Bado nampenda

LIMANYE

Member
Nov 16, 2012
24
1
Wadau hebu nisaidieni nampenda sna mume wangu na tangu tumetengana kwa muda wa mwaka na nusu sasa sijathubutu kuwa na uhusiano wowote na mwanaume mwingine tatizo mume wangu ni bondia namaanisha amekuwa akinipiga sna tangu tulipokuwa boy friend na gal friend zen anaomba msamaha kwamba ni hasira tu namsamehe hd tulipofunga ndoa kanisani nikiamini atabadilika lakini haikuwa hivyo kwani hadi tumepata mtoto 1 still ikitokea tatizo llote la kutofautiana kauli napata kipigo tena sio cha kitoto niko njia panda sijui cha kufanya kwani kwa malezi niliyolelewa ilikuwa kifo ndo kinitenganishe na mume wangu lakini imekuwa vingine kwani nimeshindwa kuendelea kuvumilia kipigo nimeludi kwetu naamini awezi kubadilika wa kuacha kunipiga kwani nimegundua hasira ni tatizo kubwa alilonalo na hadi nahisi anapokuwa na hasira awezi kujicontrol ila akishatenda kosa badae anajutia inaniuma sna ila sina jinsi coz mume wangu ndiye first boyfriend wangu na nampenda kwa dhati ila pia siko tayari kuendelea kupigwa nifanyeje??
 
Jiunge dojo kule Keko akilianzisha na wewe unajibu mapigo....
Tafuta movie ya JLo inaitwa "Enough" utaelewa.
 
Jiunge dojo kule Keko akilianzisha na wewe unajibu mapigo....
Tafuta movie ya JLo inaitwa "Enough" utaelewa.

Afanye kila kitu ila hiyo muvi HAPANA!
Mitch: What does it matter? It's not that our sex life hasn't been good. It's been great, ... But I am a man!
What, I can't hit you? ... I am a man honey, so no contest.

Gaademu him!
 
pole, hapa mwamuzi ni wewe mwenyewe.

Cost benefit analyisis inahusika.

Pima raha anayokupa mmeo na maumivu ya kipigo, kipi kina nguvu zaidi kwako, ndo ufanye maamuzi.

Kama sio kwamba ana tatizo la ukichaa, ama self esteem, unaweza ongea naye akaanza kuhuduria masomo ya kuthibiti hasira ama akaonana na wataalam wa saikolijia.

Vipi, anapiga nyasi? Maana wapiga nyasi nao huwa wana mashetani ya muda.
 
Rudiana nae ila kwa masharti makali hayo mahasira yake yakimpanda bora apige ukuta ipo siku atakutoa ngeu alafu soko lipungue.
 
pole, hapa mwamuzi ni wewe mwenyewe.

Cost benefit analyisis inahusika.

Pima raha anayokupa mmeo na maumivu ya kipigo, kipi kina nguvu zaidi kwako, ndo ufanye maamuzi.

Kama sio kwamba ana tatizo la ukichaa, ama self esteem, unaweza ongea naye akaanza kuhuduria masomo ya kuthibiti hasira ama akaonana na wataalam wa saikolijia.

Vipi, anapiga nyasi? Maana wapiga nyasi nao huwa wana mashetani ya muda.

Nyasi gani?
 
Si ufanye maamuzi tu na kuyasimamia hayo maamuzi mwisho wa siku. Kwamba nakubali maisha ya kipigo na huo ndio msalaba wangu mpaka mwisho wa maisha au naachana naye na kuishi peke yangu mpaka pale nitakapopata au kuwa tayari kuishi na mwingine.
 
Ndoa Ndoano!!! Mshafunga ndoa ya kikristo hakuna jinsi vumilia tu mpaka atakapobadirika(omba mungu ambadirishe)
 
nashukuru lakini ndoa sio mateso na kuhusu kubadilika awezi tena angekuwa ni wakubadilika nadhani angekwisha badilika nimemwombea sna bila kupata mabadiliko zaidi nimeendelea kuumia tu.
 
Nakubaliana na wewe moja kwa moja kwamba mwamuzi ni mimi na ndomaana nimeanza step ya kwanza kwa kuludi kwetu pia nimeambiwa na watu wawili watatu kuhusu kichaa naanza kuamini sasa lakini ni ngumu kumwelewesha akutane na wataalam sana sana ntaambulia kipigo kwamba namwona yeye kichaa kiukweli ni msalaba mzito sna kwani hata kama napata raha zote kipigo kinanifanya nisahau yote kuhusu nyasi nahisi.
 
Mie nakueleza DADA jifunze kupigana itakusaidia. Siku ambayo huyo mwanaume akilianzisha anakutana na muziki asioweza kuucheza.
Kesho yake akiamka na ngeu ile aibu kwa marafiki itampa adabu.
Halafu ukishajua kupigana siku hata naye akikukorofisha wewe ndio unakua wa kwanza kusupply kichapo....lazima adabu itamkaa tu
 
ahsante kwa ushauri mzuri kiukweli ndo nimeanza step one kwa kuondoka nazidi kumwomba Mungu anifungulie napaswa kufanya nn baada ya hapo kwani kiukweli siko tayari kuendelea kubeba msalaba wa kipigo tena miaka 9 imetosha ya kupigwa.
 
Pole sana dadangu kwa mitihani katika maisha...nakuomba mpe nafasi ya mwisho kwani katika dini tunafundishwa kusamehe 7 x 70...
naamini anaweza kujicontrol hasira zake but pleaseeeee..ushawahi kuchunguza ni kwa kiasi gani nawe unamkwaza mwenzio mpaka anaishia kukuchapa???...

Nyie wenzetu huwa mnapiga sana vuvuzela kiasi kwanba sie wanaume tunaishia kuwaziba mikelele yenu kwa vichapo..ila kama ukimwona kawaka unakuwa mpole na mkimya then akipoa unamchana makavu laivu ataishia kuwa mnyonge na kuanza kuogopa kuwakawaka hovyo....

Na pia nahofia ukaribu wenu kama wanandoa...mnakuwa wote kama familia mara ngapi kwa wiki?...au wote mko bize plus baba akitoka job baa akirudi saa 6 usiku wewe ushalala mnazinguana unatoka kwenda job saa 12 yani haina cha familia kuwa pamoja na kubadilishana mawazo na kuimarisha mahusiano yenu ya kindoa na kijamii.

Pia mwambie mwenzio..kama mkeo kakuudhi kuliko kumpiga ondoka nyumbani utarudi baada ya 6 hrs akikaa na wanaume wenzie huko baa hasira zitapunguwa.

tafadhali yafanyie kazi hayo coz hata mie kama mwanaume nilikuwa nashindwa kujicontroll hasira tunaishia kuchapana..ambayo ni upuuzi na utoto usio na msingi kwa wana-ndoa...thanks god nimebadilika na naweza kucontrol hasira na akizidisha nafungua mlango naenda kuangalia mpira mpaka saa 6 usiku narudi..akiendelea...huyooo kula biere mpaka tisa ucku ..akiendelea huyooo kulala guest narudi asubuhi...akizidi kuzingua siku ya pili hanioni nyumbani anaanza kunipigia kuomba yaishe coz anajuwa sipendi kugombana naye ila anataka kunilazimisha...mambo ya kupigana kisha unamuumiza then unaishia kumtibia hospital ni ujinga...pesa ya hospital tumia kupunguza stress baa na guest.

Tafadhali yafanyie kazi na ukiweza ruksa ku-copy mawazo yangu na mtumie mmeo kwenye simu yake kama text msg apate ujanja wa kuwa mume mwema au bonge la mume.
 
kwa maadili ya kiafrica sipaswi kumludishia mume wangu ngumi hata kama nami najua kupigana lakini pia ubavu wa mume wangu ni heavy siwezi hata kuhimiri kupigana nae nadhani siku hiyo ataniua kbs.
 
Back
Top Bottom