Baby Naomba Pesa Nikasuke

Elli

Platinum Member
Mar 17, 2008
55,416
85,844
Haya Tena Heri ya Christmas na Mwaka Mpya kwa Mpigo.

Watoto wamekua jamani, na wakubwa wamekuwa wadogo wanaitwa Baby!!!! Haya ndio niliyoyakuta kunako mahali hukooo MMU grounds. Kijana kawasha moto kweli kweli, kisa kaombwa au katakiwa atoe mupesa ya Msuko, Yebo yebo au Majimoto au twende kilioni mie hata sijui. Dai kubwa la kijana wangu ni hili hapa, fuata mlolongo huu mfupi;

Rose: Hello Baby wangu, jamani mbona umenisusa sana?
Juma: Mmmhh Nimekumisi Pia ( nikagundua kuwa hii nimekumisi wala haitoki moyoni)
Rose: Vipi leo tutaonana Baby?
Juma: Aaaahh ntafurahi sana maana tangu ukubali ombi langu hujawahi kunipa raha hata siku moja na mie nikajiona kidume
Rose: Kha! Yaani wewe unawaza ngono tu, kwanza wewe si una mkeo? Mimi mambo ya ngono sitaki kabisa
Juma: Sijakuelewa Dear
Rose: Ndio nimeshasema hivyo, kama unataka tuonane ili tufanye, mie siko tayari kabisa
Juma: Sasa kama mimi hunitaki kwanini unapenda pesa zangu? Acheni wizi wenu, mwezi mzima huu unanipiga Kalenda tuuu na maneno yako ya wizi....Usinipigie simu tena na namba yangu futa.
Rose: Mmmhhhh Baby hutaniwi?!!! Leo siko fresh ndio maana subiri mwezi ukiisha tu, utafurahi na moyo wako
Juma: Huo mwezi kaa nao tu, tangu uanze kusema hivyo umeshapita zaidi ya huo mwezi hakuna cha maana zaidi ya Vocha, kusuka, sijui kodi ya nyumba sijui nini........
Rose: Nitumie hata vocha basi..........................

Haya ndio niliyoyanasa mahali kwa ufupi, japo majina sio halisi. MORAL - tujifunze kuridhika na hali zetu pamoja na wapenzi wetu. Mwaka Mpya uanze na mambo mapya. Tunapoteza pesa nyingi kwa mambo yasiyo ya msingi. MUNGU awabariki mkaziangalie na kuzipigania familia zenu peke yenu.
 
Ametoka ubavuni kwake,amsikilize na avute subira,kwani anavyotoa hela ananunua? Na akitoa msaada lazima atake malipo? Mi hua natenda wema naenda zangu,hasara roho pesa karatasi na navyopenda kuchunwa!!! Nisipochunwa sina raha,na tusidanganyane kabisa hakuna asiechunwa kama huchunwi basi wewe unapiga punye..
 
Mwanaume asiyechunjwa ana mawili
1. Anapiga Punye
2. Mashine yake haifanyi kazi (imekufa) hainyanyuki kabisaaa

mwanaume lijali anachunwa 48hrs

Hahah! kula gwara mrembo..

Mi kunichuna mwisho 48hrs after 72Hrs lazima niwe nimekuchuna na wewe kwa kukusugua.
 
Back
Top Bottom