito mwilini mwake na alivaa suruali ya jinzi mpauko na mikono alikuwa ameiweka mfukoni.

Vedi alitoka pale alipokuwa akanyata na kujikinga nyuma ya pipa moja lililokuwa karibu na njia alioingilia na hapo aliweza kuona vyema upande ule kulikokuwa na mwanga wa taa.
Mtu yule safari yake iliishia kwenye kontena dogo na akalifungua kisha akaingia ndani yake.
Vedi alistajabu kidogo, tangu aingie mle ndani hajapata kuona mtu alievaa mavazi kama yale isipokuwa kila mtu alikuwa amevaa mavazi mazuri ya kuvutia na hata wahudumu na mabaharia kadhaa waliokuwa mle ndani walikuwa wamevaa mavazi maalumu kwa ajili ya sherehe ile ili watambulike kirahisi na wageni waliokuwa mle.
Sasa vipi tena mtu kuwe na mtu mwingine ambae hana mavazi maalumu na amevaa kiajabu ajabu namna ile?
Na ndani ya kile kikontena kafuata nini mtu yule.

Vedi hakuwa na wakumjibu na alitaka kutoka kuendelea na mambo mengine ila akajikuta anashindwa kufanya hivyo,hajui ni nini kilimsababisha kutaka kuendelea kubaki eneo lile.

Zilipita dakika zaidi ya tano bila kuonesha dalili ya kutoka kwa mtu yule na ndipo Vedi akataka kuondoka mana hakuona kama ni busara kuendelea kukaa pale.
Wakati anataka kunyanyuka ili aondoke,masikio yake yalinasa sauti ya muanguko wa kitu kama chuma kutokea kwenye kile kikontena,akarudi tena kujibanza pale alipokuwa awali na kutulia.
Haikupita dakika; mtu yule alieingia ndani ya kile kikontena akatoka huku akivaa kofia yake kichwani kwa mkono wa kulia.

Ajabu nyingine!

Mtu yule alikuwa amevaa miwani katika usiku ule.

Eeh makubwa!

Alijisemea Vedi huku sasa akiona mtu yule akimpita pale kwa mwendo wa haraka tofauti na mwanzo alivyoingia.

Mtu yule akatokomea akabisa na pale ndani alibaki Vedi peke yake.

Ni kiherehere chake tu kilichomsababisha aelekee kule kwenye kile kikontena,nae akaingia ndani yake.

Alikutana na giza zito na harufu kali ya kitu ambacho hakujua kama ni uozo ama ni vumbi lenye mchanganyiko wa vimiminika kadhaa.

Vedi akawasha simu Janja yake iliokuwa inamwanga wa kutosha tu kumulika mule ndani.

Tofauti na matarajio yake ya kuwa pengine mle ndani ni pachafu sana, la hasha kulikuwa ni kusafi licha ya kuwa kuna mpangilio wa meza za chuma mbili zilizokuwa zimewekwa kwa mtindo wa kulaliana, yani moja ilikuwa imesimamishwa kama kawaida na nyingine ilikuwa imesimamishwa kitako juu ya ile nyingine huku mgongo wake ukiwa umetazamana na Vedi na miguu ikiwa imetizama upande wa pili wa ile kontena.

Pale kwenye meza iliokuwa imeagamiwa na nyingine kulikuwa kuna kitabu kidogo cha kumbukumbu(Diary).

Hakukijali!!

Akapiga hatua zake taratibu na kuelekea kule ambako kulikuwa kuna miguu ya meza iliosimamishwa juu ya meza nyingine.

Alianza kwa kuona viatu vyeusi na suruali ilionza kutatuka,kisha akaona koti jeupe likiwa limefikia usawa wa magoti ya suruali aliiona.

Vedi akaanza kuingiwa na wasiwasi na alizidi kujongea na mara macho yake yakanasa taswaira ya ajabu kwenye miguu ya meza. Vedi aliruka juu na kupiga ukelele wa woga huku akirudi nyuma kwa hamaniko ya kile alichokiona.

Maiti ya mtu!!

Aliona mtu akiwa amesimama huku uhai ukiwa mbali na yeye,mtu yule alionekana kufa siku kadhaa nyuma na tayari ngozi yake ilianza kunatana na mifupa huku nyama na misuli ikiwa imeanza kuyeyuka mithili ya sponji.
Mtu yule alikuwa ameachama kuonesha alikufa kwa mateso na macho yake yalionekana kutumbuka kwa woga wa kifo kilichomkuta. Mikono ya yule mtu ilikuwa imetandazwa kwenye vyuma vilivyokuwa vinaunganisha miguu ya ile meza na miguu yake ilionekana kufungwa pamoja na kamba ambayo ilianza kuoza.

Ilikuwa picha ya kutisha machoni mwa Vedi;pombe yote ikamuisha na roho yake ikachafukwa.

Aliuwawa lini na kwanini; Vedi hakujua ila kitu pekee alichobaini ni kuwa mtu yule alikuwa amevaa mavazi maalumu ya wapishi wa meli, hasa koti lilikuwa limefanana sawa na makoti wanayovaa wapishi.

Mtu yule alikuwa baharia bila shaka kulingana na mavazi aliokuwa amevaa.

Vedi alishindwa kuelewa kwa nini jambo lile limetokea na kwanini auwawe afu aachwe mle mle ndani ya meli bila kutupwa kwenye maji au kuzikwa kabisa. Alishindwa kujua ni nini kusudi la kuihifadhiwa pale yule jamaa.

Au hawajui kama kuna mtu kafia kwenye karakana hii ya ufundi?

Hapana!!

Yule mtu aliemuona akiingia mle anaonekana anajua kinachoendelea ndani ya kikontena.

Aisee!!

Vedi alikurupuka kutoka alipokuwa na kutaka kukimbia kutoka nje ila wakati anafika kwenye meza iliobeba meza nyingine yenye maiti ya mtu, aliona tena kile kitabu kidogo cha kumbukumbu, akakiokota na kukitia kwenye mfuko wa koti la suti yake kisha akarudi tena kuitazama ile maiti na akaona kitambulisho kilichokuwa kinang’inia shingoni mwake, akaamua kukipiga picha na hapo akanasa sura nzuri ya kijana iliokuwa kwenye picha ndogo ilioambatanishwa kwenye kitambulisho kile. Ila hakuona jina kwenye kitambulisho kile na alipokuza picha aliopiga aliona likiwa kimekwanguliwa.

Kwa nini?
Hakujua sababu ya kukwanguliwa kwa jina kwenye kitambulisho kile.

Mikono ilikuwa ikimtetemeka na roho ilikuwa ikimdunda, hajawahi kuona mtu akiwa amekufa katika mateso namna ile.

Kwa nini wamekuuwa baharia!!?

Hakujibiwa na maiti ile.

Vedi aliamua kuondoka ndani ya kikontena kile, akapiga hatua chache na kabla hajatokeza kwenye mlango akasita kutoka.

Nje ya kikontena kile kulikuwa kuna mtu akiongea na mwenzie kwenye simu..
Kwa wizi wizi akarefusha shingo na kufanikiwa kuchungulia nje ya kikontena kile.

La haula!!

Alikuwa ni yule bwana aliemuona akiingia na kutoka ndani ya kikontena kile kidogo ambacho sasa yeye ndo alikuwamo.

Vedi alitamani kufanya miujiza ya kina Shumireta ya kupotea ila haikuwezekana, na alitamani apige kelele ila kwa alivyoona meli ile ilivyo hakuna ambae ambae angemsikia zaidi ya yule bwana ambae alikuwa nje ya kontena na alionekana sio mwema kabisa na wakati huu alikuwa amevua kofia na kufanya upara wake uonekane na kichwa chake kikubwa kilichojaa kisogoni.
Haieleweki sababu gani ilimfanya yule bwana avae miwani usiku.
Vedi alibaki akitetemeka.

Mara simu yake ikatetema kuashiria inaita.

Vedi akaruka juu na kuitupa chini na kuiacha ikisambaratika hovyo.

Aliiogopa mtetemo wa simu yake mwenyewe.

Yule bwana kule nje alisikia msambaratiko wa kitu kwenye kikontena kile na akageuka kutazama.

Ebanaee

Vedi mkojo uligonga hodi langoni kwa kalichumbage wake na jasho la kucha lilimtoka.

Tukutane badae!!
 
RIWAYA; BAHARIA

NA; BAHATI MWAMBA


SIMU; 0758573660


SEHEMU YA PILI


Yule bwana kule nje alisikia msambaratiko wa kitu kwenye kikontena kile na akageuka kutazama.

Ebanaee

Vedi mkojo uligonga hodi langoni kwa kalichumbage wake na jasho la kucha lilimtoka.

Bwana yule
hakuonekana kujali.

Pengine aliamini ni panya tu wanagombania mzoga au ni vyuma vilivyoko mle.

Aliendelea kuongea na simu bila wasiwasi wowote kisha alipomaliza akairudisha kwenye mfuko na kuanza kutoka tena kurudi nje ya chumba kile chenye zana za ufundi wa meli na pipa kadhaa za mafuta.

Vedi alishusha pumzi kwa nyingi na kumshukuru muumba wake.
Haraka haraka akajinyanyua pale alipokuwa ameangukia baada ya kusituliwa na mtetemo wa simu yake.
Akaanza kupapasa chini na alifanikiwa kupata mfuniko na betri na kisha kwa papara akaviunganisha na kuchukua mfuniko wa urembo(kava) na kulipachika juu kisha haraharaka akachomoka kama mshale hata vile viatu vyenye visigino virefu havikumpa shida kabisa kuzikata pepo.
Akatoa kabisa kule chini na kuanza kupanda juu kwa kasi huku akizehesabu ngazi kama mchezo na hatimae alifika kwenye korido ile ambayo kulikuwa kuna chumba alichokuwa amelala.
Akaingia harakaharaka na kufikia kitandani ambako kulikuwa kuna mkoba wake akaukwapua na kutaka kutoka, akakumbuka kitu…

Kwenye mgongo wa mfuniko wa simu na kava alikuwa amepachika kadi ya harusi iliokuwa na jina lake kamili.

Shiit!! Alimaka kwa gadhabu.

Haikuwepo!!

Aliitafuta huku na huko bila mafanikio alipekua kwenye mkoba bila kuipata na bado akili ilimwambia aliiweka kwenye mgongo wa simu yake na atakuwa ameiacha kule kwenye kile kikontena!!.

Mungu wangu!!

Alishika kichwa kwa huzuni mana asingeweza tena kurudi kule kukitafuta kikadi kile cha harusi ile.

Kitu kimoja alichohofia ni kuwa endapo polisi wangefika kuchunguza kule chini na kukikuta kadi ile basi yeye angekuwa mhusika wa kwanza kutafutwa.

Aligwaya zaidi baada ya kutokujua yule bwana aliemuona yupo upande upi hasa,kati ya usalama na watu waliohusika na mauaji yale.
Kama ni usalama na akirudi tena kule akute kile kikaratasi basi atamharibia.

Ila dah!!

Yule bwana hakufanania kuwa mtu wa usalama kwa mwonekano wake tu alionekana ni mtu wa shari shari na kichwa chake kizito kama mamumunya.
Vedi hakutaka kuendelea kuumiza akili yake kuhusu hilo jitu na kile kikaratasi, akafungua mlango na kutoka.

Ebanaee!!

Alikutana na yule bwana tena akitoka kwenye chumba cha jirani na kile alichokuwamo huku akiwa na kisu mkononi.

Vedi aliruka nyuma na kujingonga kwenye mlango huku akiachia ukelele wa woga na macho yake yakiwa kwenye kile kisu alichokuwa ameshika bwana yule huku nae akiwa ameganda kwa kushindwa kuelewa binti yule alihamanika nini baada ya kumuona.

Bwana yule akahamisha macho yake na kutazama mkono wake uliokuwa umeshika kisu,akatabasamu kifedhuli baada ya akili yake kuhisi pengine yule binti aliogopa kile kisu na namna alivyokishika.
Bwana yule akakivutia kwa juu na kisu kile kilipotelea kwenye mkono wa koti alilokuwa amevaa.

“No problem, relax and enjoy the night” alisema yule bwana huku akitabasamu kumuondoa Vedi kwenye hofu.

Vedi alianza kujisogeza huku mgongo ukiwa unajiburuza kwenye kuta za korido ile na macho yakiwa kwa yule bwana ambae nae alianza kuondoka kuelekea kule chini.
Vedi alipohakikisha yule bwana amepotelea kwenye kona nae akachomoka kwa kasi na kuelekea juu ukumbini, hakutaka tena kulala wala kuwaza kulala huku akiwa ameona jambo gumu kutazamika.

Alifika ukumbini,hakuna alichoona kipo cha kupendeza, hata watu alioona wanacheza aliona kama wanapoteza muda, waliokuwa wamekaa wanapiga soga za hapa na pale aliona kama ni watu wanaodhihaki maisha yake.

Kuna kitu kimoja kilimjia Vedi; alitamani sana kuweka bayana lile jambo na watu wakajua kinachoendelea ndani ya meli ile, lakini alijikuta akijawa na hofu kusema jambo lile na kama akisema ni nani wa kumwamini?

Aliona mtu pekee wa kumuamini ni Bi harusi Nyamizi; rafiki yake wavaa nikuvae.
Akataka kusimama kutoka alipo ili aende sehemu alipowaacha maharusi,ila hakuwaona. Aliangaza huku na huko mle ukumbini ila hakuwaona na hapo alihisi inaweza kuwa wameenda kujipumzisha baada ya hekaheka za kutwa na usiku ule.

Akataka kupiga simu, ila hakuona kama ni busara kumsumbua mtu na mkewe ambao walikuwa wamejipumzisha wakati huo.

Saa iliokuwa kwenye simu yake ilimwambia ni saa kumi kamili alfajiri.

Aliona muda haiuendi kabisa na kwa mujibu wa ratiba, wakati huo ndio wakati ambao meli ilitakiwa ifike kwenye fukwe za Pemba na kisha igeuze kurudi jijini Dar es laam na kila mtu arejee nyumbani kwake huku maharusi wakielekea jijini Nairobi kwa ajili ya fungate.

Kwake yeye aliona muda huo ni mwingi sana hadi kufika hiyo ahsubuhi ambayo ilipaswa meli itue nanga jijini Dar.

***
Shamra shamra zilikuwa zinaendelea na hata wale ambao walikuwa wamelala,sasa waliamka na kurudi tena ukumbini na wale ambao wamezoea kuukata ulabu, waliamkia supu iliokuwa imeandiliwa kwa ajili ya kukata pombe na wale wazee wa kubuma sana walikunywa supu kisha wakaendelea kugida pombe.

Ukumbi ni kama ulianza upya tena utadhani ndio sherehe zinaanza, kumbe ndio zilikuwa zinamalizikia.

Vedi alikuwa amekaa mwishoni kabisa mwa ukumbi na ambako hakukuwa na mwanga wa kutosha, alikuwa amekaa huku taswira ya maiti ikimrudia akilini mwake kila mara na ni kama aliona ikimlilia.

“Sasa unaninilia nikufanyeje!?” alijisemea peke yake akiwa amejikunyata kama kuku anaeumwa mdondo.

Wakati akiwa bado anatafakari hili na lile kuhusu kile alichokiona, mara akahisi karibu yake kuna mtu kapita, akanyanyua uso wake.

La haula!!

Alikuwa akitizama mgongo wa yule bwana ambae alionekana kama anaetafuta kitu au mtu katikati ya watu waliokuwa wakicheza na kunywa huku wengine wakiwa wamekaa kwenye viti na vilaji vyao kwenye meza.

Mtu yule alikuwa anapiga hatua taratibu huku akizungusha kichwa chake taratibu kama bundi awindae.
Hakujali msonagamano wa watu wengi waliokuwa mle ambao kimavazi ni yeye tu alienokena amevaa mavazi yasio rasimi na hayakuendana na hadhi za sherehe ile inayoelekea kufika ukomo.

Hilo hakujali bwana yule.

Kichwa chake kiliendelea kuzunguka taratibu huku akionekana kumakinika na kila mwanamke aliemuona mle ndani.

Hatimae yule bwana alipiga hatua na kuzidi kuelekea upande ambao kulikuwa kuna mpiga muziki na wachukua video kadhaa.
Akajichanganya nao, kisha akageuka na kuwa na nafasi nzuri zaidi ya kumtazama kila mtu kutokea kona ile maalumu kwa wapiga picha na muziki.
Bwana yule aliendelea kuzungusha kichwa chake alichokivika kofia huku macho akiwa ameyaziba na miwani nyeusi.

Macho ya yule bwana yaligota kwenye kona moja ambayo haikuwa na mwanga wa kutosha zaidi ya ule wa taa za rangi zilizokuwa zimefungwa upande ule.

Vedi alibaki akitetemeka baada ya kuona macho ya mtu yule yakiwa yameganda kutazama pale alipokuwa.

Hakika hakujua yule bwana alikuwa anamuwazia nini kama akiwa amemuona pale alipokuwa.

Na yakabaki maswali kadhaa kichwani mwa Vedi.

Kwa nini mtu yule kaingia mle ukumbini wakati huu? Na kwanini amtazame kiasi kile, vipi amejua kuwa aliingia kule kwenye kontena?

Mungu wangu; ananiwazia nini huyu?”alijiuliza Vedi bila kupata jibu.

“au amejua niliingia kule? Na amejuaje sasa” aliendelea kujiuliza bila kupata majibu.

Kadi!

Aliikumbuka ile kadi alioidondosha kule chini.

“ooh my God!!” alijishika kichwa Vedi baada ya kukumbuka kadi ile.

Lakini tena akajiuliza, kama ameikuta ile kadi, amejuaje kuwa ni mimi mmliki wake?

Aah shiit!! Alizidi kuchanganyikiwa Vedi.

Mtu yule alibaki akiangalia pale alipokuwa Vedi kwa zaidi ya dakika tano, kisha akamgusa mpiga picha mmoja na kumwelekeza jambo na bada ya hapo mpiga picha yule alielekeza kamera yake kule alikokuwa Vedi na kisha akapiga picha kadhaa hivi bila Vedi kutilia maanani maongezi ya mpiga picha na yule baradhuli.

Vedi hakujua kama anapigwa picha na kamera ile ambayo haikuwa na mwanga.

Vedi nae alikuwa bado anamuwaza mtu yule ambae wakati huo alikuwa ameshatoweka kwenye ukumbi ule.
.
“Mtu huyu ni nani lakini?” alijiuliza Vedi.

Mana hakuonekana kuwa ni baharia au Nahodha; hakuonekana kuwa hata tabibu wa dharura ndani ya meli ile.

Ni nani hasa ndani ya meli ile na yule mtu aliekufa kwanini hatupwi au kuzikwa?

Ebana e!

Maswali mengi kuliko majibu.

Vedi alitatizika na raha ya harusi ile kwake ikawa ni karaha huku akilaumu ni kwanini alifakamia pombe ambazo ziliishia kumletea mkojo uliompelekea kuona yale alioyaona.

**
Zilipita kama dakika kumi tu tangu mtu yule atoke ndani ya ukumbi ule, ndipo kikazuka kizazaa kilicholeta taharuki isiosemekana mwishoni mwa sherehe zile.

Ilikuwa ni wakati ambao mshehereshaji alipotangaza ya kuwa huko nje ya meli kuna binti aliejitupa ndani ya maji na sababu ya kufanya hivyo haikufahamika.

Watu wote walitoka na kuelekea nje ya ukumbi na kutazama kule ambako ilisemekana amejirusha, mabaharia kadhaa walikuwa wameshajitosa majini ili kuangalia uwezekano wa kumuona huyo aliejitupa majini.

Licha ya jitihada nyingi kufanyika kumtafuta, bado hawakufanikiwa na ndipo timu ya uokozi ilipopewa taarifa kutoka Dar es laam ili kufika hapo na kutoa msaada zaidi.

Wakati wa mapambazuko ndipo meli ipopiga honi kuashiria inafika ukomo wa safari baada ya kuzunguka baharini usiku mzima.


Nani tena kajitosa baharini? Ni vedi? Na kwanini sasa ajitose majini na kuacha ugali ukiliwa Duniani?

Kumjua aliejitosa, ungana nami hapa hapa
 
HATUTAKI RIWAYA ZENU MNAZOZIKATISHA KATIKAKATI. AMUENI MOJA KM MNAUZA AU MNATOA BURE

Sent using Jamii Forums mobile app
Sema hutaki wewe ila usisemee watu wote hapa jukwaani. Unataka riwaya zote anazotoa mwandishi aweke bure tu.

Waandishi wote hapa wameshatoa riwaya nyingi Sana bure. Binafsi mwaka jana pekee nimeweka hapa free novel Tisa mwanzo mwisho bila kuomba pesa ya mtu.

Mwaka huu tayari nimeweka free riwaya moja bure ambayo inaendelea hadi sasa(Urithi wa Gaidi).

Sapoti juhudi za wenzio kaka! Acha kulalamika.

Riwaya hii itafika mwisho, hivyo ni juhudi zako kusoma.
 
Sema hutaki wewe ila usisemee watu wote hapa jukwaani. Unataka riwaya zote anazotoa mwandishi aweke bure tu.

Waandishi wote hapa wameshatoa riwaya nyingi Sana bure. Binafsi mwaka jana pekee nimeweka hapa free novel Tisa mwanzo mwisho bila kuomba pesa ya mtu.

Mwaka huu tayari nimeweka free riwaya moja bure ambayo inaendelea hadi sasa(Urithi wa Gaidi).

Sapoti juhudi za wenzio kaka! Acha kulalamika.

Riwaya hii itafika mwisho, hivyo ni juhudi zako kusoma.
Iwekwe wazi watu wajue kama kunakulipia au la. Malalamiko ni mengi Sana humu ya watu kukatisha story kimya kimya. By the way Asante kwa kuweka baadhi ya story mpk mwisho.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Iwekwe wazi watu wajue kama kunakulipia au la. Malalamiko ni mengi Sana humu ya watu kukatisha story kimya kimya. By the way Asante kwa kuweka baadhi ya story mpk mwisho.

Sent using Jamii Forums mobile app
Anaelalamikia waadishi huyo si mpenzi wa riwaya ila anapotezea muda kwenye riwaya.

Mfano wakati nauza Mpango wa Congo,watu wengi walinifuata private na kuomba niwape bure kwa kuwa hawna pesa wakati huo, nami huwa sivungi niliwapa na wastarabu walilipa fadhila kwa nilichowafanyia. Lakini pia nilishusha bei hadi 1000/= ili kila mpenzi wa riwaya zangu apate kusoma.

Sasa ukiona mtu hadi hapo analalamika, huyo atakuwa na matatizo binafsi.

Ila wasomaji wengi huwa ni wakorofi sana Kaka. Wanatukana bila sababu na wanakejeli sana, ndio mana unakuta mtu anakasirika na kukimbia kimya kimya.

Hivyo tatizo sio la waandishi pekee, hata nyinyi wasomaji mnachangia pakubwa kukatishwa kwa riwaya, hamna lugha nzuri baadhi yenu.

Ila nadhani tukisikilizana na kuelewana hakika waandishi wengi watavutiwa kumaliza kazi zao ama kuleta kazi zao nyingi hapa jukwaani bila kinyongo.

Waandishi na wasomaji lazima tuwe na lugha moja na kusikilizana pia. Hakika waandishi watapenda kuweka kazi zao hapa jukwaani mwanzo mwisho bila kukatisha na kuuza watauza nanyi mtasapoti kiroho safi tu.
 
Anaelalamikia waadishi huyo si mpenzi wa riwaya ila anapotezea muda kwenye riwaya.

Mfano wakati nauza Mpango wa Congo,watu wengi walinifuata private na kuomba niwape bure kwa kuwa hawna pesa wakati huo, nami huwa sivungi niliwapa na wastarabu walilipa fadhila kwa nilichowafanyia. Lakini pia nilishusha bei hadi 1000/= ili kila mpenzi wa riwaya zangu apate kusoma.

Sasa ukiona mtu hadi hapo analalamika, huyo atakuwa na matatizo binafsi.

Ila wasomaji wengi huwa ni wakorofi sana Kaka. Wanatukana bila sababu na wanakejeli sana, ndio mana unakuta mtu anakasirika na kukimbia kimya kimya.

Hivyo tatizo sio la waandishi pekee, hata nyinyi wasomaji mnachangia pakubwa kukatishwa kwa riwaya, hamna lugha nzuri baadhi yenu.

Ila nadhani tukisikilizana na kuelewana hakika waandishi wengi watavutiwa kumaliza kazi zao ama kuleta kazi zao nyingi hapa jukwaani bila kinyongo.

Waandishi na wasomaji lazima tuwe na lugha moja na kusikilizana pia. Hakika waandishi watapenda kuweka kazi zao hapa jukwaani mwanzo mwisho bila kukatisha na kuuza watauza nanyi mtasapoti kiroho safi tu.
Pamoja mkuu shusha vitu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anaelalamikia waadishi huyo si mpenzi wa riwaya ila anapotezea muda kwenye riwaya.

Mfano wakati nauza Mpango wa Congo,watu wengi walinifuata private na kuomba niwape bure kwa kuwa hawna pesa wakati huo, nami huwa sivungi niliwapa na wastarabu walilipa fadhila kwa nilichowafanyia. Lakini pia nilishusha bei hadi 1000/= ili kila mpenzi wa riwaya zangu apate kusoma.

Sasa ukiona mtu hadi hapo analalamika, huyo atakuwa na matatizo binafsi.

Ila wasomaji wengi huwa ni wakorofi sana Kaka. Wanatukana bila sababu na wanakejeli sana, ndio mana unakuta mtu anakasirika na kukimbia kimya kimya.

Hivyo tatizo sio la waandishi pekee, hata nyinyi wasomaji mnachangia pakubwa kukatishwa kwa riwaya, hamna lugha nzuri baadhi yenu.

Ila nadhani tukisikilizana na kuelewana hakika waandishi wengi watavutiwa kumaliza kazi zao ama kuleta kazi zao nyingi hapa jukwaani bila kinyongo.

Waandishi na wasomaji lazima tuwe na lugha moja na kusikilizana pia. Hakika waandishi watapenda kuweka kazi zao hapa jukwaani mwanzo mwisho bila kukatisha na kuuza watauza nanyi mtasapoti kiroho safi tu.
Mpango wa Congo buku? Ofa ipo mpk sasa au imeisha?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
RIWAYA; BAHARIA

NA;BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

VITABU VILIVYOPITA.
• MPANGO WA CONGO
• DAKIKA ZA MWISHO
• URITHI WA GAIDI
• OPERESHENI JICHO LA PAKA
• SAUTI YA MTUTU
• MBWA WA GETI
• KALENDA YA IBILISI

******

--Gazeti Mwananchi—

Ndege ya shirika la ndege la Tanzania imepotea dakika ishirini tangu ilipoondoka kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa JNIA. Ndege hiyo ndogo ilibeba watalaamu wa tafiti za magonjwa ya binadamu wapatao watatu. Taarifa zaidi zinasema ndege hiyo ilikuwa ikielekea jijini mwanza katika uzinduzi wa tiba ya magonjwa ya akili na ukichaa kwa binadamu na wanyama, tiba ambayo ilikuwa imegunduliwa na watalamu hao.
Hadi gazeti hili linaingia mitamboni hakuna taarifa zaidi zinazohusu ndege hiyo na wagunduzi hao wa tiba ya magonjwa ya akili...

Siku mbilli mbele..

---Gazeti la Uhuru—

Mabaki ya ndege ya ATCL yamepatikana katika pori la akiba la Inara Njombe. Taarifa zaidi zinasema hakuna mabaki ya miili ya rubani ama matabibu waliokuwamo katika ndege hiyo. Uchunguzi zaidi bado unafanyika kubaini chanzo cha ajali hiyo na utafutaji wa abiria ambao walikuwa ni matabibu bado unaendelea ili kuthibitisha ni wazima au wamepoteza maisha. Tutazidi kukupa taarifa kupitia mitandao yetu ya kijamii kuhusu kile kinachoendelea…


----1------


Miezi nane badae

Unaweza kuwa ni ushamba ndio ulikuwa unamsumbua au la basi ni vile maji hayazoeleki. Ila kwa binti huyu ilikuwa ni ushamba na uoga tu zaidi ndivyo vilivyokuwa vikimsumbua mana kila mara alikuwa anawaza ukubwa wa bahari na vipi kama chombo walichomo kikizama? Mawazo yake yalimjengea woga katika nafsi yake na kila mara alikuwa anatajiwazia namna ambavyo atakuwa anahangaika kuinusuru roho yake wakati chombo hicho alichomo kikienda mrama.
Alichukua chupa ya pombe kali na kumiminia kwenye glasi na kufakamia funda kadhaa lengo likiwa ni kuichangmsha akili yake ili iende sawa na tukio lililokuwa likiendelea mle ndani ya meli kubwa wastani ila ya kifahari sana.
Ndani ya meli ile ya kampuni ya Serengeti Marine kulikuwa kuna tukio maalumu lililokuwa linaendelea kwenye moja ya kumbi za kisasa zilizoko mle kwa matukio maalumu.

Watu wawili walikuwa wanafunga ndoa, ndoa ambayo iliandikwa karibu na kila kituo cha radio; gazeti na runinga. Ilikuwa ni ndoa ya kifahari sana kuwahi kutokea ndani ya nchi ya Tanzania.

Vigegele vilikuwa ni kama vimemzindua binti yule ambae alikuwa amekaa mwishoni kabisa mwa ukumbi ule huku akili yake ikiwa imegawanyika mara mbili, huku akiwaza maji na huku akiwaza sherehe iliokuwa inaendelea.

Aliwatizama maharusi wale ambao walikuwa wanafuraha ya ajabu nyusoni mwao.

Akatabasamu huku na yeye akiungana na wanawake wengine kupiga vigelegele.

Harusi ile ilikuwa ni ya rafiki yake kipenzi alietwa Nyamizi.

Kiukweli katika maisha yake hakuwahi kudhani kama angefikia hatua ya kupanda meli na hakuwahi lau kufikiria kuipanda hata bahati mbaya tu,ila kwa upendo aliokuwa nao kwa rafiki yake wa karibu Nyamizi ulimfanya avunje kiapo chake cha kutokuja kuutumia usafiri huo wa majini.

Nyamizi alikuwa anaolewa na mchumba wake mfanyabiashara kijana kabisa alietwa Boneka na sherehe za ndoa yao waliamua kuzifanyia ndani ya meli ya ya Mv Upendo kutoka katika kampuni za Serengeti Marine.

Angewezaje kusimamia msimamo wake wakati rafiki yake kipenzi anafurahia ndoa yake, na angeonekanaje mbele ya watu waliojua vizuri mahusiano yake na Nyamizi!

Alihudhuria harusi ile ya aina yake na kila aliengia mle ndani alikuwa ni mtu alieheshimiwa na familia za pande mbili zote yani familia ya upande wa Boneka na familia ya upande wa Nyamizi.

Vedi alikuwa amecheza muziki na kuchoka na ndipo alipoenda kupumzika kwenye viti vilivyokuwa mle ukumbini huku watu wengine wakila na kunywa kwa furaha. Maharusi walikuwa wamekaa pahali maalumu palipokuwa pameandaliwa kwa ajili yao na kila aliehitaji kuwapa chochote alifika na kupiga nao picha na kufurahi pamoja.

Vedi pamoja na watu kadhaa walikuwa wameshafanya yote na baadhi walibaki ni kula na kunywa na wengine walielekea kujipumzisha kwenye vyumba vilivyokuwa vimeandaliwa kwa ajili yao ndani ya meli ile.

Meli ile ilikuwa imetengenezwa kwa oda maalumu ili kuvutia wateja wanaopenda kujipumzisha wakati wa safari, hivyo haikuwa na shida kwa walioikodi siku hiyo kutumia vyumba hivyo kujipumzisha na wale waliohitaji kukesha waliendelea kuserebuka wakila na kunywa.

Vedi hakuwa muumini mzuri wa kukesha ama kuserebuka usiku, hivyo pombe kidogo aliokunywa alijikuta ikimchanganya na alihitaji kujipumzisha.
Alimfuata mhudumu mmoja wa meli aliekuwapo maalumu kwa ajili ya kuelekeza watu mambo kadhaa kuhusu huduma walizohitaji. Aliomba kuelekezwa sehemu ya kulala mana alichoka kwa mserebuko aliokwisha serebuka.
Mhudumu yule alimpeleka upande wa chini wa meli ambako kulikuwa kumebaki na chumba kimoja tu baada ya vingine kuwa vimeshajaa na ni kama bahati kukipata hicho alichopata.

Alipokwisha kupewa chumba, alijitupa Kwenye kitanda kidogo kilichokuwa mle ambacho kilitosha kulala mtu mmoja tu, hakuhangaika hata kuvua viatu na usingizi ukampitia.

Ilikuwa karibu saa zima tangu alale, alisikia sauti kama za mabishano kutoka ndani ya vyumba vilivyokuwa kule chini.

Hakutilia mana sana kwa sababu kulikuwa kuna hekaheka nyingi kila pande ndani ya meli ile.

Aliendelea kuuchapa usingizi huku kichwa kikimuwia uzito wa kilo kadhaa kutokana na kugida pombe.

Mzozo uliendelea na sasa waliokuwa wanazozana walikuwa karibu na chumba chake. Vedi alistuka toka usinguzini tena, ila hakusikia kilichokuwa kikiongelewa vyema kulingana na kuwa na wenge la usingizi mzito.

Mkojo!.

Mkojo haunaga adabu siku zote, alibanwa na alijisikia kujisaidia ila kwa kuwa hakuwa mzoefu katika upandaji wa meli, hakuwa amejua upande vilipo vyoo na ukichanganya woga wa kupanda meli basi hakuwa amehangaika kabisa kujua vilipo vyoo.

Akanyanyuka kufungua kile chumba na kutoka nje ambako kulikuwa kuna korido pana na ilikuwa imetenganisha vyumba kadhaa ambavyo vingi vilikuwa vimeandikwa kuonesha vinatumika na mabaharia na vingine viliandikwa kwa kiitaliano na hakuelewa vilimaanisha nini.

Alizidi kuyumba kufuata korido ile upande mwingine tofauti na ule ambao waliingilia na baharia aliempeleka kwenye vyumba vile. Aliendelea kusonga taratibu huku kila mara akiyumba na kubeua.
Korido ile ilimfikisha hadi upande ambao kulikuwa kuna ngazi zilizokuwa zikishuka chini zaidi kwenye meli ile.

Wala hakujiuliza bali alizidi kwenda huku akisoma vyumba kadhaa vilivyokuwa na maandishi.

Kwa mbali alianza kusikia migongano ya vyuma na hewa nzito upande huo alikokuwa anaelekea.

Alikuwa amefika upande wa injini ya meli ile.

Akaamua kugeuza baada ya kuhisi hali ya hewa haiwezi kuwa rafiki nae tena.

Hakupiga hata hatua tatu akaona korido nyingine akaamua kuifuata korido hiyo ambayo ilimfikisha kwenye chumba kilichokuwa wazi na makororo mengi yalioonekana kuwa ya ufundi na dumu kadhaa za mafuta.

Kibofu kilikuwa kimejaa mkojo na ni lazima akojoe la sivyo angeadhirika.
Akaona chumba kile kinamfaa kumaliza shida zake harakaharaka ili arudi kuendelea kuukata usingizi wake kwa raha zake.

Tofauti na alivyodhani kwamba chumba kile ni kidogo,chumba kile kilikuwa kina upana wa kutosha tu na baada ya kuingia alibaini kwa mbele yake kulikuwa kuna taa zinawaka.

Hakujali!

Alianza kupapatua nguo zake za ndani na kuchuchumaaa huku akiwa amejibanza nyuma ya mapipa.
Alipokamilisha hitaji lake akasimama ili atoke kwenye kile chumba, ndipo aliposikia nyayo za miguu ya mtu ikiingia kwenye chumba kile kwa mwendo wa taratibu huku akijiongelesha peke yake.

Vedi akataka kutoka ili aendelee na hamsini zake akiamini ni miongoni mwa watu tu waliokuwa kwenye sherehe ndani ya zile meli.

Ila alijikuta anasita kutoka alipokuwa na kutulia kimya kabisa.
Mtu yule alimpita taratibu na kuelekea mbele kulikokuwa kuna waka taa.

Vedi alinyanyua kichwa chake taratibu na kumtizama mtu yule ambae alikuwa amevaa kofia kubwa ya pama kichwani mwake na koti zito mwilini mwake na alivaa suruali ya jinzi mpauko na mikono alikuwa ameiweka mfukoni.

Vedi alitoka pale alipokuwa akanyata na kujikinga nyuma ya pipa moja lililokuwa karibu na njia alioingilia na hapo aliweza kuona vyema upande ule kulikokuwa na mwanga wa taa.
Mtu yule safari yake iliishia kwenye kontena dogo na akalifungua kisha akaingia ndani yake.
Vedi alistajabu kidogo, tangu aingie mle ndani hajapata kuona mtu alievaa mavazi kama yale isipokuwa kila mtu alikuwa amevaa mavazi mazuri ya kuvutia na hata wahudumu na mabaharia kadhaa waliokuwa mle ndani walikuwa wamevaa mavazi maalumu kwa ajili ya sherehe ile ili watambulike kirahisi na wageni waliokuwa mle.
Sasa vipi tena mtu kuwe na mtu mwingine ambae hana mavazi maalumu na amevaa kiajabu ajabu namna ile?
Na ndani ya kile kikontena kafuata nini mtu yule.

Vedi hakuwa na wakumjibu na alitaka kutoka kuendelea na mambo mengine ila akajikuta anashindwa kufanya hivyo,hajui ni nini kilimsababisha kutaka kuendelea kubaki eneo lile.

Zilipita dakika zaidi ya tano bila kuonesha dalili ya kutoka kwa mtu yule na ndipo Vedi akataka kuondoka mana hakuona kama ni busara kuendelea kukaa pale.
Wakati anataka kunyanyuka ili aondoke,masikio yake yalinasa sauti ya muanguko wa kitu kama chuma kutokea kwenye kile kikontena,akarudi tena kujibanza pale alipokuwa awali na kutulia.
Haikupita dakika; mtu yule alieingia ndani ya kile kikontena akatoka huku akivaa kofia yake kichwani kwa mkono wa kulia.

Ajabu nyingine!

Mtu yule alikuwa amevaa miwani katika usiku ule.

Eeh makubwa!

Alijisemea Vedi huku sasa akiona mtu yule akimpita pale kwa mwendo wa haraka tofauti na mwanzo alivyoingia.

Mtu yule akatokomea akabisa na pale ndani alibaki Vedi peke yake.

Ni kiherehere chake tu kilichomsababisha aelekee kule kwenye kile kikontena,nae akaingia ndani yake.

Alikutana na giza zito na harufu kali ya kitu ambacho hakujua kama ni uozo ama ni vumbi lenye mchanganyiko wa vimiminika kadhaa.

Vedi akawasha simu Janja yake iliokuwa inamwanga wa kutosha tu kumulika mule ndani.

Tofauti na matarajio yake ya kuwa pengine mle ndani ni pachafu sana, la hasha kulikuwa ni kusafi licha ya kuwa kuna mpangilio wa meza za chuma mbili zilizokuwa zimewekwa kwa mtindo wa kulaliana, yani moja ilikuwa imesimamishwa kama kawaida na nyingine ilikuwa imesimamishwa kitako juu ya ile nyingine huku mgongo wake ukiwa umetazamana na Vedi na miguu ikiwa imetizama upande wa pili wa ile kontena.

Pale kwenye meza iliokuwa imeagamiwa na nyingine kulikuwa kuna kitabu kidogo cha kumbukumbu(Diary).

Hakukijali!!

Akapiga hatua zake taratibu na kuelekea kule ambako kulikuwa kuna miguu ya meza iliosimamishwa juu ya meza nyingine.

Alianza kwa kuona viatu vyeusi na suruali ilionza kutatuka,kisha akaona koti jeupe likiwa limefikia usawa wa magoti ya suruali aliiona.

Vedi akaanza kuingiwa na wasiwasi na alizidi kujongea na mara macho yake yakanasa taswaira ya ajabu kwenye miguu ya meza. Vedi aliruka juu na kupiga ukelele wa woga huku akirudi nyuma kwa hamaniko ya kile alichokiona.

Maiti ya mtu!!

Aliona mtu akiwa amesimama huku uhai ukiwa mbali na yeye,mtu yule alionekana kufa siku kadhaa nyuma na tayari ngozi yake ilianza kunatana na mifupa huku nyama na misuli ikiwa imeanza kuyeyuka mithili ya sponji.
Mtu yule alikuwa ameachama kuonesha alikufa kwa mateso na macho yake yalionekana kutumbuka kwa woga wa kifo kilichomkuta. Mikono ya yule mtu ilikuwa imetandazwa kwenye vyuma vilivyokuwa vinaunganisha miguu ya ile meza na miguu yake ilionekana kufungwa pamoja na kamba ambayo ilianza kuoza.

Ilikuwa picha ya kutisha machoni mwa Vedi;pombe yote ikamuisha na roho yake ikachafukwa.

Aliuwawa lini na kwanini; Vedi hakujua ila kitu pekee alichobaini ni kuwa mtu yule alikuwa amevaa mavazi maalumu ya wapishi wa meli, hasa koti lilikuwa limefanana sawa na makoti wanayovaa wapishi.

Mtu yule alikuwa baharia bila shaka kulingana na mavazi aliokuwa amevaa.

Vedi alishindwa kuelewa kwa nini jambo lile limetokea na kwanini auwawe afu aachwe mle mle ndani ya meli bila kutupwa kwenye maji au kuzikwa kabisa. Alishindwa kujua ni nini kusudi la kuihifadhiwa pale yule jamaa.

Au hawajui kama kuna mtu kafia kwenye karakana hii ya ufundi?

Hapana!!

Yule mtu aliemuona akiingia mle anaonekana anajua kinachoendelea ndani ya kikontena.

Aisee!!

Vedi alikurupuka kutoka alipokuwa na kutaka kukimbia kutoka nje ila wakati anafika kwenye meza iliobeba meza nyingine yenye maiti ya mtu, aliona tena kile kitabu kidogo cha kumbukumbu, akakiokota na kukitia kwenye mfuko wa koti la suti yake kisha akarudi tena kuitazama ile maiti na akaona kitambulisho kilichokuwa kinang’inia shingoni mwake, akaamua kukipiga picha na hapo akanasa sura nzuri ya kijana iliokuwa kwenye picha ndogo ilioambatanishwa kwenye kitambulisho kile. Ila hakuona jina kwenye kitambulisho kile na alipokuza picha aliopiga aliona likiwa kimekwanguliwa.

Kwa nini?
Hakujua sababu ya kukwanguliwa kwa jina kwenye kitambulisho kile.

Mikono ilikuwa ikimtetemeka na roho ilikuwa ikimdunda, hajawahi kuona mtu akiwa amekufa katika mateso namna ile.

Kwa nini wamekuuwa baharia!!?

Hakujibiwa na maiti ile.

Vedi aliamua kuondoka ndani ya kikontena kile, akapiga hatua chache na kabla hajatokeza kwenye mlango akasita kutoka.

Nje ya kikontena kile kulikuwa kuna mtu akiongea na mwenzie kwenye simu..
Kwa wizi wizi akarefusha shingo na kufanikiwa kuchungulia nje ya kikontena kile.

La haula!!

Alikuwa ni yule bwana aliemuona akiingia na kutoka ndani ya kikontena kile kidogo ambacho sasa yeye ndo alikuwamo.

Vedi alitamani kufanya miujiza ya kina Shumireta ya kupotea ila haikuwezekana, na alitamani apige kelele ila kwa alivyoona meli ile ilivyo hakuna ambae ambae angemsikia zaidi ya yule bwana ambae alikuwa nje ya kontena na alionekana sio mwema kabisa na wakati huu alikuwa amevua kofia na kufanya upara wake uonekane na kichwa chake kikubwa kilichojaa kisogoni.
Haieleweki sababu gani ilimfanya yule bwana avae miwani usiku.
Vedi alibaki akitetemeka.

Mara simu yake ikatetema kuashiria inaita.

Vedi akaruka juu na kuitupa chini na kuiacha ikisambaratika hovyo.

Aliiogopa mtetemo wa simu yake mwenyewe.

Yule bwana kule nje alisikia msambaratiko wa kitu kwenye kikontena kile na akageuka kutazama.

Ebanaee

Vedi mkojo uligonga hodi langoni kwa kalichumbage wake na jasho la kucha lilimtoka.

Tukutane badae!!
Duuh

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anaelalamikia waadishi huyo si mpenzi wa riwaya ila anapotezea muda kwenye riwaya.

Mfano wakati nauza Mpango wa Congo,watu wengi walinifuata private na kuomba niwape bure kwa kuwa hawna pesa wakati huo, nami huwa sivungi niliwapa na wastarabu walilipa fadhila kwa nilichowafanyia. Lakini pia nilishusha bei hadi 1000/= ili kila mpenzi wa riwaya zangu apate kusoma.

Sasa ukiona mtu hadi hapo analalamika, huyo atakuwa na matatizo binafsi.

Ila wasomaji wengi huwa ni wakorofi sana Kaka. Wanatukana bila sababu na wanakejeli sana, ndio mana unakuta mtu anakasirika na kukimbia kimya kimya.

Hivyo tatizo sio la waandishi pekee, hata nyinyi wasomaji mnachangia pakubwa kukatishwa kwa riwaya, hamna lugha nzuri baadhi yenu.

Ila nadhani tukisikilizana na kuelewana hakika waandishi wengi watavutiwa kumaliza kazi zao ama kuleta kazi zao nyingi hapa jukwaani bila kinyongo.

Waandishi na wasomaji lazima tuwe na lugha moja na kusikilizana pia. Hakika waandishi watapenda kuweka kazi zao hapa jukwaani mwanzo mwisho bila kukatisha na kuuza watauza nanyi mtasapoti kiroho safi tu.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha nijaribu na huku,km ni walewale,basi jf ntakuwa nimekosa simulizi kali zinazofika hadi mwisho.
Nhamie kwny jukwaa letu pendwa intelligent forum

Bado Naendelea Kujifunza
 
RIWAYA; BAHARIA

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA TATU



Watu wote walitoka na kuelekea nje ya ukumbi na kutazama kule ambako ilisemekana amejirusha, mabaharia kadhaa walikuwa wameshajitosa majini ili kuangalia uwezekano wa kumuona huyo aliejitupa majini.

Licha ya jitihada nyingi kufanyika kumtafuta, bado hawakufanikiwa na ndipo timu ya uokozi ilipopewa taarifa kutoka Dar es laam ili kufika hapo na kutoa msaada zaidi.

Wakati wa mapambazuko ndipo meli ipopiga honi kuashiria inafika ukomo wa safari baada ya kuzunguka baharini usiku mzima.

***

Vedi alishuka kwenye meli na kupita moja kwa moja hadi nje ya eneo la abiria, huko alichukua usafiri na kurudi nyumbani kwake alikokuwa amepanga.
Alipofika akaingia ndani na kujitupa kwenye sofa iliokuwa sebuleni kwake kisha akapumua kwa nguvu na kutupa viatu vyake virefu bila kujali vitakapoangukia.

Vedi alipumua kwa nguvu na kutazama juu kwa tafakuri.

Akakurupuka!

Akauendea mkoba wake mdogo uliokuwa na vitu vyake baadhi na alikuwa nao ndani ya meli.

Akaufungua na kupangua vitu kadhaa vya kujirembea pamoja na taulo ya kike ambayo aliiweka kwa dharura.

Hatimae macho yake yalipata kile alichokitaka.

Kilikuwa ni kile Kitabu kidogo cha kumbukumbu alichokichukua ndani ya kikontena wakati alipokuwa ndani ya meli.

Akakifunua!

Alikutana na mambo machache katika ukurasa wa kwanza na alipoyasoma hakuona kama ndicho alichokihitaji katika kitabu kile.

Kwanza alihitaji kujua kama kitabu kile kimeandikwa kwa matumizi sahihi ya kitabu chenyewe, yani kimeandikwa mambo muhimu ya mmiliki wake. Pia alihitaji kujua kama atafanikiwa kujua kama mmiliki aliandika jina lake na watu wake wa muhimu ikiwemo na mawasiliano yao..

Katika ukurasa uliofuata alikuta jina na tarehe.

“Banzi Kela….tarehe 06/4/2017”

Akafunua tena kurasa nyingine na alifanya hivyo ili kujiridhisha na mawazo yake.

Baada ya kusoma maelezo ya ukurasa ule akarudi tena kwenye ukurasa ambao ulikuwa na jina na tarehe na hapo ndipo alijiridhisha na fikira zake ya kuwa kitabu kile kilianza kutumika tarehe ile na yawezekana lile neno Banzi Kela ni jina na ni la mmiliki wake.

Kichwani mwake akapitisha jina hilo na umiliki wa kitabu kile.

Aliendelea kufungua kurasa moja na nyingine na kusoma yaliondikwa hatimae alifika kwenye ukurasa uliokuwa umeandikwa ujumbe maalumu kwa ajili ya mtu ambae aliamini ni mpenzi wa Banzi.

“Kwako Mamu!
Ni ukweli nakupenda sana kuliko sana yenyewe. Mamu najua unanipenda pia, ila kwa tulipofikia inabidi niwe mbali na wewe. Sio kama umenikosea la hasha ni kwa kuwa tu nataka uishi kwa amani zaidi ukiwa mbali na mimi. Hivi sasa mimi si Banzi tena ila ni marehemu mtarajiwa Banzi. Usiniulize kwanini ila kabla ya kuuliza nenda Hard Rock kwa Jezebeli anaujumbe wa matumaini yangu.” Ulisomeka hivyo ujumbe ule.

Vedi aliganda kwa sekunde kadhaa baada ya kuusoma.

Ni kawaida kwa wapenzi kuandikiana jumbe nyingi, ila ni mara chache kuandikiana jumbe za kutisha na kusononesha namna ile.

Banzi alikuwa na mpenzi anaitwa Mamu na anamtahadharisha juu ya mauti yanayotembea nae.

Mh!!

Vedi akaguna huku akijiweka sawa kwenye sofa yake.

Kwanini sasa Banzi ajitabilie kifo? Na je ujumbe ule ulimfikia Mamu mwenyewe?

Hakuwa na majibu wala wa kumjibu.

Haraka haraka akaanza kupitia kurasa moja na nyingine,alikuwa anatafuta lau mawasiliano ya huyo Mamu na aliamini kabisa mawasiliano yatakuwemo mule.

Hadi anamaliza kukipitia bado hakuwa amebahatika kuona namba yoyote ile ya simu.

Akarudia tena kupitia kwa mara nyingine, bado hali ilikuwa ile ile.

Mh!!.

Akaguna peke yake na kurudi pale kwenye ukurasa wa ujumbe wa Mamu.

Kuna kitu alikiona..

Katika ukurasa ule mwishoni kabisa kulikuwa kuna namba imeandikwa na ilikuwa ni sifuri..

Alifunua tena ukurasa mwingine na hakuona namba ila uliofuata aliona tena namba ikiwa imeandikwa na ilikuwa ni namba Saba.

Akaendelea kupitia na kuzinakili namba zile kwenye simu yake na zilikuwa ni namba kumi kwa ujumla wake.

Aisee!!
.
Vedi alishangaa akili nyingi za Banzi. Banzi alikuwa anasababu gani kuficha namba zile katika aina ile?.

Vedi alijiaminisha kabisa ya kuwa kuna kitu kilikuwa kinaendelea kwa Banzi si bure.

Akajaribu kuzipiga zile namba.

Simu haikutoka!!..

Vedi akarudia tena na hali ilikuwa ile ile.

Akatazama ntandao katika simu yake na alikuta upo chini hausomi.

Ebo!!
.
Na laini iliandika “emergency”

Aisee!!

Tatizo nini?

Hakupata wa kumjibu.

Alibaki akiwa amefadhaika.

Akajinyanyua kwenye sofa na kuelekea ndani kwake ambako alichukua ndoo ya maji na kumimina kwenye ndoo nyingine maalumu ya kuogea kisha akatoka nje na kwenda kuoga ili kuondoa uchovu wa usiku uliopita.
.

Dakika kadhaa badae alitoka na kukuta wapangaji wenzie wakiwa wamekaa vibalazani mwao, akawasabahi na kuelekea ndani kwake.

Akaanza kujiremba harakaharaka ili awahi kituo cha kusajilia laini apate utatuzi wa laini yake kisha amtafute mmiliki wa namba alioikuta kwenye kitabu cha Banzi.

Wakati anaendelea kujipara akachukua kitenzambali(rimoti) na kuwasha runinga.

Alikutana na habari ambayo ilikuwa inamalizikia ila alisikia jina lake likitajwa na kisha zikafuatia picha ambazo zilipigwa wakati mabaharia wakijitahidi kuokoa mtu aliesemekana kujitosa baharini.

Roho ilianza kwenda mbio na kushindwa kuelewa dhumuni la jina lake na picha za uokozi.

Habari iliishia na hakuambua japo maana ya kile alichokiona mwishoni.

Akarukia simu yake kwa pupa, mara akanywea kama maji katikati ya vumbi baada ya kukumbuka simu yake haisomi mtandao.

Akavaa haraka haraka na kutoka nje.
.
Ebwana eeh!

Alishangaa wadada wawili wakirukia ndani kwao kama walioona jini katikati ya kiza kinene huku wakipiga ukunga wa kuogopa.

Alisita kutoka mlangoni kwake akabaki akitizama milango ya wadada wale.

Mhh kuna nini tena?

Alijiuliza peke yake huku hisia mbaya zikianza kumwandama kichwani mwake.


“ooh no! Isiwe kweli basi” Alijisemea huku machozi yakianza kumlenga.

Kuna hisia mbaya ilipita ubongoni mwake kuhusu habari alioona inamalizikia.

Alihisi anahusanishwa katika kifo kile cha mtu kujitupa ndani ya maji.

“Au ile maiti imetupwa majini na uchunguzi umeangukia kwangu baada ya kuacha kadi ile…” Alijikuta akitoa chozi huku akianza kupiga hatua ndefu kutoka pale alipokuwa amesimama.

Haraka yake ilikuwa ni kufika kwa kijana anaesajili laini za simu aliekuwa jirani na hapo alipokuwa akiishi.

Aliihitaji laini ili awasiliane na wazazi wake na kisha amtafute mmiliki wa namba alioipata kwenye kitabu cha kumbukumbu alichokitoa ndani ya meli.

Alitembea kwa hatua za haraka haraka na kuvuka barabara kisha akapita vichochoro viwili na kutokea sehemu iliokuwa imechangamka kidogo.

Akaangaza kidogo na kumuona kijana aliemhitaji ambae wakati huo alikuwa amezungukwa na mabinti wengine wawili waliionekana kuhudumiwa.

“Mambo!” Vedi alimsabahi kijana yule huku akimshika bega kwa nyuma na kijana yule akageuka.

Loh!

Kijana akaruka juu kama shoga lililotekenywa na mtoto.

Hakuishia kuruka tu, akapiga kelele kwa sauti huku akirusha mikono yake kama mtu anaeshambuliwa na nyuki na kitendo kile kilifanya wale mabinti waliokuwa wakihudumiwa nao waanze kutimua mbio huku wakipiga kelele bila kujua wanapiga kwa sababu gani.

Vedi alivutwaika.

Macho yake hayakubanduka kwa yule kijana ambae alikuwa amefika mbali kidogo na kugeuka huku akiwaeleza jambo watu waliokuwa wameanza kujaa kumshangaa.

Vedi alishindwa kuelewa.

Macho ya Vedi yalitua kwenye meza ya kazi ya yule kijana,aliona simu janja ya kijana yule na ilikuwa bado inaonesha mwanga kuashiria ilikuwa kwenye matumizi dakika chache zilizopita.

Akavutiwa na kile alichokiona.

Akaichukua simu ile na kuanza kusoma.

Ebana eeh!

Vedi aliishiwa akili ya kufikiri na kujikuta machozi ya kimtoka huku nafsini mwake kukiwa na sauti kubwa ya kupingana na jambo lile.

Alirudi tena kusoma na hakikuwa kimebadilika kitu.

Alikuwa anasoma katika tovuti moja ya kuwa mtu aliejurusha ndani ya maji amaekolewa na kufahamika kwa jina la Vedi Mashimo mkazi wa kisutu Dar es laam.

Kisutu ndio aliishi na hilo jina ni lake na sio jina tu hata picha zilikuwapo za kwake kuonesha yeye ndie alijitosa baharini na kupoteza maisha.

Akairejesha ile simu na kupiga hatua kuelekea nyumbani kwake; Baadhi ya watu waliomfahamu wakajiweka mbali nae.

Vedi alifadhaika kwa kitendo kile,machozi yalimtoka na mwili ulimwia uzito na kujikuta akipiga hatua za kinyonga.

Akajitahidi na kurejea nyumbani kwake, ila wakati anaingia tena, majirani zake wakaanza kupiga kelele za woga huku wakiita jini jini.

Hakuwajali akaingia ndani kwake ambako wakati anatoka hakufunga mlango.

Ebana eeh!

Ndani napo hakukuta mabegi yake ya nguo na viatu na baadhi ya picha pia zilichukuliwa huku akiachiwa mkoba tu ambao alikuwa ameuangusha uvunguni mwa meza.

Akachanganyikiwa!

Haraka akatoka nje na kuelekea upande wa pili ambako aliamini waliochukua vitu vyake ni lazima waliacha usafiri huko.

Hakuamini macho yake, aliona gari la baba yake mzazi likiwa linaingia barabara kubwa likiwa linatokea pale kwake.

“aah ina maana nyumbani nao wanajua nimekufa hadi wafuate nguo zangu?” Alijiuliza huku akiwa ameweka mikono kichwani.

Vedi hakujua afanye nini katika dakika zile ili kuondoa uongo ule ambao ulikuwa unasambaa kwa kasi kama moto wa kifuu.

Nb: Maoni yako ni muhimu Sana katika kazi hii.
Karibu kwa maoni yako juu ya hiki kitu
 
RIWAYA; BAHARIA
NA; BAHATI MWAMBA
SIMU; 0758573660 SEHEMU YA TATU Watu wote walitoka na kuelekea nje ya ukumbi na kutazama kule ambako ilisemekana amejirusha, mabaharia kadhaa walikuwa wameshajitosa majini ili kuangalia uwezekano wa kumuona huyo aliejitupa majini.
Licha ya jitihada nyingi kufanyika kumtafuta, bado hawakufanikiwa na ndipo timu ya uokozi ilipopewa taarifa kutoka Dar es laam ili kufika hapo na kutoa msaada zaidi. Wakati wa mapambazuko ndipo meli ipopiga honi kuashiria inafika ukomo wa safari baada ya kuzunguka baharini usiku mzima. ***
Vedi alishuka kwenye meli na kupita moja kwa moja hadi nje ya eneo la abiria, huko alichukua usafiri na kurudi nyumbani kwake alikokuwa amepanga. Alipofika akaingia ndani na kujitupa kwenye sofa iliokuwa sebuleni kwake kisha akapumua kwa nguvu na kutupa viatu vyake virefu bila kujali vitakapoangukia.
Vedi alipumua kwa nguvu na kutazama juu kwa tafakuri.
Akakurupuka!
Akauendea mkoba wake mdogo uliokuwa na vitu vyake baadhi na alikuwa nao ndani ya meli.
Akaufungua na kupangua vitu kadhaa vya kujirembea pamoja na taulo ya kike ambayo aliiweka kwa dharura.
Hatimae macho yake yalipata kile alichokitaka.
Kilikuwa ni kile Kitabu kidogo cha kumbukumbu alichokichukua ndani ya kikontena wakati alipokuwa ndani ya meli.
Akakifunua!
Alikutana na mambo machache katika ukurasa wa kwanza na alipoyasoma hakuona kama ndicho alichokihitaji katika kitabu kile.
Kwanza alihitaji kujua kama kitabu kile kimeandikwa kwa matumizi sahihi ya kitabu chenyewe, yani kimeandikwa mambo muhimu ya mmiliki wake. Pia alihitaji kujua kama atafanikiwa kujua kama mmiliki aliandika jina lake na watu wake wa muhimu ikiwemo na mawasiliano yao..
Katika ukurasa uliofuata alikuta jina na tarehe. “Banzi Kela….tarehe 06/4/2017”
Akafunua tena kurasa nyingine na alifanya hivyo ili kujiridhisha na mawazo yake.
Baada ya kusoma maelezo ya ukurasa ule akarudi tena kwenye ukurasa ambao ulikuwa na jina na tarehe na hapo ndipo alijiridhisha na fikira zake ya kuwa kitabu kile kilianza kutumika tarehe ile na yawezekana lile neno Banzi Kela ni jina na ni la mmiliki wake.
Kichwani mwake akapitisha jina hilo na umiliki wa kitabu kile.
Aliendelea kufungua kurasa moja na nyingine na kusoma yaliondikwa hatimae alifika kwenye ukurasa uliokuwa umeandikwa ujumbe maalumu kwa ajili ya mtu ambae aliamini ni mpenzi wa Banzi. “Kwako Mamu!
Ni ukweli nakupenda sana kuliko sana yenyewe. Mamu najua unanipenda pia, ila kwa tulipofikia inabidi niwe mbali na wewe. Sio kama umenikosea la hasha ni kwa kuwa tu nataka uishi kwa amani zaidi ukiwa mbali na mimi. Hivi sasa mimi si Banzi tena ila ni marehemu mtarajiwa Banzi. Usiniulize kwanini ila kabla ya kuuliza nenda Hard Rock kwa Jezebeli anaujumbe wa matumaini yangu.” Ulisomeka hivyo ujumbe ule.
Vedi aliganda kwa sekunde kadhaa baada ya kuusoma.
Ni kawaida kwa wapenzi kuandikiana jumbe nyingi, ila ni mara chache kuandikiana jumbe za kutisha na kusononesha namna ile.
Banzi alikuwa na mpenzi anaitwa Mamu na anamtahadharisha juu ya mauti yanayotembea nae.
Mh!!
Vedi akaguna huku akijiweka sawa kwenye sofa yake.
Kwanini sasa Banzi ajitabilie kifo? Na je ujumbe ule ulimfikia Mamu mwenyewe?
Hakuwa na majibu wala wa kumjibu.
Haraka haraka akaanza kupitia kurasa moja na nyingine,alikuwa anatafuta lau mawasiliano ya huyo Mamu na aliamini kabisa mawasiliano yatakuwemo mule.
Hadi anamaliza kukipitia bado hakuwa amebahatika kuona namba yoyote ile ya simu. Akarudia tena kupitia kwa mara nyingine, bado hali ilikuwa ile ile.
Mh!!.
Akaguna peke yake na kurudi pale kwenye ukurasa wa ujumbe wa Mamu.
Kuna kitu alikiona..
Katika ukurasa ule mwishoni kabisa kulikuwa kuna namba imeandikwa na ilikuwa ni sifuri..
Alifunua tena ukurasa mwingine na hakuona namba ila uliofuata aliona tena namba ikiwa imeandikwa na ilikuwa ni namba Saba.
Akaendelea kupitia na kuzinakili namba zile kwenye simu yake na zilikuwa ni namba kumi kwa ujumla wake.
Aisee!!
.
Vedi alishangaa akili nyingi za Banzi. Banzi alikuwa anasababu gani kuficha namba zile katika aina ile?.
Vedi alijiaminisha kabisa ya kuwa kuna kitu kilikuwa kinaendelea kwa Banzi si bure.
Akajaribu kuzipiga zile namba.
Simu haikutoka!!..
Vedi akarudia tena na hali ilikuwa ile ile.
Akatazama ntandao katika simu yake na alikuta upo chini hausomi.
Ebo!!
.
Na laini iliandika “emergency”
Aisee!!
Tatizo nini?
Hakupata wa kumjibu.
Alibaki akiwa amefadhaika.
Akajinyanyua kwenye sofa na kuelekea ndani kwake ambako alichukua ndoo ya maji na kumimina kwenye ndoo nyingine maalumu ya kuogea kisha akatoka nje na kwenda kuoga ili kuondoa uchovu wa usiku uliopita.
. Dakika kadhaa badae alitoka na kukuta wapangaji wenzie wakiwa wamekaa vibalazani mwao, akawasabahi na kuelekea ndani kwake.
Akaanza kujiremba harakaharaka ili awahi kituo cha kusajilia laini apate utatuzi wa laini yake kisha amtafute mmiliki wa namba alioikuta kwenye kitabu cha Banzi. Wakati anaendelea kujipara akachukua kitenzambali(rimoti) na kuwasha runinga.
Alikutana na habari ambayo ilikuwa inamalizikia ila alisikia jina lake likitajwa na kisha zikafuatia picha ambazo zilipigwa wakati mabaharia wakijitahidi kuokoa mtu aliesemekana kujitosa baharini.
Roho ilianza kwenda mbio na kushindwa kuelewa dhumuni la jina lake na picha za uokozi.
Habari iliishia na hakuambua japo maana ya kile alichokiona mwishoni.
Akarukia simu yake kwa pupa, mara akanywea kama maji katikati ya vumbi baada ya kukumbuka simu yake haisomi mtandao.
Akavaa haraka haraka na kutoka nje.
.
Ebwana eeh!
Alishangaa wadada wawili wakirukia ndani kwao kama walioona jini katikati ya kiza kinene huku wakipiga ukunga wa kuogopa.
Alisita kutoka mlangoni kwake akabaki akitizama milango ya wadada wale.
Mhh kuna nini tena?
Alijiuliza peke yake huku hisia mbaya zikianza kumwandama kichwani mwake.
“ooh no! Isiwe kweli basi” Alijisemea huku machozi yakianza kumlenga.
Kuna hisia mbaya ilipita ubongoni mwake kuhusu habari alioona inamalizikia.
Alihisi anahusanishwa katika kifo kile cha mtu kujitupa ndani ya maji.
“Au ile maiti imetupwa majini na uchunguzi umeangukia kwangu baada ya kuacha kadi ile…” Alijikuta akitoa chozi huku akianza kupiga hatua ndefu kutoka pale alipokuwa amesimama.
Haraka yake ilikuwa ni kufika kwa kijana anaesajili laini za simu aliekuwa jirani na hapo alipokuwa akiishi.
Aliihitaji laini ili awasiliane na wazazi wake na kisha amtafute mmiliki wa namba alioipata kwenye kitabu cha kumbukumbu alichokitoa ndani ya meli. Alitembea kwa hatua za haraka haraka na kuvuka barabara kisha akapita vichochoro viwili na kutokea sehemu iliokuwa imechangamka kidogo.
Akaangaza kidogo na kumuona kijana aliemhitaji ambae wakati huo alikuwa amezungukwa na mabinti wengine wawili waliionekana kuhudumiwa.
“Mambo!” Vedi alimsabahi kijana yule huku akimshika bega kwa nyuma na kijana yule akageuka.
Loh!
Kijana akaruka juu kama shoga lililotekenywa na mtoto.
Hakuishia kuruka tu, akapiga kelele kwa sauti huku akirusha mikono yake kama mtu anaeshambuliwa na nyuki na kitendo kile kilifanya wale mabinti waliokuwa wakihudumiwa nao waanze kutimua mbio huku wakipiga kelele bila kujua wanapiga kwa sababu gani.
Vedi alivutwaika.
Macho yake hayakubanduka kwa yule kijana ambae alikuwa amefika mbali kidogo na kugeuka huku akiwaeleza jambo watu waliokuwa wameanza kujaa kumshangaa.
Vedi alishindwa kuelewa.
Macho ya Vedi yalitua kwenye meza ya kazi ya yule kijana,aliona simu janja ya kijana yule na ilikuwa bado inaonesha mwanga kuashiria ilikuwa kwenye matumizi dakika chache zilizopita.
Akavutiwa na kile alichokiona.
Akaichukua simu ile na kuanza kusoma.
Ebana eeh!
Vedi aliishiwa akili ya kufikiri na kujikuta machozi ya kimtoka huku nafsini mwake kukiwa na sauti kubwa ya kupingana na jambo lile.
Alirudi tena kusoma na hakikuwa kimebadilika kitu.
Alikuwa anasoma katika tovuti moja ya kuwa mtu aliejurusha ndani ya maji amaekolewa na kufahamika kwa jina la Vedi Mashimo mkazi wa kisutu Dar es laam.
Kisutu ndio aliishi na hilo jina ni lake na sio jina tu hata picha zilikuwapo za kwake kuonesha yeye ndie alijitosa baharini na kupoteza maisha.
Akairejesha ile simu na kupiga hatua kuelekea nyumbani kwake; Baadhi ya watu waliomfahamu wakajiweka mbali nae.
Vedi alifadhaika kwa kitendo kile,machozi yalimtoka na mwili ulimwia uzito na kujikuta akipiga hatua za kinyonga.
Akajitahidi na kurejea nyumbani kwake, ila wakati anaingia tena, majirani zake wakaanza kupiga kelele za woga huku wakiita jini jini.
Hakuwajali akaingia ndani kwake ambako wakati anatoka hakufunga mlango.
Ebana eeh!
Ndani napo hakukuta mabegi yake ya nguo na viatu na baadhi ya picha pia zilichukuliwa huku akiachiwa mkoba tu ambao alikuwa ameuangusha uvunguni mwa meza.
Akachanganyikiwa!
Haraka akatoka nje na kuelekea upande wa pili ambako aliamini waliochukua vitu vyake ni lazima waliacha usafiri huko.
Hakuamini macho yake, aliona gari la baba yake mzazi likiwa linaingia barabara kubwa likiwa linatokea pale kwake.
“aah ina maana nyumbani nao wanajua nimekufa hadi wafuate nguo zangu?” Alijiuliza huku akiwa ameweka mikono kichwani.
Vedi hakujua afanye nini katika dakika zile ili kuondoa uongo ule ambao ulikuwa unasambaa kwa kasi kama moto wa kifuu.
Nb: Maoni yako ni muhimu Sana katika kazi hii.
Karibu kwa maoni yako juu ya hiki kitu
maoni yangu tupia dozi ya kutosha mkuu
 

Similar Discussions

14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom