Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,498
- 9,279
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Karagwe, Benson Bagonza, alipohojiwa na MwanaHALISI Online juu ya maoni yake kuhusu sakata la CHADEMA.
Sakata hilo liliibuka baada ya wanachama 19 wakiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Halima Mdee kuapishwa kuwa wabunge wa viti maalumu na Spika wa Bunge, Job Ndugai Jumanne ya tarehe 24 Novemba 2020.
Wanachama hao wanadaiwa kwenda kinyume na msimamo wa Chadema wa kutopeleka bungeni wawakilishi wake, wakipinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020, kwa madai mchakato wake haukuwa huru na wa haki.
Alipouliza sababu za mgongano huo, Askofu Bagonza amesema Tanzania inakabiliwa na tatizo la mmomonyoko wa maadili, kwa kuwa watu wanaheshimu matokeo kuliko mchakato.
“Nadhani kuna mpalaganyiko wa kimaadili katika Taifa letu, kwamba mara nyingi tuna heshimu matokeo kuliko mchakato. Nchi yenye maadili ina heshimu michakato kuliko matokeo, nchi isiyo na maadili ina heshimu matokeo kuliko mchakato,” amesema Askofu Bagonza.
Kiongozi huyo wa kiroho amesema, wanachama hao wa Chadema waliokubali uteuzi ubunge viti maalumu wameheshimu matokeo badala ya mchakato uliotengeneza nafasi hizo.
“Penye maadili unahehsimu mchakato kuliko matokeo, pasipo na maadili unaheshimu matokeo, mchakato unauacha maadamu ufike unapokwenda, waliokubali uteuzi wa ubunge viti maalumu wameheshimu matokeo na si mchakato,” amesema Askofu Bagonza.
Kufuatia sintofahamu hiyo, Askofu Bagonza amekishauri Chadema kichukue hatua kwa wahusika bila kujali upendeleo.
“Tukio hili sio la kwanza kutokea katika historia ya nchi yetu, kwa hiyo, ningeshauri lishughulikiwe kama mengine yalivyoshughulikiwa yenye sura kama hii. Ili kuepusha mgongano wa kimaslahi,” amesema Askofu Bagonza.
Wito huo wa Bagonza umekuja siku moja baada ya Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika kuwaomba Watanzania kuishauri Kamati Kuu ya chama hicho, namna ya kulishughulikia suala hilo.
Sakata hilo liliibuka baada ya wanachama 19 wakiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Halima Mdee kuapishwa kuwa wabunge wa viti maalumu na Spika wa Bunge, Job Ndugai Jumanne ya tarehe 24 Novemba 2020.
Wanachama hao wanadaiwa kwenda kinyume na msimamo wa Chadema wa kutopeleka bungeni wawakilishi wake, wakipinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020, kwa madai mchakato wake haukuwa huru na wa haki.
Alipouliza sababu za mgongano huo, Askofu Bagonza amesema Tanzania inakabiliwa na tatizo la mmomonyoko wa maadili, kwa kuwa watu wanaheshimu matokeo kuliko mchakato.
“Nadhani kuna mpalaganyiko wa kimaadili katika Taifa letu, kwamba mara nyingi tuna heshimu matokeo kuliko mchakato. Nchi yenye maadili ina heshimu michakato kuliko matokeo, nchi isiyo na maadili ina heshimu matokeo kuliko mchakato,” amesema Askofu Bagonza.
Kiongozi huyo wa kiroho amesema, wanachama hao wa Chadema waliokubali uteuzi ubunge viti maalumu wameheshimu matokeo badala ya mchakato uliotengeneza nafasi hizo.
“Penye maadili unahehsimu mchakato kuliko matokeo, pasipo na maadili unaheshimu matokeo, mchakato unauacha maadamu ufike unapokwenda, waliokubali uteuzi wa ubunge viti maalumu wameheshimu matokeo na si mchakato,” amesema Askofu Bagonza.
Kufuatia sintofahamu hiyo, Askofu Bagonza amekishauri Chadema kichukue hatua kwa wahusika bila kujali upendeleo.
“Tukio hili sio la kwanza kutokea katika historia ya nchi yetu, kwa hiyo, ningeshauri lishughulikiwe kama mengine yalivyoshughulikiwa yenye sura kama hii. Ili kuepusha mgongano wa kimaslahi,” amesema Askofu Bagonza.
Wito huo wa Bagonza umekuja siku moja baada ya Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika kuwaomba Watanzania kuishauri Kamati Kuu ya chama hicho, namna ya kulishughulikia suala hilo.