Tamati
JF-Expert Member
- May 15, 2017
- 1,085
- 1,956
Hali bado tete siku hadi siku huku janga la Corona likiendelea kumea kila kukicha.
Hatma ya kupata riziki ya halali na ya kueleweka angalau mlo mmoja kwa siku bado giza nene. Kupata kibarua cha halali imekuwa changamoto sana kwa upande wangu. Najitajidi kuzunguka kila siku na kuomba kwa watu ninaoona wanaweza kunipatia kibarua ila nagonga mwamba.
Katika kuzunguka kwangu kote kutafuta kibarua nimebaini kuwa bila kujuana na mtu ni vigumu kupata kibarua.
Ndugu zangu wana JF naombeni yeyote mwenye kibarua hasa katika maeneo ya kibaha, Pwani (ninaishi Kibaha) anipatie ili niweze kufanya kazi ya halali na nipate riziki ya halali hatimaye niweze kupeleka mkono kinywani.
Tuendelee kujikinga na Corona na Mungu atuepushe na janga hili.
Hatma ya kupata riziki ya halali na ya kueleweka angalau mlo mmoja kwa siku bado giza nene. Kupata kibarua cha halali imekuwa changamoto sana kwa upande wangu. Najitajidi kuzunguka kila siku na kuomba kwa watu ninaoona wanaweza kunipatia kibarua ila nagonga mwamba.
Katika kuzunguka kwangu kote kutafuta kibarua nimebaini kuwa bila kujuana na mtu ni vigumu kupata kibarua.
Ndugu zangu wana JF naombeni yeyote mwenye kibarua hasa katika maeneo ya kibaha, Pwani (ninaishi Kibaha) anipatie ili niweze kufanya kazi ya halali na nipate riziki ya halali hatimaye niweze kupeleka mkono kinywani.
Tuendelee kujikinga na Corona na Mungu atuepushe na janga hili.