BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,006
Bado dunia ina watu wema hata kama ni wachache. Jana nilielezea kisa cha Jaji mmoja ambaye alidai mwenye bahati kushikana mkono na mimi. Ni kauli kubwa sana kuambiwa toka nizaliwe. Hadi nikatamani nijipitishe pale "Central" wanikamate kwa uchochezi halafu kesi apelekewe yule Jaji 🤣
Siku moja nilipewa taarifa za mtoto Pili aliyezaliwa kichwa kikubwa, mgongo wazi na sehemu ya utumbo wake ikiwa nje. Ikanigusa sana hasa baada ya kuambiwa baba yake ni marehemu, mama ni mgonjwa na bibi anayewalea ni mlemavu. Nikalazimika kusafiri hadi Arusha kuwaona.
Nikakaa Arusha siku 5. Asubuhi moja nikiwa kwenye hoteli niliyofikia akaja meneja akaniuliza kama ni Malisa. Nikamjibu ndio. Akafurahi sana. Akaniuliza gharama za kusafiri hadi huku nani anakulipia? Nikamwambia nalipa mwenyewe. Akastaajabu kidogo kisha akaniambia "kaka una moyo wa ajabu sana. Naomba nilipie gharama zako hapa hotelini." Akapewa bill akalipa.
December nikiwa natoka Mwanza, ndugu yangu akanipigia akasema "nina rafiki yangu anamiliki hoteli Morogoro ni mfuasi wako mitandaoni. Ameomba kama utaweza kufika Moro ulale kwenye hoteli yake angalau akusalimie." Nikiwa na rafiki zangu watatu tukafika na kulala kwa gharama za mmiliki.
Siku moja nikiwa Dodoma nilijaza mafuta kwenye kituo fulani, meneja wa hicho kituo akaniruhusu niende bila kulipa chochote. "Kaka nenda tu, nitaclear. Unafanya kazi kubwa sana kwenye jamii"
Siku moja nikiwa ofisini nikapigiwa simu na rafiki yangu mmoja. "Kaka unaweza kupata nafasi ukaja ofisini kwangu leo?" Nikamwambia "nipo tight kidogo kaka naomba nije saa 11 nikitoka ofisini" akajibu "sawa kaka hamna shida, nitakuwepo hadi saa 2 usiku"
Tulipokutana akasema "Unafanya kazi kubwa sana ya jamii. Najua unatumia muda wako na wakati mwingine fedha zako kuwafikia wahitaji. Wengi hatujali sana unapoteza mangapi, tunachojali ni kuona wahitaji wanasaidika. Mimi na Mkurugenzi mwenzangu tumeona tuchangie angalau mafuta lita mbili unapokua katika safari zako za kusaidia wahitaji" Akanipa hundi ya $1,000.
Hakika watu wema bado wapo. Nawashukuru wote mlioniunga mkono kurudisha tabasamu kwa watanzania wenzetu mwaka 2020. Tuzidi kushirikiana mwaka 2021. Mungu awabariki sana.
Baba Nicole AKA Malisa GJ
Siku moja nilipewa taarifa za mtoto Pili aliyezaliwa kichwa kikubwa, mgongo wazi na sehemu ya utumbo wake ikiwa nje. Ikanigusa sana hasa baada ya kuambiwa baba yake ni marehemu, mama ni mgonjwa na bibi anayewalea ni mlemavu. Nikalazimika kusafiri hadi Arusha kuwaona.
Nikakaa Arusha siku 5. Asubuhi moja nikiwa kwenye hoteli niliyofikia akaja meneja akaniuliza kama ni Malisa. Nikamjibu ndio. Akafurahi sana. Akaniuliza gharama za kusafiri hadi huku nani anakulipia? Nikamwambia nalipa mwenyewe. Akastaajabu kidogo kisha akaniambia "kaka una moyo wa ajabu sana. Naomba nilipie gharama zako hapa hotelini." Akapewa bill akalipa.
December nikiwa natoka Mwanza, ndugu yangu akanipigia akasema "nina rafiki yangu anamiliki hoteli Morogoro ni mfuasi wako mitandaoni. Ameomba kama utaweza kufika Moro ulale kwenye hoteli yake angalau akusalimie." Nikiwa na rafiki zangu watatu tukafika na kulala kwa gharama za mmiliki.
Siku moja nikiwa Dodoma nilijaza mafuta kwenye kituo fulani, meneja wa hicho kituo akaniruhusu niende bila kulipa chochote. "Kaka nenda tu, nitaclear. Unafanya kazi kubwa sana kwenye jamii"
Siku moja nikiwa ofisini nikapigiwa simu na rafiki yangu mmoja. "Kaka unaweza kupata nafasi ukaja ofisini kwangu leo?" Nikamwambia "nipo tight kidogo kaka naomba nije saa 11 nikitoka ofisini" akajibu "sawa kaka hamna shida, nitakuwepo hadi saa 2 usiku"
Tulipokutana akasema "Unafanya kazi kubwa sana ya jamii. Najua unatumia muda wako na wakati mwingine fedha zako kuwafikia wahitaji. Wengi hatujali sana unapoteza mangapi, tunachojali ni kuona wahitaji wanasaidika. Mimi na Mkurugenzi mwenzangu tumeona tuchangie angalau mafuta lita mbili unapokua katika safari zako za kusaidia wahitaji" Akanipa hundi ya $1,000.
Hakika watu wema bado wapo. Nawashukuru wote mlioniunga mkono kurudisha tabasamu kwa watanzania wenzetu mwaka 2020. Tuzidi kushirikiana mwaka 2021. Mungu awabariki sana.
Baba Nicole AKA Malisa GJ