Bado maisha anayoishi Rais wa Tanzania na viongozi wa juu, ni ya kifahari sana! Hayaakisi maisha ya masikini walio wengi Tanzania

jmushi1

Platinum Member
Nov 2, 2007
24,989
22,521
Wakuu, sina hata haja ya kuelezea sana! Wote tunafahamu maisha ya viongozi wakuu wa nchi akiongozwa na rais wa nchi!

Sijatumia neno “wanyonge”, kwasababu huo unyonge ndo umetumika kuwafanya wananchi wazidi kuwa masikini wa kutupwa!

Nimetumia neno masikini, kwasababu wako wengi pamoja na utajiri wa rasilimali tulio nao. Na hata rasilimali watu ni utajiri mkubwa sana kwa mataifa yenye kujielewa!

Lakini kwetu, sidhani kama tunafahamu mishahara ya viongozi, lakini nafahamu wanatutegemea wananchi kwa kila kitu! Kuanzia kuvaa, kula, kunywa, kulala, kusafiri, nyumba, magari ya kifahari, vinywaji! Na bado wanajijengea makasri pamoja na mapesa mengi kwenye akaunti za nchini na nje ya nchi!

Huyu kiongozi wa sasa, anasema yeye anapenda wanyonge na kuwatetea. Hivi kweli bado anakula pale ikulu na chakula inateremka kabisa?🤦🏾‍♂️Wakati kila siku kuna watu wanakufa kwa “malnutrition’s”, pamoja na magonjwa yenye kuzuilika.

Kuna member aliweka post hapa, ambapo waziri mkuu anasalimia masikini wa Tanzania, ambao ni wengi sana, lakini ukimtizama, utadhani ni kiongozi aliyetokea kwenye mataifa tajiri kabisa duniani. Ndiyo sisi ni matajiri kwa rasilimali, lakini viongozi ndo wamezuia utajiri huo usionekane kwa wananchi.

Nina amini tutapata insight nzuri zaidi hapa kwa wenye kufahamu zaidi. Lakini ni wazi kuwa hili wimbi la watia nia, wananchi wameona ndo njia pekee ya kujiingizia kipato cha uhakika kabisa bila hata jasho.

Ni wakati wetu sisi wananchi kubadili huu mfumo, ili kuhakikisha tunapata watumishi wa kweli. Isiwe faida ama utajiri tu kujiingiza kwenye siasa na uongozi, bali iwe utumishi wa kujitolea.
 
Hana lolote. That's why wanaomfananisha na Thomas Sankara huwa wanakosea sana.

Thomas Sankara alipungunza mshahara wake na wa mawaziri,akaacha kutumia BMW na Benz,wakawa wanatumia magari ya kawaida. Aliboresha sector za afya,kilimo,kujenga makazi ya wasiyojiweza n.k

Ila Magufuli anaishi maisha ya juu huku wananchi wake majority wakiishi chini ya dola moja kwa siku. Aliwadanganya million 50 kila kijiji. Sijui kampeni za safari hii atawadanganya vipi.
 
Hana lolote. That's why wanaomfananisha na Thomas Sankara huwa wanakosea sana.
Thomas Sankara alipungunza mshahara wake na wa mawaziri,akaacha kutumia BMW na Benz,wakawa wanatumia magari ya kawaida. Aliboresha sector za afya,kilimo,kujenga makazi ya wasiyojiweza n.k
Ila Magufuli anaishi maisha ya juu huku wananchi wake majority wakiishi chini ya dola moja kwa siku. Aliwadanganya million 50 kila kijiji. Sijui kampeni za safari hii atawadanganya vipi.
Magufuli anapokea mshahara mdogo sana tu wa shilingi milioni 9, tena ni mhanga wa kukosa nyongeza ya mshahara kwa kipindi cha miaka mitano sasa maana watumishi wote wa umma hawajapewa nyongeza.

Kazi ya urais ni ngumu sana ni kwa vile tu ni mzalendo na anatupenda "wanyonge" ndio maana amejitolea kufanya kazi hii ngumu.

Mshahara wa Rais Magufuli wawa gumzo Kenya
 
Wote wezi,MTU analipwa 10M+,harafu anasema kiongozi wa wanyonge,imeandikwa wapi kwamba Rais,makamu,PM,spika,walipwe mamilioni kibao?

Kwanini wasilipwe kama watumishi wengine,Kama Raisi alipwe millioni 3 tu,wengine wote 1M,

Tunawapa magari,mikopo,viinua mgongo vya kutisha,

Ubunge uwe miaka 10,baada ya hapo,wakapambane na hari zao,na wao wakajiajiri kwenye kufuga kuku,na bata Kama sie
 
Hana lolote. That's why wanaomfananisha na Thomas Sankara huwa wanakosea sana.
Thomas Sankara alipungunza mshahara wake na wa mawaziri,akaacha kutumia BMW na Benz,wakawa wanatumia magari ya kawaida. Aliboresha sector za afya,kilimo,kujenga makazi ya wasiyojiweza n.k
Ila Magufuli anaishi maisha ya juu huku wananchi wake majority wakiishi chini ya dola moja kwa siku. Aliwadanganya million 50 kila kijiji. Sijui kampeni za safari hii atawadanganya vipi.
Hakuna mtu anayetaka kuishi kinyonge siyo Rais wala Hao wapinzani huo ndiyo ukweli, hata wee ukipewa nafasi utakuwa walewale

Ova
 
Siyo kweli kwani aliahidi 2016 kuweka salary slip yake ili kuonyesha mshahara wake kwa Watanzania lakini alishindwa kufanya hivyo.

Mshahara wake ni $192,000 kwa mwaka karibu milioni 440 na gharama zake zote na familia yake zinalipwa na walipa kodi.

Magufuli anapokea mshahara mdogo sana tu wa shilingi milioni 9, tena ni mhanga wa kukosa nyongeza ya mshahara kwa kipindi cha miaka mitano sasa maana watumishi wote wa umma hawajapewa nyongeza.

Kazi ya urais ni ngumu sana ni kwa vile tu ni mzalendo na anatupenda "wanyonge" ndio maana amejitolea kufanya kazi hii ngumu.

Mshahara wa Rais Magufuli wawa gumzo Kenya
 
Wote wezi,MTU analipwa 10M+,harafu anasema kiongozi wa wanyonge,imeandikwa wapi kwamba Rais,makamu,PM,spika,walipwe mamilioni kibao?
Kwanini wasilipwe kama watumishi wengine,Kama Raisi alipwe millioni 3 tu,wengine wote 1M,
Tunawapa magari,mikopo,viinua mgongo vya kutisha,
Ubunge uwe miaka 10,baada ya hapo,wakapambane na hari zao,na wao wakajiajiri kwenye kufuga kuku,na bata Kama sie
Watu wengine mnatia aibu sana!
 
Hakuna mtu anayetaka kuishi kinyonge siyo Rais wala Hao wapinzani huo ndiyo ukweli, hata wee ukipewa nafasi utakuwa walewale

Ova
Hapana aisee. Mimi nikiwa kiongozi nitahakikisha naweka mazingira ya watu kujitoa kwenye umaskini. Hata mshahara wangu nitapunguza. Imagine wangepunguza mishahara yao Rais mpaka wabunge na wakasema hizo pesa wazielekeza kutoa million 50 kwa kila kijiji kama walivyoahidi. Si wangebadili maisha ya wanakijiji ?Ukitaka kujua hawana habari na wananchi kila leo hao wabunge wanajiongezea maslahi.
 
Magufuli anapokea mshahara mdogo sana tu wa shilingi milioni 9, tena ni mhanga wa kukosa nyongeza ya mshahara kwa kipindi cha miaka mitano sasa maana watumishi wote wa umma hawajapewa nyongeza.

Kazi ya urais ni ngumu sana ni kwa vile tu ni mzalendo na anatupenda "wanyonge" ndio maana amejitolea kufanya kazi hii ngumu.

Mshahara wa Rais Magufuli wawa gumzo Kenya
Kama kweli ana uchungu na wanyonge kwa nini asiupunguze mpaka million 3?Maa na hana charges zozote,matibabu bure,services zote bure,marupurupu kibao.
 
👊🏽👊🏽👊🏽👊🏽👊🏽 You’re the type of the leader that we need in our beautiful country.

Hapana aisee. Mimi nikiwa kiongozi nitahakikisha naweka mazingira ya watu kujitoa kwenye umaskini. Hata mshahara wangu nitapunguza. Imagine wangepunguza mishahara yao Rais mpaka wabunge na wakasema hizo pesa wazielekeza kutoa million 50 kwa kila kijiji kama walivyoahidi. Si wangebadili maisha ya wanakijiji ?Ukitaka kujua hawana habari na wananchi kila leo hao wabunge wanajiongezea maslahi.
 
Back
Top Bottom