GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,099
Elimu ya Tanzania imetumika miaka mingi kumuandaa kijana kuajiriwa na Serikali au Sekta binafsi, Watu ambao wamepata bahati ya kuajiriwa na mfumo huu wa elimu wao wanaona mfumo huu upo sawa kabisa
Mambo yanayoshangaza na kusikitisha zaidi watu wale wale ambao wanaona mfumo upo sawa wa elimu yetu wanahangaika kuwatafutia kazi vijana na ndugu zao maofisini kwa udi na uvumba
Mfumo wa elimu yetu tumeurithi toka kwa mkoloni, Mkoloni alimpa mtu mweusi elimu kwa lengo la mtu mweusi kuja kumtumikia mkoloni, Elimu aliyoitoa mkoloni haikumuandaa mtu mweusi kufikiri nje ya anachofundishwa darasani
Tangu mwaka 2000 mpaka sasa mwaka 2021 maelfu ya vijana wamehitimu vyuo vikuu ndani ya nchi, Waliobahatika kuajiriwa ni chini ya asilimia moja ya wahitimu wote
Kijana anatumia miaka takribani kumi na saba kutafuta elimu toka shule ya msingi mpaka Chuo Kikuu, Elimu ambayo nje ya cheti kijana hawezi kusimama na kujitetea
Tufanye kitu gani tutoke hapa tulipo na tusonge mbele kwa matumaini
Mosi, Watoto wetu wakishafanikiwa kujua kusoma na kuandika lugha yetu kwa ufasaha na lugha baadhi za kigeni, Wazazi pamoja na shule wawapime watoto wanahitaji wafanye kitu gani na wanapendelea kitu gani, Tuwaendeleze watoto kwa vitu wanavyohitaji na baadhi kama masomo ya teknolojia yawe ya lazima
Masomo ya lugha za computer yaani Coding yawe ni lazima kwenye elimu ya msingi, Masomo ya kutengeneza App yawe ni lazima hapa kwenye elimu ya msingi. Watoto wafundishwe matatizo tulionayo na jinsi watavyoweza kuyatatua kwa teknolojia
Miaka mitano inatosha kwa elimu ya msingi kwa watoto wetu kuweza kuelewa Basics au msingi wa wapi tunalipeleka Taifa hili
Pili, Hakuna haja ya vijana kusoma masomo zaidi ya kumi Katika ngazi ya kati ya Sekondari yaani Kidato Cha kwanza mpaka nne, Kidato Cha kwanza mpaka nne kiwe ni kipindi cha vijana kufundishwa mahesabu na teknolojia, Masomo ya Kompyuta kwa vitendo na Matumizi ya mahesabu kwa vitendo ndio muda wake hapa
Nafahamu hatuna walimu wenye uwezo wa vitendo na wala hatuna maabara za kuwaandaa hawa vijana, Lakini ni muda muafaka kuanza na shule chache na kuingia gharama za kuazima walimu toka China na Marekani
Tatu, Watoto wakitoka Kidato Cha nne waelekee vyuo vya kati vya kisasa sio hizi Amazoni College au University of Iringa au University of Dodoma au Sua au Udsm( Hivi ni vyuo ambavyo watoto wanaandaliwa kukariri mambo ili wafaulu tu mitihani na kutafuta ajira)
Elimu za vyuo kama Udsm, Sua, Udom na rafiki zao kama IFM na CBE vilishafeli kitambo sana kwa kutoa elimu za kukariri
Vyuo vya kati ndio ambavyo ilipasa pesa za IMF za corona na baadhi ya mikopo kuelekeza kununua mitambo ya kisasa ya computer na Machine za high Tech kwa ajili ya vijana kujifunza
Nne, Urafiki wetu na Mabeberu ulenge kutujengea uwezo na tuwatumie mabeberu vizuri, Pesa za Loan Board zitumike kuwapeleka vijana Field huko Google, Amazon, NASA, Microsoft. Na baadhi wapelekwe kwenye mazoezi huko London School of Economics wakajifunze, Harvad School of Medicine.
Ni muda wa kukaa chini na Balozi wa Marekani na China kuongea nao kuhusu mpango wa vijana wetu kila mwaka zaidi ya Mia tano kwenda kujifunza mazoezi kwenye taasisi zao za teknolojia za kati na kubwa ili tuhamishie uwezo wa teknolojia Nyumbani
Tano, Kundi la vijana wapenda masomo ya historia na Sanaa lipewe kipaumbele kidogo tofauti na sasa, Vyuo vyetu wamejaa vijana wa masomo ya uchekeshaji na uigizaji, Uigizaji Katika sociology, Political science, Fine art na watoto wao wanaolingana
Sita, Walimu wetu wa vyuo vikuu hawana uwezo wa kumuandaa kijana tena kujitegemea, Walimu tulionao sasa ni zao la watu waliokariri mambo kwa muda mrefu sana
Ni muda tupate walimu wa vitendo, Hawa walimu wa nadharia wa kuandaa notes na kutunga Test hawatufai tena hapa Tanzania
Serikali iwaondoe walimu wasiokuwa na umuhimu vyuo vikuu hasa wale ambao hana uwezo wa vitendo, Waletwe wataalamu toka China na Marekani kupima uwezo wa hawa walimu wetu Katika kila sekta toka Engineering, Accounting mpaka kozi za usanii
Nje ya Cheti cha darasani, Vijana waliomaliza chuo kikuu kwa sasa hawawezi kusimama, Ukimpokonya cheti chake ukamuuliza Haya sasa simama songa mbele lazima atadondoka tu
Tujiulize maswali muhimu kwa lengo la kusaidia hawa vijana wetu
Je kijana anapomaliza chuo kikuu mfano udsm au udom, Sua. Tukichukua cheti chake atafanya kitu gani huku uraiani, Walimu wa vyuo vikuu hawana uwezo kuwaandaa vijana tena kwa sasa
Je kila kijana neno kujiajiri ni kuuza nguo, maandazi, Nyanya, Mikate, mitumba na kuanzisha duka kariakoo?
Hitimisho
Tuna watu ambao wamesoma na wamepata taaluma ya vitendo kwa juhudi zao na ujanja wao, Ni muda wa kuwatumia hawa watu, Kuna watu wanafanya kazi Serikalini na Sekta binafsi wana uwezo mkubwa kwa vitendo kuliko hawa walimu waliopo vyuo vikuu kwa sasa,
Ni kuboresha mazingira tu na kuwa ondoa walimu wote ambao hawana uwezo kufundisha kwa vitendo
Mazingira yakiboreshwa hata mimi Gussie Nipo tayari kwenda Front line kugawa mbinu za kupambana kwa wanafunzi wetu kisiasa na hata kukabiliana na Biashara za kimataifa na kuachana na hawa wabunge wa kujua kusoma na kuandika tu
Tusipowaza matumbo yetu na Mamlaka tunaweza jenga Taifa imara kwa watoto na Vizazi vijavyo
Mambo yanayoshangaza na kusikitisha zaidi watu wale wale ambao wanaona mfumo upo sawa wa elimu yetu wanahangaika kuwatafutia kazi vijana na ndugu zao maofisini kwa udi na uvumba
Mfumo wa elimu yetu tumeurithi toka kwa mkoloni, Mkoloni alimpa mtu mweusi elimu kwa lengo la mtu mweusi kuja kumtumikia mkoloni, Elimu aliyoitoa mkoloni haikumuandaa mtu mweusi kufikiri nje ya anachofundishwa darasani
Tangu mwaka 2000 mpaka sasa mwaka 2021 maelfu ya vijana wamehitimu vyuo vikuu ndani ya nchi, Waliobahatika kuajiriwa ni chini ya asilimia moja ya wahitimu wote
Kijana anatumia miaka takribani kumi na saba kutafuta elimu toka shule ya msingi mpaka Chuo Kikuu, Elimu ambayo nje ya cheti kijana hawezi kusimama na kujitetea
Tufanye kitu gani tutoke hapa tulipo na tusonge mbele kwa matumaini
Mosi, Watoto wetu wakishafanikiwa kujua kusoma na kuandika lugha yetu kwa ufasaha na lugha baadhi za kigeni, Wazazi pamoja na shule wawapime watoto wanahitaji wafanye kitu gani na wanapendelea kitu gani, Tuwaendeleze watoto kwa vitu wanavyohitaji na baadhi kama masomo ya teknolojia yawe ya lazima
Masomo ya lugha za computer yaani Coding yawe ni lazima kwenye elimu ya msingi, Masomo ya kutengeneza App yawe ni lazima hapa kwenye elimu ya msingi. Watoto wafundishwe matatizo tulionayo na jinsi watavyoweza kuyatatua kwa teknolojia
Miaka mitano inatosha kwa elimu ya msingi kwa watoto wetu kuweza kuelewa Basics au msingi wa wapi tunalipeleka Taifa hili
Pili, Hakuna haja ya vijana kusoma masomo zaidi ya kumi Katika ngazi ya kati ya Sekondari yaani Kidato Cha kwanza mpaka nne, Kidato Cha kwanza mpaka nne kiwe ni kipindi cha vijana kufundishwa mahesabu na teknolojia, Masomo ya Kompyuta kwa vitendo na Matumizi ya mahesabu kwa vitendo ndio muda wake hapa
Nafahamu hatuna walimu wenye uwezo wa vitendo na wala hatuna maabara za kuwaandaa hawa vijana, Lakini ni muda muafaka kuanza na shule chache na kuingia gharama za kuazima walimu toka China na Marekani
Tatu, Watoto wakitoka Kidato Cha nne waelekee vyuo vya kati vya kisasa sio hizi Amazoni College au University of Iringa au University of Dodoma au Sua au Udsm( Hivi ni vyuo ambavyo watoto wanaandaliwa kukariri mambo ili wafaulu tu mitihani na kutafuta ajira)
Elimu za vyuo kama Udsm, Sua, Udom na rafiki zao kama IFM na CBE vilishafeli kitambo sana kwa kutoa elimu za kukariri
Vyuo vya kati ndio ambavyo ilipasa pesa za IMF za corona na baadhi ya mikopo kuelekeza kununua mitambo ya kisasa ya computer na Machine za high Tech kwa ajili ya vijana kujifunza
Nne, Urafiki wetu na Mabeberu ulenge kutujengea uwezo na tuwatumie mabeberu vizuri, Pesa za Loan Board zitumike kuwapeleka vijana Field huko Google, Amazon, NASA, Microsoft. Na baadhi wapelekwe kwenye mazoezi huko London School of Economics wakajifunze, Harvad School of Medicine.
Ni muda wa kukaa chini na Balozi wa Marekani na China kuongea nao kuhusu mpango wa vijana wetu kila mwaka zaidi ya Mia tano kwenda kujifunza mazoezi kwenye taasisi zao za teknolojia za kati na kubwa ili tuhamishie uwezo wa teknolojia Nyumbani
Tano, Kundi la vijana wapenda masomo ya historia na Sanaa lipewe kipaumbele kidogo tofauti na sasa, Vyuo vyetu wamejaa vijana wa masomo ya uchekeshaji na uigizaji, Uigizaji Katika sociology, Political science, Fine art na watoto wao wanaolingana
Sita, Walimu wetu wa vyuo vikuu hawana uwezo wa kumuandaa kijana tena kujitegemea, Walimu tulionao sasa ni zao la watu waliokariri mambo kwa muda mrefu sana
Ni muda tupate walimu wa vitendo, Hawa walimu wa nadharia wa kuandaa notes na kutunga Test hawatufai tena hapa Tanzania
Serikali iwaondoe walimu wasiokuwa na umuhimu vyuo vikuu hasa wale ambao hana uwezo wa vitendo, Waletwe wataalamu toka China na Marekani kupima uwezo wa hawa walimu wetu Katika kila sekta toka Engineering, Accounting mpaka kozi za usanii
Nje ya Cheti cha darasani, Vijana waliomaliza chuo kikuu kwa sasa hawawezi kusimama, Ukimpokonya cheti chake ukamuuliza Haya sasa simama songa mbele lazima atadondoka tu
Tujiulize maswali muhimu kwa lengo la kusaidia hawa vijana wetu
Je kijana anapomaliza chuo kikuu mfano udsm au udom, Sua. Tukichukua cheti chake atafanya kitu gani huku uraiani, Walimu wa vyuo vikuu hawana uwezo kuwaandaa vijana tena kwa sasa
Je kila kijana neno kujiajiri ni kuuza nguo, maandazi, Nyanya, Mikate, mitumba na kuanzisha duka kariakoo?
Hitimisho
Tuna watu ambao wamesoma na wamepata taaluma ya vitendo kwa juhudi zao na ujanja wao, Ni muda wa kuwatumia hawa watu, Kuna watu wanafanya kazi Serikalini na Sekta binafsi wana uwezo mkubwa kwa vitendo kuliko hawa walimu waliopo vyuo vikuu kwa sasa,
Ni kuboresha mazingira tu na kuwa ondoa walimu wote ambao hawana uwezo kufundisha kwa vitendo
Mazingira yakiboreshwa hata mimi Gussie Nipo tayari kwenda Front line kugawa mbinu za kupambana kwa wanafunzi wetu kisiasa na hata kukabiliana na Biashara za kimataifa na kuachana na hawa wabunge wa kujua kusoma na kuandika tu
Tusipowaza matumbo yetu na Mamlaka tunaweza jenga Taifa imara kwa watoto na Vizazi vijavyo