Back 3 mchawi!

Azikiwe

Senior Member
Nov 13, 2009
190
19
cid:image002.jpg@01CAAF23.7F470F40


Mfanyakazi ya ndani anayedaiwa kuwanga akiwa katika kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani cha Ubungu (UBT) tayari kusafirishwa kurejeshwa kwao Morogoro baada ya tuhuma hizo za kuwangaAbambwa na ndumba kibao na ungo

  • <LI class=MsoNormal style="COLOR: black; mso-margin-top-alt: auto; mso-margin-bottom-alt: auto; mso-list: l0 level1 lfo3">Asimulia mambo ya kutisha
  • Maombi yasaidia kumnasa
VITUKO simanzi vimetawala nyumbani kwa Mzee Naftal Chacha (60), mkazi wa Ukonga ambaye ni mstaafu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), baada ya hausigeli wake, Odillia Mikka (15), kukutwa chumbani kwake akiwanga huku akiwa amekaa ndani ya ungo.

Ilikuwa kama mchezo wa kuigiza katika nyumba hiyo baada ya mtoto wa mwenye nyumba hiyo aliyejitambulisha kwa jina la Miriam Naftal kumkuta msichana huyo akiwa amechuchumaa ndani ya ungo uliosheheni ndumba kibao pamoja na nguo za ndani za mtoto mkubwa wa kike wa familia hiyo.

Miriam baada ya kuingia katika chumba hicho ghafla alianza kupiga mayowe kumshtua msichana huyo ambapo familia nzima iliyokuwamo ndani ya nyumba hiyo iliingia chumbani huko ili kujionea kinachoendelea.

Baada ya kufika umati wa watu walimshuhudia hausigeli huyo akiwa ameshikwa na butwaa na walipomhoji alidai kuwa amechukua nguo za ndani za msichana wa mwenye nyumba huyo, Bhoke Naftal, ili azipeleke kwa bibi yake anataka kumuua kwa kumuweka msukule.

Kutokana na kauli hiyo mwenye nyumba hiyo ambao ni Wasabato walianza maombi ndipo hausigeli huyo aliyefikia nyumba hiyo Desemba 24, 2009, alipoanza kujieleza mambo mbalimbali anayoifanyia familia hiyo kwa kushirikiana na bibi yake anayeishi kijiji cha Kitete mtaa wa Yangeyange Morogoro.

Hausigeli huyo alidai kuwa tangu afike katika nyumba hiyo bibi yake amekuwa akija usiku na hutembelea vyumba vyote vya nyumba hiyo na kuichezea familia nzima.

Amesema kazi hiyo aliinza tangu akiwa na umri wa miaka minne ambapo mafunzo hayo aliyapata kwa bibi yake ambapo tangu aanze amefanikiwa kumuua mtoto mdogo wa miaka miwili wa tajiri yake mmoja anayeishi Morogoro ambaye hadi sasa wamemuweka msukule.

Ameongeza kuwa alimuua mtoto huyo aliyekuwa na umri wa miezi mitatu ndani ya nyumba hiyo. Baada ya kukiri kufanya kitendo hicho, wanafamilia ya mtoto huyo walimpiga na kumtimua kazi bila ya kumpa hata senti tano.

Akizungumza na gazeti hili, hausigeli huyo amesema mara baada ya kufika katika nyumba hiyo bibi yake alikuja usiku na kumuomba damu ya Miriam Naftari (25), mtoto wa mwenye nyumba hiyo ambaye alikwenda kumchukua Morogoro bila kumuaga.

Amesema kuwa usiku huo alijitahidi kumnyonya damu dada huyo aliyekwenda kumchukua lakini jitihada zilikwama kwa kuwa dada huyo alikuwa ameokoka.

Kutokana na hali hiyo, bibi akaamua achukue nguo za dada mkubwa wa familia ya Mzee Naftal ili wamtoe kafara ambapo ilitakiwa afe jana ndipo aliamua kuchukua nguo ili amkabidhi bibi yake huyo.

Msichana huyo amedai kuwa akiwa kwenye maandalizi hayo ndipo Miriam alipogundua kisha kupiga kelele kabla ya yeye kutimiza azima yake. Kwa hiyo familia iliamua kuchukua uamuzi wa kumfikisha kituo cha Polisi Stakishari kwa ajili ya hatua zaidi ambapo kulifunguliwa kesi namba STK/RB/ 2520/2010 iliyoripotiwa jana.

Akizungumza na gazeti hili, baba wa familia hiyo, Mzee Naftal, amesema anamshukuru Mungu kwa kuwa familia hiyo ni ya watu wenye kumcha Mungu kwani tangu hausigeli huyo afike katika nyumba hiyo kulikuwa na mabadiliko ndani ya nyumba hiyo ikiwa ni pamoja na homa za watoto zisizokwisha.

Amesema kuwa wakati mwingine walikuwa wakilazimika kukesha kwa ajili ya maombi kutokana na kuchoka na vituko vinavyotokea mara kwa mara usiku.

“Kwa kweli ilikuwa ni hali ya kutisha kwani kila baada ya siku mbili mtoto anaumwa mara huyu kesho huyu lakini hatukuacha maombi ambayo ndiyo yametoa majibu,” amesema.

Habari hii itaendelea kesho ambapo tutawaelezea zaidi kuhusiana na namna ambavyo hausigeli huyo alikuwa akiifanyia familia hiyo na pia jinsi alivyokuwa akitumia ndumba na utaalam wake wa kurusha ndege hewani usiku.
 
Back
Top Bottom