Elitwege
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 5,154
- 10,809
Mbunge wa jimbo la Morogoro kusini mashariki ambaye pia ni meneja wa msanii nguli hapa nchini Diamond Platnumuz, amewananga na kuwaita wanaharakati uchwara walioshindwa siasa za kuiondoa CCM madarakani na sasa wamehamia kushindana na mtu mmoja ambaye ni mwanamuziki Diamond Platnumz!
Babu Tale ameshangazwa na watu hao na kusema baada ya watu kama Tundu Lissu kushindwa kuichafua nchi hivi sasa wamehamia kumchafua mtu mmoja anayejipatia mkate wake kupitia muziki kwa kuiwakilisha nchi yake vizuri sana kimataifa.
Babu Tale amesema watu hao ni wanafiki na hawatafanikiwa kwani riziki anatoa mwenyezi Mungu pia hizo tuzo haziamuriwi na kura za hao wanaharakati wanafiki.
Huwezi kuhubiri Demokrasia huku ukiwananga wenzio wanaochagua wanachokipenda, Wasafi ipo CCM kabla ya hao wanafiki wa mitandaoni.
Babu Tale ameshangazwa na watu hao na kusema baada ya watu kama Tundu Lissu kushindwa kuichafua nchi hivi sasa wamehamia kumchafua mtu mmoja anayejipatia mkate wake kupitia muziki kwa kuiwakilisha nchi yake vizuri sana kimataifa.
Babu Tale amesema watu hao ni wanafiki na hawatafanikiwa kwani riziki anatoa mwenyezi Mungu pia hizo tuzo haziamuriwi na kura za hao wanaharakati wanafiki.
Huwezi kuhubiri Demokrasia huku ukiwananga wenzio wanaochagua wanachokipenda, Wasafi ipo CCM kabla ya hao wanafiki wa mitandaoni.