Babu wa Loliondo, Dawa za kuongeza Nguvu za Kiume vyaibua mjadala Bungeni

K-Boko

JF-Expert Member
Aug 3, 2013
697
218
Suala la Babu wa Loliondo limeibuka tena Bungeni ambapo Mh. Dk. Dalali Peter Kafumu (Igunga) ametaka kujua status ya tiba ya Babu na kauli ya Serikali.

Naibu Waziri wa Afya akajibu kuwa dawa ya Babu imethibitishwa haina madhara kwa mtumiaji ila suala la kupona ni imani kati ya mtoaji wa dawa na mpokeaji wa dawa! Pia suala la matangazo ya dawa za jadi za kuongeza nguvu za kiume na urefu wa maumbile ya kiume likajitokeza kujua kama Serikali imeruhusu matangazo hayo.

Naibu Waziri akasema matangazo ya namna hiyo hayaruhusiwi kwa mujibu wa Sheria namba 23 ya mwaka 2002 inayosimamiwa na Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala pamoja na Sheria ya Vyombo vya Habari na Utangazaji. Ametoa agizo kwa wakurugenzi, waganga wakuu wa mikoa na wilaya kulitekeleza agizo hilo!
 
Naibu Waziri wa Afya akajibu kuwa dawa ya Babu imethibitishwa haina madhara kwa mtumiaji ila suala la kupona ni imani kati ya mtoaji wa dawa na mpokeaji wa dawa!

Serikali yetu ina viongozi wajinga sana, ukisoma kwa makini hili jibu ndio utagundua kuwa tunaongozwa na misukule.

Unawezaje kuiita kemikali fulani ni dawa kama haujaithibitisha kama inatoa tiba???

Kwenye sekta ya utabibu na ufamasia huwa hakuna kitu kinachoitwa tiba ya imani, bali madawa na tiba nyinginezo zozote huwa ni matokeo ya tafiti za muda mrefu.

Sasa inakuwaje Waziri anachomekea suala la imani kwenye suala linalohitaji uchunguzi na utafiti wa kisayansi???

Hii nchi hii, eenh Mungu tusaidie waja wako
 
Back
Top Bottom