Babu Tale: Wanaharakati uchwara siasa zimewashinda sasa wanashindana na Diamond Platnumz

Elitwege

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
5,154
10,809
Mbunge wa jimbo la Morogoro kusini mashariki ambaye pia ni meneja wa msanii nguli hapa nchini Diamond Platnumuz, amewananga na kuwaita wanaharakati uchwara walioshindwa siasa za kuiondoa CCM madarakani na sasa wamehamia kushindana na mtu mmoja ambaye ni mwanamuziki Diamond Platnumz!

Babu Tale ameshangazwa na watu hao na kusema baada ya watu kama Tundu Lissu kushindwa kuichafua nchi hivi sasa wamehamia kumchafua mtu mmoja anayejipatia mkate wake kupitia muziki kwa kuiwakilisha nchi yake vizuri sana kimataifa.

Babu Tale amesema watu hao ni wanafiki na hawatafanikiwa kwani riziki anatoa mwenyezi Mungu pia hizo tuzo haziamuriwi na kura za hao wanaharakati wanafiki.

Huwezi kuhubiri Demokrasia huku ukiwananga wenzio wanaochagua wanachokipenda, Wasafi ipo CCM kabla ya hao wanafiki wa mitandaoni.

 
Mbunge wa jimbo la Morogoro kusini mashariki ambaye pia ni meneja wa msanii nguli hapa nchini Diamond Platnumuz, amewananga na kuwaita wanaharakati uchwara walioshindwa siasa za kuiondoa CCM madarakani na sasa wamehamia kushindana na mtu mmoja ambaye ni mwanamuziki Diamond Platnumz!

Babu Tale ameshangazwa na watu hao na kusema baada ya watu kama Tundu Lissu kushindwa kuichafua nchi hivi sasa wamehamia kumchafua mtu mmoja anayejipatia mkate wake kupitia muziki kwa kuiwakilisha nchi yake vizuri sana kimataifa.

Babu Tale amesema watu hao ni wanafiki na hawatafanikiwa kwani riziki anatoa mwenyezi Mungu pia hizo tuzo haziamuriwi na kura za hao wanaharakati wanafiki.

Huwezi kuhubiri Demokrasia huku ukiwananga wenzio wanaochagua wanachokipenda, Wasafi ipo CCM kabla ya hao wanafiki wa mitandaoni.


Elitwege of all the donkeys!Bubu Tale ndiyo role model wako wa nyakati hizi?Shame dame!Huwa huishiwi vibweka na kutuonesha akili zako hugotea wapi!🤣🤣🤣🤣🤣
 
Babu tale anakosea sana kuliingilia hili swala kisiasa. Atayaona matokeo yake. Bora angekaa kimya au angeiga busara za Diamond mwenyewe
Madhara gani jomba? Kwamba wasafi kuwa ccm ndo italeta shidaa..hahaha..kwa tarfa yako tuu..mashabiki wa music bongo huwa hawanaga hata story na mavyama ya siasaaa..wao wanaangalia ngoma tu na kuzichezaaaa....
 
Mwanaharakati si mwanasiasa. Mwanaharakati hupiga kote kote......Ukweli uko wazi, akiwa kama mwanamuziki maarufu Diamond na wanasanii wengine wote alipaswa kuwa neutral kama dada Judith Lady Jaydee. Kujitanabaisha kuwa wao ni ccm au cdm kwa waziwazi pasipo haya wamekosea sana. Siku wanamuziki vipenzi wa upinzani wakiwa nominated nao watakumbana na zengwe, na ikitokea chama kingine kikachukua nchi hata kama ni kwa kutotarajia, wasanii mashabiki wa ccm lazima watafanyiwa zengwe.

Music is a universal language, haipaswi mwanamuziki attached kwa tabaka lolote la kisiasa au chama cochote
 
Mwanaharakati si mwanasiasa. Mwanaharakati hupiga kote kote......Ukweli uko wazi, akiwa kama mwanamuziki maarufu Diamond na wanasanii wengine wote alipaswa kuwa neutral kama dada Judith Lady Jaydee. Kujitanabaisha kuwa wao ni ccm au cdm kwa waziwazi pasipo haya wamekosea sana. Siku wanamuziki vipenzi wa upinzani wakiwa nominated nao watakumbana na zengwe, na ikitokea chama kingine kikachukua nchi hata kama ni kwa kutotarajia, wasanii mashabiki wa ccm lazima watafanyiwa zengwe.

Music is a universal language, haipaswi mwanamuziki attached kwa tabaka lolote la kisiasa au chama cochote
Yani akae neutral kukufurahisha wewe?
Jinga kabisa
 
Madhara gani jomba? Kwamba wasafi kuwa ccm ndo italeta shidaa..hahaha..kwa tarfa yako tuu..mashabiki wa music bongo huwa hawanaga hata story na mavyama ya siasaaa..wao wanaangalia ngoma tu na kuzichezaaaa....
Jaribu kuliwaza hili kibiashara, achana na mambo ya ushabiki wa kisiasa.
 
Back
Top Bottom