Badala ya kuomba UNEMPLOYMENT BENEFIT tunataka tunapigia kelele PENSION

Mdanganywa

JF-Expert Member
Jun 15, 2009
620
342
Najua suala la pension limetaimiwa vizuri na watu. Si kwamba lina hoja ya kutisha hadi nchi nzima ikatetemeka, bali waliolikuza walicheza na uelewa wa wananchi kuhusu masuala ya Social Security.

Inaeleweka kwamba watanzania wengi ni wagumu kusoma vitabu. Ni wengi kiasi cha kutisha.

Hivyo, unapoleta hoja ambayo wana uelewa kiduchu basi hicho kiduchu kitapigiwa kelele kupita kiasi. Na kama mleta hoja hukupima matokeo ya unacholeta basi kelele hizo zitakufundisha adabu na ukicheza unaweza kubwaga manyanga.

Ndicho kilichotokea kwenye suala hili la SSRA ambalo thread humu zimepungua.

Hoja ya wengi humu ilikuwa je, iweje mtu afukuzwe kazi akiwa na miaka 35 halafu asubiri miaka 20 ndipo apate hela yake ya Pension.

Anayeuliza swali hili ukweli ni swali ambalo ni rahisi kujibu katika mazingira fulani lakini yapo mazingira utatumia nguvu nyingi kueleweka.

Hivi kweli kwenye conference ya wasomi wa Social Security, hili swali lina ugumu gani? Pale IFM kuna watu wanachukua degree ya Social Security. Swali hili ni rahisi kabisa kujibu pale.

Lakini tabu ni kuliuliza swali hili kwenye public. Hakika utakuwa unaleta fujo maana hapo humjibu profesa anayeshisha Social Security exam bali unawajibu watanzania ambao wamekariri kwamba ukifukuzwa kazi unachukua pension yako. Hakika hapo ukumbuke kwamba ukilijibu kama unavyomjibu yule profesa basi kuna hatari hata ya chama chako kuondoka madarakani kwenye uchaguzi ujao iwe CHADEMA au CCM.

Tuje sasa kwenye topic ya leo. Pamoja na yote hayo, kilichoonekana ni kwamba kumbe pressure ya watu inaweza kufanya serikali ikabadili jambo liwe watu wanavyotaka. Sina matatizo na hili.

Lakini jambo kubwa kwangu ni kwamba kwa nini tusiutumie mwanya huu ili Tanzania iwe na UNEMPLOYMENT BENEFIT. Maana ile hoja kwamba mtu akifukuzwa akiwa na miaka 35 isingekuwa na nguvu kama kuna UNEMPLOYMENT BENEFIT scheme. UNEMPLOYMENT BENEFIT ni kiasi unacholipwa kukidhi maisha yako kama hukuajiriwa.

UNEMPLOYMENT BENEFIT ikiwepo basi hapo ndipo kweli tunakuwa tunaingia kwenye Social Security haswa. Kwa hiyo najua thread hii inaweza kuleta majibu ya kila aina lakini tutakuwa tumefaidika na wale watakaotufafanulia kuhusu uwezekano wa kufikia hatua ya kupata UNEMPLOYMENT BENEFITS.

Hela inayoibiwa na kufichwa huko nje ingefaa kabisa kuboresha schemes kama hizi na kusingekuwa na kelele kama tulizoona baada ya SSRA kutangaza utaratibu wao kwa mujibu wa sheria.
 
Mheshimiwa mdanganywa, je unadhani kuintroduce unemployment benefit ni rahisi hivyo? Usisahau universal pension Ndio
Inategemewa kuanza mwaka Kesho (govt financial year) na hatuna uhakika financing itakuwaje and for how long.

Pili kama social security so far haijaweza kufika kwenye informal sector itaweza unemployment benefit?

Tatu coverage kwa formal sector ni less than 10% ukileta unemployment benefit financing itatoka wapi? Level ya unemployment katika Tanzania ikoje?

Nne nilitegemea agenda ya sasa ni hata hiyo formula ya pension iboreshwe, kila Mfuko una formula yake. Hiyo ndyo kero kubwa kwa beneficiaries so far.

Pia social security schemes zinaaply principles za insurance so pooling up of risk has a lot to do with coverage in general.

Je hiyo Mifuko Ina Hao wataalamu unaowasema? Topic yako ni Nzuri sana ikijadiliwa objectively naamini itatoka elimu kuhusu SS. Mwisho kilichofanywa na SSRA ni sahih kitaalamu kuna modalities tu zinazohitajika ambazo nategemea zikiboreshwa na kutengenezewa kanuni basi tutaelekea kwenye comprehensive SS.

Queen Esther
 
Hivi kweli kwenye conference ya wasomi wa Social Security, hili swali lina ugumu gani? Pale IFM kuna watu wanachukua degree ya Social Security. Swali hili ni rahisi kabisa kujibu pale.

Hujakosea kujiita "Mdanganywa", kwanza huenda uko nje ya nchi sababu unapendekeza utafikiri hujui Tanzania kuna serikali ya aina gani kati ya "Serikali inayotumikia wananchi" na "Serikali inayotumikiwa na wananchi" au "Genge la Wezi"

Pili hujui Serikali ya Magamba ina agenda gani ya Siri kuhusu hizo pesa za Wafanyakazi.

Tatu bado una amini, wanafunzi walioko vyuoni kama wa IFM ndo wanajua kila kitu kuzidi wenye degree na wasio nazo waliokataa pesa zao zisichukuliwe na mafisadi.

Nne hujui ni kipi rahisi kukidai na kukipata, je pesa yako mwenyewe au isiyo yako?

kwa ujumla umekurupuka, kama una matatizo ya kusahau mapema nakukumbusha, madai ya wazee wa EAC, Mwl. Irenge aliye mfundisha JK wa Ukweli alikufa akiwa na miaka 120 bila kulipwa Pension yake sembuse sisi tuliopangiwa miaka 55! Mpaka sasa kuna wastaafu wanalipwa baada ya miezi 4 tena kwa mafungu halafu unadhani bado una Serikali!
 
Bro mawazo yako ni mazuri ila kufikiria Unemployment benefit ni kuirudisha nyuma nchi hii. Nchi ina fursa nyingi sana hivyo suala la Unemployment halipo kabisa. Kila mtu hapa anaweza kupata ajira nzuri. Benfits hizo ukianzisha watu wetu walivyo wavivu ndiyo wataacha kabisa kufanya kazi. Suala la pension lipo wazi sana maana ile ni savings nimekatwa kwenye mshahara wangu hivyo suala la kulipwa ni la lazima.
 
Bro mawazo yako ni mazuri ila kufikiria Unemployment benefit ni kuirudisha nyuma nchi hii. Nchi ina fursa nyingi sana hivyo suala la Unemployment halipo kabisa. Kila mtu hapa anaweza kupata ajira nzuri. Benfits hizo ukianzisha watu wetu walivyo wavivu ndiyo wataacha kabisa kufanya kazi. Suala la pension lipo wazi sana maana ile ni savings nimekatwa kwenye mshahara wangu hivyo suala la kulipwa ni la lazima.
Ninavyofahamu mimi hayo mafao ya kutokuwa na ajira si mafao ya maisha yako yote, sana sana ni miezi sita tu. Tena wakati unalipwa na mfuko wa hifadhi, wewe mwenyewe unatafuta kazi na Idara/Taasisi ya Ajira inakusaidia. Kama Idara ya Ajira imekupatia kazi ya kusafisha mabanda ya kuku na wewe unaikataa, ndio siku mafao ya kutokuwa na ajira yanapoota mbawa.

Hilo la kuwa kila mtu hapa anaweza kupata kazi nzuri kakunong'oneza nani? Kuna vijana wangapi waliomaliza vyuo vikuu hawana ajira, hawana fursa za kujiajiri, serikali yetu haikuwaandaa waweze kujiajiri wala haiandai fursa za kujiajiri kwa wale waliojitayarisha wenyewe. Ukifungua kiduka cha mafuta ya taa, bizari na vitunguu vya mafungu tu utatozwa kodi mpaka nywele zinyonyoke wakati wanaochimba madini wanasamehewa kodi.

Mafao ya kutokuwa na ajira ni muhimu sana ikiwa mpango wa kutokupatiwa chako mapema utafuatwa.
 
Hujakosea kujiita "Mdanganywa", kwanza huenda uko nje ya nchi sababu unapendekeza utafikiri hujui Tanzania kuna serikali ya aina gani kati ya "Serikali inayotumikia wananchi" na "Serikali inayotumikiwa na wananchi" au "Genge la Wezi"

Pili hujui Serikali ya Magamba ina agenda gani ya Siri kuhusu hizo pesa za Wafanyakazi.

Tatu bado una amini, wanafunzi walioko vyuoni kama wa IFM ndo wanajua kila kitu kuzidi wenye degree na wasio nazo waliokataa pesa zao zisichukuliwe na mafisadi.

Nne hujui ni kipi rahisi kukidai na kukipata, je pesa yako mwenyewe au isiyo yako?

kwa ujumla umekurupuka, kama una matatizo ya kusahau mapema nakukumbusha, madai ya wazee wa EAC, Mwl. Irenge aliye mfundisha JK wa Ukweli alikufa akiwa na miaka 120 bila kulipwa Pension yake sembuse sisi tuliopangiwa miaka 55! Mpaka sasa kuna wastaafu wanalipwa baada ya miezi 4 tena kwa mafungu halafu unadhani bado una Serikali!

Suala la kutoaminika kwa serikali hii ya mafisadi kwa si tatizo sana. Kwa sababu najua hilo ni tatizo jingina ambalo ni kichaa tu ambaye hachukizwi nalo na tunalipigania kila kona na kila dakika na kila tunavyoweza, iwe maofisini, mtaani hata huku JF.

Lakini ufisadi au upuuzi wa serikali ya CCM usisababishe tukashindwa kuibua hoja zingine za manufaa ya nchi hii.

TUkikubali mawazo yako, basi mafisadi wataendelea kufisadi wakijua kwamba ufisadi wao utatukatisha tamaa kuyasema mapy akama haya niliyoleta.

Hivi unadhani fisadi wa serikalini aliezoea pressure chache akiona sasa watanzania wanadai hata UNEMPLYMENT BENEFITS, basi wewe inadhani unavyodhani lakini yeye hapo thread hii inamnyima usingizi kwa sababu anajua sasa tunaamsha kilio kingine ambacho leo ninaongelea mimi humu JF lakini siku moja watanzania watamiminika barabarani kuyadai ninayosema kwa njia ya maandamano na hii niwasiwasi kwake.


Mimi nimeleta UB, wewe lete jingine watu watasoma utakuwa umeongeza uelewa wa mambo tunayodai. Jamaa zako hapo juu wamechangia na binafsi nimeongeza uelewa na siajabu siku za mbele tukaboresha hii mada ili tuweze kuingia kwenye SS ya kikwelikweli na si blahblah zilizopo.
 
Ndugu mleta mada kuna jambo unatakiwa ulielewa mapema sana, this is Tanzania, ukisinzia unaachwa feri.

Kwa nini nasema hivi. The problem hapa sio watanzania na uelewa mdogo, tatizo hapa ni mwenendo wa serikali na hii mifuko ya jamii. Hii mifuko kwa kiasi kikubwa imekosa umakini katika kutumia michango ya wafanyakazi ikishirikiana bega kwa bega na serikali. Ripoti ya CAG imeeleza vizuri uozo huo, kuna karibu bil 450 UDOM, na mpaka leo hata mikataba ya kulipana bado haijasainiwa. Machinga complex, Jengo la TISS etc, kote huku mifuko hii imeweka fedha bila uhakika wa kupata fedha zake. Ikumbukwe pia kuwa serikali ni bingwa wa kukopa bila kulipa. Ina madeni sugu ya huduma za maji na umeme na kiasi kikubwa ilihusika kuiua TTCL, why should we trust this govt?

Kilichopo hapa ni kutoaminiana kati ya wafanyakazi na mifuko yao, hasa kutokana na mahaba yao na serikali "sikivu", swali kubwa linapaswa kuwa, je wafanyakazi wanafanya makosa kutokuwa na imani na mifuko hii?
 
Tatizo la SSRa tulitegemea kwanza itawabana serikali warudishe pesa za wafanyakazi walizojichotea kwenye miradi ambayo mingi yao haina tija kwa wachangiaji,pili kubresha mafao ya wafanyakazi lakini wao wamekimbilia kuwabana wafanyakazi kwanza kwani hata huko walikokopi hizo sheria mifuko ile inalindwa na serikali huwa hawajichotei pesa kama huku.
Hao wataalamu unaosema wako IFM wengi wamekariri walichofundishwa wakati hali halisi ni tofauti
 
Najua suala la pension limetaimiwa vizuri na watu. Si kwamba lina hoja ya kutisha hadi nchi nzima ikatetemeka, bali waliolikuza walicheza na uelewa wa wananchi kuhusu masuala ya Social Security. Inaeleweka kwamba watanzania wengi ni wagumu kusoma vitabu. Ni wengi kiasi cha kutisha. Hivyo, unapoleta hoja ambayo wana uelewa kiduchu basi hicho kiduchu kitapigiwa kelele kupita kiasi. Na kama mleta hoja hukupima matokeo ya unacholeta basi kelele hizo zitakufundisha adabu na ukicheza unaweza kubwaga manyanga. Ndicho kilichotokea kwenye suala hili la SSRA ambalo thread humu zimepungua. Hoja ya wengi humu ilikuwa je, iweje mtu afukuzwe kazi akiwa na miaka 35 halafu asubiri miaka 20 ndipo apate hela yake ya Pension. Anayeuliza swali hili ukweli ni swali ambalo ni rahisi kujibu katika mazingira fulani lakini yapo mazingira utatumia nguvu nyingi kueleweka. Hivi kweli kwenye conference ya wasomi wa Social Security, hili swali lina ugumu gani? Pale IFM kuna watu wanachukua degree ya Social Security. Swali hili ni rahisi kabisa kujibu pale. Lakini tabu ni kuliuliza swali hili kwenye public. Hakika utakuwa unaleta fujo maana hapo humjibu profesa anayeshisha Social Security exam bali unawajibu watanzania ambao wamekariri kwamba ukifukuzwa kazi unachukua pension yako. Hakika hapo ukumbuke kwamba ukilijibu kama unavyomjibu yule profesa basi kuna hatari hata ya chama chako kuondoka madarakani kwenye uchaguzi ujao iwe CHADEMA au CCM. Tuje sasa kwenye topic ya leo. Pamoja na yote hayo, kilichoonekana ni kwamba kumbe pressure ya watu inaweza kufanya serikali ikabadili jambo liwe watu wanavyotaka. Sina matatizo na hili. Lakini jambo kubwa kwangu ni kwamba kwa nini tusiutumie mwanya huu ili Tanzania iwe na UNEMPLOYMENT BENEFIT. Maana ile hoja kwamba mtu akifukuzwa akiwa na miaka 35 isingekuwa na nguvu kama kuna UNEMPLOYMENT BENEFIT scheme. UNEMPLOYMENT BENEFIT ni kiasi unacholipwa kukidhi maisha yako kama hukuajiriwa. UNEMPLOYMENT BENEFIT ikiwepo basi hapo ndipo kweli tunakuwa tunaingia kwenye Social Security haswa. Kwa hiyo najua thread hii inaweza kuleta majibu ya kila aina lakini tutakuwa tumefaidika na wale watakaotufafanulia kuhusu uwezekano wa kufikia hatua ya kupata UNEMPLOYMENT BENEFITS. Hela inayoibiwa na kufichwa huko nje ingefaa kabisa kuboresha schemes kama hizi na kusingekuwa na kelele kama tulizoona baada ya SSRA kutangaza utaratibu wao kwa mujibu wa sheria.
Hakika wewe ndiye uliye kariri kama kasuku. Wafanyakazi wakikubali kulipwa UNEMPLOYMENT BENEFIT, serikali itaweka kiwango kidogo sana kama Tsh. 20,000/= mwezi na kwa kipindi cha miezi mitatu au sita tu kisha inasitisha usubiri 55yrs! Pia hakuna huduma zingine utakazopata wewe na wategemezi wako toka mifuko ya jamii mpaka ufikishe 55yrs! HUU NI WENDAWAZIMU!
 
Last edited by a moderator:
Suala la kutoaminika kwa serikali hii ya mafisadi kwa si tatizo sana. Kwa sababu najua hilo ni tatizo jingina ambalo ni kichaa tu ambaye hachukizwi nalo na tunalipigania kila kona na kila dakika na kila tunavyoweza, iwe maofisini, mtaani hata huku JF.

Lakini ufisadi au upuuzi wa serikali ya CCM usisababishe tukashindwa kuibua hoja zingine za manufaa ya nchi hii.

TUkikubali mawazo yako, basi mafisadi wataendelea kufisadi wakijua kwamba ufisadi wao utatukatisha tamaa kuyasema mapy akama haya niliyoleta.

Hivi unadhani fisadi wa serikalini aliezoea pressure chache akiona sasa watanzania wanadai hata UNEMPLYMENT BENEFITS, basi wewe inadhani unavyodhani lakini yeye hapo thread hii inamnyima usingizi kwa sababu anajua sasa tunaamsha kilio kingine ambacho leo ninaongelea mimi humu JF lakini siku moja watanzania watamiminika barabarani kuyadai ninayosema kwa njia ya maandamano na hii niwasiwasi kwake.


Mimi nimeleta UB, wewe lete jingine watu watasoma utakuwa umeongeza uelewa wa mambo tunayodai. Jamaa zako hapo juu wamechangia na binafsi nimeongeza uelewa na siajabu siku za mbele tukaboresha hii mada ili tuweze kuingia kwenye SS ya kikwelikweli na si blahblah zilizopo.

Kama unatambua mafisadi wanatuibia kwa njia mbalimbali kwa kutumia madaraka yao, je wanapokuja na hoja za kuchukua pesa zako utakubali tu kisha uanze mchakato wa kuomba pesa ambazo siyo zako?

Kwanini hawa copy mambo mema yanayofanywa na serikali makini katika kuwahudumia wananchi au wafanyakazi? Mfano, kujenga nyumba na kuwapangisha kwa bei ya chini kabisa au kuwapa wafanyakazi wakae bure ili waweze wakilitumikia Taifa vizuri zaidi!

Kuwe na shule zitakazotoa elimu ya kiwango cha juu kama zinavyofanya serikali zingine ili watoto wetu sisi wafanya kazi na mafisadi wasome pamoja?
 
Hoja ya wengi humu ilikuwa je, iweje mtu afukuzwe kazi akiwa na miaka 35 halafu asubiri miaka 20 ndipo apate hela yake ya Pension.

Anayeuliza swali hili ukweli ni swali ambalo ni rahisi kujibu katika mazingira fulani lakini yapo mazingira utatumia nguvu nyingi kueleweka.

Hivi kweli kwenye conference ya wasomi wa Social Security, hili swali lina ugumu gani? Pale IFM kuna watu wanachukua degree ya Social Security. Swali hili ni rahisi kabisa kujibu pale.

Lakini tabu ni kuliuliza swali hili kwenye public. Hakika utakuwa unaleta fujo maana hapo humjibu profesa anayeshisha Social Security exam bali unawajibu watanzania ambao wamekariri kwamba ukifukuzwa kazi unachukua pension yako.

.

kiongozi sasa mbona wewe hujajibu swali hilo rahisi au umejibu?
 
Back
Top Bottom