Bado CCM itaendelea kunufaika na ujinga wa Watanzania

FK21

JF-Expert Member
May 27, 2019
7,626
9,302
Habari za wakati huu.

Naomba leo nije na hili suala ya CCM kuendelea kuneemeka na ujinga wa watanzania walio wengi. Ujinga wa Watanzania ni mtaji wa CCM kuendelea kutawala zifuatazo ni moja ya mbinu chache zinazoonesha watanzania wameshikwa akili na kikundi kidogo cha watu.

KUTENGENEZA MATATIZO NA KUYATATUA
hili suala ni tatizo ambalo CCM tanzania imelitengeneza kwa kujua watanzania watanong'oa waje walitatue ili serikali ionekane ni sikivu hili suala linaonesha jinsi gani serikali ya CCM imekuwa ya matukio na propaganda.

UJINGA WA WATANZANIA KUAMINISHWA UPINZANI SIO UZALENDO
Hili swala la kujimilikisha uzarendo kwa Wana CCM kwamba ukiwa CCM tu Basi wewe ni mzalendo wanaokuwa wako upande wa vyamba mbadala ni wahalifu hili suala limeshika Hadi akili ya baadhi ya wanaojiita wasomi PhD holder aloyesoma bado anamezwa na hii propaganda je mjinga asiyesoma aliye kahama ushetu?

Nchi hii ni yetu sote awe CHADEMA, ACT, UDP yeyote anatakiwa kuwa kupata haki kama wananchi wengine wa chama tawala.

Kuvipiga vita vyama mbadala kunapelekea kuibuka kwa wimbi la vijana wenye uroho wa madaraka wako radhi wamtukane kiongozi yeyote wa upinzani ili wapate uteuzi hii inasikitisha Sana kama vyama pinzani havina umuhinu viondolewe tubaki na chama kimoja.

USHAURI WANGU KWA VIONGOZI WA CCM
Najua viongozi wengi wa CCM mnapenda kufanya vitu kwa kukurupuka sana suala la tozo kama itabadilisha itafedhehesha viongozi wengi sana na kama ingekuwa ni nchi ya kueleweka wangetakiwa kujiuzuru Eric shigogo , Abas tarimba, Zungu,

Na baadhi ya wengine wasio na uchungu na wananchi waliokuwa wanatetea ivyo vitu badirikini
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom