Habari za kuaminika ni kwamba kuna mpango wa kuiuza Bagamoyo kwa 'wawekezaji' kupitia mpango wa epz.kwa kuanzia, wamechukua zinga yote kwa kubadili ramani mara tatu na kuwadhulumu wananchi malipo yao huku wakiwatisha viongozi wao na kuwaamuru wakae kimya vinginevyo...wananchi wa zinga tayari wametishia kutishiriki sensa kama hawatapewa malipo yao,viwanja walivyoahidiwa na ramani ya kwanza kufuatwa. Kisha mpango wa kamal estates au mtu mwingine kubadili matumizi ya ardhi hayatakubalika hata kama mtalazimisha,tunajua ameomba kufanya hivyo. Je ni nia yenu watoto wetu waje kukosa sehemu ya kuishi? Je sisi hatuhitaji upepo wa pwani hata kama nyumba zetu ni za makuti?kuna sababu gani ya kubadili ramani kinyemela hadi kufikia kilomita mbili ng'ambo ya barabara kuuYA DAR-B'MOYO? Jeuri ya fedha na vitisho havisaidii, vinginevyo marehemu Ghadaffi angeendelea kuwepo kwa fedha na madavu yake.
Wananchi wa wilaya ya Bagamoyo tuna haki ya kubakia kwenye makazi yetu ya asili na wote mmjjuuue hilo.wapnda amani wote naomba muone namna ya kuwasaidia wananchi waZinga-Bagamoyo na kwingineko wasidhulumiwe na kuishia kuwa manamba kwenye nchi yao.
Wananchi wa wilaya ya Bagamoyo tuna haki ya kubakia kwenye makazi yetu ya asili na wote mmjjuuue hilo.wapnda amani wote naomba muone namna ya kuwasaidia wananchi waZinga-Bagamoyo na kwingineko wasidhulumiwe na kuishia kuwa manamba kwenye nchi yao.