Badala ya kuhangaika kunishukuru, kafanye nilivyokufanyia kwa mwingine mbele ya safari na siku zote

Mwanamayu

JF-Expert Member
May 7, 2010
11,349
6,476
Tabia mbaya ya wengi wa madereva Bongo, hasa Dar es Salaam ni kutokuruhusu madereva wengine kuingia barabara kuu ingawaje sheria inawapa wao maamuzi hayo. Lakini, kuna wakati mwingine nao utaka kuingia njia kuu.

Yawezekana hawa ndio wanaolazimisha. Na inawezekana wanabania wengine kulipiza kisasi, lakini je, unayembania ndiye aliyekubania mwanzo?

Sasa nikikuruhusu, kama ambavyo mara nyingi ufanya, badala ya kuhaha na mi-hazard lights yako kushukuru, tafadhari kamfanyie na mwingine.

Wengi wakiwa mbele yangu baada ya kuwaachia njia, hawaruhusu wengine. Halafu, mkiruhusiwa, basi muingie walau watano kama mpo zaidi ya watano, badala ya kutaka kuingia wote.

Jamani, tuwe wastaarabu!
 
Barabarani huwa kuna watu wanajieleza matabia yao hata nyumbani huko wakoje.

Usipomjali mwenzako ni dalili ya roho mbaya na umimi, shala out kwa wanangu wote wanaonedesha gari kali kali huwa hawana haraka yaani ukiomba handle anakuruhusu.

Sio wa V8 STK,na nduguzake lakini.
 
Tatizo letu Wabongo/Waafrika wengi ni ubinafsi na kukosa ustaarabu na utu, sio barabarani tu angalia hata makazini au serikalini, mtu akishapata nafasi anapambana kujilimbikizia yeye tu bila hata kuwahurumia walio chini yake, kiongozi anajilimbikizia mabilioni ya fedha za serikali Uswis halafu wananchi wanakufa kwa kukosa madawa, chakula, maji n.k halafu wananchi wanamsifu kua ni mjanja hajaicha familia yake kizembe kama baba wa taifa.
 
Back
Top Bottom