Bagonza: Kuna dalili za kuliangamiza Taifa kwa sababu watu wanaamini uongo na kumchukia mtu anayesimamia ukweli

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,495
9,275
Watanzania wametakiwa kusimamia ukweli na kutoyumbishwa katika imani yao ili kuliokoa Taifa lisiangamie.

Wito huo umetolewa leo Jumatano Desemba 9, 2020 na Askofu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe, Dk Bensoni Bagonza wakati akihubiri katika ufunguzi wa Sinod ya 22 iliyofanyika shule ya sekondari Mukire jimbo la Mabira Wilaya ya Kyerwa.

Amesema mara nyingi uongo unaweza kuliangamiza Taifa hivyo lazima kila mtu kuwa tayari kusimamia ukweli na kukubali gharama za kusema ukweli huo.

"Mara zote msema kweli lazima achukiwe na kutengwa hivyo uwe tayari kusimamia, mara nyingi ukiwa muongo watakushirikisha ila ukisema ukweli watasema kwa huyo hata msipoenda, " amesema Dk Bagonza.

Amesema kuna dalili za kuliangamiza Taifa kwa sababu watu wanaamini uongo na kumchukia mtu anayesimamia ukweli.

Askofu Bagonza amesema Petro alitakiwa kuikana nafsi yake lakini wakati huu watu wanajitesa wenyewe kwa kupenda starehe na vitu vyepesi na ndiyo maana Taifa linaweza kuangamizwa.

Amesema kanisa si mali ya mtu na siyo taasisi binafsi bali ni mali ya Yesu hivyo wanaopanga kwa namna yoyote kuliangamiza hawatashinda maana Yesu alisema juu ya mwamba atalijenga kanisa na atalilinda.

Chanzo: Mwananchi
 
Askofu gani kila sku kuongelea mambo ya siasa, yupo yupo tu, huyu ni moja ya maaskofu wabovu sijawah ona, Yesu alisema "enendeni ulimwenguni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi wangu" huyu yeye kila siku kuongelea mambo ya Kaisari, Yesu mwenyewe alisema hakuja duniani kukabiliana na Warumi yaan kwake masuala ya siasa haikuwa Primary mission, na akasema wazi kama ingekuwa shida yake kubadili mkondo wa siasa wa kirumi watumishi wake wangempigania maana ni issue simple tu.

Huyu Askofu anafanya mambo ya hovyo sana, kiufupi analichafua sana Kanisa kuingia kwenye misuguano ya Kisiasa, KKKT inatakiwa imtimue mara moja, la sivyo taswira ya Kanisa itachafuliwa, ni mchumia tumbo Tu anayetaka kujinufaisha na siasa.
 
Yule jamaa anayejiita namba moja, hakika ndiye namba moja wa uwongo
Sasa wamekuja na maigizo ya vx la milion 400 huko Geita wakati hizo Gari zimejaa kila wizara wilayani mpaka CCM kote wanatumia hayo hayo magari, wamegundua baadhi ya watanzania ni wajinga wakiona maigizo ya huko Geita watajua Serikali ya mtukufu inajua kubana matumizi wataipenda kwa nguvu.

Pesa inayotumika kuwanunua covid 19 , kudidimiza demokrasia kuidhoofisha chadema ni pesa nyingi mno inaweza kununua Toyota vx za milion 400 kibao lakini wadanganyika hawaoni hilo wamebakia kushabikia mbinu za CCM kulazimisha kupendwa kwa njia haramu za kishetani.
 
Askofu gani kila sku kuongelea mambo ya siasa, yupo yupo tu, huyu ni moja ya maaskofu wabovu sijawah ona, Yesu alisema "enendeni ulimwenguni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi wangu" huyu yeye kila siku kuongelea mambo ya Kaisari...
Kukemea uongo ndio injili yenyewe! Tatizo lenu kila kitu hamjui, haishangazi mmekuwa watu wa mapambio tu!
 
Hivi huyo askofu mbona kila siku anahangaika na mambo ambayo hata waumini wake pia hawana muda nayo?

Kama waumini waliamua kumsurubu na Tundu Lisu wake bado yeye hawezi kujifunza?
Mbona askofu Shoo yeye hutoka kwa muda kisha anaendelea na mambo ya mungu?

Sidhani kama huyo bagonza ana utukufu wa mungu moyoni kwake zaidi ya kuongozwa na shetani kifuani kwake, maana kila siku anakosa usingizi wakati hata anao waongoza wanalala usingizi.

Nini kinamsibu katika uongozi huu?
Ajitokeze aseme, maana hata waumini wake anawambia mambo amabayo hawakwenda kuyafuata huko kanisani.

Wao wameenda kupata nguvu ya mungu ili waweze kupata baraka za mwenyezi mungu, yeye anaenda kuwambia mambo ya siasa.
Kama kuna muumizi kazurumika basi bagomza akafungue kesi kumtetea ili akamilishe upendo wake kwa watu wake.

Kwa kiongozi wa dini kulalama kila siku kwa mawazo yake wakati waumini wake wanaendelea na maisha bila kulalama basi kuna tatizo moyoni mwake.
 
Askofu gani kila sku kuongelea mambo ya siasa, yupo yupo tu, huyu ni moja ya maaskofu wabovu sijawah ona, Yesu alisema "enendeni ulimwenguni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi wangu" huyu yeye kila siku kuongelea mambo ya Kaisari, Yesu mwenyewe alisema hakuja duniani kukabiliana na Warumi yaan kwake masuala ya siasa haikuwa Primary mission, na akasema wazi kama ingekuwa shida yake kubadili mkondo wa siasa wa kirumi watumishi wake wangempigania maana ni issue simple tu.

Huyu Askofu anafanya mambo ya hovyo sana, kiufupi analichafua sana Kanisa kuingia kwenye misuguano ya Kisiasa, KKKT inatakiwa imtimue mara moja, la sivyo taswira ya Kanisa itachafuliwa, ni mchumia tumbo Tu anayetaka kujinufaisha na siasa.
Wewe mwenyewe ni mbovu unawezaje kuona? acha ufala wako moja ya nguzo ya Dini au kiongozi wa Dini tena wa ngazi ya Asikofu ni kuongea ukweli siyo kuwa mnafiki kama viongozi wengine wa Dini, acha unafiki wako unajipendekeza upate uteuzi kwa njia haramu za kishetani, Asikofu alichafua kanisa kivipi? Mambo ya hovyo yapi?

Umevuta Bangi Mbona umejitoa fahamu kiasi hicho? Kuikosoa Serikali kusema ukweli ni kuichafua kanisa? Acha uijinga wako Tambua kuwa watanzania wameamka sasa hawataki makanisa misikiti wala unafiki wa kidini wanataka ukweli viongozi wa Dini wakweli wasaidie Taifa siyo kuendekeza unafiki kama wako na wa Bakwata.
 
Mwambie Askofu akumbuke huu ulimwengu sio wetu, na mwenye mamlaka na huu ulimwengu sio yule ambaye Askofu anamtumikia, hivyo asishangae sana kwa yote yanayotokea hapa ulimwenguni, hivyo kusifia uongo ndio moja ya mapendezo ya mtawala wa ulimwengu na wafuasi wake.
Mara mia kuukataa unafiki kuliko kujitoa fahamu kisa uteuzi kukumbatia unafiki, Siku zote unafiki hukwamisha maendeleo ndiyo maana Tanzania hakuna maendeleo licha ya kuwa na rasilimali nyingi kuliko mataifa mengi Duniani kutokana na kusheheni wanafiki wengi kupita Nchi zote ulimwenguni
 
Waumini wa wapi hawataki ukweli? Ukiona muumini hapendi ukweli huyo yupo kwenye list ya wanafiki, Siasa inagusa maisha ya watanzania wote na ni mojawapo ya nguzo za Dini lazima viongozi wa Dini wakemee maovu uonevu na mabaya yanayotendwa na wanadiasa, acheni kuendekeza unafiki wa kishamba, unafiki ni Sumu ya maendeleo, kwa kung’ang’ania unafiki ni vigumu Tanzania kupiga hatua kimaendeleo.
 
Tayari kumevurugika korido za Ufipa.

Mzee anawatafutia unabii
Tanzania kama siyo unafiki mda huu ingekuwa ni Nchi tajiri kuliko mataifa yote mikubwa Duniani Duniani kutokana na kusheheni rasilimali nyingi kupita mataifa yote ulimwenguni, sasa kwa kuwa inakumbatia unafiki wenye kuzaa ufisadi na mambo ya hovyo ndiyo maana hakuna maendeleo mpaka sasa.
 
Back
Top Bottom